China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

Nilisikia eti jamaa wa Silent Ocean siku hizi hawasafirishi loose cargo? Sasa sisi akina yakhe tunasafirishaje mizigo yetu kutokea China? Vifaa vya ujenzi mkuu biashara yake ikoje huko? Nina mpango wa kuja kufuatilia hivyo vifaa (ingawa sasa kikwazo kinakuwa kujua kampuni ya kusafirishia mizigo), maana aliyenielekeza aliniambia silent ocean ndo wazuri sasa nao ndo hivyo tena!
mkuu hizi taarifa za silent ocean kutochukua loose cargo hazikuwa za kweli .nilifatilia na nimeweka mawasiliano yao hapa kwenye thread unaweza kuwasiliana nao moja kwa moja.
 
mkuu hizi taarifa za silent ocean kutochukua loose cargo hazikuwa za kweli .nilifatilia na nimeweka mawasiliano yao hapa kwenye thread unaweza kuwasiliana nao moja kwa moja.
Asante kiongozi wangu kwa taarifa! Wafanyabiashara wote wangekuwa na moyo mnyoofu wa kutoa msaada wa kimawazo kama wako, watu wangepiga hatua kimaendeleo! Kipilipili umekuwa wa msaada sana katika hii thread ya biashara za China, MUNGU akubariki!
 
Eti Kipilipili ni miezi ipi mizuri kwa kufanya safari za China? Yaani kuepuka baridi, mvua (hizi zinasababisha hadi land slide) n.k? Asante!
 
Wakuu wenye uelewa katika hili naomba msaada,

Ninahitaji kuwa na home industry, itayohusika na izaloshaji wa mvinyo.

mahitaji yangu ni vifaa vya kufungashia bidhaa(plastic) na kifaa cha kupimia alcohol.

Nahitaji kujua brand za mashine na bei zake
 
Eti Kipilipili ni miezi ipi mizuri kwa kufanya safari za China? Yaani kuepuka baridi, mvua (hizi zinasababisha hadi land slide) n.k? Asante!
mkuu inategemea unafanya biashara ya aina gani. kuna biashara ambazo ukija wakati wa summer masoko ni mengi na bidhaa ni nyingi mfano bidhaa kama nguo(tunazovaa nyumbani ambazo nyingi ni nyepesi na kwa huku huvaliwa wakati wa summer) ukija wakati wa winter miez ya november-march hutapata machaguo mengi kwa sababu maduka mengi yatakuwa yanauza nguo za winter. lakini pia kama wewe ni mfanyabiashara wa spare parts kuja kipindi cha baridi inaweza kukupunguzia gharama za nauli mana kipindi hiki mashirika ya ndege huwa na ofa nyingi na pia abiria wanaosafiri ni wachache kwa hiyo bei ya nauli iko chini...kwa hyo inategemea mkuu
 

Attachments

  • BUSINESS CARD.jpg
    BUSINESS CARD.jpg
    63.1 KB · Views: 216
Mkuu, in most cases hawa jamaa wanahitaji MALI GHAFI kama vile MBAO zenye ubora ili kutengenezea samani mbalimbali. Pia wanahitaji sea products kama samaki wa aina mbalimbali kwa ajili ya kusindika.
Bidhaa nyingine ambazo watanzania tunaweza kuuza kwao ni kahawa, matunda hasa maembe! Juice ya maembe iko ghali sana China na nadhani ni kwa sababu wao hawalimi.
Nyama ya NG'OMBE hasa wanaotoka huku kwetu ni WATAMU ukilinganisha na nyama inayouzwa China ambayo haitoshelezi soko. . Ikumbukwe kuwa kuku na kitimoto ndio nyama rahisi inayoliwa na wachima
mkuu tafadhali naomba unisaidie ni jins gan nitapata masoko china ili niweze kupeleka bidhaa kule I mean kamchakato kazma plz
Mkuu, in most cases hawa jamaa wanahitaji MALI GHAFI kama vile MBAO zenye ubora ili kutengenezea samani mbalimbali. Pia wanahitaji sea products kama samaki wa aina mbalimbali kwa ajili ya kusindika.
Bidhaa nyingine ambazo watanzania tunaweza kuuza kwao ni kahawa, matunda hasa maembe! Juice ya maembe iko ghali sana China na nadhani ni kwa sababu wao hawalimi.
Nyama ya NG'OMBE hasa wanaotoka huku kwetu ni WATAMU ukilinganisha na nyama inayouzwa China ambayo haitoshelezi soko. . Ikumbukwe kuwa kuku na kitimoto ndio nyama rahisi inayoliwa na wachima
 
uzi mzuri saana
je ile safari ya kwenda thailand imefikia wapi wakuu
 
Siko la asali sina details za soko lake hapa China.

Natoa wito kwa wengine wanaotaka ku export bidhaa zao nje ya nchi wanitumie majina ya vitu hivyo kisha nitavituma kwa wahusika
Mkuu nahitaji kufahamu juu ya kununua mtumba online kutoka china hapa namainisha belo za mtumba sijui hata pakuanzia lakini je mfano nikiwa na kianzio cha milioni tatu au nne naweza kuanzisha biashara yakuimport mzigo?
Msaada wako unahitajika kwangu hata pia mawazo
 
NIMEPATA RAFIKI/WORKMATE AMBAYE TUTAENDA NAYE NA KUNUNUA MZIGO PAMOJA NA KUJA KUUZA PAMOJA-TUTAFUNGUA DUKA K/KOO
 
Habari wana jukwaa,

Kumekuwa na ongezeko kubwa la wafanyabishara kutoka Tanzania kwenda China kufanya biashara mbalimbali kama nguo, vipuri vya magari na pikipiki, vifaa vya electronics nk. Najua kuna thread nyingi zimewahi kuzungumzia biashara za China, lakini nimuombe mkuu Invisible aifanye hii iwe sticky thread ili iwe refernce point kwa kila anaehitaji kufanya biashara China.

Nitaeleza KIDOGO Kuhusu biashara za China.
BIASHARA YA NGUO: hii inapendwa sana kufanywa na kina dada japo wanaume pia wapo. Wengi walio wageni na biashara hii wamejikuta wakipata hasara hasa wanapofika tu miji kama Guanzhou na kuanza kununua nguo bila kuangalia hali ya soko Tanzania ikoje.

Hujikuta wakinunua nguo on their perspective and not customers perspective! Kinachowavutia machoni mwao ndicho wanachonunua kwa matarajio watauza tu. Wengine wananunua na wanapofika na mzigo kariakoo wanakuta mzigo kama huo uloshaingia a week/month before hivyo kujikuta wanauza kwa bei ya hasara.

Ushauri: jaribu kutafuta wateja kabla Tanzania , wakupe order na sample kisha ukifika China nunua kile walichokuagiza.Pia jitahidi ujue ni fashion gani bongo iko sokoni na mpaka mzigo umefika bongo,je bado hiyo fashion ulionunua itakuwa inauza? Mind you kwamba biashara ya nguo hasa za WANAWAKE zinaendeshwa kwa nguvu ya soko na fashion hubadilika mara kwa mara!Biashara ya nguo za watoto au wanaume kidogo fashion zake zinakaa muda mrefu ukilinganisha na za wanawake.

BIASHARA YA VIFAA VYA ELEKTRONIKI kama simu na accessories zake, music system n.k
Miji mizuri ya kununua mzigo kwa biashara hii ni Shenzhen na Honkong ,japo mji wa Guanzhou pia ni maarufu isipokuwa fake products kwa Guanzhou ni kubwa zaidi. Changamoto kubwa ya biashara hii ni FAKE PRODUCTS. Angalia wateja wako ni watu wa namna gani. Most low income earners ambao kwa Tanzania ndio wengi, wanapenda cheap price.

Kwahiyo, ukinunua genuine products huwezi kuuza bongo kwa sababu bei itakuwa iko juu na wao watashindwa. Kwa hiyo jua needs and wants za customers wako kabla hujaamua kununua mzigo.Kwa mtu mwenye mtaji mdogo unaweza kuanza na kununua phone acssesories na simu chache tu za bei ya chini, utakuwa unaongeza idadi ya simu kidogo kidogo kadri mtaji unavyokua.Pia kama una mtaji mkubwa unaweza kuingiza used products kama photocopier machines ila jitahidi uwe na orders kabla hujaleta kwa sababu ukija nazo nyingi bila order zinaweza kukaa muda mrefu ukajikuta unaanza kula mtaji.

Wakati unasafirisha photocopier machines jitahidi ununue vitu vidogo vidogo kama vile memory cards, USB cards, power banks nk na uviweke pamoja ndani ili ukija bongo wakati unasubiri kuuza photocopier machines unauza hivyo vitu vidogo vidogo ili kupata faida kidogo kidogo na kuhakikisha huli mtaji.

Kumbuka hapa utasafirisha kwa meli na huwa wanapima CBM na sio uzito kwa hiyo hivyo vitu vidogo vidogo cost yake ya kusafirisha itakuwa imemezwa na hizo machines.Photocopier machines nimetoa kama mfano wa moja ya bidhaa lakini vipo vimashine vingi tu ambavyo unaweza kusafirisha kama:Mashine za juice ya miwa, hizi zimekuwa na demand kubwa sana kwa sasa Tanzania. Wateja wake wapo , kama utakuwa na mtaji mzuri unaweza kununua hizi na kuleta. Nyingi ni portable na modern. Ni kiasi cha kutafuta orders na kisha kuleta.
Kuangalia bei mbalimbali za bidhaa tembelea:
Find quality Manufacturers, Suppliers, Exporters, Importers, Buyers, Wholesalers, Products and Trade Leads from our award-winning International Trade Site. Import & Export on alibaba.com

Made-in-China.com mobile- Connecting Buyers with China Manufacturers, Suppliers & Products

www.taobao.com (hii ni ua kichina, tumia browser ya google chrome na tumia kitufe cha translation ili ije kwa kingereza)

USAFIRI: Zipo kampuni nyingi zinazosafirisha mizigo kwa njia ya ndege na meli. Kampuni kama THE LAND, SILENT OCEAN ni baadhi tu na hizi zina ofisi zao pale pale Guanzhou na bei zake zinatofautiana kutegemeana unasafirisha kwa njia gani yaani ndege au meli. Na unapolipia wao ndio huhusika na clearance na kila kitu, wewe ukifika bongo unachukua tu mzigo wako kwenye Ghala lao.
Website ya baadhi ya makampuni ni:
Silent Ocean Limited - Specialized in International Cargo Shipping

NAULI:nauli zinategemea season na pia unataka kusafiri lini. Kipindi cha high season kama ,july, august bei zinakuwa juu. Kama kwa mfano unatarajia kusafiri July basi ikifika april kata tiketi mapema . Mara nyingi kunakuwa na offer kwenye mashirika ya ndege kwa hiyo pendelea kutembelea website zao.
Pia nauli inategemea na shirika la ndege unalotaka kusafiria na pia daraja unalotaka kukaa.
Kwa wafanyabiashara wengi hutumia ethiopian airline kwa sababu huwa wanatoa kg nyingi kuliko wengine.
Pita kwa mawakala posta na kariakoo au search google kupata bei mbalimbali za nauli. Unaweza kutenga bajeti ya USD 900-1200 Kwa nauli kwa economy class
Angalia bei za NAULI hapa:
International Flights, Airfares, Tickets - Fly Ethiopian

Qatar Airways

https://www.klm.com/?_e_pi_=7,PAGE_ID10,8626374365


MALAZI: Hapa nitazungumzia mji wa Guanzhou ambao ndio wenye wafanyabiashara wengi wa mataifa mbalimbali hasa Afrika. Zipo hoteli za hadhi tofauti, bei kutoka 120 yuan(36,000 Tsh) ikiwa ni bei ya chini labisa na kuendelea kutegemeana na mfuko wako. Maeneo kama "shaobei lu" ni maarufu kwa watu weusi na utakisikia kiswahili kila baada ya hatua kadhaa. Hoteli za pembeni ya mji bei huweza kuwa chini mpaka yuan 100.
Angalia range ya bei za hoteli hapa:
GuangZhou hotels: cheap rates in GuangZhou by China Hotels Reservation


CHAKULA: zipo hoteli nyingi Guanzhou na shenzen zinazomilikiwa na foreigners na wanauza chakula kizuri japo kiko ghali kidogo, ila kama unahitaji chakula cha bei ya chini na ambacho ni HALAL (wengi huhofia kulishwa mbwa,kitimoto,nk) unaweza kula kwenye sehemu nyingi ambazo huuza wachina waislamu wenye asili ya Xinjiang ambao huuza HALAL food kwa bei poa kuanzia Yuan 15(4500 Tsh) na kuendelea kutegemea na aina ya chakula ulichoagiza. Kuwa makini na vyakula mana wale wenzetu huwa wanakula vyakula vingi vya "ajabu ajabu".

LUGHA: wachina hutumia lugha yao kwa kila kitu. Katika miji ya biashara kama Guangzhou wachina wafanyabiashara huongea kingereza cha mawasiliano(kibovu) ila mnawasiliana na kuelewana. Pia lugha ya ishara inatumika pale panapokuwa na language barrier . Hata kama hujui kabisa kingereza unaweza kuchagua bidhaa na kisha mkapatana bei. Wenzetu wana utaratibu wa kutumia calculator kukuandikia bei, hivyo na wewe utaandika ya kwako mpaka mtafikia makubaliano. Nashauri download application yoyote ya TRANSLATION kama pleco nk ili ikusaidie kwenye mawasiliano unapokwama andika neno unslohitaji kwa kingereza kisha tafsiri kwa kichina na muoneshe mchina hilo neno, itasaidia kurahisisha mawasiliano

Nimegusa juu juu vitu vichache mno kuchokoza mada ili wengine waongezee uzoefu na iwe msaada kwa kila anaetaka kufanya biashara China.

Karibuni tujadili na kusaidia wengine
#hii thread ni educative, ahsante Mkuu!!
 
Huu Uzi uko vizuri lakini kwa mtazamo inaonekana wengi tunatamani kwenda China kununua mzigo tatizo lipo kwenye mitaji.

Kwamba ni kiwango gani cha mtaji kitafaa kwenda nacho ili ukirudi uweze kumudu ushindani.

Nasikia wachina wanapunguza bei kulingana na ukubwa wa mzigo wako unaochukua,
Hivyo ni vizuri wenyewe uzoefu muwatahadharishe wanaotegemea kwenda na Pesa kidogo wakitegemea wakirudi waweze kushindana na makampuni yanayoagiza mizigo kama God one au Sunda.
Nadhani wataishia kulaumu na kupoteza mitaji yao kidogo.
 
Huu Uzi uko vizuri lakini kwa mtazamo inaonekana wengi tunatamani kwenda China kununua mzigo tatizo lipo kwenye mitaji.

Kwamba ni kiwango gani cha mtaji kitafaa kwenda nacho ili ukirudi uweze kumudu ushindani.

Nasikia wachina wanapunguza bei kulingana na ukubwa wa mzigo wako unaochukua,
Hivyo ni vizuri wenyewe uzoefu muwatahadharishe wanaotegemea kwenda na Pesa kidogo wakitegemea wakirudi waweze kushindana na makampuni yanayoagiza mizigo kama God one au Sunda.
Nadhani wataishia kulaumu na kupoteza mitaji yao kidogo.
Ni kweli mkuu suala la mtaji ni changamoto kwa wengi,japokuwa tusitishike na haya makampuni makubwa. Hata Roma haikujengwa siku moja kama watu wasemavyo.cha msingi ni kuanza na hicho hicho kidogo mtu alichonacho na akiwa ndani ya biashara tayari atagundua vingi ambavyo akiwa nje hawezi kugundua wala kuwa na tajiriba(experience) navyo.
Hawa wafanyabiashara wadogo nashauri wawe wana"segment" soko lao kwa kuangalia ni aina gani ya wateja watawahudumiwa .Hii itasaidia kupanua soko na kuwafikia wateja wa hadhi,kada na madaraja tofauti.
 
Back
Top Bottom