Waziri Mkuu Kassim Majaliwa Ametangaza Ongezeko la Wagonjwa Wapya wa Corona Nchini 196. Tanzania Bara Wagonjwa 174 na Zanzibar 22. Amesema kuwa visa vya maambukizi ya Virusi vya Corona nchini Tanzania vimeongezeka na kufikia 480.
Vifo vingine 6 vya wagonjwa COVID-19 vimeongezeka na kufanya jumla ya vifo kufikia 16 Tanzania, wagonjwa waliopona wamefikia 167. “uzushi wa kwamba kila kifo ni cha corona sio sahihi kuna magonjwa mengine yanayoua”
Waziri Mkuu akinukuliwa, amesema...
''Kuanzia Aprili 23 - Aprili 28,2020 tumepata wagonjwa wapya wa Corona 196 ambapo kati ya hawa Bara wapo 174 na Zanzibar 22 ambao Waziri wa Afya Zanzibar ameshawatangaza, hii inafanya jumla ya visa vya Corona Tanzania kufikia 480 kutoka 284 ambavyo vilitangazwa Aprili 22''