Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Corona imekuja kuumbua uongo wa dini

Maada nyingine mnapokuwa mnajadili kuweni makin sana maana mnaweza kumkosea Muumbaji wa yote . Haya yote yalishatabiriwa katika vitabu vitakatifu na sasa yanatimia hapo ndo utambue kwamba mwisho wa sayari yetu umekaribia kikubwa ni kurekebisha matendo yetu kabla ya kiama . Mungu hapimwi ndugu

Ila matendo ya wachungaji wa leo sio uthibitisho wa uwepo wa Mungu ama laaa! Imani yako ndo itakuponya wala sio wachungaji asanten wakuu


Sent using Jamii Forums mobile app

Acha upotoshaji kijana

Imani ingekua inaponya kama wewe unavyotuaminisha hapa basi tusingeona vatican na mekka wakipiga marufuku watu kwenda kuhiji kwao kwa kuogopa corona wakati wakijua kabisa kua ukiwa na imani unapona

It's Scars
 
Scars,
DINI ni mpango wa mwanadamu kumtafuta Mungu, imeumbua dini nyinginna ndio maana kua dini moja kubwa wakaamua kufunga misa zao, wakafuata wale wa MECCA sasa WOKOVU ambao uliletwa na YESU ndio umebaki na ndio mpango wa Mungu kuwakomboa wanadamu na dhaambi zao, hawa watu wa wokovu wanadamu
Na mpaka sasa kipindi cha pili na dakika za nyogeza bado dini haijafanikisha kumpata huyo mungu

It's Scars
 
Na tatizo la watanzania mnapenda sana KUONGOPEWA KULIKO UKWELI.
viongozi wa dini NI watu kama sisi. Hawana mamlaka yoyote au nguvu zozote za kuzuia au kuponesha magonjwa.
Ila leo akitokea kiongozi wa dini anasema anatibu corona.
MTAKIMBILIA HUKO.
sababu mnapenda kudanganywa.
NA WAO WANAJUA. Scars,

Sent using Jamii Forums mobile app
Ningependa kuongopewa basi ungeniona nikishoboka na hizi dini

Sipendwi kuongopewa na ndo maana nikiuliza maswali ambayo wao walitaka kupotosha kupitia dhana ya imani naambiwa nakufuru

It's Scars
 
Ninachotambua nikuwa MUNGU yupo.... (Majaribu haya budi kuja)
Binadamu anamkumbuka Mola wake wakati wa taabu, tena anataka ajibu maombi yake haraka sana kiasi cha mate aliyotema chini yasikauke.

Asante Mungu
 
laiti kweli wangekua wanaroho mtakatifu anaewapa maono, nadhani wangekua msaada mkubwa sana yanapokuja majanga kama haya maana wangeomba kuoneshwa dawa watu wakapona bt na wao wamejawa na hofu na wanawasubiri madaktari kama waamuz wa hili na si mungu anaewapa maono
Roho mtakatifu ni hadithi ambayo inazungumzika vitabuni na makanisani tu lakini kiuhalisia haipo

It's Scars
 
Na ndo maana viongozi wa dini wamekaa kimya.
SABABU WAMEJUA KUWA HAKUNA MAOMBI YATAKAYO TIBU CORONA.
sasa NINYI MNALAZIMISHA MTAPELIWE.
akina gwajima wanawacheki tu.
Wanatafuta njia ZA KUJA KUWATAPELI.
Maana HAMSIKIII.
Ningependa kuongopewa basi ungeniona nikishoboka na hizi dini

Sipendwi kuongopewa na ndo maana nikiuliza maswali ambayo wao walitaka kupotosha kupitia dhana ya imani naambiwa nakufuru

It's Scars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa Waislam unawaone bure kabisa, wao hawana mambo ya kusema wanaponesha wagonjwa kwa miujiza.

Hii ishu tuwaulize moja kwa moja wakristo ambao kila siku tunaona wanaponesha wagonjwa,viwete wanatembea, wenye kansa wanapona...
Ukiwaza kidogo lazima uje na fikra ndogo kama hizi, I'm sorry for that

Kama kweli watu wa dini wanaweza kuuondoa huu ugonjwa kwa maombi basi serikali isingepiga marufuku na hata wao walikua na haki ya msingi kikatiba kujijeteta

Serikali imegundua kua maombi si chochote na ndo maana hata wao wenyewe wadini hawajaweka pingamizi

Kama kweli maombi yanafanya kazi sana kwanini tunawaona wanavaa mask huku wakihamasisha na wangine wavae kama kweli maombi yanafanya kazi?

Mfano katika nchi kama ya saudia arabia wale serikali yao yote inafata misingi ya dini lakini kwanini wamekua mstari wa mbele kukataza watu kutoka mataifa mengine wasiende mekka kama kweli power ya maombi inafanya kazi kama tunavyoaminishwa?



It's Scars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hautakiwi kuleta hoja kujadili kitu usichokiamini kama huamini katika dini ni bora kukaa kimya.
 
Poleni na majukumu ya hapa na pale sasa na kale yanayowafanya msilale, niende moja kwa moja kwenye mada husika.

Kama kweli maombi yanafanya kazi kwa namna ambayo tunaaminishwa, kwanini viongozi wa dini wameungana kutekeleza agizo la kuvunja mirundamano ikiwemo mijumuiko ya kiibada ili kuikwepa korona?

Kama walifanya maombi kwa lengo la kuizuia corona isiingie nchini, lakini tunaona corona imeingia, nini kinachokufanya uwaamini kua maombi ya sasa wanayojipanga kuyafanya yataitokomeza corona mazima?

Haya mambo probably si magumu ila ugumu tunauweka sisi kwa kuweka mizaha kwa kutumia kivuli cha dini.

Hivi mfano hawa madaktari wetu na sekta ya afya kiujumla wangejumuika kwenye maombi kwa kuamini kwamba maombi ni njia madhubuti ya kutatua matatizo kama haya katika kila janga la ugonjwa. Kama ambavyo watu wa dini wamekua wakituhimiza kufanya, je tungefanikisha kutibu gonjwa lipi kwa maombi?

Ngoma inaingia tanzania wabongo tulijitia wachamungu sana kua tumepewa mamlaka ya kukanyaga nyoka na n'ge hivyo ukimwi kwetu sio tishio.

Lakini tunachokiona mpaka saizi mapasta na masheikh wanachukua vidonge kwa siri sana. Lakini pamoja na hayo hatuwaoni wakijisalimisha kua wameshindwa kudhibiti ukimwi kwa maombi yao.

Mungu ambaye tunamtolea sadaka kila siku halafu katika matatizo kama haya kajichimbia tu wala hatuoni juhudi zake, huyu si mungu wakuabudiwa. Ni sawa na rafiki mnafki ambaye kwenye matanuzi mkiwa viwanja mnakua naye karibu sana halafu ikatokea siku umeishiwa anakukimbia.

Wahubiri wanahubiri huku wamevaa face mask at the same time wanasema damu ya yesu ni tiba ya kila kitu. What a joke but i ain't laughing?

Tunaambiwa ukiwa na imani waweza kuamisha hadi milima lakini sikutegemea kuona vatican, mekka ziwe kipaumbele kukataza watu wasiende kwao kwa hofu ya korona.

Mungu muweza wa yote yuko wapi mbona kawasusia msala madaktari wetu halafu yeye amesizi tu eti mpaka aamshwe kwa maombi?

Kwanini mungu mjuzi wa yote na muweza wa yote ahitaji maombi?

Mbona kwenye zile hadithi za gharika na sodoma na gomora huyu mungu ali-respond haraka sana kwanini asifanye hivyo kwenye janga hili linalomaliza ndugu zetu na kudhoofisha hali ya uchumi wetu?

Hivi kweli mungu huyu yupo kweli? Maana viongozi wetu wa dini nao wanaathirika mpaka inafikia hatua italy makanisa yameshehena maiti inamaana yeye haoni?

Kwanini Mungu ahitaji maombi yetu ili aweze ku-solve matatizo yetu, ilihali anaelewa hitaji la moyo wetu hata kabla hatujasema?

====

Chukua tahadhari kwa kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya Corona haidhibitiwi kwa maombi bali kwa kuepuka makatazo ambayo yameainishwa na shirika la afya

Mkuu Scars nimeziona hoja zako. Naomba mkuu ujue kwamba huu ugonjwa unaweza kuwa ni kidole cha Mungu kuunyeyekeza ulimwengu na ni vyema ukajua kwamba kupitia ugonjwa huu wengi wanaweza kumrudia Mungu. Mkuu Scars mbali na ulichoandika hapo juu, nakuhakikishia hata wewe ukiona ndugu kadhaa wa familia yako wameondoka kwa huu ugonjwa utaanza kuwaza kumtafuta Mungu. Sasa hili la watu waliotarajiwa kutuongoza kuelekea kutumia Imani kuonyesha kutokuwa na Imani wao wenyewe ni udhaifu wa kibinadamu tu.

Hili la kufuata angalizo lililotolewa na mamlaka ya afya kuhusu Corona na haliondoi lile hitaji ya watu kuendelea kumtumaini Mungu kwa Maombi.

Ahsante
 
Kumekuwa na mbwembwe nyingi za wachungaji, mitume na manabii kukitokea matatizo yoyote katika jamii wakijinasibu kuyamaliza kwa uwezo waliopewa.

Mara nyingi wao hutunga vitu na kusisitiza wameoneshwa na Mungu na kutamka kuviondoa. Wakijinasibu wakati mwingine hata kusema wanawaponya watu walioathirika na virusi vya UKIMWI.

Naomba niseme kati ya watu wamekuwa wasanii ni hao manabii pamoja na waumini wao wasio na uelewa ambao huacha kufanya kazi na kuwaita baba zao.

Sasa nasema Corona hii hapa, iondosheni Tanzania. Au yatatueni machangamoto ya ndoa zenu huko nyumbani kwenu. Jihadharini na kudanganya watu kujifanya mnaponya kumbe mnatumia wasanii.

Nachukia wanaoigiza

Sent using Jamii Forums mobile app
Kwanza hakuna watu waoga kufa kama watu wadini. Lakini ukiwakuta madhabahuni wanavyohubiri utasikia "ukiwa na yesu au roho mtakatifu basi kifo sio tishio kwako"


Kwanini wanaogopa kufa wakati sisi ndugu zetu wakifa mapadre na masheikh wakati wa ibada za maziko wamekua wakisema "sisi tulimpenda ila mungu alimpenda zaidi" na kuna muda wanaenda mbali kabisa na kusema kua kifo ni mpango wa mungu

Kama kweli mtu akifa mungu anakua amempenda zaidi kwanini wao wajikinge na mask au kukataza watu wasiende kuhiji kwa kuogopa kufa kwa maambukizi ya korona?



It's Scars
 
Wakati wa janga la njaa miaka mitatu na nusu watu walipokula mavi ya njiwa vipi hapakuwa na nabii au wakati Israel wametekwa kwenda Babeli hapakuwa na nabii?
Hahahaa watasema kile kipindi walikua kwenye trial version mungu alikua akiwajaribu ila kwa uwezo wa roho mtakatifu jaribu lile walilishinda

It's Scars
 
Scars,
Kwa maana nyengine ni kwamba kumbe tunaweza kuaminishwa jambo la kisayansi na kumbe jambo hilo lisiwe kweli.

Kwenye sayansi tunaambiwa kunafanyika tafiti na sio imani,ila mbona kuna utata wengine wanasema kuna virusi vya ukimwi na wengine wanasema hakuna virusi vya ukimwi? Na wote ni wanasayansi wenye kutofautiana hivyo na wana ushahidi wao wa kisayansi.

Kuwepo kwa utata katika sayansi ambayo inafanywa na watu ambao hawana uwezo wote wala ujuzi wote, wala sio jambo la kustaajabisha.

Tutasema tu kua probably kwasababu ya udhaifu wao ndio maana hayo yanatokea na wao hawakua na namna ya kuweza kuepuka kufanya hivyo kwasababu hawakua na uwezo wote wala ujuzi wote wa kufanya bila kukosea.

Sasa kwa mungu mwenye sifa hizo za ujuzi wote, upendo wote na uwezo wote huoni mungu huyo kuumba huu ulimwengu ambao umejaa magonjwa na mabalaa ya kila rangi bado ni utata?

It's Scars
 
Mambo ya imani ni magumu.

Usitegemee mara zote uombe na Mungu akujibu on the sport.

Hata Mfalme Daudi kuna wakati alikosea Mungu akawapiga tauni ya siku tatu taifa lilikaribia kuisha.

Hata wana wa Israeli walikuwa wakimkosea Mungu anawapiga au na vita au na maradhi hadi watubu.

Hao watumishi wa leo nao ni watu kama wewe wengi wao wana makandokando kibao. Mungu anawatazama kwanza watubu warejee kwake.

Hata hivyo tuamini tu kuwa wapo wachache wanaoomba na Mungu anasikia.


Sent using Jamii Forums mobile app
Kama mambo ya imani ni magumu utajuaje kua imani yako sahihi kuliko ya mwingine?

It's Scars
 
Imani ina taratibu zake,sio kama unavyotaka wewe.Hata sayansi ina taratibu zake,ili iwe ni sayansi,sivyo unavyotaka wewe.Kwa mfano,unataka kufanya jaribio lolote la sayansi,ni lazima uende maabara, maalumu iliyojemgwa kwa kazi hiyo,huwezi kwenda sokoni ukafanya jaribio la sayansi ukapata majibu sahihi.Vile vile ukitaka kupiga picha ya X Ray,huwezi kupiga nje kwenye mwanga wa jua,kuna chumba maalumu,kilichojengwa kwa ajili ya X Ray's.Nk.
Kwa hiyo imani ina taratibu zake,na sayansi ina taratibu zake.
Acha upotoshaji kijana

Imani ingekua inaponya kama wewe unavyotuaminisha hapa basi tusingeona vatican na mekka wakipiga marufuku watu kwenda kuhiji kwao kwa kuogopa corona wakati wakijua kabisa kua ukiwa na imani unapona

It's Scars

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom