Corona Virus: Rais Magufuli ahutubia Taifa - Machi 22, 2020 - Wagonjwa Tanzania wafikia 12

Corona Virus: Rais Magufuli ahutubia Taifa - Machi 22, 2020 - Wagonjwa Tanzania wafikia 12



Wataliano waliweka rehani afya za raia wao kwa kutanguliza uchumi badala ya afya sasa wanavuna walichopanda ni kuzikana tu hata Waziri Mkuu wao kabwaga manyanga...Kiburi cha mtaliano kimehamia hapa na sisi ndani ya wiki nne tutaufyata na kunyenyekea tu hakuna jinsi..

Sisi tunafuata nyayo za kiburi na dharau za mtaliano lakini tunamwomba Mwenyezi Mungu atufumbie macho tusiwe kama Wataliano yaani Mungu yupi huyo mwenye ubaguzi?

Kila mtu atavuna alichopanda: Tumethamini uchumi na kudharau afya zetu sasa tutegemee kupoteza uchumi na afya kwa mkupuo mmoja

Mwenyezi Mungu aliuliza maswali mawili muhimu sana:-

1) Hivi uhai wako siyo muhimu kweli zaidi ya mkate?

2) Hivi mwili wako siyo muhimu kweli zaidi ya mavazi?

Ndani ya wiki nne kuanzia leo tutapata majibu ya uhakika kama sala zetu za kubaguliwa zimejibiwa... Mwenyezi Mungu alituagiza magonjwa ya mlipuko na ya kuambukiza tunapaswa kujitenga kwa quarantine sisi tunasema business as usual... Sasa tunamkaidi khalafu tunategemea matokeo tofauti... Four weeks tutajua nini maana ya unyenyekevu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
We are ready to bury our own people in attempt to gain political popularity. Poor CCM
IMG-20200322-WA0060.jpeg
IMG-20200322-WA0061.jpeg
IMG-20200322-WA0062.jpeg
IMG-20200322-WA0063.jpeg
Screenshot_20200322-190825.jpeg


Don't make a promise you can't fulfill...
 


Wataliano waliweka rehani afya za raia wao kwa kutanguliza uchumi badala ya afya sasa wanavuna walichopanda ni kuzikana tu hata Waziri Mkuu wao kabwaga manyanga...

Sisi tunafuata nyayo lakini tunamwomba Mwenyezi Mungu atufumbie macho tusiwe kama Wataliano yaani Mungu yupi huyo mwenye ubaguzi?

Kila mtu atavuna alichopanda: Tumethamini uchumi na kudharau afya zetu sasa tutegemee kupoteza uchumi na afya kwa mkupuo mmoja

Mwenyezi Mungu aliuliza maswali mawili muhimu sana:-

1) Hivi uhai wako siyo muhimu kweli zaidi ya mkate?

2) Hivi mwili wako siyo muhimu kweli zaidi ya mavazi?

Ndani ya wiki nne kuanzia leo tutapata majibu ya uhakika kama sala zetu za kubaguliwa zimejibiwa...

Sent using Jamii Forums mobile app
Wewe jilinde kama wewe na familia ukitegemea Magu umechemsha yeye siku zote iko 'offside' with the outside world yani kituko cha dunia.....

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuache kujiombea majanga kufanya hivyo ni ujinga... ya Italia imekuwa sio bahati kwao siokwamba wao ndiyo walizembea kuliko nchi zote hko ulaya!!
Serikali inafanya kazi yake nasisi tuendelee kujilinda na kuomba neema ya Mungu huku tukiishauri serikali bila nongwa
 
Magufuli hataki kuwaudhi viongozi wa dini kuzuia mikusanyiko wasije kukosa sadaka.

Huko ulaya na amerika wala makanisa hayakuhitaji serikali kuzuia mikusanyiko, yalizuia yenyewe ila huku hawawezi kwa sababu wanategemea sadaka, watu wasipoenda kanisani mwezi mzima watakufa njaa.

Saudi Arabia na Vatcan city nyumbani kwa dini wamezuia mikutano ila sisi tulioletewa tunadhani tunaweza kuomba corona ikaisha, vatcan wameshindwa kuomba?

Tumefunga shule ila tumeruhusu mikutano ya ibada, watoto watakosa corona shuleni ila wataipata makanisani. Hakukua na haja ya kufunga shule na vyuo kama mambo ndio haya, tungeendelea kuomba.
 
Hiyo Karantini siku 14 ilibidi iwe imeanza kufanyika toka mwanzoni kabisa, ila hatujachelewa sana
 
Kila mtu anathawabu yake na adhabu yake, huwezi ukajua ni kwanini raia wa Italia wanakufa kama kuku,kuliko wachina ambao ndio chanzo cha korona, huwezi kujua makusudi ya Mungu kwa Italia,Mungu mwenyewe ndiye anayejua kwanini karuhusu kipigo cha namna hii kiwapate raia wa Italia, cha msingi ni kufuata masharti na kuendelea kumuomba Mungu atuepushe na baraa hili.
 
Tuache kujiombea majanga kufanya hivyo ni ujinga... ya Italia imekuwa sio bahati kwao siokwamba wao ndiyo walizembea kuliko nchi zote hko ulaya!!
Serikali inafanya kazi yake nasisi tuendelee kujilinda na kuomba neema ya Mungu huku tukiishauri serikali bila nongwa
Subirini ufike Tandale kwa Mtogole ndio mtajua huu ugonjwa ni hatari
 
Siyo wasafiri wote."Ni wale tu wanaotoka nchi zilizoathirika sana na ugonjwa" - Magufuli.
=> Wasafiri wote wanaoingia nchini, Watalazimika kuwekwa Sehemu ya kujitenga [Karantini] kwa gharama zao wenyewe kwa siku 14 hata kama ni mwenyeji.
 
Kila mtu anathawabu yake na adhabu yake, huwezi ukajua ni kwanini raia wa Italia wanakufa kama kuku,kuliko wachina ambao ndio chanzo cha korona, huwezi kujua makusudi ya Mungu kwa Italia,Mungu mwenyewe ndiye anayejua kwanini karuhusu kipigo cha namna hii kiwapate raia wa Italia, cha msingi ni kufuata masharti na kuendelea kumuomba Mungu atuepushe na baraa hili.
Hivi kwa nini tuna watu wajinga namna hii. Ndio maana ccm inawabeba ktk malori aisee kwenda kuwapigia kura. Ila kwa akili hizi ninyi lazima mtakufa sanaa ujinga wenu ndio kifo chenu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni kweli maana hata Italy imewachukua mwezi kuanza kufa kama kuku.

Sasa hivi Italy kukuta wamekufa watu 700 kwa siku hata siyo kitu cha ajabu.
 
Mkuu Unadhani wataliano waliyaomba,na kama waliyaomba,walimwomba nani na wapi?
Tuache kujiombea majanga kufanya hivyo ni ujinga... ya Italia imekuwa sio bahati kwao siokwamba wao ndiyo walizembea kuliko nchi zote hko ulaya!!
Serikali inafanya kazi yake nasisi tuendelee kujilinda na kuomba neema ya Mungu huku tukiishauri serikali bila nongwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tuache kujiombea majanga kufanya hivyo ni ujinga... ya Italia imekuwa sio bahati kwao siokwamba wao ndiyo walizembea kuliko nchi zote hko ulaya!!
Serikali inafanya kazi yake nasisi tuendelee kujilinda na kuomba neema ya Mungu huku tukiishauri serikali bila nongwa
Hakuna anayejiombea majanga. Ila huo ndio uhalisia.

Italy walizembea toka ugonjwa unaingia. Angalia vitu vya kutetea.
 
Back
Top Bottom