China(PRC) na Taiwan(ROC) bado wapo kwenye civil war

China(PRC) na Taiwan(ROC) bado wapo kwenye civil war

Republic Of China [ ROC ] chini ya chama cha kibepari cha Kuomitang chini ya Sun Yat Sen na baadae Chiang Kai sheki ilikuwa imeoza inanuka rushwa, sera mbovu za umiliki wa ardhi, ufisadi, Uongozi mbovu ndipo Mao Zedong akachukizwa na hiyo hali akaanza kujifunza falsafa za kijamaa kupitia vitabu na magazeti yaliyokuwa yanaandika habari kuhusu nchi ya kijamaa ya Urusi chini ya Lenin ndipo Mao akajikusanya na wenzake Kumi akiwemo Zhuo Enlai na kuanzisha Chama cha kijamaa kwenye boti 1921 ili kuja kuleta ukombozi wa hayo matatizo yanayo sababishwa na chama Cha kibepari cha Kuomitang hasa hasa tatizo la umiliki wa ardhi kwa wakulima . Mao alitembea vijiji kwa vijiji kwa miguu kuwaeleza wachina dhima nzima ya kijamaa ambavyo itaweza kuwasaidia kukomesha matatizo yao chini ya serikali dhalimu ya kibepari ya Kuomitang.wachina waliowengi wakaanza kuamini falasa za kijamaa za Mao[ Maoism] na kuanza kujiunga na chama Cha kikomunisti Cha China [ CPC ] kwa ajili ya kupinga serikali ya Kuomitang . Wachina waliowengi wengi na kwa wingi waliongezeka katika kujiunga na CPC na kuunga juhudi za mapambano huku China ikiwa imepasuka vipande viwili vya kifalsafa ujamaa wale waliokuwa wanaunga juhudi za CPC na wanachama wa CPC na kipande kingine wale waliokuwa wanaunga mkono sera za kibepari za Kuomitang . Mnamo mwaka 1927 wanachama wa CPC wakaanzisha jeshi lao kwa ajili ya ukombozi waliolipachika jina la People's Liberation Army [ PLA ] kwa ajili ya kuitoa madarakani Kuomitang .
Na mwaka huohuo 1927 vikaanza Vita vya wenyewe kwa wenyewe baina ya wachina wanaounga mkono chama cha kikomunisti cha China [ CPC ] na wachina wanaounga mkono chama cha Kuomitang . CPC ikiwa na jeshi la ukombozi wa watu wa China [ PLA ]likipambana na Kuomitang ikiwa na jeshi la China Nationalist Army Vita vikapiganwa kwa awamu ya kwanza mpaka 1937 na 1945 wakati wa Vita vya pili vya dunia wote kwa pamoja waliungana ili kupambana na kumtoa Japan ndani ya maeneo ya China baada ya kumshinda na kumtoa japan china wakati wa Vita vya pili vya dunia . Mnamo mwaka 1947 Vita vya wenyewe kwa wenyewe vikarudi tena na hii ikiwa ni awamu ya pili ya Vita kwa nguvu na kwa umoja jeshi la watu wa China [ PLA ] chini ya wanachama wa CPC na wachina wanaounga mkono sera za kijamaa lilipigana mpaka mwaka 1949 na kuwashinda jeshi la China Nationalist Army chini ya Kuomitang na waka kimbilia Kisiwani na ndipo ikazaliwa Jamhuri ya watu wa China [ PEOPLE'S REPUBLIC OF CHINA ] chini ya chama cha kikomunisti cha China [ CPC ] chini ya mwenyekiti Mao Zedong na Rais wa Jamhuri ya watu wa China.
 
Na mwaka huohuo 1927 vikaanza Vita vya wenyewe kwa wenyewe baina ya wachina wanaounga mkono chama cha kikomunisti cha China [ CPC ] na wachina wanaounga mkono chama cha Kuomitang . CPC ikiwa na jeshi la ukombozi wa watu wa China [ PLA ]likipambana na Kuomitang ikiwa na jeshi la China Nationalist Army Vita vikapiganwa kwa awamu ya kwanza mpaka 1937 na 1945 wakati wa Vita vya pili vya dunia wote kwa pamoja waliungana ili kupambana na kumtoa Japan ndani ya maeneo ya China baada ya kumshinda na kumtoa japan china wakati wa Vita vya pili vya dunia . Mnamo mwaka 1947 Vita vya wenyewe kwa wenyewe vikarudi tena na hii ikiwa ni awamu ya pili ya Vita kwa nguvu na kwa umoja jeshi la watu wa China [ PLA ] chini ya wanachama wa CPC na wachina wanaounga mkono sera za kijamaa lilipigana mpaka mwaka 1949 na kuwashinda jeshi la China Nationalist Army chini ya Kuomitang na waka kimbilia Kisiwani na ndipo ikazaliwa Jamhuri ya watu wa China [ PEOPLE'S REPUBLIC OF CHINA ]
Nakubaliana na wewe, waliokimbia kwa sasa, yaani Taiwan hawadai chochote cha Mainland China,sasa kwa nini China itake kutawala mstakabali wao? Umeshinda umechukua sehemu kubwa, sasa kwa unifuate na kutaka kuchukua changu? Kwangu mimi is not fair.
 
Nakubaliana na wewe, waliokimbia kwa sasa, yaani Taiwan hawadai chochote cha Mainland China,sasa kwa nini China itake kutawala mstakabali wao? Umeshinda umechukua sehemu kubwa, sasa kwa unifuate na kutaka kuchukua changu? Kwangu mimi is not fair.
China wanachotaka ni peacefully Unification na Taiwan kwa kuwa wao PRC ndio walioshinda Vita hivyo ardhi yote ya China wao ndio wenye mamlaka nayo . China hawataki kuwaua wala kuwafukuza ndugu zake kule kisiwani Ila China wanataka Kisiwa chao cha Taiwan kurudi katika himaya yao China Beijing huku wakiendelea kuwaacha Taiwan katika mfumo wao wa kiutawala Kama ilivyo Macau na Hongkong.
 
Nakubaliana na wewe, waliokimbia kwa sasa, yaani Taiwan hawadai chochote cha Mainland China,sasa kwa nini China itake kutawala mstakabali wao? Umeshinda umechukua sehemu kubwa, sasa kwa unifuate na kutaka kuchukua changu? Kwangu mimi is not fair.
Pia unapaswa ufahamu hata Taiwan [ ROC ] nao pia wanaitaka China mainland ndio maana wao kisiwa wanajiita Taiwan na mainland wanaiita west taiwan😀 kwa hiyo wanaamini pia ile ni ardhi yao nao pia wanaitaka ili kurudisha REPUBLIC OF CHINA mpaka Mainland.
 
Pia unapaswa ufahamu hata Taiwan [ ROC ] nao pia wanaitaka China mainland ndio maana wao kisiwa wanajiita Taiwan na mainland wanaiita west taiwan😀 kwa hiyo wanaamini pia ile ni ardhi yao nao pia wanaitaka ili kurudisha REPUBLIC OF CHINA mpaka Mainland.
Sikujua kama ni policy ya Taiwan...
 
Kabla ya vita ya pili ya Dunia, China ilikuwa ikiongozwa chama cha Wakoumitang. Wakiita nchi yao Republic of China. Hawa walikuwa chini ya Kai Shek. Wakoumitang walifanya kazi kubwa sana kuiunganisha China. Wakikomesha wababe wa kivita vurugu zingine. Lakini wakatokea wapinzani wao. Wacommunist chini ya Mao.

Hivyo China ikaingia kwenye civil war. Wakati na karibu na WWII Japan ikaivamia China. Serikali ya wakoumitang ilipigana sana vita dhidi ya wajapan. Huku wacommunist wakiendelea kukua na sometimes wakipgana vita kuzidi kuwadhoofisha wakoumitang. Japo na kwa namna walishiriki kupigana na wajapan.

Baada ya Japan kushindwa vita ya pili ya dunia, wacommunist wa Mao wakaibuka wakiwa na nguvu sana, huku wakoumitang wakiwa hoi kabisa. Basi kwenye muendelezo wa civil war yao, wakoumitang wakashindwa na kukimbilia kisiwa cha Taiwan. Wasomi, matajiri wakakimbia na mali nyingi kwenda Taiwan. Huku nyuma wacommunist wakaunda serikali yao, People republic of China(PRC). Wale waliokimbilia Taiwan wakiendelea kujiita(ROC) na wakidai kuwa wao ndiyo wenye kutawala China yote. Na sehemu ya mpango wao ilikuwa ni kurudi tena kutawala China yote.

Mwanzoni hata UN iliitambuq serikali iliyopo Taiwan kama serikali halali ya China yote. Lakini baadaye wakabadilika, wakiitambua serikali iliyo China bara kama serikali ya China yote.
So huu mgogoro ni muendelezo tu wa vita vya wenyewe kwa wenyewe. Hakuna hero wala villain.
Mkuu me nainawanachelwa tu wachapane ili wajue nani mbabe
 
China wanachotaka ni peacefully Unification na Taiwan kwa kuwa wao PRC ndio walioshinda Vita hivyo ardhi yote ya China wao ndio wenye mamlaka nayo . China hawataki kuwaua wala kuwafukuza ndugu zake kule kisiwani Ila China wanataka Kisiwa chao cha Taiwan kurudi katika himaya yao China Beijing huku wakiendelea kuwaacha Taiwan katika mfumo wao wa kiutawala Kama ilivyo Macau na Hongkong.
Kesi Hongkong naona tofauti, China wanataka hovyo, lakini kushinda vita hakuwapi haki! Ni nguvu ndio iliyotumika.Wachina wanataka hivyo, what is wrong na Wataiwan wakitaka wanavyotaka! Sioni egitimacy ya madai ya China kwa Taiwan, kama ambavyo sitaona madai ya Taiwan kwa Mainland China pia, walichukua path tofauti,kila kundi kina uhuru wa kuamua path yake. Kwangu mimi naona China naye anaamua kuwa beberu.
 
Kesi Hongkong naona tofauti, China wanataka hovyo, lakini kushinda vita hakuwapi haki! Ni nguvu ndio iliyotumika.Wachina wanataka hivyo, what is wrong na Wataiwan wakitaka wanavyotaka! Sioni egitimacy ya madai ya China kwa Taiwan, kama ambavyo sitaona madai ya Taiwan kwa Mainland China pia, walichukua path tofauti,kila kundi kina uhuru wa kuamua path yake. Kwangu mimi naona China naye anaamua kuwa beberu.
Jambo la kwanza tunapaswa kufahamu kuwa China[ PRC ] ndio mshindi wa Vita na ndio mwakilishi wa China UN kwa hiyo ana mamlaka yote ya kudai na kulinda ardhi yake hata angekuwa China [ ROC ] mshindi wa Vita naye angekuwa na mamlaka hayo. Pia tunapaswa kufahamu kuwa kisiwa cha china [ Taiwan ] kilikuwa chini ya koloni la Japan licha ya kuwa Japan alishindwa Vita lakini alikiacha huru Ila hakukirudisha chini ya himaya ya China mainland kwa hiyo China mainland pia inamamlaka ya kurudisha kisiwa chake chini ya himaya yake.
 
Jambo la kwanza tunapaswa kufahamu kuwa China[ PRC ] ndio mshindi wa Vita na ndio mwakilishi wa China UN kwa hiyo ana mamlaka yote ya kudai na kulinda ardhi yake hata angekuwa China [ ROC ] mshindi wa Vita naye angekuwa na mamlaka hayo. Pia tunapaswa kufahamu kuwa kisiwa cha china [ Taiwan ] kilikuwa chini ya koloni la Japan licha ya kuwa Japan alishindwa Vita lakini alikiacha huru Ila hakukirudisha chini ya himaya ya China mainland kwa hiyo China mainland pia inamamlaka ya kurudisha kisiwa chake chini ya himaya yake.
Hivi unaona UN ilikuwa right? Mara ngapi UN imetoa maamuzi sio sahihi! Uamuzi sahihi ulikuwa zote ziingizwe UN kama mataifa tofauti.Taiwan haikuwa right kuiwakilisha China nzima.Ukiikubalia China lazima uje na sera ya mwenye nguvu mpishe!.Nashangaa kwa nini husemi Taiwan ina mamlaka ya kuirudisha China kwenye mamlaka yake!
 
Aleyn: China na Taiwan ni nchi moja, lakini kisiasa walichukua nji tofauti, upande wa utawala wa zamani, yaani wa Chang Kai Shek,waliamua kumpisha Mao mainland China na kwenda Taiwan. Ungekua labda ulifanyika uchaguzi na kundi moja likashinda angalau upande ulioshinda ninge sympathize nao, Mao aliingia kwa nguvu,Wachina hawakushirikishwa kuwa wanataka Ukomunisti, ambao hawautaki wakaenda Taiwan,sasa nani mwenye haki dhidi ya mwenzie.Na hata ukifanya referendum leo,watu wa Mainland China wataitaka Taiwan, na watu wa Taiwan hawataitaka Mainland China.Ndio maana kwa upande claims za China zinaweza kuwa pia za Taiwan.
Nmekusoma mkuu
 
Hivi unaona UN ilikuwa right? Mara ngapi UN imetoa maamuzi sio sahihi! Uamuzi sahihi ulikuwa zote ziingizwe UN kama mataifa tofauti.Taiwan haikuwa right kuiwakilisha China nzima.Ukiikubalia China lazima uje na sera ya mwenye nguvu mpishe!.Nashangaa kwa nini husemi Taiwan ina mamlaka ya kuirudisha China kwenye mamlaka yake!
Mja
China wanachotaka ni peacefully Unification na Taiwan kwa kuwa wao PRC ndio walioshinda Vita hivyo ardhi yote ya China wao ndio wenye mamlaka nayo . China hawataki kuwaua wala kuwafukuza ndugu zake kule kisiwani Ila China wanataka Kisiwa chao cha Taiwan kurudi katika himaya yao China Beijing huku wakiendelea kuwaacha Taiwan katika mfumo wao wa kiutawala Kama ilivyo Macau na Hongkong.
Na wewe umeingizwa kwenye propaganda za peacefully Unification! Haya mabomu na mameli ya Kavita yayoizunguka Taiwan leo ndio kutaka "Peacefully Unification " Please Ndugu ya Mjamaa wa kisasa kubali China ana elements zote za Imperialistic nation, na hapo bado hajawa sole super power
 
Nmekusoma mkuu
Mkuu, Taiwan na China waliisha chukua njia tofauti, kuna kipindi mwanzoni Mainland China ilipokuwa shaghala bagala wakati wanajenga ujamaa, Taiwan ilikuwa juu na mjanja mpaka ikapewa kiti UN kuwakilisha China nzima,kwangu mimi hiyo pia haikuwa sawa, wao hawakuwa na legitimacy ya kuiwakilisha China mainland.
Kwa kutaka kurebisha kosa hilo,UN ikafanya kosa tena, ikamwondoa Taiwan na kuiingiza China, kwa nini wasiwaingize kama mataifa mawili tofauti! Ukiwauliza UN leo je China wana haki ya kuichukua Taiwan,hawana jibu! Kama Palestine ina uwakilishi UN why Taiwan.
China inaidanganya dunia na "Peacefully Unification " angalia ilivyokuja juu Pelosi aliposema anaenda Taiwan. Hili jambo ni kitendwawili cha kihistoria, ndio, na China inataka kutumia nguvu tu, na itaweza siku Marekani ikianguka chali, na dunia tutakua tumepata beberu mwingine.
 
Nakubaliana na wewe, waliokimbia kwa sasa, yaani Taiwan hawadai chochote cha Mainland China,sasa kwa nini China itake kutawala mstakabali wao? Umeshinda umechukua sehemu kubwa, sasa kwa unifuate na kutaka kuchukua changu? Kwangu mimi is not fair.
Nasoma posts zako kwa makini na ninakuelewa sana yaani.
 
China wanachotaka ni peacefully Unification na Taiwan kwa kuwa wao PRC ndio walioshinda Vita hivyo ardhi yote ya China wao ndio wenye mamlaka nayo . China hawataki kuwaua wala kuwafukuza ndugu zake kule kisiwani Ila China wanataka Kisiwa chao cha Taiwan kurudi katika himaya yao China Beijing huku wakiendelea kuwaacha Taiwan katika mfumo wao wa kiutawala Kama ilivyo Macau na Hongkong.
Huu ni ujinga anaofanya China, utake unification ya nini wakati ulishampiga na yeye akaamua kukimbilia mbali na wewe? Mtu ameenda mbali kwa ajili ya kujisalimisha, sasa unamfatilia wa nini, si umuache na maisha yake? Kwa kweli kwa hili Taiwan yupo sahihi kabisa.
 
Pia unapaswa ufahamu hata Taiwan [ ROC ] nao pia wanaitaka China mainland ndio maana wao kisiwa wanajiita Taiwan na mainland wanaiita west taiwan[emoji3] kwa hiyo wanaamini pia ile ni ardhi yao nao pia wanaitaka ili kurudisha REPUBLIC OF CHINA mpaka Mainland.
Ndo zichapwe sasa, mshindi abebe ardhi.
 
Na mwaka huohuo 1927 vikaanza Vita vya wenyewe kwa wenyewe baina ya wachina wanaounga mkono chama cha kikomunisti cha China [ CPC ] na wachina wanaounga mkono chama cha Kuomitang . CPC ikiwa na jeshi la ukombozi wa watu wa China [ PLA ]likipambana na Kuomitang ikiwa na jeshi la China Nationalist Army Vita vikapiganwa kwa awamu ya kwanza mpaka 1937 na 1945 wakati wa Vita vya pili vya dunia wote kwa pamoja waliungana ili kupambana na kumtoa Japan ndani ya maeneo ya China baada ya kumshinda na kumtoa japan china wakati wa Vita vya pili vya dunia . Mnamo mwaka 1947 Vita vya wenyewe kwa wenyewe vikarudi tena na hii ikiwa ni awamu ya pili ya Vita kwa nguvu na kwa umoja jeshi la watu wa China [ PLA ] chini ya wanachama wa CPC na wachina wanaounga mkono sera za kijamaa lilipigana mpaka mwaka 1949 na kuwashinda jeshi la China Nationalist Army chini ya Kuomitang na waka kimbilia Kisiwani na ndipo ikazaliwa Jamhuri ya watu wa China [ PEOPLE'S REPUBLIC OF CHINA ] chini ya chama cha kikomunisti cha China [ CPC ] chini ya mwenyekiti Mao Zedong na Rais wa Jamhuri ya watu wa China.
Wachina hawajawahi kumshinda mjapan chief wamshukuru Mmarekan na nyuklia yake mpaka leo wangekuwa wamekaliwa.
 
Wachina hawajawahi kumshinda mjapan chief wamshukuru Mmarekan na nyuklia yake mpaka leo wangekuwa wamekaliwa.
Kitali: Kama Mmarekani asingemtwanga na Atomic mjapani au Mjapani asingeanzisha Vita na Mmarekani, labda China ingepata uhuru wake miaka ya 60! Japan was more advanced nation miaka ya 1930 na China ilikuwa primitive kwa maana ya primitive licha ya historia yao ndefu.
Huwezi kuamini Japan iliitawala China na kuinyanyasa vibaya, Kuingia kwa Mmarekani kuliikata nguvu ya Japan ndio kina Mao wakapata nguvu.Damu nyingi mno ilimwagika China kujitoa mikononi mwa Japan...
 
Hivi unaona UN ilikuwa right? Mara ngapi UN imetoa maamuzi sio sahihi! Uamuzi sahihi ulikuwa zote ziingizwe UN kama mataifa tofauti.Taiwan haikuwa right kuiwakilisha China nzima.Ukiikubalia China lazima uje na sera ya mwenye nguvu mpishe!.Nashangaa kwa nini husemi Taiwan ina mamlaka ya kuirudisha China kwenye mamlaka yake!
Jambo la msingi hapa tunapaswa kushauriana ni kuwa maamuzi ya UN yangepaswa kuwa ni :-
i, Kuvunja serikali ya Hongkong
ii, Kuvunja serikali ya Macau
iii, Kuvunja serikali ya Taiwan
Na wote hawa kwa pamoja wangeungana na China PRC kuzaa China moja isiyokuwa na serikali nyingi kitu ambacho hata serikali ya Beijing imekuwa ikipendekeza na kupigia kelele jambo hili .
 
Kitali: Kama Mmarekani asingemtwanga na Atomic mjapani au Mjapani asingeanzisha Vita na Mmarekani, labda China ingepata uhuru wake miaka ya 60! Japan was more advanced nation miaka ya 1930 na China ilikuwa primitive kwa maana ya primitive licha ya historia yao ndefu.
Huwezi kuamini Japan iliitawala China na kuinyanyasa vibaya, Kuingia kwa Mmarekani kuliikata nguvu ya Japan ndio kina Mao wakapata nguvu.Damu nyingi mno ilimwagika China kujitoa mikononi mwa Japan...
Uko sahihi sana mkuu👍.
 
Back
Top Bottom