CNN: 'Don't use birth control,' Tanzania's President tells women in the country

Upuuzi gani kama mtu anakuambia chapa kazi na endelea kufyatua?Au humo kichwani mwako ni sifuri?Kama unapiga kazi it means utapata kipato kitakachoweza kuendesha maisha yako vizur,sasa kwanini usizae?Au unamattz ya uzaz hii kauli ya kuzaa imekukera?
Hivi kuna watu wanaochapa kazi kama masikini? Ndugu yangu haujatembea ukajionea hapa unataka kusema masikini hawafanyi kazi ndiyo maana ni masikini?
Ndugu lazima tukubali amepotoka kigezo cha kuzaa sana kisiwe kuchapa kazi bali kiwe mafanikio kama umechapa kazi haujafanikiwa huna haja ya kuzaa halafu usiangalie leo tu angalia na kesho. Kuwa na uwezo wa kulisha watoto nane leo isikupe kiburi. Angalia kama umejiwekeza vizuri kiasi kwamba hata kesho ukipata ajali ya mguu ukashindwa kufanya kazi una miradi ya kulisha hao watoto nane au ndiyo utaingia nao barabarani kuomba kwa kisingizio cha ulemavu?

Jifikirie je ukifariki leo mke wako ana uwezo wa kulea na kusomesha ao watoto nane je unaacha mali gani za kumuwezesha mkeo kuhudumia watoto nane kama ukifariki au ndiyo mkeo aanze kulaumu mashemeji na mawifi zake kuwa hawamsaidii. Unajua vile ndugu wanalia kwa uchungu mtu mwenye familia kubwa akifariki wanajifikiria mzigo walioachiwa marehemu alikuwa anawatoto 11 wote wapo shule mabamdogo na maanti wapo watatu wanalia jinsi watavyogawana mzigo.
 

FAKE NEWS YA MABEPARI ALICHOSEMA RAIS KAMA UNA UWEZO WA KIFEDHA ZAA TU NA CHA MSINGI ZAIDI AMESEMA WATU WAFANYE KAZI...HIYO YA KUFANYA KAZI MBONA HAWAKUIANDIKA?
 
Hata asili hupotea mkuu, wakati wa kuzaa tu ni tawala mbili baada ya nchi kupata uhuru, kwasasa ukiwa ni mtu unaewaza kwa kurudi nyuma kuwa kila mtoto anakuja na bahati yake unaweza kuendelea kuzalisha watoto watakaoishi ktk maisha duni, mazingira magumu mtaani kwa kukosa mahitaji muhimu kama elimu, huduma ya afya, milo mitatu mavazi nk.
Kila kitu kimebalika ktk dunia ya sasa, usipompatia mwanao wala elimu ya sekondari basi tegemea kutengeneza vibaka, vibega, wapiga debe, wanaojiuza nk.
Ukweli utatuweka huru, kuzaa kwa mpango na malengo kutatusaidi kuhimili mambo mengi ktk ulimwengu huu wa sayansi na teknolojia kwa familia zetu.
 
Waache waandike. Naona wanaandika hadi sketi fupi... Gazeti kama hili ni vichekesho kweli. Waandike basi na mirandi inayozindua.

Nafikiri unamaanisha Miradi punguza pressure edit kwanza. Sasa kama kweli unamaanisha miradi hiyo sio nyuzi kwa wajuaji hiyo ndio kazi yake aliyoomba kufanya na tena azindue mingi zaidi kuzindua sio habari. Presidaa kufundisha watu kuzaa wakati sio mtaalam wa afya hiyo lazima imake headlines.
 

The President may have a point here....in Russia the population was declining...but under PUTIN measures have been taken , now it is rising slightly...
 
mama yako na baba wenyewe wamezaa kama nyumbu leo unajifanya mjanja, ongea kweli wewe acha unafiki, wewe kwenu ni wa 7
Kwa hiyo wewe unafuata akili za baba yako na mama yako sisi tulitegemea uwe bora zaidi yao kwa kuiga mazuri yao na kuacha pale unapoona hawakuenenda sawia?
 
kwani kakutaza wewe kuzaa kamoja?
Hivi nani kawaambia Uzazi wa mpango ni kuzaa mmoja au wawili?Mbona mnakuwa wajinga kiasi hiki wafia magufuli?
Mtu anaweza akawa na watoto 6 Ila akawa amezingatia Uzazi wa mpango kuliko hata aliyezaa watoto 3!!
Uzazi wa mpango ni kupanga kuzaa muda na wakati unaotaka,na si kuacha liwalo na liwe!
 
Mtoto wa saba kuzaliwa kwenye familia ndio Waziri
 

Somehow you are missing the point...Rais kama amenukuliwa vema ameweka au kusema na sualaau issue ya kufanya kazi...zaa watoto wengi na ufanye kazi ili uwalishe..point hapa nyingine kubwa ni kwamba Watanzaniatufanye kazi...watoto wakowasikimbilie mijini...uwafanye wafanye kazi huko huko vijijni..wazalishe mali na siyo kuja mijini kuuza soda, tambi, apple, juice za Azam na kadhalika kwenye vituo vya mabasi...
 

Una hoja hapa...
 
Hili la kuzaa ninaunga mkono hoja ya JPM.Russia na baadhi ya nchi za ulaya sasa hivi wapo katika kampeni ya kuongeza idaidi ya watu.Mwenye uwezo na azae kwa hata mungu alisema tuje kuijaza dunia.
Unalinganisha Urusi na Tanzania? serikali zao na jamii zinauwezo wa kuwatimizia mahitaji ya msingi, chakula, elimu, makazi hata kuwalipa unemployed, sisi hata wanafunzi elimu ya juu tumeshindwa tunabagua.
 
Al Jazeera pia...
Tanzania's John Magufuli advises against birth control
 

Ukweli ni huu. Serikali ya Magufuli haina mpango wala maandalizi yoyote ya ku-handle population growth..!!Huu ni uhuni na ubabaishaji. Kila Mtz anajua shule hazitoshi,waalimu hakuna, madeski hakuna(rejea ombaomba ya Bashite fenicha za waalimu) huduma za afya ni duni,kuna mamilioni ya kina mama wanakufa wakti wa kujifungua, watoto wanakufa kwa Utapiamlo, etc...!!

Hivi sasa elimu bure inatolewa kwa ubaguzi....Mikopo ya Vyuo vikuu inatolewa kwa ubaguzi sababu ni kwamba Serikali ya Magufuli haina FEDHA au uwezo wa kuwasomesha watoto maskini wa Wakulima na Wafanyakazi kwa mikopo tena watakayoilipa wakipata ajira...!!!
Leo Rais anapayuka jukwaani ati watu wazaane tu bila mpango lakini yeye mwenyewe ana watoto 2 tu...!!!
 
Kiukweli njia za uzazi wa mpango zina madhara mengi tu kwa kinamama....mm namuunga mkono raisi
 
Lkn njia hz zina some bad side effects!!! VP mkeo akiipata moja mojawapo mfano cancer za mfumo wa uzazi si utamkimbia wew ?? Tupime pia
 
HV unazjua complications za hz njia lkn au mnaandika tu!!!
 
Kwani sera ya uzazi wa mpango unasemaje? Mimi ndiyo maana anasema watu hamujui Sera ya uzazi wa mpango inasemaje ndiyo maana mnapinga kitu msichokijua. Rais amesema watu wasitumie vizuizi wazae tu huu ni uzaaji holela. Sera ya uzazi wa mpango ndiyo inayosaidia mtu kuzaa watoto atakao wamudu na kwa wakati alio tayari. Sasa kama Rais hataki uzazi wa mpango halafu anataka watu wazae watoto wanaweza kuwalea which is which? Hamuoni kwamba jamaa hajui anachokiongea? Hivi hamjui kuwa kinyume cha uzazi wa mpango ni uzazi holela wa bahati mbaya yaani mimba iingie wakati wowote ambao hata wahusika hawakutegemea, hapo ndiyo unakuta watoto wanapishana mwaka mmoja mmoja hii kiafya ina madhara kwa mama na mtoto. Tupo humu tunasapoti alichosema Rais bila kupima utafikiri siyo wasomi. Ni wazi elimu ya afya uzazi salama inahitajika nchi hii leo kusingekuwa na hoja hizi kama elimu ya afya ya uzazi ingeanzia kwa Rais mwenyewe. Ipo haja ya kuhakikisha Magu anaelimishwa kuhusiana na kila sera zinazotekelezwa na serikali yake. Hii kauli ni wazi kuwa sera nyingi hazijui hata leo ukimuuliza faida za uzazi wa mpango hawezi kukutajia hata moja hii ni aibu. Kweli taifa hili wasomi ndiyo hawajui elimu ya afya ya uzazi kweli its shame. Ndiyo maana tunasema huko nje lazima watucheke.
 
Watetezi wa Jiwe mtapata tabu sana kila siku kufanya damage control, tafuteni utaratibu wa kumuwahi kabla hajaropoka, ni jambo la kawaida maadui zake na vyombo vya habari vya nje vinachukulia hiyo loop hole kufanya propaganda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…