Mkunazi Njiwa
JF-Expert Member
- Apr 22, 2023
- 8,538
- 7,559
Si kweli....Kikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Kama ndivyo aliwezaje kudumu muda wote huo?!!!
Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Si kweli....Kikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Unaona sasa ulivyo muongo eti wazungu wa UK hawajali elimu sana! Jidanganye labda kwa kazi ya kubeba boksi. Haujui lolote nakuhakikishia SK kimemtoa BBC elimu na kashindwa na Mkenya ndio yeye na wenzake wakatoa wengine wakakimbilia Idhaa ya Kiswahili ya Uturuki. BBC bila elimu na kumbuka dunia inapika kwenye bahari ya mabadiliko makubwa sio hizi Local media sina akina Swebe,Baba Levo,Kitenge, Kumwembe na akina Jose Mara zilivyojaza upuuzi na ujinga mtupu. Tena ukome kusema UK hawajali elimu vile vyuo vyao unajua wanavyozilinda kupokea watu wajinga kama wewe.Sio rahisi BBC kumuachisha kazi mfanyakazi hapo London labda kama huzijui vema employment laws za Uingereza. Ni rahisi tu ndani ya miaka 2 ya mwanzo wa ajira lakini hata hiyo ina discrimination disclaimer, baada ya hapo sio rahisi- ni mchakato mrefu sana. Kumbuka pia kwamba wazungu wa UK hawajali sana elimu ya darasani, wanajali sana uzoefu kazini na ndio maana wanakazania sana apprentships, work expirences etc kwa watoto wao. na kuna makamuni hutoa degree kwa uzoefu wa kazi pekee. Nakuomba tu acha kutoa sweeping statements bila ushahidi maana defamation itakuhusu.
Na kilichompeleka BBC ni nini?Kikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Na Wilaya ya Lulandala iko waziMkuu uko sawa kabisa maana kuna wilaya mbili Wilaya Ya TEMEKE na wilaya Ya HANDENI hazina Ma DC kutokana na uteuzi wa juzi na jana
Kilichoelezwa Hapa na kumposa kikeke Ni kavideo chake Cha kudhiaki hoja ya bandari kwa kuchapisha maudhui ktk mtando wake wa Instagram na Kisha kushare na followers wakeHakuna salamu hapa, naingia kwenye mada moja kwa moja. Kama ilivyokuwa kwa Tido Mhando aliyetolewa BBC na kuletwa kusimamia TBC, ndivyo ilivyokuwa kwa Salim Kikeke. Taarifa za kiintelejensia zinapenya kuwa ndugu Kikeke aliombwa kung’atuka BBC ili arudi nchini kuandaliwa kuwa msemaji wa serikali. Baada ya kufika nchini alisubiri kwa muda mama aachie nafasi ya uteuzi bila mafanikio. Ndipo akaamua kwenda kujishikiza pale EFM ili mama akipangua nafasi za uteuzi yeye ateuliwe kuwa msemaji wa serikali. Inavyoonekana ni kama vetting bado ilikuwa haijakamilika.
Baadaye upekuzi ulipofanyika kwa kina zaidi, ikaonekana nafasi ya usemaji wa serikali haitamfaa. Nafasi ile inamfaa mtu muongeaji na mwenye uwezo wa kuelekezwa kusema uongo akatoka hadharani kuusema na kuutetea kwa macho makavu. Kikeke ni mtu wa msimamo na asiyefundishwa nini cha kuongea. Ni mtu mwenye kusimamia maadili ya habari na anamuogopa Mungu. Ni vigumu sana kumwambia aende hadharani kusema uongo kwa lengo tu la kutetea jambo au madudu ya serikali.
Hiki ndiko kilichomponza kijana wa watu licha ya kushawishiwa kurudi nyumbani apewe kazi na serikali lakini kazi aliyoahidiwa amekuja kupewa mtu mwingine. Wafanyakazi wa BBC huwa wanafundishwa maadili ktk taaluma ya habari yanawafanya waive sawasawa na kutokubali kuyumbishwa.
Tukumbuke pia Tido Mhando misimamo yake ni sawa na ya Kikeke. Tido aliombwa kurudi nchini akapewa TBC. Baada ya kunyesha msimamo usioyumba katika kusimamia ukweli kwenye habari, serikali ikamtupa nje na kisha kumfungulia kesi ya bandia ya uhujumu uchumi. Mpaka sasa nadhani hiyo kesi anateseka nayo mahakamani.
Kumbuka mtu kaacha kazi BBC anakolipwa mamilioni ya paundi za kingereza anashawishiwa kurudi nyumbani apewe kazi nzuri halafu hapewi! Hii sio sawa. Kama kazi hakuna au huna uhakika wa kumpa kazi, ni bora wangemuacha abaki BBC aendelee kuvuna paundi zake angerudi nyumbani afungue media awaajiri vijana wenzake.
Tazama mfano wa Abdalla Bulembo Majura aliyevuna paundi za kutosha akiwa BBC aliporudi nyumbani amefungua kituo cha redio ABM FM kule Dodoma amewaajiri vijana wa kitanzania wanapata ridhiki zao za kila siku bila tatizo. Kama Kikeke angeachwa aendelee kukaa BBC hadi astaafu angerudi nchini akiwa na paundi za kutosha akafungua kituo cha TV au redio akawaajiri vijana wenzake. Sio haki kumuahidi mtu kuacha kazi ya pesa nyingi halafu anarudi nyumbani kwa matumaini ya kupewa kazi, anatoswa mazima. Tabia hii sio nzuri na haitoi mfano mzuri kwa vijana wachapa kazi kama Kikeke.
USHAURI WANGU
Naishauri serikali impangie kazi nyingine ndugu Salim Kikeke kwa kuwa wameamua kugawa nafasi yake kwa mtu mwingine kinyume na makubaliano. Huu mchezo wa kutosana ukiendelea, itakuwa vigumu kuwashawishi vijana wezalendo kutoka ughaibuni kurudi nyumbani kuitumikia nchi yao. Nchi hii ni yetu sote, sio mali ya kikundi fulani cha watu.
Nawasilisha.
Hili ndo tatizo la wabongo... huwa hampendani!Kumbe wale waswahili wenzetu watangazaji wa idhaa ya kiswahili ya BBC wanalipwa mamilioni ya paundi ya Uingereza kila mwezi!
Hana shule Ni mtu smart Sana akili zake siyo sawa na zakoKikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Ninakubaliana na Wewe 100%, kwani alimaliza form four mwaka 1988, Makumira sekondari akalamba Division 4.Kikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.
Yaan wanaropoka tu! Wakishakutana wote mazwazwa hawana kazi za kufanya wanajazana ujinga tu 😂Kumbe hata hujui unaloongea BBC imefunga ofisi zake huko uingereza unasingizia eti kaacha kazi ili aje Tanzania kupewa kazi na serikali. Hii redio mbao hii [emoji1787][emoji1787]
Division 4 sio mwisho wa maisha... baadae alisoma kilimo na uandishi wa habari akaenda Ulaya na akasoma mpaka akafikia ngazi ya masters kwa taarifa yako. Na hivi sasa yeye ni bora kuliko waliopataga division 1Ninakubaliana na Wewe 100%, kwani alimaliza form four mwaka 1988, Makumira sekondari akalamba Division 4.
Unamaliza shule na F4, unataka akasema msemaji wa Serikali ipi?Division 4 sio mwisho wa maisha... baadae alisoma kilimo na uandishi wa habari akaenda Ulaya na akasoma mpaka akafikia ngazi ya masters kwa taarifa yako. Na hivi sasa yeye ni bora kuliko waliopataga division 1
Wewe na kikeke nani mwenye maajabu?Wanamkuuuuza huyo SK, wakati hana maajabu yoyote.
-Kaveli-
Toka lini hujui kusoma?Kwani msemaji wa serikali ameshachaguliwa? ni nani
Alifikaje bbc na kukaa miaka yote hiyo huku akiwa ni muhuni muhuni? Wivu utakuua kwa taarifa yako haumzidi kikeke kuanzia mafanio,umaarufu na connectionKikeke hana shule yule ni mhuni mhuni tu. Kilichomtoa BBC ni shule sio kingine.