Confirmed: Ni Simba SC vs Nkana Red devils

Confirmed: Ni Simba SC vs Nkana Red devils

Ngoja wenye chama wao waje Mkuu uone watakavyopovuka. Nimeongea hii kitu na mtu jana akabisha natamani angekuwa humu akaona ulichokiandika.

Huo ndio ukweli. Nakazia maneno yako Boss.
Naona nipo humu
 
We!!!we!!! kule zambia ndio soka lilipozaliwa afrika. Chama angekua kiboko kuliko aliowaacha kule wasingekubali kuja kucheza mchangani huku...kule kuna mijichama iliyokubuhu
Usijekugeuka tena kama ulivyofanya kwa mbabane mkuu wakati mwingine kupiga kimya ni zaidi ya busara
 
We!!!we!!! kule zambia ndio soka lilipozaliwa afrika. Chama angekua kiboko kuliko aliowaacha kule wasingekubali kuja kucheza mchangani huku...kule kuna mijichama iliyokubuhu
Huo ni uvivu wa kufikiri. Wangekuwana wachezaji wazuri basi kessy asingepata namba. Lakini pia wangekuwa na wachezaji wazuri ukiisoma link hii ambayo inaonyesha wana wachezaji wawili tu ndio walioitwa Zambia National Team

https://www.lusakatimes.com/2018/07/29/zambia-national-football-team-head-coach-names-squad/
 
Nakumbuka mwaka 1994 kwenye michuano hii hii matokeo yalikuwa kama sikosei simba 2 Nkana 1 pale shamba la bibi, kule Lusaka Nkana 4 Simba 1. Simba Kali kabisa ya Mwameja, Deo mkuki,Aswile Godwin, Masatu George, Hussein Masha, Nteze John, Edward Chumila, Madaraka seleman,Duwa Said, Athuman China nk ikatolewa. Ngoja tusikilizie simba ya Manula na wenzake.
Mechi hiyo naikumbuka vyema,maana nilikuwa mwokota mipira (almaarufu enzi hizo "Chipukizi"), na kwenye hiyo mechi ya Simba SC vs Nkana Red Devils ya mwaka 1994 nilikuwa zamu kuokota mipira.Nakubali mechi ilikuwa kali na vikosi vilivyosheheni wachezaji mahiri.

Nawakumbuka majirani zangu akina RAMADHAN LENNY (RIP),EDWARD " Edo" CHUMILA (RIP) na GEORGE MASATU walivyopiga soka maridadi siku hiyo (hawa niliishi nao mtaa mmoja,Wailes maeneo ya Temeke,na ingawa nilikuwa under 18 nilipenda kukaa nao kwenye kijiwe cha " Squad"ambacho mastaa wengi wa Simba waliokuwa wakiishi Temeke walipenda kukutana,jirani na bar ya Bulyaga).Hao jamaa walipambana na wababe wenzao wa Nkana FC;namkumbuka beki wao KENNEDY MALITORI,na kaka yake KENNETH MALITORI,bila kumsahau JACOB BANDA,na somebody LUNGU (nadhani alikuwa ndugu wa JOHN LUNGU,ambaye baadaye mchezaji wetu NTENZE JOHN "LUNGU" alipachikwa jina hilo akifananishwa na Mzambia huyo).

Kwa ufupi,Simba walishinda 2-1 nyumbani,na wakafa 4-1 kule Zambia kwa figisu nyingi za soka la Africa.Na please,tusikariri maisha;Simba ya leo ITASHINDA na kuingia group stage.Na hata hivyo Nkana ya leo ya akina Hassan Kessy,si sawa na ile Nkana imara ya akina Kennedy na Kenneth Malitori.
 
Acha MAHABA NEGATIVE chama anacheza timu ya taifa ya Zambia. Unataka kutuambia kuwa hao Nkana Wana wachezaj gan zaid ya wachezaj wa timu ya taifa.
We!!!we!!! kule zambia ndio soka lilipozaliwa afrika. Chama angekua kiboko kuliko aliowaacha kule wasingekubali kuja kucheza mchangani huku...kule kuna mijichama iliyokubuhu
 
We!!!we!!! kule zambia ndio soka lilipozaliwa afrika. Chama angekua kiboko kuliko aliowaacha kule wasingekubali kuja kucheza mchangani huku...kule kuna mijichama iliyokubuhu
Unamjua makamu kapteni wa taifa la Zambia?
 
Kwenye hicho Kikosi cha Chipolopolo mbona sioni jina la Chama au Triple C au macho yangu?
Ungetumia akili kidogo ungegundua kwamba wachezaji walioitwa ni wa ndani kwa camp ya siku 3.
Wachezaji wote wanaocheza nje hawakuitwa.
Tripple C sio mchezaji wa mchezo mchezo.
Wacha chuki na uzushi.
 
Ungetumia akili kidogo ungegundua kwamba wachezaji walioitwa ni wa ndani kwa camp ya siku 3.
Wachezaji wote wanaocheza nje hawakuitwa.
Tripple C sio mchezaji wa mchezo mchezo.
Wacha chuki na uzushi.
Kwani mwezi wa 6 mwaka 2018 Cloutus Chama alikuwa tayari ni mchezaji wa Simba? Nadhani alikuwa bado yuko Zambia. Hivyo kama aliitwa tungeliona jina lake. Ni hayo tu mkuu
 
Hata kusoma tarehe inakushinda ilikuwa tarehe 29 July 2018. Hivi julai ndio mwezi wa sita kwa kiswahili.
Wacha ubishi wa kijinga. Ukweli hauwezi kubadilika kwa kubadilisha tarehe.
CHAMA ni vice captain wa Chipolopolo.
Hupendi kachukue ndimu upunguze kichefuchefu.Katafute link nyingine.
 
Mechi hiyo naikumbuka vyema,maana nilikuwa mwokota mipira (almaarufu enzi hizo "Chipukizi"), na kwenye hiyo mechi ya Simba SC vs Nkana Red Devils ya mwaka 1994 nilikuwa zamu kuokota mipira.Nakubali mechi ilikuwa kali na vikosi vilivyosheheni wachezaji mahiri.

Nawakumbuka majirani zangu akina RAMADHAN LENNY (RIP),EDWARD " Edo" CHUMILA (RIP) na GEORGE MASATU walivyopiga soka maridadi siku hiyo (hawa niliishi nao mtaa mmoja,Wailes maeneo ya Temeke,na ingawa nilikuwa under 18 nilipenda kukaa nao kwenye kijiwe cha " Squad"ambacho mastaa wengi wa Simba waliokuwa wakiishi Temeke walipenda kukutana,jirani na bar ya Bulyaga).Hao jamaa walipambana na wababe wenzao wa Nkana FC;namkumbuka beki wao KENNEDY MALITORI,na kaka yake KENNETH MALITORI,bila kumsahau JACOB BANDA,na somebody LUNGU (nadhani alikuwa ndugu wa JOHN LUNGU,ambaye baadaye mchezaji wetu NTENZE JOHN "LUNGU" alipachikwa jina hilo akifananishwa na Mzambia huyo).

Kwa ufupi,Simba walishinda 2-1 nyumbani,na wakafa 4-1 kule Zambia kwa figisu nyingi za soka la Africa.Na please,tusikariri maisha;Simba ya leo ITASHINDA na kuingia group stage.Na hata hivyo Nkana ya leo ya akina Hassan Kessy,si sawa na ile Nkana imara ya akina Kennedy na Kenneth Malitori.
kaka yatosha tu kumwambia kuwa hii ndo Simba ya Chama, Kagere na Okwi
 
Back
Top Bottom