Corona: Tanzania kuzuia chakula na bidhaa zingine kupelekwa Kenya

Kitendo cha mkulima wa Tanzania kuuza Kenya haimaanishi kwamba Tanzania hakuna soko, je China, USA, Japan wanapoleta Mali zao kuuza Africa inamaana kwamba Afrika ni soko kubwa kuliko kwao?.

Tunapowauzia wakenya, maana yake ni kwamba tinazalisha zaidi na tunachokihitaji, kwahiyo hapa nyumbani "Supply is more than demand" kwahiyo bei hapa lazima iwe chini. Qatar wanazalisha mafuta mengi kuliko wanayohitaji, ndio sababu bei ya Petrol na Diesel kwao ipo chini kuliko huku kwetu.

Jambo muhimu lazima ujue ni kwamba, Chakula kinahitajika sana, WFP wapo tayari kununua chakula chetu chote cha ziada, nchi za DRC, Rwanda, Zambia, Zimbabwe, Malawi na Msumbiji, zote wanahitaji chakula chetu, Kenya sio soko muhimu sana, Kenya inahitaji Chakula chetu zaidi kuliko sisi tunavyohitaji soko lao.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ni Mtanzania ila niseme tu kuna mitanzania mijinga sijapata ona. Sasa mkizuia bidhaa za kilimo kwenda Kenya si zitaharbika hasara itakuwa kwa nani sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hakuna cha kuwajibu, hatuna ugomvi, hawajaanzisha ugomvi. Kenya wanapigana na korona kwa njia zao. Inapaswa tuwaheshimu. Wanahitaji tuendelee kufanya biashara ndo maana hawajazuia magari ya mizigo.
 
Wewe, kama unalima bila kujua masoko muhimu ya Tanzania, hilo ni tatizo lako.

Sent using Jamii Forums mobile app
Unaleta siasa kwenye biashara za watu. Dunia nzima nchi nyingi wamefunga mipaka badala muwe adhesive na sheria za watu ili msaidie flow za bidhaa za wakulima zizidi kwenda sokoni mnaleta ukaidi. Mwisho wa siku aumiaye ni mkulima sio wewe.

Majuzi Kuna malori hapo Horohoro yalirudishwa na zilikuwa bidhaa za mboga mboga na matunda na mengi yaliharibika.. hiyo n hasara kwa mkulima

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hao wakulima wanaolima bila kujua wapi watapeleka kuuza na kujua taratibu za soko husika na kusabisha bidhaa zao kuoza ni watu wajinga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nenda kwanza ujue soko linahitaji nini kabla ya kwenda kulima, kama hujui mbinu za KILIMO hilo ni tatizo lako

Sent using Jamii Forums mobile app
Unajua gharama za kugeuza hayo malori hapo mpaka wa Kenya ukauze mzigo Burundi au Congo, the same kwa malori yaliyo mpaka wa Malawi na Zambia. Ubaya sisi Watanzania vichwa maji. Sasa Kama wewe hujawahi kulima hata mchicha utajuaje haya Mambo yanavyoenda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu, mi nikiwasikiliza hawa viumbe napata hasira. Yani Mh. Na praise team hawaambiliki. Kama waziri anatamka asilimia 9% (aprox 4,500,000) ya watanzania wana kisukari na Corona imeonekana kuua zaidi ya robo ya hili kundi je tupo tayari kuzika zaidi ya watu milioni moja?!

Wanachofanya nikutuchezea physiological game, wamekazana "kila mmoja achukue tahadhari" ili mambo yakiharibika watu wajilaumu wenyewe wasilaumu serekali. Wakati huko kuchukua tahadhari ni impossible bila serekali kuingilia kati. Mfano nimeenda hotelini kula, naletewa msosi naanza kula, anakuja mteja mwingine anakaa upande wa pili tunatizimana, chances za kuambukizana zipo juu sana. Ni jukumu la serekali kuhakikisha biashara zote zinafata muongozo wa social distancing, huwezi ukamuachia mfanyi biashara ajisimamie. Hali hii ipo kwenye baa, usafiri wa umma n.k

Nasikitika sana!!
 
Mimi ni mtanzania ila niseme tu kuna mitanzania mijinga sijapata ona... Sasa mkizuia bidhaa za Kilimo kwenda Kenya si zitaharbika hasara itakuwa kwa Nani sasa

Sent using Jamii Forums mobile app
Hukumuoma baba yako mjinga ila Watanzania wengine. Hiyo inabaki kuwa katika mtizamo, kama baadhi tunavyokuona ndezi hapa, na hasara uloyomsababishia baba yako na taifa kwa ujumla.

Umeambiwa malori ya bidhaa yapite, wewe umekurupukia bidhaa zimezuiwa, bidhaa gani sasa zimezuiwa?
 
Hakuna cha kuwajibu, hatuna ugomvi, hawajaanzisha ugomvi. Kenya wanapigana na korona kwa njia zao. Inapaswa tuwaheshimu. Wanahitaji tuendelee kufanya biashara ndo maana hawajazuia magari ya mizigo.
Kama wanapigana na corona ni jambo jema, lakini corona haiingizwi na madereva wa tz, kama mnabisha muulizenu m7 na Kagame hali ikoke baada ya matamko ya kipimbi.
 
Haha wanaolia ni nyinyi, sisi tumefunga border tu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…