China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

China: Fursa za biashara, usafiri na masoko

Hello!

Nguo na urembo inabidi uende China kwenye masoko ili uweze kuchagua mwenyewe

Masoko yapo katika miji ya
1. Guangzhou - hapa unaweza kupata kila kitu unachohitaji, lakini kwa kiasi kikubwa nguo zao ni low quality
2. Yiwu -
3. Shanghai -
4. Shenzhen - Nguo, handbags na viatu vizuri. Quality zao ni nzuri pia. Urembo sina hakika
Mkuu hongera kwa kuwapa mwanga watanzania wenzako wenye nia ya kujikwamua kibiashara, na mie niombe kupewa muongozo nahitaji kufanya biashara ya nguo za jeans za kike na kiume toka china ni mji gani naweza kupata bidhaa zenye ubora mzuri na kwa bei nzuri?
Na kingine ningependa kujua kati ya china, bangkok au hongkong ni wapi muafaka kuchukulia mzigo?
 
Mkuu hongera kwa kuwapa mwanga watanzania wenzako wenye nia ya kujikwamua kibiashara, na mie niombe kupewa muongozo nahitaji kufanya biashara ya nguo za jeans za kike na kiume toka china ni mji gani naweza kupata bidhaa zenye ubora mzuri na kwa bei nzuri?
Na kingine ningependa kujua kati ya china, bangkok au hongkong ni wapi muafaka kuchukulia mzigo?

1. Jeans - zipo nyingi sana pale guangzhou. Lakini jeans nyingi za Guangzhou zipo na madoido ya west africa. Ukitulia katika masoko na maduka ya pale Guangzhou unaweza pata jeans nzuri sana.

2. Kila eneo lina taste zake
China - kuna kila aina ya products NZURI na MBAYA zoote zipo na unazipata kwa urahisi

Thailand - Huwa naenda kula bata, sijui kuhusu nguo za kule.

Hongkong - Iko poa sana, ina nguo nzuri sana, lakini bei zake ziko juu kidogo.


Ushauri:
- Nenda China kupitia hongkong, nunua mzigo pale. Waachie ma-agent wa kutuma mizigo kwenda TZ. Usiingie na mizigo mingi kwenda China, ni risk
- Kamata train ya haraka pale Hongkong ingia China-Guangzhou fanya manunuzi yako pale
- Nenda shenzhen mji karibu na Guangzhou fanya manunuzi yako pale, kisha rudi Guangzhou
- Funda mizigo yako, rudi Tanzania kaanze kuuza
 
1. Jeans - zipo nyingi sana pale guangzhou. Lakini jeans nyingi za Guangzhou zipo na madoido ya west africa. Ukitulia katika masoko na maduka ya pale Guangzhou unaweza pata jeans nzuri sana.

2. Kila eneo lina taste zake
China - kuna kila aina ya products NZURI na MBAYA zoote zipo na unazipata kwa urahisi

Thailand - Huwa naenda kula bata, sijui kuhusu nguo za kule.

Hongkong - Iko poa sana, ina nguo nzuri sana, lakini bei zake ziko juu kidogo.


Ushauri:
- Nenda China kupitia hongkong, nunua mzigo pale. Waachie ma-agent wa kutuma mizigo kwenda TZ. Usiingie na mizigo mingi kwenda China, ni risk
- Kamata train ya haraka pale Hongkong ingia China-Guangzhou fanya manunuzi yako pale
- Nenda shenzhen mji karibu na Guangzhou fanya manunuzi yako pale, kisha rudi Guangzhou
- Funda mizigo yako, rudi Tanzania kaanze kuuza
Nashukuru sana kiongozi nitalifanyia kazi hili.
 
Asante mkuu. Ameen

Mkuu Kipilipili,

Nikushukuru kwa maelezo na majibu mazuri ktk thread hii. Nimesoma pages nyingi tu za uzi huu lakini naomba nikuulize maswali yafutatyo hata kama kuna sehemu (nyuma) mmezungumzia ila mimi sijaona:

1. Container dogo ili lijae linahitaji mzigo mkubwa kiasi gani na gharaza za container kutoka China mpaka Dsm ni kiasi gani kwa makadirio?
2. Kwa uzoefu wako,ni mji gani una supply stationery goods (& its accessories)+ ream papers karibia za aina zote na zinapatikana hapo kwa pamoja ikiwa ni pamoja na computer accessories, photocopiers. + wino mbali mbali (brand and used)
3. Kwa bidhaa za stationeries tajwa hapo juu nikiandaa mil.20 (ya mzigo tu) china nitapata mzigo wa kuniwezesha kuja kuuza kama supplier/wholesaler (quantity) au ni mzigo unaofaa kuuweka dukani na kuuza kama Retailer? Nataka kufahamu ni mtaji kiasi gani unaweza ukawa mzuri kufanyia biashara ya aina hii kama wholesaler (niuze kwa bei ya jumla) aua kama retailer (kununua mzigo kwa ajili ya kuuza rejareja tu)
4. Kwa uzoefu wako, ni nchi gani nje na china ambazo zina produce products tajwa hapo (with quality) juu kwa friendly price? which country between them ni nzuri kwa wajasiliamali wa kitanzania?

Mwisho, nikuombe uniPM contacts zako kama hutojali.
Thank you in advance.
 
Mkuu Kipilipili,

Nikushukuru kwa maelezo na majibu mazuri ktk thread hii. Nimesoma pages nyingi tu za uzi huu lakini naomba nikuulize maswali yafutatyo hata kama kuna sehemu (nyuma) mmezungumzia ila mimi sijaona:

1. Container dogo ili lijae linahitaji mzigo mkubwa kiasi gani na gharaza za container kutoka China mpaka Dsm ni kiasi gani kwa makadirio?
2. Kwa uzoefu wako,ni mji gani una supply stationery goods (& its accessories)+ ream papers karibia za aina zote na zinapatikana hapo kwa pamoja ikiwa ni pamoja na computer accessories, photocopiers. + wino mbali mbali (brand and used)
3. Kwa bidhaa za stationeries tajwa hapo juu nikiandaa mil.20 (ya mzigo tu) china nitapata mzigo wa kuniwezesha kuja kuuza kama supplier/wholesaler (quantity) au ni mzigo unaofaa kuuweka dukani na kuuza kama Retailer? Nataka kufahamu ni mtaji kiasi gani unaweza ukawa mzuri kufanyia biashara ya aina hii kama wholesaler (niuze kwa bei ya jumla) aua kama retailer (kununua mzigo kwa ajili ya kuuza rejareja tu)
4. Kwa uzoefu wako, ni nchi gani nje na china ambazo zina produce products tajwa hapo (with quality) juu kwa friendly price? which country between them ni nzuri kwa wajasiliamali wa kitanzania?

Mwisho, nikuombe uniPM contacts zako kama hutojali.
Thank you in advance.
Tumsubiri Kipilipili
 
Mkuu, je bidhaa kufuata China au kununua ktk tovuti kama Alibaba.com ipi gharama ni nafuu?
 
Habari wana jukwaa,

Kumekuwa na ongezeko kubwa la wafanyabishara kutoka Tanzania kwenda China kufanya biashara mbalimbali kama nguo, vipuri vya magari na pikipiki, vifaa vya electronics nk. Najua kuna thread nyingi zimewahi kuzungumzia biashara za China, lakini nimuombe mkuu Invisible aifanye hii iwe sticky thread ili iwe refernce point kwa kila anaehitaji kufanya biashara China.

Nitaeleza KIDOGO Kuhusu biashara za China.

BIASHARA YA NGUO:
hii inapendwa sana kufanywa na kina dada japo wanaume pia wapo. Wengi walio wageni na biashara hii wamejikuta wakipata hasara hasa wanapofika tu miji kama Guanzhou na kuanza kununua nguo bila kuangalia hali ya soko Tanzania ikoje.

Hujikuta wakinunua nguo on their perspective and not customers perspective! Kinachowavutia machoni mwao ndicho wanachonunua kwa matarajio watauza tu. Wengine wananunua na wanapofika na mzigo kariakoo wanakuta mzigo kama huo uloshaingia a week/month before hivyo kujikuta wanauza kwa bei ya hasara.

Ushauri: Jaribu kutafuta wateja kabla Tanzania , wakupe order na sample kisha ukifika China nunua kile walichokuagiza.Pia jitahidi ujue ni fashion gani bongo iko sokoni na mpaka mzigo umefika bongo,je bado hiyo fashion ulionunua itakuwa inauza? Mind you kwamba biashara ya nguo hasa za WANAWAKE zinaendeshwa kwa nguvu ya soko na fashion hubadilika mara kwa mara!Biashara ya nguo za watoto au wanaume kidogo fashion zake zinakaa muda mrefu ukilinganisha na za wanawake.

BIASHARA YA VIFAA VYA ELEKTRONIKI
kama simu na accessories zake, music system n.k

Miji mizuri ya kununua mzigo kwa biashara hii ni Shenzhen na Honkong ,japo mji wa Guanzhou pia ni maarufu isipokuwa fake products kwa Guanzhou ni kubwa zaidi. Changamoto kubwa ya biashara hii ni FAKE PRODUCTS. Angalia wateja wako ni watu wa namna gani. Most low income earners ambao kwa Tanzania ndio wengi, wanapenda cheap price.

Kwahiyo, ukinunua genuine products huwezi kuuza bongo kwa sababu bei itakuwa iko juu na wao watashindwa. Kwa hiyo jua needs and wants za customers wako kabla hujaamua kununua mzigo. Kwa mtu mwenye mtaji mdogo unaweza kuanza na kununua phone acssesories na simu chache tu za bei ya chini, utakuwa unaongeza idadi ya simu kidogo kidogo kadri mtaji unavyokua. Pia kama una mtaji mkubwa unaweza kuingiza used products kama photocopier machines ila jitahidi uwe na orders kabla hujaleta kwa sababu ukija nazo nyingi bila order zinaweza kukaa muda mrefu ukajikuta unaanza kula mtaji.

Wakati unasafirisha photocopier machines jitahidi ununue vitu vidogo vidogo kama vile memory cards, USB cards, power banks nk na uviweke pamoja ndani ili ukija bongo wakati unasubiri kuuza photocopier machines unauza hivyo vitu vidogo vidogo ili kupata faida kidogo kidogo na kuhakikisha huli mtaji.

Kumbuka hapa utasafirisha kwa meli na huwa wanapima CBM na sio uzito kwa hiyo hivyo vitu vidogo vidogo cost yake ya kusafirisha itakuwa imemezwa na hizo machines.Photocopier machines nimetoa kama mfano wa moja ya bidhaa lakini vipo vimashine vingi tu ambavyo unaweza kusafirisha kama: Mashine za juice ya miwa, hizi zimekuwa na demand kubwa sana kwa sasa Tanzania. Wateja wake wapo , kama utakuwa na mtaji mzuri unaweza kununua hizi na kuleta. Nyingi ni portable na modern. Ni kiasi cha kutafuta orders na kisha kuleta.

Kuangalia bei mbalimbali za bidhaa tembelea:
Find quality Manufacturers, Suppliers, Exporters, Importers, Buyers, Wholesalers, Products and Trade Leads from our award-winning International Trade Site. Import & Export on alibaba.com

Made-in-China.com mobile- Connecting Buyers with China Manufacturers, Suppliers & Products

www.taobao.com (hii ni ya kichina, tumia browser ya google chrome na tumia kitufe cha translation ili ije kwa kingereza)

USAFIRI NA USHAURI:
Zipo kampuni nyingi zinazosafirisha mizigo kwa njia ya ndege na meli. Kampuni kama GNM, THE LAND, SILENT OCEAN, CHOICE AIR CARGO, MOKHA AGENCY ni baadhi tu na hizi zina ofisi zao pale pale Guanzhou na bei zake zinatofautiana kutegemeana unasafirisha kwa njia gani yaani ndege au meli. Na unapolipia wao ndio huhusika na clearance na kila kitu, wewe ukifika bongo unachukua tu mzigo wako kwenye Ghala lao.

Pia wapo Watanzania ambao hawana kampuni lakini nao wanasafirisha mizigo hasa hasa kwa ndege. Hapa natoa angalizo, hakikisha mtu unayemtumia kusafirisha awe ANAAMINIKA na tafuta watu ambao wamewahi kuhudumiwa na yeye! Vinginevyo Utapigwa na kuingizwa mjini uje hapa kulalamika. Chukia tahadhari! Sio wote ni waaminifu na pia sio wote wakorofi.

Website ya baadhi ya makampuni ni:
Silent Ocean Limited - Specialized in International Cargo Shipping

Kampuni hizi nilizozitaja hapa zinahusika na usafiri lakini pia kama utakuwa na lolote unalotaka kujua kuhusu biashara ya China watafute na uwaulize.

Usafiri wa meli huchukua kati ya siku 25-60 kutegemeana na kampuni. Usafiri wa ndege siku 10-21 itategemea na unapotumia.

Baadhi ya mashirika makubwa ya usafiri shaji mizigo duniani kwa ndege nayo pia yapo China na yanaleta mizigo Tanzania. Sitayataja hapa kwa sababu isijekuonekana naharibu biashara zao . lakini unaponunua mzigo sishauri sana kuyatumia ikiwa utasafirisha kwa ndege kwani gharama zao ziko juu sana. Mpaka unaupata mzigo wako unakuwa hoi bin taaban! Yatakuchaji nauli, na bado yatakuchaji kodi tena ya hali ya juu mpaka upate mafua ghafla[emoji16].

Unaposafirisha kwa ndege hakikisha bidhaa yako haina battery au kimiminika mana makampuni mengi hayataki bidhaa za namna hiyo. Mfano: Usafirishaji wa simu umekuwa na changamoto sana kusafirisha kwa ndege hasa kama ni mzigo mkubwa kutokana na simu kuwa na battery. Bidhaa kama simu hakikisha unatuma kwa meli ili kuepuka usumbufu.

Unaponunua mzigo kwa supplier hakikisha sana anakutumia picha ya mzigo ulivyo kabla hajautuma kwa wasafirishaji. Pia mwambie nje aandike mzigo wako kwa maker pen au abandike karatasi na aweke jina lako, namba yako ya simu, ataje ndani ni bidhaa gani, na aandike pia idadi .Mfano:
Miss Kipilipili
Mobile:+2557XXXXXXX
Product name: Kipilipili Coconut Oil
(Kama ni mashine aandike MODEL number)
100pcs.
Kisha abandike maelezo hayo juu ya package yako. Hii itasaidia sana wakati wa clearance na pia ikitokea mzigo umepotea au umekuwa misplaced ni rahisi kufanya tracking.

KUFUNGA MZIGO: Kama umeenda China mwenyewe, hakikisha unakuwepo wakati wa kufunga mzigo. Usichague bidhaa, kisha wakakwambia njoo kesho tutakuwa tumeshaufunga au tutakuwa tumeshapeleka kwa shipping agent wako! Hakikisha umeona nini kipo ndani kabla hawajafunga. Na kama mzigo wamepeleka kwa agent wako basi mwambie agent aukague wakati wa kuupokea na hakikisha supplier wako anajua kuwa mzigo ukifika kwa agent utakaguliwa. hii itasaidia usipigwe! Wapo Suppliers sio waaminifu


NAULI: Nauli zinategemea season na pia unataka kusafiri lini. Kipindi cha high season kama, July, August bei zinakuwa juu. Kama kwa mfano unatarajia kusafiri July basi ikifika april kata tiketi mapema . Mara nyingi kunakuwa na offer kwenye mashirika ya ndege kwa hiyo pendelea kutembelea website zao.

Pia nauli inategemea na shirika la ndege unalotaka kusafiria na pia daraja unalotaka kukaa.

Kwa wafanyabiashara wengi hutumia ethiopian airline kwa sababu huwa wanatoa kg nyingi kuliko wengine.

Pita kwa mawakala posta na kariakoo au search google kupata bei mbalimbali za nauli. Unaweza kutenga bajeti ya USD 900-1200 Kwa nauli kwa economy class
Angalia bei za NAULI hapa:
International Flights, Airfares, Tickets - Fly Ethiopian
Qatar Airways
KLM Royal Dutch Airlines – Flights | Vliegtickets | Flüge

MALAZI: Hapa nitazungumzia mji wa Guanzhou ambao ndio wenye wafanyabiashara wengi wa mataifa mbalimbali hasa Afrika. Zipo hoteli za hadhi tofauti, bei kutoka 120 yuan(36,000 Tsh) ikiwa ni bei ya chini labisa na kuendelea kutegemeana na mfuko wako. Maeneo kama "shaobei lu" ni maarufu kwa watu weusi na utakisikia kiswahili kila baada ya hatua kadhaa. Hoteli za pembeni ya mji bei huweza kuwa chini mpaka yuan 100.

Angalia range ya bei za hoteli hapa: GuangZhou hotels: cheap rates in GuangZhou by China Hotels Reservation


CHAKULA: Zipo hoteli nyingi Guanzhou na shenzen zinazomilikiwa na foreigners na wanauza chakula kizuri japo kiko ghali kidogo, ila kama unahitaji chakula cha bei ya chini na ambacho ni HALAL (wengi huhofia kulishwa mbwa,kitimoto,nk) unaweza kula kwenye sehemu nyingi ambazo huuza wachina waislamu wenye asili ya Xinjiang ambao huuza HALAL food kwa bei poa kuanzia Yuan 15(4500 Tsh) na kuendelea kutegemea na aina ya chakula ulichoagiza. Kuwa makini na vyakula mana wale wenzetu huwa wanakula vyakula vingi vya "ajabu ajabu".

LUGHA: Wachina hutumia lugha yao kwa kila kitu. Katika miji ya biashara kama Guangzhou wachina wafanyabiashara huongea kingereza cha mawasiliano(kibovu) ila mnawasiliana na kuelewana. Pia lugha ya ishara inatumika pale panapokuwa na language barrier.

Hata kama hujui kabisa kingereza unaweza kuchagua bidhaa na kisha mkapatana bei. Wenzetu wana utaratibu wa kutumia calculator kukuandikia bei, hivyo na wewe utaandika ya kwako mpaka mtafikia makubaliano. Nashauri download application yoyote ya TRANSLATION kama pleco nk ili ikusaidie kwenye mawasiliano unapokwama andika neno unslohitaji kwa kingereza kisha tafsiri kwa kichina na muoneshe mchina hilo neno, itasaidia kurahisisha mawasiliano

Nimegusa juu juu vitu vichache mno kuchokoza mada ili wengine waongezee uzoefu na iwe msaada kwa kila anaetaka kufanya biashara China.

Karibuni tujadili na kusaidia wengine






NB: Naomba nisifuatwe PM, Mwenye shida au maswali aulize hapa hapa ntajibu kwa faida ya wote.
Gachuma jr,
Huu hapa sasa.
 
Mkuu Kipilipili,

Nikushukuru kwa maelezo na majibu mazuri ktk thread hii. Nimesoma pages nyingi tu za uzi huu lakini naomba nikuulize maswali yafutatyo hata kama kuna sehemu (nyuma) mmezungumzia ila mimi sijaona:

1. Container dogo ili lijae linahitaji mzigo mkubwa kiasi gani na gharaza za container kutoka China mpaka Dsm ni kiasi gani kwa makadirio?
2. Kwa uzoefu wako,ni mji gani una supply stationery goods (& its accessories)+ ream papers karibia za aina zote na zinapatikana hapo kwa pamoja ikiwa ni pamoja na computer accessories, photocopiers. + wino mbali mbali (brand and used)
3. Kwa bidhaa za stationeries tajwa hapo juu nikiandaa mil.20 (ya mzigo tu) china nitapata mzigo wa kuniwezesha kuja kuuza kama supplier/wholesaler (quantity) au ni mzigo unaofaa kuuweka dukani na kuuza kama Retailer? Nataka kufahamu ni mtaji kiasi gani unaweza ukawa mzuri kufanyia biashara ya aina hii kama wholesaler (niuze kwa bei ya jumla) aua kama retailer (kununua mzigo kwa ajili ya kuuza rejareja tu)
4. Kwa uzoefu wako, ni nchi gani nje na china ambazo zina produce products tajwa hapo (with quality) juu kwa friendly price? which country between them ni nzuri kwa wajasiliamali wa kitanzania?

Mwisho, nikuombe uniPM contacts zako kama hutojali.
Thank you in advance.
1. A) Kontena dogo ni takriban 68CBM. Hivyo ili ulijaze linahitaji CBM hizo. mfano: kwa bidhaa ya ‘rimu’ za karatsi za A4, wanafungasha rim 5 katika kila boksi 1. kwenye kontena la 20FT huwa zinaingia boksi 1,680 . Ama kama mzigo wako ni mchanganyiko yaani karatatasi na bidhaa nyinginezo kama computer nk basi zingatia tu idadi ya CBM.
B). Gharama za kontena kwa makadirio:
Hapa kuna mambo mawili; MOS, ama upeleke mzigo wako kwenye shipping company ambayo inafanya kila kitu na utapokea mzigo wako kwenye ghala lao DSM. Yaani ukishawapa mzigo China, basi wewe huhangaiki na lolote unasubiri tu mzigo wako ofisini kwao Dsm. Gharama za hii hutofautiana kutoka kampuni hadi kampuni, na pia kutoka bidhaa moja hadi bidhaa nyingine. Yaani hakuna bei jumuishi (flat rate) kwa bidhaa zote, kila bidhaa huwa na gharama yake. mfano anaeleta kontena la milango kodi yake na gharama nyingine zitakuwa tofauti na anaeingiza kontena la viatu au vifaa vya kilimo.
PILI, ‘supplier’ akusafirishie mzigo hadi bandarini Dsm na kisha wewe ufanye mwenyewe ‘clearance’.
Njia zote mbili zina faida na hasara. Njia ya kwanza faida yake ni kuwa unaepukana na usumbufu wa clearance na pia unakuwa umeshajua gharama kamili ya kusafirisha mzigo na kukitokea chochote ama gharama bandarini kupanda au vipi , wewe unakuwa huhusiki na lolote. Hivyo huwi na presha! Hasara ya njia ya kwanza ni kwamba wakati mwingine (si mara zote) gharama unayolipa inaweza ikawa kubwa kuliko kama ungefanya clearance mwenyewe. Gharama hapa najumlisha pia na gharama za usumbufu!
Ama njia ya pili, uzuri wake ni kuwa unaweza kuokoa pesa kwa gharama kuwa nafuu ukilinganisha na njia ya kwanza.
Hasara ya njia hii ni kuwa risk zote za mzigo huwa unazibeba wewe, na wakati mwingine kuna ibuka gharama nje ya mahesabu uliyopiga kabla na ndio hapo unaposikia watu wameacha mizigo yao mpaka inapigwa ‘sadakalau[emoji16]’. Pia jiandae na usumbufu na pia uwe tayari na ’KUFUNIKA KOMBE...’ (nadhani umenielewa, kama hukuelewa rudi darasani kwa mwl wako wa kiswahili[emoji16])
Ushauri wangu: Sitatoa gharama za makadirio hapa, mwanzo wa uzi niliweka mawasiliano ya makampuni, wasiliana nao ujue bei zao za sasa zikoje na ufanye ulinganifu. Pia tafuta supplier kama watatu alibaba wakupe quotations, halafu hizo quotations tafuta clearing agents bongo wakupe makadirio ya kusafirisha na kodi ikiwa utasafirisha mwenyewe. kisha fanya ulinganifu wa njia ya kwanza na ya pili.
2. Mji: Guangzhou utapata vyote ila kama unataka bidhaa nzuri nenda Yiwu.
3. Mara nyingi huwa nakwepa sana kujibu kuhusu MTAJI. Nahofia kumkatisha mtu tamaa au kumpa matumaini makubwa. 20M ni kubwa na pia ni ndogo! Itategemea wewe mwenyewe! Mfano wewe umetaja vifaa tofauti vya stationaries kama unataka ununue vyote hivyo kwa 20M basi ni ndogo na utauza rejareja tu TZ na China hutapata bei nzuri kwa sababu utakua unanunua kidogo kidogo. Lakini, kama 20M ni ya bidhaa AINA moja tu basi huwenda ukapata bei ya jumla China na ukauza jumla TZ. mfano kama utanunua rim moja china kwa dola 1, maana yake kontena dogo itakuwa lina rim 1680 X 5=8400, hivyo utalipa $8400 (sawa tsh 19,320,000) hii ni kwa bidhaa moja tu na ni EXW price yaani bei ya kiwandani tu, haujautoa mzigo hata nje ya geti la kiwanda. Pata picha sasa unataka ununue wino, computer nk.
ZINGATIA: Watanzania tumezoea ukinunua pc 2 au 3 za bidhaa tunataka tupewe bei ya jumla. China ni tofauti. Kila kiwanda huwa na Minimum Oder Quantity (MOQ), usipoifikisha hupewi bei ya jumla. Mfano wakikwambia MOQ ni rim 2000 basi hata ukinunua 1000 watakupa bei ya rejateja, wakati kwa TZ mteja hapo ni bonge la wholesaler[emoji16]!
Hivyo suala la mtaji kiasi gani, siwezi sema, itategemea wewe unataka nini na ni kwa kiwango gani! hata milioni 1 ni mtaji pia, inategemea tu na scale of business unayotaka kufanya.
4. Kuhusu nchi mbali na China, sina ufahamu wa kutosha, japokuwa Wahindi nao wamekuwa na bidhaa nzuri katika baadhi ya bidhaa.
ZINGATIA: Wengi wanataka bidhaa BORA halafu ziwe ‘friendly price’. HILI HALIWEZEKANI.
Kuna mitazamo potofu kuhusu bidhaa za china kuwa ni FAKE au za ubora wa chini. China ina bidhaa zote BORA SANA na MBAYA SANA, akili yako ukiiweka kwenye BEI TU basi utaangukia kwenye bidhaa MBAYA SANA, ukibadili vigezo vyako vya ununuzi na kuiweka akili yako kwenye UBORA wa bidhaa basi utapata bidhaa nzuri japo BEI inakuwa imechangamka kidogo.
Wafanyabiashara wengi wanataka wanunue vya bei rahisi ili waje TZ wauze bei pendwa (rahisi) bila kujua wanaharibu brand zao na watauza mwanzoni tu ila baadae wateja huambiana kuwa kwa fulani vitu vyake hovyo tu na hutawaona tena.
Za kuambiwa changanya na zako mkuu (naamini umenielewa)! Wakati mwingine kujipambanua kitofauti kibiashara ni bora kuliko kufuata mkumbo! Jifunze kupitie kampuni ya APPLE hawana presha! bidhaa yao iko ghali na wakitoa tolea jipya watu wanakesha usiku kucha kwenye foleni ili wawe wakwanza kununua! Linganisha na wale wanaouza simu ina kila kitu mpyaaaa kwa elfu 70 tu! [emoji16]
Mchina kasoma wateja na amefanya makert segmentation! Mfuko wako ndio utaamua ujiweke kwenye tapo lipo la soko ama mzingatia bei au ubora! vyote anakupa, chaguo ni lako! Nawe wasome wateja wako!
Nakutakia mafanikio mema. Pole kwa gazeti na some spelling errors muda wa kuedit sina.
IMG_20181016_084918.jpeg
 
Mkuu, je bidhaa kufuata China au kununua ktk tovuti kama Alibaba.com ipi gharama ni nafuu?
Siwezi kutoa jibu la moja kwa moja hapa mana swali lipo ‘too general’. mfano: kuna vitu vya kujiuliza kwanza kama AINA ya bidhaa, kuna aina za bidhaa unaweza kuja China mwanzoni tu na ukishaweka mambo sawa na supplier na mtu wa kukagua mzigo wako kabla haujatumwa TZ basi huwi na haja tena ya kuingia gharama za kusafiri kila mara, Au pia ukipata supplier muaminifu unaweza ukawa unanunua mtandaoni tu na huwi na haja ya kusafiri.
KIWANGO cha bidhaa. Kama kiwango cha bidhaa ni kidogo hakuna haja yakusafiri, ni bora ununue tu mtandaoni
Njia nyingine ya manunuzi ni kupitia kampuni za kitanzania zinazofanya huduma ya sourcing kutoka China. Kampuni/watu binafsi waliopo China na wana maduka/ofisi TZ unaweza kuwatumia wakakununulia na kukuletea hadi ulipo Tanzania ama kwa kukupa bei ya kiwandani kisha unawalipa service fee ya kukuhudumia na mzigo ukifika TZ unautoa mwenyewe bandarini au uwanja wa ndege AU wakununulie na kukusafirishia kila kitu na wao kuweka faida yao kidogo. Cha msingi angalia njia ipi ina nafuu kwako! Ila hakuna jibu la moja kwa moja kwamba ukinununua alibaba ni rahisi kuliko ukija china (au kinyume chake). itategemea Aina ya bidhaa, kwango cha bidhaa, njia unayotaka kusafirisha bidhaa, ukubwa wa bidhaa yenyewe , kundi la bidhaa katika malipo ya kodi (inalipiwa kodi au ina msamaha wa kodi), nani atakaehusika kusafirisha mzigo nk, haya ni mambo ya msingi kuyajua na ndio ukiyafanyia uchambuzi utabaini njia gani ni nafuu ama kununua mtandaoni au kuja mwenyewe china.

Zingatio: watanzania baadhi wanaweza wasimwamini mtanzania mwenzao aliepo china na ana kampuni TZ iliyosajiliwa halali na ana physical address Tanzania LAKINI wakamwamini mchina waliemuona alibaba tu akawatumia quotation nje ya alibaba, wakalipana nje ya alibaba, halafu mambo yakiwa hayakwenda sawa wanarudi sasa kwa watanzania waliopo china ili wasaidiwe kuwatafuta hao supplier wakichina kusolve tatizo. Yote hii wanaoana wakiwatumia wachina wanakwepa gharama!
Nashauri sana tena sana TUJIFUNZE biashara hizi za online kwanza kabla ya kuamua kuzifanya.
Pia kama zipo kampuni za kitanzania zinazosource kutokea china moja kwa moja na zenye physical address Tanzania basi ni bora kuzifanyia utafiti, na ukijiridhisha ingia nao mikataba ya kisheria na agiza kupitia wao ikiwa huna uwezo wa wewe mwenyewe kuja china.
Cases za mitandaoni zimekuwa nyingi!
 
huu uzi ni mzuri sana na nimejifunza kitu kikubwa ikiwa tunaweza kufanya export nje itakuwa tija maradufu hasa tukisafirisha bidhaa zilizo kamilika au kusafirisha bidhaa ambazo tumeziongezea thamani,mkuu keep it going
 
huu uzi ni mzuri sana na nimejifunza kitu kikubwa ikiwa tunaweza kufanya export nje itakuwa tija maradufu hasa tukisafirisha bidhaa zilizo kamilika au kusafirisha bidhaa ambazo tumeziongezea thamani,mkuu keep it going
mkuu, unachosema ni sahihi. Export watanzania wengi bado tuko nyuma, na mara zote tumekuwa watu wa kulalamika au akionekana mmoja amejaribu basi ataandamwa na ‘nipe michongo basi’, ‘ulifanyaje?’ ‘nipe deal basi’. Cha kushangaza hata ukiwapa watu taarifa hakuna anaekuwa tayari kukomaa nazo na kuzifanyia kazi ipasavyo.
Kingine ni kwamba , wengi wetu tunataka kila mtu atoke kivyake..hakuna anaeamini on joint venture wala patnership. Na ukiona imefanywa patnership basi ni ya ‘kujuana’ na mara nyingi si ya kisheria na mwisho wake watu wanashikana uchawi. udugu na urafiki unakufa.
Ngoja nikupe mfano wa wakenya jinsi walivyojiongeza kwenye export, sisi tupo tu tunabaki kulalamika ohooo sijui sera zetu za export sijui zina nini...blah blah nyiiiingiiii...
Angalia Wakenya ‘walivyojiongeza’!
Tuliowengi tunapenda shortcut! Hatuko tayari kufuata utaratibu wala "compliance". Tukipewa utaratibu tunaona mlolongo ni mreeeeefu na tunaachana nao mapema! Tumeridhika na changamoto za shamba na soko la ndani, hatujawa na utayari wa kutosha kuzikabili changamoto za nje! Wapo wachache tu, ila tuliowengi hatutaki
"kusumbuka".
Ukimtumia mkulima wa TZ file lenye kurasa 30 tu umwambie asome humo kuna fursa ya masoko ya nje, kwanza ANAWEZA HATA ASISOME KABISA! Na akisoma basi atasoma kurasa mbili tatu ataachia hapo hapo!
Halafu na yeye nae atatuma kwenye group jingine aonekane na yeye "wamo"!

Soko la nje linahitaji kufuata vigezo na masharti yake! Sisi hatuko tayari kuendana na vigezo vya wateja wa soko la nje!
Kama wakenya wananunua bidhaa TZ, Wanachokwenda kufanya kwao ni KUONGEZA THAMANI TU ili kuendana na MATAKWA ya soko la nje! Na hapa ndipo wanapotuacha nyuma!. Nitoe mfano wa packaging.
Wakenya wana packaging nzuri MNO! sisi bado hatujawa tayari kubadilika! Tukiletewa package nzuri na zenye ubora hakuna anaenunua! Tunasingizia zinauzwa ghali na kuwalaumu wanaozileta kuwa wanataka kutajirika kwa kuwaumiza wakulima! Tumezoea zile zile "yeboyebo" za bei rahisi za sh 100-250! Lakini Package ndio inayovuta na kulinasa jicho la mteja kabla hata hajajua ubora wa kilichomo ndani!

Nafahamu changamoto za mkulima ni nyingi labda "sera", pembejeo nk lakini hizi ni changamoto karibia Afrika nzima! Ila mkulima mwenyewe akiamua kwa dhati kuwa wa tofauti na kuangazia soko la nje, basi INAWEZEKANA!
Tubadili Attitude zetu! bila ya hivyo
tutaendelea kulalamika kila siku. TUJIONGEZE! Tuache blah blah nyingi, Vitendo ndio viwe vingi kuliko maneno
#MaoniTuSioSheria
 
mkuu, unachosema ni sahihi. Export watanzania wengi bado tuko nyuma, na mara zote tumekuwa watu wa kulalamika au akionekana mmoja amejaribu basi ataandamwa na ‘nipe michongo basi’, ‘ulifanyaje?’ ‘nipe deal basi’. Cha kushangaza hata ukiwapa watu taarifa hakuna anaekuwa tayari kukomaa nazo na kuzifanyia kazi ipasavyo.
Kingine ni kwamba , wengi wetu tunataka kila mtu atoke kivyake..hakuna anaeamini on joint venture wala patnership. Na ukiona imefanywa patnership basi ni ya ‘kujuana’ na mara nyingi si ya kisheria na mwisho wake watu wanashikana uchawi. udugu na urafiki unakufa.
Ngoja nikupe mfano wa wakenya jinsi walivyojiongeza kwenye export, sisi tupo tu tunabaki kulalamika ohooo sijui sera zetu za export sijui zina nini...blah blah nyiiiingiiii...
Angalia Wakenya ‘walivyojiongeza’!
Tuliowengi tunapenda shortcut! Hatuko tayari kufuata utaratibu wala "compliance". Tukipewa utaratibu tunaona mlolongo ni mreeeeefu na tunaachana nao mapema! Tumeridhika na changamoto za shamba na soko la ndani, hatujawa na utayari wa kutosha kuzikabili changamoto za nje! Wapo wachache tu, ila tuliowengi hatutaki
"kusumbuka".
Ukimtumia mkulima wa TZ file lenye kurasa 30 tu umwambie asome humo kuna fursa ya masoko ya nje, kwanza ANAWEZA HATA ASISOME KABISA! Na akisoma basi atasoma kurasa mbili tatu ataachia hapo hapo!
Halafu na yeye nae atatuma kwenye group jingine aonekane na yeye "wamo"!

Soko la nje linahitaji kufuata vigezo na masharti yake! Sisi hatuko tayari kuendana na vigezo vya wateja wa soko la nje!
Kama wakenya wananunua bidhaa TZ, Wanachokwenda kufanya kwao ni KUONGEZA THAMANI TU ili kuendana na MATAKWA ya soko la nje! Na hapa ndipo wanapotuacha nyuma!. Nitoe mfano wa packaging.
Wakenya wana packaging nzuri MNO! sisi bado hatujawa tayari kubadilika! Tukiletewa package nzuri na zenye ubora hakuna anaenunua! Tunasingizia zinauzwa ghali na kuwalaumu wanaozileta kuwa wanataka kutajirika kwa kuwaumiza wakulima! Tumezoea zile zile "yeboyebo" za bei rahisi za sh 100-250! Lakini Package ndio inayovuta na kulinasa jicho la mteja kabla hata hajajua ubora wa kilichomo ndani!

Nafahamu changamoto za mkulima ni nyingi labda "sera", pembejeo nk lakini hizi ni changamoto karibia Afrika nzima! Ila mkulima mwenyewe akiamua kwa dhati kuwa wa tofauti na kuangazia soko la nje, basi INAWEZEKANA!
Tubadili Attitude zetu! bila ya hivyo
tutaendelea kulalamika kila siku. TUJIONGEZE! Tuache blah blah nyingi, Vitendo ndio viwe vingi kuliko maneno
#MaoniTuSioSheria
waswahili hasa vijana husema nakuunga mkono mpaka mguu, kitu kingine ambacho hatamie nilikuja gundua tena kwakujifanyia uchunguzi mwenyewe ni ile kudhamiria toka moyoni, hilo ni swala linalotusumbua pia mtu anaweza kuona maandiko ka ulivyoandika na kufuatilia maandiko ya wengine walochangia na kutamani sana ila akitoka hapo kwa muda anasahau na hakumbuki tena ka alisema atafanya. inakuwuwa kama habari ya mpanzi na mbegu zilizo mwagika sehemu mbalimbali. kikubwa nadhani tunakila namna yakudhamiria na kuangalia soko la utoaji wa bidhaa nje ila zilizoongezewa thamani ule ujinga wakuuza ngozi elfu 20/= then tunakuja nunua kiatu 200 000/= twapaswa kuacha sasa
 
Mkuu ukitaka kwenda china Nauli tsh. Ngapi now go and return,,na utaratibu wao upoje wa kupata visa Kipilipili Na wajuvi wengine wanaojielewa,,,nna mil 20 nataka nijilipue kufuata bidhaa
 
Mkuu Kipilipili, naweza kupata plastic pollen traps baada ya muda gani kutoka kwa jamaa zako? Naomba namba yako ya simu tafadhali.
 
Check your inbox, halafu ukiwa hapa jf uwe unatumia neno MKUU ndio title mujarab, mana jinsia za watu humu ni kitendawili
Hahaha Mi Nilivyomaliza tu kusoma nikaitambua jinsia yako ...Sema sio muhimu ....Shukran Sana kwa Taarifa iliyoshiba like hii uliyetuzawadia ...
 
Asante mkuu. Ameen
Habar yako kaka, samahan kwa usumbufu mm ni msichana naitwa Sabrina,Naishi tz ila juz kat nimepata fursa ya biashara China, yan kuchukua madera tz kupeleka China kuuza ,shida yangu ni moja jinsi ya kupeleka mzigo China na changamoto zake zipoje,na je ktk pita pita zako ushawai ona biashara ya madera huko China ,na wanauza kwa yuan ngapi?
 
Mkuu, in most cases hawa jamaa wanahitaji MALI GHAFI kama vile MBAO zenye ubora ili kutengenezea samani mbalimbali. Pia wanahitaji sea products kama samaki wa aina mbalimbali kwa ajili ya kusindika.
Bidhaa nyingine ambazo watanzania tunaweza kuuza kwao ni kahawa, matunda hasa maembe! Juice ya maembe iko ghali sana China na nadhani ni kwa sababu wao hawalimi.
Nyama ya NG'OMBE hasa wanaotoka huku kwetu ni WATAMU ukilinganisha na nyama inayouzwa China ambayo haitoshelezi soko. . Ikumbukwe kuwa kuku na kitimoto ndio nyama rahisi inayoliwa na wachima[/QUO
Habar yako mkuu naomba kuuliza et biashara ya madera huko China Ipo VIP,maana kuna mtu Ameniambia madera China yanavalika sana na hakuna zaid yanatoka,bongo je ww unaiyonaje hii biashara naitwa Sabrina
 
Back
Top Bottom