COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu

COINCIDENCE: Moja ya ushahidi wa uwepo wa Mungu

Katika suala hili, ni kwamba kuna watu hawajui chochote na ujifanya wajuaji. Hii inanikumbusha wakati nasoma ,,nilipokuwa darasa la kwanza nilijiona mi ndo msomi kuzidi wenzake, halikadhalika kila ninapokuwa level nilijiona kuwa nime elimika sana...ila ukweli sivyo. Katika suala la Mungu ni kwamba binadamu hawezi kulichunguza na kupata majibu anayotaka yeye. Kwa sababu binadamu kuna point ikiwa hawezi fanya jambo fulani....mfano kuna kiwango maalum binadamu anaweza kusikia sauti au mlio wa kitu, hiko kiasi kikizidi au kupungua hawezi sikia huo mlio ( audible range). Na pia kuna visible range ya binadamu, ikiwa kitu kitakuwa nje ya hiyo range hawezi kuona colour yoyote. Pia hata ktk uwezo wetu wa kukimbia pia upo limited, huwezi fananisha kukimbia kwa cheetah na binadamu. Nasuala la kufikiri pia, kuna range yetu ya kufikiri.....ukifika hapo huwezi kuendelea kufikiria tena, ila kifuatacho kitakuwa ni kufur au kuamua kuwaza vitu vingine. Mungu awabariki..

Kwa hiyo kama binadamu ana mwisho wa uwezo wake hilo linathibitisha kuwepo kwa mungu?

Kati ya anayesema kuna mungu ambaye hawezi kumthibitisha na anayekataa uwepo wa mungu huyo mpaka uthibitisho uwepo nani anajifanya mjuaji?

Kujifanya mjuaji kwangu mimi ni kudai unajua kitu usichojua.

Mimi sikubali kuwepo kwa mungu kwa sababu silijui hilo.

Wanaosema mungu yupo bila ya kuwa na uwezo wa kuthibitisha hilo ndio wanaojifanya wajuaji.
 
Ukishakubali hilo imeshakubali kwamba mabaya yameruhusiwa kuwepo na mungu, kabla binadamu hajakuwepo.

Kwa maana yasi geruhusiwa na mungu, binadamu hata asingeweza kuyafanya.

Sasa swali langu mimi linahusu hapo ambapo mungu alikuwa anaumba ukimwengu, kabla ya binadamu kuwepo.

Kwa nini kaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani?

MwenyezMungu ametuumba na ametupa utashi wa kutambua jambo jema na baya. Na pia ameziacha huru nafsi zetu kutenda tutakacho ili iwe km mtihani siku ya mwisho,waonekane watakaofeli na kufaulu.
 
Kwa hiyo kama binadamu ana mwisho wa uwezo wake hilo linathibitisha kuwepo kwa mungu?

Kati ya anayesema kina mungu ambaye hawezi kumthibitisha na anayekataa uwepo wa mungu huyo mpaka uthibitisho uwepo nani anajifanya mjuaji?

Kujifanya mjuaji kwangu mimi ni kudaibunajua kitu usichojua.

Mimi sikubali kuwepo kwa mungu kwa sababu silijui hilo.

Wanaosema mungu yupo bila ya kuwa na uwezo wa kuthibitisha hilo ndio wanaojifanya wajuaji.
Toa sababu za kukufanya usikubali kuwa Mungu yupo....
 
MwenyezMungu ametuumba na ametupa utashi wa kutambua jambo jema na baya. Na pia ameziacha huru nafsi zetu kutenda tutakacho ili iwe km mtihani siku ya mwisho,waonekane watakaofeli na kufaulu.

Hajaziachia nafsi zetu kutenda tutakacho.

Angeweza kuruhusu turudi nyuma katika muda, lskini hakutupa uhuru huo.

Pia, angeweza kuturuhusu kuamua kama tunataks kuzaliwa au hatutaki.

Hskutupa uamuzi huu mkubwa sana.

Kwa hiyo hii habari ya kwamba mungu anapenda kitupa uhuru tuamue tutakacho ni uongo.

Halafu mungu mjuxi wa yote na meenye uwezo wote kea nini ahitaji kutupa sisi binadamu mtihani wskati anajua kila kitu?

Mwalimu asiyejua yote anaweza kumpa mwanafunzi mtihani ili ajue mwanafunzi anajua nini.

Mungu anampa mwanadamu mtihani ili iweje?
 
Blah blah miiingi
Huyo Mungu mbona najificha ficha hivi na haelewiki?

Tatizo la mungu kutojidhihirisha kwa njia ya wazi isiyopingika kwa wote nikishaliulizis swali hapa, na mpaka leo sijapewa jibu.
 
MwenyezMungu ametuumba na ametupa utashi wa kutambua jambo jema na baya. Na pia ameziacha huru nafsi zetu kutenda tutakacho ili iwe km mtihani siku ya mwisho,waonekane watakaofeli na kufaulu.
Hawa watu wana ajenda ya siri ya kuchanganya akili za watu, ilihali wao wanapata nafasi ya kufanya mambo yao. Ukisha aminishwa Mungu hayupo ina maana hutakuwa na nguvu ya kukemea hata maovu yanayotendeka mfano ushoga n.k...kwahyo hawa watu wanakuja kwa kasi sana. Tujitahidi kuwaelimisha ili umma usipotoshwe ndugu, tujadili nao tutafika tu..na wataelewa kwa kudra za Mwenyezi-Mungu
 
Toa sababu za kukufanya usikubali kuwa Mungu yupo....

Sababu kubwa ya kutokubali mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo ni uwepo wa mabaya kwenye ulimwengu huu.

Mungu huyu alikuwa na uwezo wa kuumbs ulimwengu wowote alioutaka, ukiwamo ule ambao mabaya hayawezekani.

Haiyumkiniki akaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
 
Hawa watu wana ajenda ya siri ya kuchanganya akili za watu, ilihali wao wanapata nafasi ya kufanya mambo yao. Ukisha aminishwa Mungu hayupo ina maana hutakuwa na nguvu ya kukemea hata maovu yanayotendeka mfano ushoga n.k...kwahyo hawa watu wanakuja kwa kasi sana. Tujitahidi kuwaelimisha ili umma usipotoshwe ndugu, tujadili nao tutafika tu..na wataelewa kwa kudra za Mwenyezi-Mungu

Hapana.

Kuna watu wanaamini mungu mpaka wamefika kupewa dhamana za kidini na ni mashoga, wauaji (kwa jina la mungu nonetheless) etc.

Kuna wengine hawaamini mungu lakini wametoa maisha yao kuhudumia jamii kwa moyo wote.

Tatizo unalolionesha wewe katika post yaki ni lack of exposure.

Your frame of reference is probably very small by the looks of how generalized and myopic your conclusions are.
 
Hajaziachia nafsi zetu kutenda tutakacho.

Angeweza kuruhusu turudi nyuma katika muda, lskini hakutupa uhuru huo.

Pia, angeweza kuturuhusu kuamua kama tunataks kuzaliwa au hatutaki.

Hskutupa uamuzi huu mkubwa sana.

Kwa hiyo hii habari ya kwamba mungu anapenda kitupa uhuru tuamue tutakacho ni uongo.

Halafu mungu mjuxi wa yote na meenye uwezo wote kea nini ahitaji kutupa sisi binadamu mtihani wskati anajua kila kitu?

Mwalimu asiyejua yote anaweza kumpa mwanafunzi mtihani ili ajue mwanafunzi anajua nini.

Mungu anampa mwanadamu mtihani ili iweje?

Unachanganya uhuru na uwezo.
 
Sababu kubwa ya kutokubali mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hayupo ni uwepo wa mabaya kwenye ulimwengu huu.

Mungu huyu alikuwa na uwezo wa kuumbs ulimwengu wowote alioutaka, ukiwamo ule ambao mabaya hayawezekani.

Haiyumkiniki akaumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati alikuwa na uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote wa kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
Jaaah...kwahiyo kumbe ni hayo tu..! Mabaya wanaoleta si binadamu wenyewe, kwa mfano ww umetambua vyema kuwa kuna mabaya duniani..je hakuna mambo mema pia duniani?
 
Nimesoma mijadala ya watu pamoja na ya mleta uzi na nimegundua kwamba BINADAMU NDIO AMEMTENGENEZA / AMEMUUMBA MUNGU KUTOKANA NA KUSHINDWA KUPATA MAJAWABU YA VITU MBALIMBALI VILIVYOMZUNGUUKA.
Hayo ni mawazo yako wewe kulingana na uelewa wako ...! Kwani ww unajuaje? Kulingana na wewe je Mungu yupo au hayupo?
 
Tatizo la mungu kutojidhihirisha kwa njia ya wazi isiyopingika kwa wote nikishaliulizis swali hapa, na mpaka leo sijapewa jibu.

Kwani angeamua kufanya hivyo ndiyo ingekuaje?maana unachokiuliza hapo ni maamuzi yake.
 
Hayo ni mawazo yako wewe kulingana na uelewa wako ...! Kwani ww unajuaje? Kulingana na wewe je Mungu yupo au hayupo?
Mie nipo katikati kuna mazingira huwa naamini uwepo wake na kuna mazingira huwa naamini kutokuwepo kwake. Kwa sababu wakati mwingine huwa naona hizi dini ni kama mapokeo flani hivi
 
Naamini Mungu yupo kwa asilimia zote

Swali halikuwa kama unaamini, swali likikutaka uthibitishe kwamba yupo.

Viwili hivi ni tofauti.

Kama hujui tofauti kati ya kuamini na kuthibitisha, nitajuaje kama una basic requirements za kuweza kushiriki mjadala huu?
 
Kwani angeamua kufanya hivyo ndiyo ingekuaje?maana unachokiuliza hapo ni maamuzi yake.

Huwezi jusema maamuzi yake wakati hujaweza kuthibitisha kwamba yupo.

Kama hayupo, hawezi hata kufanya maamuzi.

Unaweza kuthibitisha kwamba yupo?

Hilo ni moja.

Pili, kusema "hayo ni maamuzi yake" bila kiweza kuelezea maamuzi hayo kayafikia kwa logic gani ni kukibali kwamba humuwlewi huyu mungu, unamkubali kwa upofu.
 
Back
Top Bottom