China itapata wakati mgumu sana kwa Taiwan kuliko Russia kwa Ukraine

China itapata wakati mgumu sana kwa Taiwan kuliko Russia kwa Ukraine

Kama marekani kaufyata, namuunga mkono katika hili,ashughulike na urusi kwanza,kujiunga katika vita pande mbili kwa wakati mmoja ingemuhathiri sana,
 
IMG_4666.jpg


Huku na kule.
 
Hakuna mtu mwenye akili timamu anaeweza kuamini ku Mmarekani anaweza kuingia vita na China kwa sababu ya Taiwan.
 
Brilliant!! Mkuu thanks a lot kwa hoja yako yenye mshiko - kinacho nishangaza mimi ni watu kushindwa au kupuuzia kuangalia ramani wakatafakari umbali wa kutoka mashariki au magharibi ya pwani ya Merikani kuja kwenye bahari ya Uchina kuna umbali gani? Tukiwekea maanani kwamba Uchina ya sasa sio ya mwaka 47 Wachina siku hizi wamejizatiti sana katika masuala ya Navy, hasa hasa their formidable anti ship missiles especially: air craft carrier killer missiles type DF-36 zenye uwezo mkubwa wa kuzamisha aircraft carriers hata zikiwa in mid Pacific or Atlantic oceans, hapo hatujazungumzia MACH 15/20 Hypersonic Missiles ambazo US na UK hawana kinga dhidi ya makombora hayo hatari yenye uwezo vile vile wa kuzamisha aina zote za meli za kivita-sasa swali hapa ni: hivi US/UK watapitisha wapi meli za kuwezesha kuiwekekea blockade Uchina kwenye eneo la Taiwan Strait au strait of Malacca-kwa maneno mengine meli za NATO specifically US zitapitia wapi kabla hazijazamishwa na Uchina wakati teknolojia ya siku hizi ni rahisi kuiwezesha Uchina ku-track nyenendo za Meli za kijeshi za USA in real time kwa kutumia satellites za aidha Uchina au Urusi au Iran au zote kwa pamoja zikawezesha missiles ku-zero on US/UK Naval ships na kuzizamiswa katikati ya Bahari za Pacific au Atlantic kabla hazijafika Uchina.

Haya tuje kwenye suala la idadi ya Military bases ambazo Merikani anamiliki mashariki ya mbali, binafsi naona hiyo si hoja ya kuzitia wasi wasi Uchina au Urusi kambi hizo zote zinaweza kushambuliwa na kuchakazwa vibaya kwa makombora hatari ya Kichina na Urusi hata Korea ya Kasikazini uwezo huo wanao sana,na kusema kweli ukichunguza kwa umakini military bases hizo za kimerikani wala hazina military assets/materiel nyingi kivile na idadi ya wanajeshi wanao ishi kwenye makambi hayo niya kawaida kabisa, hivyo maadui wake ni rahisi kuzi-contain bases hizo in no time.

Ebu sasa tuangalie mfano mmoja kuhusu umakini pamoja na Ulinzi in general wa Military bases za Wamerikani around the World: kama nakumbuka vizuri miaka miwili/mitatu iliyo pita kambi mbili za jeshi la Merikani zilishambuliwa na roketi za Wairan, zikaharibu majengo kadhaa ya kambi na kutifua runways za ndege - wanajeshi kadhaa wa Merikani walipata madhara licha ya kujichimbia/jificha kwenye mahandaki yaliyo imarishwa kwa zege, walipo tonywa mapema kwamba Iran hiko mbioni kushambulia military bases mbili za jeshi la Merikani, hilo alikusaidia kitu ndio maana wanajeshi wengi ilibidi wakimbizwe Kuwait, Ujerumani na Merikani kupewa matibabu,kutokana na kupata madhara ya ubongo kutikiswa na shockwave ya mlipuko, binafsi huwa najiuliza: hivi kama Iran ingerusha roketi zilizo sheheni thermobaric payloads si wanajeshi wote wangekufa kutokana kukosa hewa na mapafu kuwa punctured, kwa bahati nzuri kutokana na UTU Iran hakufanya ukatiri wa kurusha roketi zenye madhara mkubwa kwa binadamu wenzake, badala yake Wairan walirusha roketi zilizo sheheni conventional high explosives tu na sio fuel air bombs/termobaric bombs

Tukirudi kuzungumzia uwezo wa Wachina ku-track movement za meli za Vita na submarine za USA in real time kwa kutumia satellite na sonars, wala hilo halishangazi hata kidogo maana siku hizi nyaja ya sayansi na teknolojia ime-grow sana na haihodhiwi na Taifa moja tu, hilo likumbukeni sana - ukweli ni kwamba linapo kuja suala la silaha - Uchina na Urusi zimekwisha ipiku USA kwenye silaha za kisasa kabisa, mfano: Hypersonic missiles and glide Vehicles, Submarine Drones, Supercavitation torpedoes za kuzamisha meli na submarine at high speed huku ikiwa imezama ndani ya Bahari.
Wewe mchambuzi kutoka (Yombo Vituka Institute for International and Strategic Studies) kitu ambacho hujui ni kwamba hizo silaha unazozitaja ni silaha ndogo sana kwa taifa kama Marekani.

Mataifa kama Russia na China yana tabia ya kuonyesha silaha zao kwenye sherehe zao za kitaifa kitu ambacho hakipo kwa nchi za magharibi, kwa hivyo huwezi kujua silaha zao.

Na kama unafikiri ni mchezo basi Russia ijaribu kuishambulia nchi yoyote ya Nato ndio utaona silaha ambazo hata huzijui japo nashangaa unasema hawana silaha hizo ulizozitaja lkn zote zina majina ya kiingereza na wala hujazitaja kwa kichina wala kirusi..!!
 
Ubaya wa mambo kwa china ni kwamba technologia yao yote asili yake ni Marekani ndio ujinga mkubwa wa hawa China walioufanya miaka nenda miaka rudi,

Mchina amekuwa akipewa watalaamu kutoka US na mambo mingi ya technologia wataalam wametoka US
 
Yes. Lakini jua pia, ikitokea vita, China ataweza tengeneza silaha nyingi zaidi na kwa muda mfupi na gharama ndogo kuliko US.

Ukiangalia man power ya China, na aina yao ya uongozi, wanaweza badilisha viwanda vingi na watu wengi kutengeza silaha na kujiunga na Jeshi.

Nadhani wateweza gonga copy mpaka za HIMARS za US [emoji12]. Tena kwa idadi kubwa na haraka zaidi.

Ndiyo maana nasema hela yangu na weka kwa mchina.
Ha ha ha ha ha ha ha ha eti wakatoa copy nyingi zaidi hata za HIMARS. Moja ya kitu ambacho China amekosa pia ni experience ya modern warfare.
 
Nipo nyuma yako bro [emoji41][emoji41][emoji41]

Ukizingatia us amechoka mbinu zake nyingi wadau wameshazishtukia na ndio maana maeneo mengi tu wadau wanamdindia anaishia kuweka vikwazo.

Kipind ipo kwenye ubora alikua anatoa maelezo machache eidha uunge mkono au uwe mpinzan lkn sasa hv hana ubavu wa kutoa kaul za kibabe hivyo
 
China kwanza wamechelewa sana kuivamia Taiwan ,wamezembea hadi US kajenga base yake pale,US ana marine combat's zaid ya 20,000 ,ndege za kivita zaid ya 200 ,manowari ,pia ana base nyingine kisiwa cha japani ambacho ni karibu sana na Taiwan ,yani kiufupi Taiwani wamejiweka sawa.

Changamoto nyingine ni kwamba kisiwa hicho kipo umbali wa km 175 kutoka China, hivyo China akitaka kukivamia itabidi awe na meli kubwa zenye uwezo wa kubeba vifaa na zana za vita ,na hiz meli zitakua zinatembea taratibu hii itakua rahisi kushambuliwa na morden ant-ship messile ,pia Taiwan wameshatega mabomu ya kwenye maji kuzunguka kisiwa kizima ,mabomu haya yaliyotengenezewa UK yana uwezo wa kuharibu hadi submarine za kisasa.

Changamoto nyingine kuna kakisiwa kadogo ka Taiwan ambacho kiko umbali wa km 70 toka China haka kakisiwa kamejazwa wanajeshi na zana za kivita na ulinzi mkali hivyo kabla China hajafika Taiwan kwenyewe itamgharimu sana hapa.

Changamoto nyingine ni geography ya hichi kisiwa cha Taiwan aisee mji na mji kumetengwa na misitu mikubwa na mabonde mengi hii nayo. changamoto.

Changamoto nyingine ni jinsi ya kufanya uvamizi wa kushtukiza,unjua kwenye vita ukitaka ushindi wa asubuhi kamata anga la mpinzani aisee kwa Taiwan siyo rahisi maana anga lake linaendeshwa kisasa ,sawa na anga la France au German ,siyo choka mbaya Ukraine wasio na hata rada za maana

Lingine ni kuwa hichi kisiwa sio choka mbaya kama Ukraine wao wamenunua ndege za kisasa,technology zilizoenda shule ,ni wataalamu wa udukuz,wakisaidiwa na japani na US.

Changamoto ya mwisho ni kwamba kisiwa hichi kimeingia makubaliano na US ya kulindana hivyo hapa US anaingia direct, siyo kule kwa zelesky anatumiwa kifaa kimojakimoja tena kwa tabu.

Sitegemei kama China wataivamia Taiwan ,itaishia kupiga mikwara tuu.

Mama anatinga huko next week ngoja tuone ,yajayo yanafurahisha
China bado yaihesabia Taiwan kuwa ni moja ya majimbo yake na yaweza kuivamia siku moja ili kutimilisha hiyo kauli yao.

Pia China hawajachelewa yaweza kuichukua Taiwan kwa bila kutumia nguvu ya kijeshi kwa kushindilia ushirikiano wa kuchumi kama ambavyo imefanya majuzi pale Xi alipotembelea kisiwa cha Hong Kong tena kwa njia ya reli.

Lakini pia China yaweza kuivamia Taiwan wakati wowote ikitaka na marekani isifanye lolote kwa kuzingatia kuwa hivi karibu ndege za kivita za China zimekua zikifaya doria la anga zima la eneo hilo bila shida.

Na kama ikitokea China kuvamia Taiwan basi kisiwa hicho hakitakuwa na uwezo wa kujilinda na jeshi lake litamezwa mara moja. China ni nchi pekee duniani ukiondoa marekani ambayo ina matumizi makubwa ya fedha kwenye jeshi na ikitokea yaivamia Taiwan basi utashuhudia China ikitumia nguvu zake kwenye jeshi la maji, anga, ardhini, makombora ya kisasa, ndege za kisasa za kivita (ambazo hizijawahi kutumika) na pia mashambulizi ya mitandao au "Cyber-attacks".

Hata hivyo, bado Taiwan na jeshi lake la watu 80,000 kulinganisha na China yenye jeshi la watu zaidi ya milioni mbili, wanaweza kupunguza makali ya mashambulizi kwa kiasi fulani kwa kuzuia askari wa miamvuli na wanamaji (amphibious forces) na kuanzisha mashambulizi kama yale ya Vietnam yaani kulala kikambare na kushambulia kwa kustukiza huku wakingojea msaada wa kijeshi kutoka nje kwa Marekani na washirika wake hususan Korea Kusini na Japan.

Taiwan yapokea silaha nyingi inouziwa na Marekani hivyo inaweza kuwa na akiba ya kutosha kwa kujihami pale mwanzo wa vita.

Lakini bila shaka kama kawaida ya wamarekani kwenye masuala ya diplomasia na sera ya nje yaani "foreign policy", bado yaitambua sera ya China isemayo "One- China policy" yaani Marekani kuitambua China na serikali yake moja tu yenye makao makuu Beijing na ina ushirikiano nayo China na sio Taiwan.

Ndio kusema kuwamba Marekani imekuwa ikitoa kauli tata za kindumilakuwili kuhusu kuingia vitani kuisadia Taiwan endapo itavamiwa na China lakini hapohapo washauri wa serikali wakisema hilo halitakuwa jambo sahihi.

Hata hiyo ziara ya huyo bibi mchokozi Nancy Pelosi ambayo anaanzia Singapore na kuishia Japan sidhani kama atathubutu kutua Taipei kwani wachina wameishasema Marekani isicheze na moto.

Mwisho nikuulize hivi wadhani hayo yote ulosema ya Taiwan kujiandaa hayajaonwa na satellite za mchina?
 
Ubaya wa mambo kwa china ni kwamba technologia yao yote asili yake ni Marekani ndio ujinga mkubwa wa hawa China walioufanya miaka nenda miaka rudi,

Mchina amekuwa akipewa watalaamu kutoka US na mambo mingi ya technologia wataalam wametoka US
Kifupi ni kwamba, ANACOPY TEKNOLOJIA KUTOKA MAGHARIBI.
 
Wewe mchambuzi kutoka (Yombo Vituka Institute for Strategic Studies) kitu ambacho hujui ni kwamba hizo silaha unazozitaja ni silaha ndogo sana kwa taifa kama Marekani.

Mataifa kama Russia na China yana tabia ya kuonyesha silaha zao kwenye sherehe zao za kitaifa kitu ambacho hakipo kwa nchi za magharibi, kwa hivyo huwezi kujua silaha zao.

Na kama unafikiri ni mchezo basi Russia ijaribu kuishambulia nchi yoyote ya Nato ndio utaona silaha ambazo hata huzijui japo nashangaa unasema hawana silaha hizo ulizozitaja lkn zote zina majina ya kiingereza na wala hujazitaja kwa kichina wala kirusi..!!
Kwanini nchi za NATO zisiishambulie RUSSIA ambayo inaonesha silaha zake hovyo hovyo
Imeivamia UKRAINE imeingia SYRIA iliingilia VENEZUELA
Imefanya majeshi ya FRANCE yasepeshwe kule MALI
taifa pekee lakuivamia RUSSIA ni RUSSIA yenyewe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe mchambuzi kutoka (Yombo Vituka Institute for International and Strategic Studies) kitu ambacho hujui ni kwamba hizo silaha unazozitaja ni silaha ndogo sana kwa taifa kama Marekani.

Mataifa kama Russia na China yana tabia ya kuonyesha silaha zao kwenye sherehe zao za kitaifa kitu ambacho hakipo kwa nchi za magharibi, kwa hivyo huwezi kujua silaha zao.

Na kama unafikiri ni mchezo basi Russia ijaribu kuishambulia nchi yoyote ya Nato ndio utaona silaha ambazo hata huzijui japo nashangaa unasema hawana silaha hizo ulizozitaja lkn zote zina majina ya kiingereza na wala hujazitaja kwa kichina wala kirusi..!!

Kwanini nyie msianze pale Moscow? Russia anaingia nchi yoyote ya NATO na hakuna kitu wanafanya. Mbona lithuania mmeachia??[emoji23][emoji23]
 
Wewe mchambuzi kutoka (Yombo Vituka Institute for International and Strategic Studies) kitu ambacho hujui ni kwamba hizo silaha unazozitaja ni silaha ndogo sana kwa taifa kama Marekani.

Mataifa kama Russia na China yana tabia ya kuonyesha silaha zao kwenye sherehe zao za kitaifa kitu ambacho hakipo kwa nchi za magharibi, kwa hivyo huwezi kujua silaha zao.

Na kama unafikiri ni mchezo basi Russia ijaribu kuishambulia nchi yoyote ya Nato ndio utaona silaha ambazo hata huzijui japo nashangaa unasema hawana silaha hizo ulizozitaja lkn zote zina majina ya kiingereza na wala hujazitaja kwa kichina wala kirusi..!!
Kiazi nyingine hii unaisi vita inapiganwa Kwa mihemko nchi yoyote itakayoatarusha usalama WA Rusia itapigwa Tu alafu labda nikwambie Tu ule muungano WA NATO ni kwaajili ya nchi NNE Tu Marekani, France, uingereza na kidogo Germany awoo wengine ni kama chambo usitegemee vita vikizuka Marekani ataaribu uchumi wake Kwa kuipigania Poland au Latvia au Lithuania iloo sahau watatoa silaha Tu Ila kwenda front sahau
 
Kiazi nyingine hii unaisi vita inapiganwa Kwa mihemko nchi yoyote itakayoatarusha usalama WA Rusia itapigwa Tu alafu labda nikwambie Tu ule muungano WA NATO ni kwaajili ya nchi NNE Tu Marekani, France, uingereza na kidogo Germany awoo wengine ni kama chambo usitegemee vita vikizuka Marekani ataaribu uchumi wake Kwa kuipigania Poland au Latvia au Lithuania iloo sahau watatoa silaha Tu Ila kwenda front sahau
DuDuh muuza kahawa mbona hainekani nataka kahawa anichanganyie na tangawizi
 
Back
Top Bottom