Corona: Japo ni janga, pia ni fursa. Tanzania bado hakuna maambukizi, tupunguze panic, tuongeze Elimu. WB kumwaga mihela, tuchangamkie fursa

Corona: Japo ni janga, pia ni fursa. Tanzania bado hakuna maambukizi, tupunguze panic, tuongeze Elimu. WB kumwaga mihela, tuchangamkie fursa

Pascal Mayalla,
Pamoja na kuongea mambo ya fursa, umekosea sana kusema hakuna mtz aiyeambukizwa hapa nchini, maana inachukua angalau siku 11 mpaka mtu kugunduika kuwa ameambukizwa, hasa baada ya kuanza kuonyesha dalili! Sijui kwa nini umeamua kupotosha hivi!

Tuombe Mungu hao wate waliokutana na wagonjwa waCovid-19 wasiwe na maambukizi! Maana kama watakuwa na maambujizi mfumo wetu wa afya hautaweza kuhimili!

Badara ya kupaka matope wenye taaluma zao, we ungeendelea na brabra zako tu na siyo kukurupuka na kutoa hitimisho kwa mambo usiyoyajua! Kosa gani aliofanya daktari juu ya mask kwa mfano?
 
Umeandika daktari alituingiza Chaka alipokuwa anaongelea kuhusu uvaaji wa mask tuambie basi unachofahamu wewe kuhusu uvaaji wa mask.

Maana daktari alisema wanaotakiwa kuvaa ni wahudumu wa afya wanaohudumia wagonjwa wa Corona na wagonjwa wenyewe ili wasiambukize wengine embu tuambie alikosea wapi.
Kwa hili amebwabwaja tu!
 
Wewe si ulimtuhumu technically na ukamwita Shetani baada ya kuona Corona ni fursa kisiasa, so wewe sio shetani kwa kuona ni fursa kiuchumi?!

Wewe ni kilaza sana, I was respecting you a lot but as for now you are stupid baboon#

Sent using Jamii Forums mobile app
Usimwite binadamu mwenzio nyani tafadhali! Hata mimi kwa kuna sehemu kanikwaza...ila bado ni binadamu!
 
Paskali ww ni motivation speaker, huna fursa yoyote uliyotumia kama ww zaidi ya kushauri wengine wafanye. Vinginevyo nitajie shughuli yoyote uliyofungua nije niione ni kesho.
Mkuu Tindo asante kuniita motivation speaker, kila Jumamosi asubuhi, Saa 1:30 hadi 3:00 asabuhi, nakuwa Star TV live, kuwapiga msasa madogo kwenye fani, kupitia kipindi cha Jicho Letu Ndani Habari, esho tunazungumzia Corona.
P
 
Siyo kwamba hakuna maambukizi bali vipimo hamna/havifanyiki!
Kwenye mipaka yetu yote tunapima joto kila anayeingia, ukikutwa tuu na homa, unachukuliwa vipimo vya ziada. Hao wagonjwa wote 6 wamewekwa karantini, na watu wote waliokutana nao wamechukuliwa vipimo, hakuna aliyeambukizwa.
P
 
Mkuu kama serikali imefilisika waseme tu wananchi waichangie, umesahau jinsi wana ccm waliweza kumchangia Mashinji milioni 30 ndani ya siku mpaka akashangaa, wakiamua kuendeleza harambee kwa siku 40 mfululizo ni billioni 1.2, nchi ina hela bwana !
 
Mamia ya wageni wanapitia airports bila kuwa detected na mwishowe wanajichanganya na wenyeji kama ilivyokuwa kwa mwana FA!Uganda hadi sasa hivi haijagundua kisa chochote mpaka sasa hivi ila wamefunga mipaka yao yote ila sisi Tanzania akina Polepole ndiyo wanatoa matamko ya kupambana na Corona! Hatupo serious!
No we are very serious, tumeweka madaktari official borders zote, kila anayeingia tunampima, wageni wote kutoka nchi zenye Corona, wanaingia kwenye 14 days mandatory self quarantine.
Sasa serikali imetoa list ya official spokespersons wa kuzungumzia Corona na sio kila mtu.
P
 
Wanabodi,

Kuna msemo wa Kiswahili usemao "Kufa Kufaana", wakati watu wanahangaika na janga la Corona, wengine wanaangazia namna ya kutumia changamoto kuzibadili kiwa fursa, yaani turning problems, obstacles, challenges or adversaries into opportunities.

Tangu dunia na taifa letu kukumbwa na janga la ugonjwa wa Corona, Tanzania kama Taifa, tumepanic, kila mtu ni mtaalam wa Corona, Viongozi wa serikali wakiwemo wataalamu wetu wa afya wanatoa contradictory statements kwenye media tena mbele ya Waziri wa Afya, elimu ya jinsi ya kujikinga inayotolewa ni elimu duni, hatuna vifaa vya usafi kwenye public places zetu ni mwendo wa vitisho na panic kwa kwenda mbele huku hakuna elimu yoyote proper inayotolewa na chombo chochote cha habari zaidi ya uhamasishaji wa kinga ili kuzuia.

Bandiko langu sio la kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa Corona au jinsi ya kujikinga, bali mimi naangazia fursa za Corona.

Kwenye kila changamoto, pia huwa kunajitokeza fursa. Concentration kubwa sasa ni kinga watu wame panikishwa na kuiona Corona kama balaa kubwa la ajabu hivyo tuko kwenye chaos hivyo kazi yangu mimi ni kuwatuliza na kuwapa michongo ya fursa mbalimbali zinazoletwa na janga hilo la Corona kwa hoja kuws japo Corona ni janga, lakini pia ni fursa, Watanzania tusiishie tuu ku concentrate kwenye janga la Corona tukajisahau kabisa na kushindwa kuziangazia fursa za Corona. Janga la Corona linaandamana na fursa mbalimbali, mfano tayari Benki ya Dunia, WB imemwaga mihela ya kufa mtu kwa ajili ya kufidia mdororo wa Kiuchumi unaosababishwa na Corona.

Kwavile tangu kulipuka kwa ugonjwa huu wa Corona, so far hakuna Mtanzania yoyote aliyeambukizwa virusi vya Corona akiwa nchini Tanzania, waathirika wote 6 waliogungulika Tanzania so far, hakuna hata mmoja aliyeambukizwa Corona nchini Tanzania, wote wameambukizwa virusi vya Corona huko waliko ambukizwa, na kuvileta hapa nchini lakini licha ya ku interact na watu wote walio changamana nao, hakuna hata Mtanzania mmoja aliyeambukizwa virusi vya Corona, hivyo at this moment naweza kusema, ugonjwa wa Corona ni ugonjwa wa wazungu huko huko nchi za ulaya zenye baridi na hata mgeni akija Tanzania na virusi vyake, atabaki navyo mwenyewe, Watanzania hatuambukiziki, hivyo sasa tupunguze panic ya ugonjwa wa Corona, lets compose ourselves tuchangamkie fursa mbalimbali zinazoletwa na ugonjwa huu wa Corona.

Fursa hizi ni za aina mbili, fursa za kitaifa kama Tanzania as nchi kuchangamkia fursa hii ya World Bank
World Bank Group Increases COVID-19 Response to $14 Billion To Help Sustain Economies, Protect Jobs

Fursa nyingine ni kama hizi
Hapa sasa naomba Watanzania wenzangu wenye jicho la kiangazia fursa mbalimbali
  1. Fursa za uandaaji wa vipindi vya redio, television na online vya uelimishaji umma kuhusu ugonjwa wa Corona, yaani public information Programs, sasa ni kila mtu anasema lake, nilimshuhudia mtaalamu wa Afya, Daktari bingwa akiwa mbele ya Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu, akizungumzia uvaaji wa mask, kiukweli alichemsha na analiingiza chaka taifa zima, hivyo nikaona hapa kuna fursa, kama hata Waziri wa Afya hajui kuhusu masks na anaingizwa chaka, vipi kuhusu sisi akina kajamba nani?.
  2. Serikali inasisitiza kutumia running water lakini hatuna vifaa vya running water kwenye public places kama hivi​
  3. Hivyo ukitengeneza hivi na kuviuza, afisi zote, public palaces zote, maduka yote, vituo vyote vya mabasi, stendi zote, vituo vya dala dala, masokoni etc, what an opportunity?
  4. Watanzania tunahimizwa kutumia hand sanitizers, hatuna sanitizers za kutosha Watanzania wote. Hivyo hii ni fursa kwa simple home made sanitizers kutumika, the simplest ni maji ya chumvi, chumvi ya kawaida ina clorine, tengeneza maji ya chumvi, pack, piga pesa!.
  5. fursa ya watu kununua ma dumu makubwa ya real sanitizers na kuyapack kwenye vichupa vidogo na kuuzia watu, japo kwenye hili, huwezi zuia matapeli kujaza maji mengi na kuweka vitone tuu vya sanitizers kuweka harufu.
  6. Soon mtashuhudia wale wauza ukwaji wa Bhakresa wakiuza sanitizers.
  7. Tuendelee kuweka fursa mbalimbali nitakuwa nazi update hapa.
Kwa wale wa Ibada leo, Ijumaa Kareem,
Kwa wale wenzangu na mimi, nawatakia Furahi Dei njema, sisi wa maji makali, Corona haituhusu!.

Paskali.

Kaka Mayala, naomba niongelee kitu kimoja tu kwenye ujumbe wao: hivi vifaa/vyombo vya kunawia mikono. Pamoja na ubora wake na ukweli kwamba vinaweza kuwa msaada mkubwa kufanya usafi wa mikoni, vina kasoro kubwa kutumika kwenye muktadha wa mapambano ya Covid19. Nifafanue.
  1. Ushahidi wa kisayansi unaonesha kwamba kunawa mikono kwa maji na sabuni kwa wastani wa sekunde 20, kunaondoa virusi vya Covid19 ambayo mtu anaweza akawa amevipata kwa kushika kitu au mahali palipoangukiwa na aerosols au droplets za mtu mwenye maambikzi au kwa kushikana mkono na mwenye maambukizi.
  2. Kwenye unawaji huu, kuna maneno kama manne ambayo ni kewords za kuzingatiwa kwenye mchakato (1) MAJI, (2)YANAYOTIRIRIKA, (3)SABUNI, na (4) MUDA (sekunde 20 au ziada).
  3. Kwa nini maji yanatakiwa kutiririka na sio kunawa kwenye besini? Ni kwa sababu kunawa kwenye beseni kuna uwezekano mkubwa wa virusi kubaki kwenye chombo au maji ambayo umenawia na hivyo ukawa hujafanya lolote la kusaidia.
  4. Hivi vyombo ulivyoviweka hapa maji machafu baada ya kunawa yana virusi (tuchukulie aliyenawa kakamata virusi wa Covid19). Katika harakati za kuyamwaga hayo maji na namna ya ku-handle chombo kilichotumika kukinga (besini) kuna kila dalili vikahatarisha mtu kushika virus walewale waliootolewa kwenye mikono.
  5. Hivyo basi, iwapo vyombo hivi vinatumika kunawia mikono (kutokana na uhaba wa maji ya bomba) ni vema haya mebeseni yakatoholewa yawe kama sink ili mtu anaponawa maji yasisimame bali yakamwagike chini. Au hiyo ndoo iwekwe mahili ambapo mtu akinawa maji yanamwagika chini na sio kwenye beseni.
  6. Kinyume na hapo, hizo beseni za kukinga maji machafu zinaweza kusaidia kumbembeleza na kumsambaza Corona

    Ni muhim pia kukumbuka kunawa na kujifuta na tissue na kuzitupa. Kwa kuwa sio kila mtu anaweza kupata tissue maalumu za kufutia mikono, taulo inaweza kutimika ila mhusika awe na uhakika anaitumia yeye mwenyewe kwa kazi hiyo tu na hakuna mtu ataigusa. Hayo yakishindikana, basi ni vema kunawa, kung'uta mikono hewani na uache ikauke yenyewe.

    MM togolani
 
Mkuu Tindo asante kuniita motivation speaker, kila Jumamosi asubuhi, Saa 1:30 hadi 3:00 asabuhi, nakuwa Star TV live, kuwapiga msasa madogo kwenye fani, kupitia kipindi cha Jicho Letu Ndani Habari, esho tunazungumzia Corona.
P

Hamna shida kaka, nitakua mbele ya TV nipate hayo madini. Uzungumzie pia na tume shirikishi ya uchaguzi, huenda huku jukwaani unashindwa kuielezea.
 
Tangu mwezi wa 11 mkuu, na waliokufa ni wengi sana, unasikia mtu wako wa karibu kafa ghafla ukiuliza unaambiwa pneumonia
Ila kiukweli watu wame-panic tu.

Huku mtaani kwetu watu wanavaa gloves na masks bila hata kuzingatia utaratibu.

Huu ugonjwa tunao tangu December na hakuna aliyekufa, labda awe immunocompromised.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanufaika wa hizo pesa za WB, watakuwa wanachama dola, muuza ndoo na maji ya chumvi kamwe huo msaada hautomfikia...

Everyday is Saturday.................... 😎
Kwa vyovyote vile, sio kila mmoja mmoja atafaidika;
Kama ambavyo ikitokea leo Wizara ya Fedha akifanikisha zoezi la kuipata hiyo grant na ikawa kwenye account za BoT, si kila mmoja anauwezo wa ku-develop business plan ya kuomba mkopo wa machinery, purchase of raw materials ambavyo in turn tutapunguza imports ili kusambaza kwa soko la ndani na hizo fedha zikabakia ndani na baadhi ya Watanzania wakapata ajira na TRA ikaongeza tax base kutokana na uwekezaji huu.

Ngoma ipo kwenye how quick as a nation we'll be proactive to seize such an opportunity kwa faida ya mama Tanzania.

Bahati mbaya, baadhi ya walio kwenye authority ambao ni jukumu lao kuomba, jambo kama hili they feel ni kama haliwahusu maana pay-check yake ipo tu mwisho wa mwezi. Aki-facilitate mtonyo uje, au asipofanya hivyo, haoni kama ina athari kwenye nini atavuta mwisho wa mwezi.

To be honesty, we have very few people who thinks in big picture.

Tanzania, Tanzania nakupenda kwa moyo wote
 
No we are very serious, tumeweka madaktari official borders zote, kila anayeingia tunampima, wageni wote kutoka nchi zenye Corona, wanaingia kwenye 14 days mandatory self quarantine.
Sasa serikali imetoa list ya official spokespersons wa kuzungumzia Corona na sio kila mtu.
P
Siyo kweli! Kama ni kweli mbona mwanaFA hakuwekwa karentini siku 14 alipotoka south Afrika?
 
Back
Top Bottom