China yakemea vikali ziara ya Nancy Pelosi Taiwan

China yakemea vikali ziara ya Nancy Pelosi Taiwan

SNAP J

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2013
Posts
7,106
Reaction score
8,043
Kumekucha. Mambo yanazidi kunoga.

Msemaji wa Waziri wa mambo ya nje wa China Bwana Wang Wenbin ameionya Marekani kuwa endapo Nancy Pelosi (US house speaker) atafanya ziara ya kuitembelea Taiwan, August mwaka huu, basi taifa hilo linaloaminika kuwa ndio lenye nguvu ya kiuchumi kwa sasa duniani litaijibu US kwa namna ambayo siyo tu inayoweza kupelekea kuvunjika kwa uhusiano wao wa kidiplomasia, bali pia inaweza hata kuwa ya kijeshi.

Msemaji huyo alisema adhma ya Pelosi kutaka kufanya ziara yakeTaiwan ni cha kichokozi, kwani ni sawa na kuingilia uhuru na mambo ya ndani ya Uchina.

"We are seriously prepared," Msemaji huyo alinukuliwa akisema.

..."and United States should be held responsible for any serious consequences", Mr. Wang aliongezea.

Ifahamike Serikali ya kikomunisti ya China inatambua Taiwan kuwa kama ni sehemu ya ardhi yake, wakati Taiwan yenyewe inataka kujitenga kutoka katika taifa hilo.

Mwezi April mwaka huu Pelosi alihairisha ziara hiyo kutokana na kuugua maradhi ya uviko-19.
 
Pelosi ameenda Ukraine na mrusi super power wa mchongo hakua na la kufanya pamoja na ndaro zake zote, na hao China wataishia kulaani tu lakini hawataweza kualisha ata fataki. China ipo chini ya Marekani ile technologia waliyokuwa wanapewa na Marekani miaka nenda miaka rudi hawakujua madhara yake sasa wanaunya unya
 
Pelosi ameenda Ukraine na mrusi super power wa mchongo hakua na la kufanya pamoja na ndaro zake zote, na hao China wataishia kulaani tu lakini hawataweza kualisha ata fataki. China ipo chini ya Marekani ile technologia waliyokuwa wanapewa na Marekani miaka nenda miaka rudi hawakujua madhara yake sasa wanaunya unya
Tulia dawa ikuingie vizuri, taifa la marekani ni gaidi, limefanya ugaidi nchi nyingi mlikua mkifurahi sana
 
Pelosi ameenda Ukraine na mrusi super power wa mchongo hakua na la kufanya pamoja na ndaro zake zote, na hao China wataishia kulaani tu lakini hawataweza kualisha ata fataki. China ipo chini ya Marekani ile technologia waliyokuwa wanapewa na Marekani miaka nenda miaka rudi hawakujua madhara yake sasa wanaunya unya
Teknolojia yote ya china ipo chini ya marekani?🤔
 
Pelosi ameenda Ukraine na mrusi super power wa mchongo hakua na la kufanya pamoja na ndaro zake zote, na hao China wataishia kulaani tu lakini hawataweza kualisha ata fataki. China ipo chini ya Marekani ile technologia waliyokuwa wanapewa na Marekani miaka nenda miaka rudi hawakujua madhara yake sasa wanaunya unya
Mbona unaongea pumba

Lini Russia waliwahi kusema kwamba Ukraine ni sehemu ya nchi yake , !? Yaani ulitaka Russia wamzuie Nancy kwenda ktk nchi nyingine Ambayo inajulikana duniani kuwa ni Taifa huru

Hauoni kuwa case ya china na Taiwan na hiyo ya Russia na Ukraine ni vitu viwili tofauti !?

Wanacho lalamika china ni kwamba Wana itambua Taiwan kuwa ni sehemu ya china , so ikitokea Nancy akaenda Taiwan kukutana na viongozi wa Taiwan Kwa viongozi wa china wanaona ni sawa na kuchochea Treason,

Yaani inawezekana vipi Kiongozi mkubwa wa taifa as prime minister atoke nje ya nchi kisha aje kukutana na Mkuu wa mkoa wa kigoma badala ya kukutana na raisi, !? Wewe unaona Ina make sense!?
 
Back
Top Bottom