Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

Clouds Media wafungiwa kwa siku 7, kwa kutangaza Takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume

WATAFUNGULIWA KABLA YA SIKU SABA KUISHA.

KAMA KUNA MTU ANABISHA ASEME.
NINA UHAKIKA 100% MAGUFULI HAWEZI KUWAACHA WATOTO PENDWA WASISIKIKE HEWANI 7 DAYS. NEVER!

KUNA AMRI ITATOKA JUU MUDA SI MREFU!.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
 
Tatizo la watangazaji wa clouds Ni kujifanya wao wajuaji wa Kila kitu. Kujifanya watoto wa mjini wao, kujifanya wao Kila mtu tajiri au kiongozi wao ndo wanamjua Zaid wao.
 
And then it started.., or rather it continues? 🤔
 
Nyie hamjagundua plan

Lissu ataanza kampeni DSM

Vyombo hivi vya habari sasa hivi kwenye kipindi rasmi cha kampeni ni vigumu kuvidhibiti kutotangaza habari za wapizani 100%, yaani wataanza kutupia tupia, na hilo watawala hawalitaki!

Kwa hiyo plan ni ifungie Cloud Media ambayo inasikilizwa na wananchi wengi zaidi kuliko vyombo vingine ili kupisha kimbunga cha Dar, maana CHADEMA wamejiandaa kufungulia kampeni Dar

Sasa Dar ikikubali kwa Lissu, ni rahisi mikoa mingine kuitika!

Kwa hiyo watawala wanataka siku CCM wakiwa Dar, Cloud Media itakuwa imeshakuwa huru kurusha mikutano ya CCM na hivyo kuwapa CCM coverage kubwa.

Eleweni hii michezo ya kisiasa inavyochezwa nyie
Wewe mwaka 2015 ulikuwa jela ? Mwaka 2015 ndo ulikuwa mwaka mgumu sana ktk chaguzi walizowai kushiriki CCM sidhani kama uchaguzi huu unawaumiza kichwa CCM ndo maana toka Chadema waanze kupiga kelele umeona nani wa CCM anajibu kwa maana ya kudharau ingekuwa wanayosema Chadema yana inpact au damage kwa Chama na serikali bhasi kila siku ungemuona Polepole au Msemaji wa serikali Mr Hassan mbele ya waandishi wa habari kujibu hzo ngonjera za Lissu na chadema

Clouds fm wamefanya kosa na adhabu ipo kisheria kabisa kama unakumbuka Channel ten walishawai kufanya hvyo kwa matokeo ya uchaguzi wa zanzbar ukiacha kila TV au Radio kutangaza matokeo wakt mwenye mamlaka hayo ni NEC utakuwa umeleta Contradiction kwa walaji wa habari kwani kila chombo kitamtangaza mtu ambae wanadhani wao ameshinda

Kuhusu clouds kuongozwa kwa kusikilizwa sijui takwimu hzo umezotoa wapi ukizungumzia Radio inayosikika nchi nzima mpk bibi yako kijijini anaisikia ni TBC taifa haya kwani Serikali inashindwa kuwambia Clouds wasirushe mkutano wenu mpk waifunge? Hv unajua hasara wakatayoipata Clouds kwa siku 7 unajua ni matangazo mangapi itabidi wa warudishe pesa kwa vile hayakuruka muda maalumu uliopangwa ? Acheni ramli za kipuuzi wenzenu wanapewa likizo ya siku 7 bila malipo nyumbani nyinyi mnaleta siasa zenu hapa
 
Ung'amuzi wako hauna mantiki kwasababu Lissu hategemei vyombo vya habari, Lissu ni habari usikilize radio usisikilize utamsikia tu
 
Muda huu Eng. Kilaba anazungumza na vyombo vya habari, anatangaza kuifungia Clouds Media TV na Radio kuanzia kesho tarehe 28 hadi tarehe 3 septemba, kuanzia dakika hii hadi jioni Clouds media isitishe matangazo yote na irushe tangazo la kuomba radhi hadi jioni, kosa ni kutangaza wagombea waliopita bila kupingwa
Nonsense. Vipi hao Wakurugenzi ambao walitangaza? Nilimsikia Msimamizi wa Jimbo la Ruangwa akitangaza tena kwa mbwembwe kuwa Majaliwa amepita bila kupingwa. Yeye anachukuliwa hatua gani?
 
Waifungie tu Great Thinkers huwa hawasikilizi Clouds FM... alisikika mwanaJF mmoja akisema.
Mara ya mwisho kusikiliza Clouds FM ilikuwa wakati madogo wangu M.L. Chris na Seba (Deo) Maganga walipokuwa wakitangaza.
 
Umeona sasa!!! only smart people will understand this.........hivi lini chadema wanakuja na chombo chao??
Tanzania daima liko wapi? kama Clouds inafanyiwa hivyo je Chadema itafanyiwaje? Watawezana na hizo faini za kila siku?

Tukubali tu kwamba nchi imeharibiwa na sisi tukikenua meno na kuishia kulalama tu humu mitandaoni!

Unakumbuka vyombo vya habari wakati wa Kikwete? vilikua huru na watu walipenda hata kusikiliza taarifa za habari..siku hizi ni TBC tu tena matukio ya kuapishana au kufungua makongamano na habari za SGR au tazama anga!

Nchi imekua familia ya mtu mmoja hii analotaka yeye ndio linalokua.. shame!
 
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imevifungia vituo vya habari vya Clouds TV na Radio kwa siku saba kuanzia kesho Agosti 28 na adhabu ya kuomba radhi siku nzima ya leo kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji na kanuni ndogo za utangazaji za Uchaguzi.

TCRA imesema kosa walilolifanya ni kutangaza takwimu za Uchaguzi ambazo hazijathibitishwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC). Hii ni adhabu ya 2 ndani ya mwezi huu kwa Clouds baada ya kipindi chake cha Jahazi kufungiwa siku chache zilizopita.

View attachment 1549643

=====

The Tanzania Communication Regulatory Authority has on Thursday August 27 banned Clouds TV and Clouds FM for Seven days with immediate effect.

The authority said in a press conference today that the station has been banned after it announced election statistics that had not been approved by the National Electoral Commission.

On Wednesday NEC said the station had aired results that showed that certain Members of Parliament aspirants had sailed through unopposed after other contestants failed to meet nomination criteria in certain constituencies.

Earlier this month TCRA banned a radio programme (Jahazi) from the same station for allegedly promoting immorality in the society.

Zaidi, soma;

Uchaguzi 2020 - Tanzania: The National Elections Regulations(2020) - Mambo muhimu ya kuzingatia

When will NEC approve and publish any statistics, if at all? They are scheming along with their CCM counterparts to see how they can cook the data and lie to the public in favour of Magufuli?

We know everything they are doing, it's just a matter of time before the mask is finally lifted for the world to see who is behind all the pain this country bhas been going through.

Just a matter of months.
 
Wafungiwe maisha ni wapuuzi sana
Mimi Clouds huwa siwasikilizi hata siku moja na siwapendi kwani ni vibaraka.

Ile Clouds ya mwanzoni kabisa ndiyo ilikuwa pure entertainment studio na hata siku moja walikuwa hawaweki mambo ya siasa. Ila natoa tahadhari.

Hata kama adui yako akipatilizwa na hizi sheria za kikandamizaji zilizobuniwa na hawa watawala waoga, usifurahie.

Hao wamefungiwa siku saba tu, lakini target yao ni kufanya media ziogope na inaonekana kuna maandalizi ya kuja kufungia chombo huru tena kwa muda mrefu.
 
Watafunguliwa kabla ya siku saba kuisha.

Kama kuna mtu anabisha aseme.

Nina uhakika 100% magufuli hawezi kuwaacha watoto pendwa wasisikike hewani 7 days. Never!

Kuna amri itatoka juu muda si mrefu!.

Sent from my Infinix Zero 3 using JamiiForums mobile app
Hapa nakuunga mkono kufungia siku 7 redio na tv inayotazamwa na namba 1 sio rahisi.

Hilo sio gazeti la tanzania daima wala mwanahalisi.
 
Back
Top Bottom