Corona Virus: Rais Magufuli ahutubia Taifa - Machi 22, 2020 - Wagonjwa Tanzania wafikia 12

Zanzibar wana kamati yao I guess. Walishapiga stop mdege kuleta watalii na kwa yule "mtalii" atakayekaidi na kuingia Zenji, atawekwa kwenye mandatory quarantine for 14 days kwa mfuko wake. Yaani unaweza kukuta wakapelekwa hotel za bei mbaya sana
Sampuli wanaleta Dsm!
 
Hili sio swali ni jibu, kamati yoyote ya kitaifa kwenye jambo lolote inahusisha Zanzibar.
P
Hata mambo yasiyokuwa ya Muungano? Mbona Zanzibar wamesitisha safari zote za kimataifa lakini huku Tanganyika sisi tunasema tutapokea wageni lakini tutawachambua kwa mafungu? (Wale wanaoyokea nchi hatarishi wakae karantini na wengine wanaingia free).

Nadhani hii sii sawa. Sote kama nchi tuhukue hatua zinazofanana na kwa kushirikiana. Nadhani hii kamati ni ya Tanganyika ndiyo maana imeenda kwa waziri mkuu. Ingekuwa ya Muungano ingekuwa kwa Rais.

Greetings. Naomba radhi kama kuna makosa nimeandika nikiwa na hisia.
 
Hivi kwanini hapa kwetu hawazuii mikusanyiko ya kwenye ibada kama kanisani na misikitini? Wanaogopa kitu gani?
In God we Trust
 
Wakuuu Leo rais amehutubia, taifa ambapo ameeleza mipango ya serikali katika kupambana na corona, na changamoto zinazoikumba nchi katika kipindi kigumu hiki na ametoa maelekezo kadhaa, kiujumla mheshimiwa rais ameeleza vizuri Sana na Mimi nimemuuunga mkono kwa hotuba yake Nzuri Sana

Ila Nimeshangaa watu wanamponda na kumshambulia na kukosoa hotuba yake wengi wakisema afunge mipaka na wengi wanapinga kauli yake kuwa watu wachape kazi, wakuuu Mimi nampingaga Rais kwa mambo mengi Lakini Kwa hotuba yake ya Leo nampongeza na kumuunga mkono kwa asilimia Mia.
Nawashauli wakuuu kuwa tusisite kumkosoa rais katika mambo ambayo hayaendi sawa pasipo kuogopa mtu yoyote tupase Sauti, Lakini tusipinge hata yaliyomazuri anayofanya rais tumuunge mkono kwa mazuri na tujizuie kumkosoa kwa kila japo

Wakuuu ujue heli nusu Shari kuliko Shari kamili, heli tupate tatizo moja tutapambana nalo kuliko kupambana na matatizo mawili kwa Wakati mmoja, hatuwezi kupoteza watu Kwa ugonjwa na tukapoteze wengne kwa njaaa, jamani hivi tukifunga mipaka watanzania wanategemea Kutoka ndio wale weng hupata vitu toka nchi za jirani kila Siku ndio wale, je wewe hao watu utaweza kuwalisha? Hivi watu wasiende kazini kuchapa Kazi utaweza kuwalisha? Dar watu wengi zaid ya nusu ni vibarua wanaotegemea kutoka wakafanye Kazi ili walipwe kwa Siku warudi nyumbani watoto wale, mama ntilie hivyo hivyo, wakuuu acha Kabisa kuhangaika ili watu wasiende kazini, mipanga ifungwe watu watakufa na njaaa kwa wingi kuliko kufa na corona tumuuunge Mkono rais tuache hao wanao pinga kila kitu na kulazimisha eti mipaka ifungwe hao hawajui Tanzania ilivyo

Rais katoa hotuba Nzuri Sana tumuunge mkono

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tutamkosoa sana kwani all that was waste of time
 
Hivi ina maana wageni kutoka nchi ambazo hazijaathirika na huo ugonjwa hawatahusika na karantini? Mzaha sio mzaha?
 
You can say that again! Kuna watu wanaoangalia nani kasema kitu na kujitokeza kupinga kwa sababu tu ni yeye aliyesema na siyo kwa sababu hawakubaliani na kilichosemwa. Hii ndiyo hoja niliyokuwa naisema mara nyingi. Kuna mambo ambayo wapinzani wake wengine walikuwa wakisema ayafanye. Mara baada ya yeye kuyafanya hayo wanageuka na kuanza kumlaumu. Tuache mambo ya kivyama. Tuone kwamba tuna tatizo la kitaifa na tutoe ushirikiano wa kulitatua.
 
Tanzania tusizoee mambo ya kamati kila janga, wizara ya Afya na wizara nyingine zinaweza kutekeleza majukumu yote yenye kuhusu Corona.

Hizo kamati tutaunda ngapi jamani.
 
Tutavuka salama kwenye hili janga,tukifuata vizuri maelekezo ya wataalamu wetu wa afya !! Inshaallah
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…