Coronavirus: Rais Magufuli awaomba Watanzania kumuomba Mungu kwa siku tatu

Coronavirus: Rais Magufuli awaomba Watanzania kumuomba Mungu kwa siku tatu

Aisee umenichekesha sana kipindi hichi

Yani hili janga limewafichua wanafiki sana
Hatuna nabii kama Nathan ,hatuna mtume kama Yohana Mbatizaji wanaoweza kukemea dhambi za wakuu
 
Watanzania tuache ukaidi tutakwisha, hili janga alisema mwanzoni waziri ummy kuwa likiingia hatutaliweza tuache ukaidi tuchukue hatua kabla halijaenea mikoa mingne, tutatafutana kwa tochi walahi tuzuie, kuzuia ni kuzuri kuliko kutibu hatutaweza tufunge masoko, makanisa na mabar plz mwekekezeni bwana Yule na mshaurini Sana, tutatengwa huko mbeleni na wenzetu, hata hao marafiki majirani walahi watatukana watatukataa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumuomba MUNGU ili akuepushe na janga ukiwa umeita vyomba vya habari vinakumlika ni unafiki wa kiwango cha lamii, yaani unamuomba MUNGU kwa kujianika kwenye TV kwa kugaramia ili uonekane kwa bwana yule kuwa unaomba, huu ni ujuha, huyo MUNGU mnaemuomba kwa staili hiyo mnamjua kweli?

Kibaya zaidi, hawa watu walionekana kuanza mumshukuru bwana yule kabla ya maombi, yaani badala ya kumuomba MUNGU kwa kuwapatia nafasi hiyo, matokeo yake wakaaanza kumshukuru bwana Yule huku wakikodolea kamera ili kuhakikisha bwana Yule anawashika sura zao wasije wakawa wamemaliza maombi na bwana Yule akawa hajawafahamu.

Aiseee tuna kazi kubwa sana ya kufanya nchi hii walahi.

OK namalizia kuuliza swali:

Je, hiyo amri ya take away inahusu na sisi wanywaji? Je, kwa maaana hiyo tukienda bar tuwe tunafungiwa na kuondoka? Khaaaa! watoa muongozo wamepangaranyika mapema sana na ikitokea hili janga likafumuka hata huyu Makonda walahi hutamuona hadharani atabaki ndani akichungulia dirishani kama Bashiru Ally na Polepole.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni Nakushauri ukienda baa usitumie gilasi asilani, kunywa kwenye chupa.
 
Watanzania tuache ukaidi tutakwisha, hili janga alisema mwanzoni waziri ummy kuwa likiingia hatutaliweza tuache ukaidi tuchukue hatua kabla halijaenea mikoa mingne, tutatafutana kwa tochi walahi tuzuie, kuzuia ni kuzuri kuliko kutibu hatutaweza tufunge masoko, makanisa na mabar plz mwekekezeni bwana Yule na mshaurini Sana, tutatengwa huko mbeleni na wenzetu, hata hao marafiki majirani walahi watatukana watatukataa

Sent using Jamii Forums mobile app
Jana na leo waziri ummy mwalimu amenyuti Tu ili mioyo yetu ipowe lakini list ya wagonjwa bado anayo tena ni kubwa anachofanya sasa ni kutoa idadi baada ya siku2 ili watanzania tusiendelee kupanic, subiri kuanzia Kesho utasadiki maneno Yangu pale list mpya ya wagonjwa itakapotolewa
 
Kama Rais namna ya kukabiliana na hili janga anatuambia tusali?



Sent from my iPhone using JamiiForums
Ukiondoa North Korea ni kiongozi gani wa dunia amewataka wananchi wake waache kusali? Ni Jambo baya kupotosha alichosema Rais...mnapotosha makusudi kwa lengo lipi/gani??? Rais ameshasema Mara nyingi tuchukue hatua na tahachari dhidi ya Corona...viongozi wengine wa serikali akiwamo waziri mkuu nao wamesema hivyo...Rais wetu amesema pia kwamba pamoja na kuchukua hatua na tahadhari dhidi ya Corona pia tumuombe Mwenyezi Mungu atuepushe na janga hili...Sasa Happ nyie wapinzani wa JPM ndipo mnaposhikilia kwamba eti Rais emesema tusali tu tutapona...huu ni uzushi uliovuka mipaka...
 
Sijui kama umemuelewa!!! Anamaanisha kuwa hao wenye dini yao na maombi yao, Roman's, corona inawasulubu,
Hili gonjwa ni la kisayansi tufate maelekezo ya wanasayansi wetu lasivyo tutaangamia

Sent using Jamii Forums mobile app
Mimi sijamuelewa kama wewe ila nafahamu nachokisema..Sayansi ni maarifa na maarifa yanatoka kwa Mungu..
Maarifa/Kipaji ulichonacho si chako bure tu kwa kuwa ulienda Darasani.
Kusali ni kujishusha ili kupata rufaa kwa mungu japo ashushe maarifa ya kupatikana dawa..Kila mtu kwa imani yake afanye Ibada..
Watu wengi wanashindwa kutofautisha Ibada na mambo yanyoambatana wakati wa ibada(siasa,hamasa za kijamii,propaganda pengine na uongo)
Ibada ya ukweli LAZIMA ifanye kazi.
Je Ibada yako ni sahihi?
Maarifa/Sayansi yako ni sahihi?
Wakati wa shida maarifa yako unafikiri yanakuja tu kichwani kisa una Ubongo?
NB: Mimi si mhubiri ila natambua Imani yako ndio itakuokoa au kukuangamiza..
 
Wakuu, Corona imekuja kutufunza kuwa Dunia inahitaji hospitali nyingi zaidi kuliko Makanisa/misikiti. Pia dunia inahitaji zaidi wahudumu wa afya kuliko wachungaji/mashehe feki!

Wakati tuko bize na maombi, wagonjwa idadi inaongezeka! Jamani serikali yangu tuache mzaha.

Naomba kila hospitali za rufaa mikoani zipewe mamlaka ya kupima na kutoa tiba za Corona, tupime watu wengi tuokoe kizazi hiki.... Kuchelewa kuchukua hatua ni kuongeza maambukizi na vifo.

Watu wasali majumbani, ila tuboreshe mfumo wa afya zaidi ndio utatuokoa sio kujazana nyumba za ibada...

Thank me later!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu, Corona imekuja kutufunza kuwa Dunia inahitaji hospitali nyingi zaidi kuliko Makanisa/misikiti. Pia dunia inahitaji zaidi wahudumu wa afya kuliko wachungaji/mashehe feki!

Wakati tuko bize kuomba wagonjwa idadi inaongezeka! Jamani serikali yangu tuache mzaha.

Naomba kila hospitali za rufaa mikoani zipewe mamlaka ya kupima na kutoa tiba za Corona, tupime watu wengi tuokoe kizazi hiki.... Kuchelewa kuchukua hatua ni kuongeza maambukizi na vifo.

Watu wasali majumbani, ila tuboreshe mfumo wa afya zaidi ndio utatuokoa sio kujazana nyumba za ibada...

Thank me later!!!

Sent using Jamii Forums mobile app
Maombi ni ufilauni
 
Asante sana Mkuu. Huwa nafanya sana hiyo ya ndimu au limao kabla hata ya Corona. Hii imenisaidia mno mambo mengi. Huwa nakula sana spices kuchemsha na mbogamboga blending kupata smoothie.
Ukiwa muumini wa ndimu na limao viwanda vya madawa vitafungwa.Idea ya ndimu inakausha damu imetoka viwandani ili kuwaogopesha watu wasitumie ndimu nao wakakosa biashara
 
Tutashinda kwa imani
Thats the bold and strong move, huku tukizingatia tahadhari zitolewazo ndio njia pekee itakayoyuvusha katika hili. Tukisema tunapambana we are doomed!

Naimani wote watu 50+mill tutakutana 31 dec kusherehekea mwaka mpya tukiwa wazima wa afya tele. Tupambane na hofu ndio mbaya zaidi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom