China yasamehe baadhi ya madeni ya Tanzania

China yasamehe baadhi ya madeni ya Tanzania

Ukishaona mikataba haitajwi wazi badala yake wanajifichia kwenye vijineno mkakati jua tumepigwa kama kawaida!.

Hata kwenye Roho Tour walituzuga watawataja wafadhili wa safari hadi leo kimyaaaa wanadhani wananchi wote hamnazo tumesahau!.
 
Ikiwa ni mwendelezo wa ziara ya kiserikali ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa CCM Ndg. Samia Suluhu Hassan nchini China.

Leo tarehe 03 Novemba 2022, China imesamehe baadhi ya madeni ya Tanzania.

Sambamba na hilo; Rais Samia Suluhu Hassan na Rais wa China Xi Jinping wameshuhudia utiaji saini mikataba 15 ya kimkakati hii leo jijini Beijing inayolenga kuimarisha ushirikiano, biashara na uwekezaji baina ya nchi hizo mbili.

View attachment 2406015
View attachment 2406016

View attachment 2406017
It doesn't make sense at all...

Unasemehewa mkopo wa TZS 34.7bn halafu wakati huohuo huyo huyo anakupa mkopo mwingine wa $56.72m sawa na karibu na TZS 1.31trn...!

Hii imekaaje..?
 
Kusema “mikataba 15 ya kimkakati”, bila kutaja ni mikataba gani ni sawa na bure tu. Sasa hiyo taarifa inamsaidia mwananchi wa kawaida kivipi?

Hapo hakuna tofauti na mikataba ya siri. Wangesema na hiyo mikakati ndo tutoe maoni. Maana ukiona kuna madeni yamesamehewa, halafu mikataba haitajwi, basi kuna uwezekano tumepigwa.
Nashukuru umeuona ulaghai huo.
Nilitikisa kichwa niliposoma hilo gazeti la Zuhura hapo juu. Hawa watu wanawadharau sana waTanzania siku hizi.

Hata hayo madeni tunayodaiwa na wachina hawasemi ni kiasi gani tunachodaiwa, sehemu ya ulaghai wenyewe.

Siyo kwamba wamesahau, au kuona si muhimu kuyataja hayo, bali ni uamzi wa maksudi kabisa kufunika kombe!

Halafu angalia ujuha wanaodhani waTanzania wanao: "Miradi iliyosajiriwa ya bilioni 9.6" inakuwa ni sehemu muhimu ya kutueleza sisi wapumbavu ili tushangilie! Hiyo dola bilioni tisa, nusu yake tu ingeanzishwa hali ingekuwa ni tofauti na ilivyo sasa!

Huyu mama katoka na zaidi ya dola bilioni 7, kule Arabuni; sasa kuna bilioni 9 za China!
 
Watanzania wenzangu nadhani mnajionea wenyewe jinsi gani Rais wetu anavyotumiwa kuwaweka watu kwenye position kubwa za madaraka, ambao kimsingi hawapo hapo kwa maslahi ya nchi bali kwa malengo ya baadhi ya watu ambao wanafaidika na utendaji wa huyo waziri na kuwa kwake hapo.
Umemdharau sana huyo mama anayewateua hao mawaziri.

Huwa siwaelewi sana watu kama wewe, sijui lengo lenu huwa ni nini hasa mnapojitoa akili kiasi hiki.
 
Hakika Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania Tunayopaswa Kujivunia Na kuiheshimu, Amejenga Imani kwa kila mtu juu ya Tanzania yetu, kila mtu na kila Taifa kwa Sasa linatamani kushirikiana na Tanzania, Kila mtu anajiona Fahari kuwa na ukaribu wa kibiashara na Tanzania, Tanzania ya Nyerere kidiplomasia imerejeshwa na Rais Samia, Ni Kama Nyerere amezaliwa ndani ya Mama Samia, Tuendelee kutegemea makubwa kutoka kwa Rais Samia katika kuvutia wawekezaji watakao Leta fursa za ajira kwetu vijana
Mh.Samia ni mwanadiplomasia mzuri sana kuliko Hayati JPM lakini hawezi kuwa bora kuliko Kikwete na kumfananisha na Nyerere ni kutomtendea haki Nyerere. Yule alikuwa wa kiwango kingine kabisa bado hajapatikana wa kumfananisha naye.
 
Hahaaa unazani kwa nini hio.mikataba haiwekwi wazi waka kujua majina yake? Wewe hio.mikataba 15 unaijua? Unazani kwa nini haiwekwi wazi?
Bora wadai iwekwe wazi bungeni kuliko kudhania tumepigwa tu bila kuwa na ushahidi mahsusi. Upuuzi huu
 
Asante mchina, lakini bado tunataka utuondolee nusu ya madeni tuliyo kuwa nayo kwa kwao jamani, maana nao pia wanafaidika sana na nchi yetu!
 
Wachina sio MAFALA mpaka wasamehe bure pesa Yao kila mtu anajua kilichompeleka Samia China ni mkataba wa bandari ya bagamoyo na gesi ya mtwara kwakifupi nchi amepewa mchina tayari pia kuna mikataba mingine mingi Tanzania imeingia na China.

tumeshapigwa tayari acha watuzuge kusamehe madeni.
Ulitaka upewe wewe? Kuna mijitu haioni zuri lolote lifanywalo na serikali, sijui ni ukosefu wa elimu?! Wee wadhania makubaliano yanakuja bure bure tu? Kuna nchi ngapi duniani zataka maslahi kutoka China? The fact kwamba rais amefanikiwa kufikia makubaliano hayo inaonesha ubingwa wa kukinaisha na kutoa hoja. Si lazima kwa China kuwekeza Tanzania, wala Tanzania si chochote katika maslahi mapana ya China. Nyie watu mlishibishwa uzalendo mchwara na aliyeondoka mwaona Tanzania ni kama kitovu cha dunia!
 
Masharti haya si bora tu tulipe deni au wadau mnasemaje?
 

Attachments

  • Screenshot_20221104-144522_WhatsApp.jpg
    Screenshot_20221104-144522_WhatsApp.jpg
    267.7 KB · Views: 4
Hakika Rais Samia Ni zawadi kwetu watanzania Tunayopaswa Kujivunia Na kuiheshimu, Amejenga Imani kwa kila mtu juu ya Tanzania yetu, kila mtu na kila Taifa kwa Sasa linatamani kushirikiana na Tanzania, Kila mtu anajiona Fahari kuwa na ukaribu wa kibiashara na Tanzania, Tanzania ya Nyerere kidiplomasia imerejeshwa na Rais Samia, Ni Kama Nyerere amezaliwa ndani ya Mama Samia, Tuendelee kutegemea makubwa kutoka kwa Rais Samia katika kuvutia wawekezaji watakao Leta fursa za ajira kwetu vijana
Hata wewe ukiwa mtu wa kutoa offer kila mtu atakupenda. Hali kadhalika nchi ikiwa inagawa rasilimali hovyo kila mtu ataipenda
 
Hao waliosamehewa ni makosa gani hayo , hlo hlo deni lililosamehewa Tanzania haiwez shindwa kulipa ...!!
 
Huyu ndio Rais aliyefanikiwa ndani ya muda mfupi Sana kujenga uchumi wa nchi unaogusa maisha ya mtanzania, kila mtu anaguswa na maendeleo makubwa ya uchumi wetu,
Maendeleo ya uchumi tunayaona kweli, litre ya mafuta ya kula ef 6 huku kilo ya maharage elfu 4 ndani ya mwaka tu
 
Nasikia Kuna uozo mwingi sanaaa,
Bandari ya bwagamoyo ndo Basi tenaaa macho kuvimba wanaichukua,
 
Hivi ni bilioni 31 ya madafu, au mimi ndo sioni.......
 
Back
Top Bottom