China kazi anayo dhidi ya Mmarekani, Biden aweka vikwazo maradufu

Nafikiri hii mifumo ukomunisti na ubepari inahitaji mixture iliweze kuwin vizuri ni kama nyama kwenye sambusa.

Ni ngumu kusema uwe mkomunisti 100% au mbepari 100%
 
Nafikiri ni suala la maslahi tu.

Maana mchina mwenyewe ukomunisti ana ufahamu na ubepari ameuonja so mifumo yote anajua kucheza nayo sijajua sana kuhusu U.S kwenye ukomunisti maana kwenye ubepari ni mabingwa.
 
Ulaya nao ni kama wana mlia timing tu mchina sio punde atapigwa furushi as long as U.S kaanza kuvuta nyuzi tegemea na E.U kuvuta nyuzi licha ya kwamba BYD wapo katika hatua za kufungua kiwanda huko huko Europe.
Kwa Europe ni ngumu kaka.
Maana mwaka huu viongozi wa Ulaya wengi wamemiminika Beijing na wengine wamekubali kujiunga BRI ikiwemo Italy.
Ulaya washakubali mapigo kiufupi.
 
Kwa Europe ni ngumu kaka.
Maana mwaka huu viongozi wa Ulaya wengi wamemiminika Beijing na wengine wamekubali kujiunga BRI ikiwemo Italy.
Ulaya washakubali mapigo kiufupi.
Tuchukulie mfano kwenye EVs unaonaje uhai wa makampuni yao ya magari katika soko la ushindani na makampuni ya China. Je, EU wataacha hivi hivi lipite ?
 
Market size ya marekani ni ndogo sana 300m population, 1 8bn pple china 2bn pple Africa 1bn pple, kwahiyo hilo ni dogo sanaa aliwezi ku affect uchumi wake.
Umeangalia market size tu ,jaribu kuangalia power na influence yake worldwide.
Eti Africa!!! Biashara kubwa za dunia hazioni Africa kama targeted market kwao.
China akipewa option achague Kati ya Brazil na Africa atachagua Brazil.
 
Sasa hivi Wachina wala hawatishwi na protectionism na ban za Marekani hazijawahi kuwashusha kiuchumi

Ni kama Marekani wanajisumbua tu

Wameona chip war wamefeli sasa wamehamia kwenye high tariffs on Chinese industrial goods

Marekani ilipofikia imefeli ku-compete na China na dunia imejionea, sio kwenye tech wala industrial manufacturing

Biden na Trump wanapokezana kiti cha uraisi lakini wote wamekaa kwa mwamba Xi Jinping
 
Ushindani umekuwa mkubwa na marekani ni kama ushindani unamuelemea hivi ukifuatiza toka matokeo ya trade war wakati wa trump masuala ya Huawei na matokeo yake sasa.

Masuala ya Chips na inavyo backfire wao wenyewe U.S na washirika wake Netherlands, Japan na SK nafikiri U.S anapaswa kuja na mbinu mpya za kumkabili mchina.
 
Kazi ipo soko limevamiwa.

Inabidi washushe bei bidhaa zao je, mabepari wa kizungu watakubali hii kweli ?
Hawawezi wakishusha hawatapata faida

China ina advantages nyingi sana inapohusu manufacturing kuanzia upatikanaji wa materials, R&D centres, skilled personnel, supply chain, critical technologies kama industrial robots, artificial intelligence, machine learning, computerized algorithms n.k

Mfano magari ya Tesla 95% ya components zinatengenezwa China. Well Marekani amepiga ban China-made EVs, ila EVs za Tesla kutoka China zinaingia Marekani zikiwa zimetengenezwa kwa vifaa 95% kutoka China sio mbaya kwa uchumi wa China

Ilikuwa Tesla wafungue kiwanda cha
Energy Storage Gigafactory India ila Elon Musk baada ya kupima kaona bora ajenge tena China. Kashapewa eneo lingine Shanghai aanze ujenzi mara moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…