China yasamehe baadhi ya madeni ya Tanzania

China yasamehe baadhi ya madeni ya Tanzania

Hakika Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania Tunayopaswa Kujivunia Na kuiheshimu, Amejenga Imani kwa kila mtu juu ya Tanzania yetu, kila mtu na kila Taifa kwa Sasa linatamani kushirikiana na Tanzania, Kila mtu anajiona Fahari kuwa na ukaribu wa kibiashara na Tanzania, Tanzania ya Nyerere kidiplomasia imerejeshwa na Rais Samia, Ni Kama Nyerere amezaliwa ndani ya Mama Samia, Tuendelee kutegemea makubwa kutoka kwa Rais Samia katika kuvutia wawekezaji watakao Leta fursa za ajira kwetu vijana
Unawaza kwa kutumia ndumku? Akiliza za kipuuzi hizi, hata Zambia walianza hivyo hivyo
 
Kusema “mikataba 15 ya kimkakati”, bila kutaja ni mikataba gani ni sawa na bure tu. Sasa hiyo taarifa inamsaidia mwananchi wa kawaida kivipi?

Hapo hakuna tofauti na mikataba ya siri. Wangesema na hiyo mikakati ndo tutoe maoni. Maana ukiona kuna madeni yamesamehewa, halafu mikataba haitajwi, basi kuna uwezekano tumepigwa.
Haitatajwa mkuh, Mingi ni ya kuuza nchi kwa Wachina.
 
Toa ushahidi tumepigwaje. Vinginevyo wewe ndio utakuwa FA*##la. Watu mpo kuzusha tu hata uhakika wa uzushi haupo. Hii Tabia acheni bwana
Hahaaa unazani kwa nini hio.mikataba haiwekwi wazi waka kujua majina yake? Wewe hio.mikataba 15 unaijua? Unazani kwa nini haiwekwi wazi?
 
Wewe ndio nenda huko Facebook unakoshinda wewe ili utaachie sisi huku tunakotumia Uhuru wetu kutoa mawazo yako, nenda Facebook ndio ukachaguage aina ya mawazo unayoyataka wewe na usiyoyataka na kuwataka uwa block ili wabaki wanao fanana akili na wewe
Uhuru gani wewe? Unaweza kuta unashingilia.ujinga wakati.ndugu zako wanakufa kwa umasikini kule bushi
 
Uhuru gani wewe? Unaweza kuta unashingilia.ujinga wakati.ndugu zako wanakufa kwa umasikini kule bushi
Unataka Uhuru gani zaidi ya huu unaoutumia hapa kutukana watu badala ya kushughulisha ubongo wako kuleta mawazo yenye tija hapa
 
Wamemaliza magogo tu na samaki
Wamesamehe deni? Kweli mwafrika atabaki kuwa mwafrika tu
 
Haitatajwa mkuh, Mingi ni ya kuuza nchi kwa Wachina.
Hata mimi nahisi hivyo hivyo. Ni wazi kuwa kwa kusamehe madeni na mikataba ya siri, kuna “quid pro quo”, ambayo tumepigwa ndo maana hakuna uwazi.
 
Tumshukuru Mungu kwa kusamehewa baadhi ya madeni.
 
Kila siku yupo kwenye ndege haogopi kweli??
 
Zanzibar Ni sehemu ya Tanzania Usituletee ubaguzi wako hapa, Sasa Tanzania diplomasia yetu ya uchumi inafanyiwa kazi kivitendo
Kuipongeza Zanzibar kupata Terminal II, ndiyo ubaguzi! Umekula maharage ya wapi kada wa ccm!
 
Wachina sio MAFALA mpaka wasamehe bure pesa Yao kila mtu anajua kilichompeleka Samia China ni mkataba wa bandari ya bagamoyo na gesi ya mtwara kwakifupi nchi amepewa mchina tayari pia kuna mikataba mingine mingi Tanzania imeingia na China.

tumeshapigwa tayari acha watuzuge kusamehe madeni.

Nilifikiri nchi kapewa waarabu .wa Oman na UAE..?
 
Ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kiserikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. Samia Suluhu Hassan nchini China.

Leo tarehe 03 Novemba 2022, China imesamehe baadhi ya madeni ya Tanzania.

Sambamba na hilo; Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa China Xi Jinping wameshuhudia utiaji saini mikataba 15 ya kimkakati hii leo jijini Beijing inayolenga kuimarisha ushirikiano, biashara na uwekezaji baina ya nchi hizo mbili.

View attachment 2406015
View attachment 2406016

View attachment 2406017

Pia akirudi mwambieni Rais wetu kuwa waziri wake wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Mbalawa hatufai tena.
Mambo aliyoyatoa Bungeni ni haibu kwa waziri msomi kama yeye. Alitakiwa ajiuzuru mara moja.









Yaani Professor mzima ameshindwa kutoa maelezo juu ya mwendelezo wa mkataba ambao unasadikika ku-exist baina ya serikali na hiyo kampuni iliyo tajwa ambayo ilitakiwa isiwepo tena. Mtu anajiuliza, inakuwaje serikali iwe na umiliki wa 100% hisa, lakini kampuni nyingine ambayo haiko tena, ndiyo ikusanye mapato na kuilipa serikali kwa mkataba upi? Na kidheria inakuwaje kuwaje hapo? Wakati waziri yupo? Anafanya kazi gani mda huo wote?

Watanzania wenzangu nadhani mnajionea wenyewe jinsi gani Rais wetu anavyotumiwa kuwaweka watu kwenye position kubwa za madaraka, ambao kimsingi hawapo hapo kwa maslahi ya nchi bali kwa malengo ya baadhi ya watu ambao wanafaidika na utendaji wa huyo waziri na kuwa kwake hapo.

Mama alikwisha onywa mara kadhaa na watu wenye ku-sense harufu mbaya juu ya uteuzi wa huyo Professor. Nafikiri Mama atakuwa amejionea mwemyewe kuwa chaguo lake la kumrudisha huyo mtumishi ni kazi ya bure.
Mama anatakiwa atambue kuwa sio watu wote wanao kuwa rehabilitated kwa kurudishwa madarakani wanakuwa wamejifunza vitu.

Issue ya Waziri Mbalawa inanikumbusha nyuma kwenye issue ya Professor Mhongo na yale mambo ya Makinikia. Inawezekana vipi waziri husika mwenye uzoefu kama yeye kushindwa kuliona hilo bomu lilipo? Hiyo kwangu ni ishara ya uzembe na ukosekanaji wa uadilifu wa huyo waziri.

Mama Waziri wako Professor Mbalawa hayuko serious na malengo yako. Bado anatenda mambo kwa misingi ya "Business as usual", lakini kimantiki ni Boya tu huyo. Hana Power ya kufanya kazi kwa ufanisi. Hii wizra ni nyeti sana inatakiwa iwe na mwenye vision na maarifa mapana. Vijana wengi wanategemea ufanisi wa hii wizara.

Ni kitu cha kustaajabu sana kuwa leo ndiyo tunasikia pia kuwa hata ule mradi wa SGR kipande cha tano kuzoka Tabora mpaka Kigoma nacho mpaka leo, takribani miaka miwili sasa, haujaanza kutekelezwa wakati Waziri husika na wasaidizi wake akina Kadogosa wapo na wanaendelea kuudanganya umma na wewe Rais kuwa mambo yanakwenda murua. Hivi Mtendaji mkuu wa serikali yuko wapi? Na anafanya nini?

Mama kama wewe baafa ya haya yote badunamshilikilia tu huyo waziri basi endelea, sisi tumemalizana naye.

Asante sana Mama, wewe ni Rais mzuri sana unaye ipenda nchi yako. Hawa ndiyo watendaji watakao tuvusha.
Endelea tu kutuchagulia watu wazuri kama hao. Watanzania wanakushukuru sana.

Mungu ibariki Tanzania na watu wake!
 
Back
Top Bottom