WAKILI MSOMI AFAFANUA : HUKUMU HII YA MADAI ITAMZONGA MWANAHARAKATI HURU CYPRIAN MUSIBA KWA MIAKA 12
Mwanasheria msomi wakili Emmanuel Augustino anasema Je sheria inasemaje ikiwa mwanaharakati huru Cyprian Majura Musiba akishindwa kulipa kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu
Inawezekana Cyprian Majura Musiba hana hela , hilo halijalishi anatufahamisha mwanasheria msomi.
Hukumu hii ya Mahakama Kuu inaishi miaka 12 hivyo hata kama leo mwaka 2023, Cypria Musiba hana hiyo fedha basi Bernard Carmillus Membe anaweza kusubiria siku Musiba akiibuka kiutajiri ndani ya miaka yote 12 tangu hukumu kukaziwa .
Hivyo deni hilo Cyprian Musiba alilowajibishwa nalo kupitia hukumu hii atakuwa anatembea nayo shingoni hadi atekeleze wajibu wa kulipa fidia kama madai (decree) ya Mahakama Kuu ilivyoamuru .
Namna nyingine ni kumfunga mdaiwa Cyprian Majura Musiba kama mfungwa wa kimadai ambapo Benard Membe pia inawezekana ....
Mwanasheria msomi anaturejesha katika mfano wa hukumu ya kesi ya madai ktk mahakama ya biashara namba 80 / 2006 aliyoamua jaji F. Werema kuhusu kesi ya madai ya Euro Africa Bank (T) Ltd dhidi ya Wolfgang, Christine Springer & wenzake walipe deni .... sasa kabla ya miaka 12 kuisha mwaka 2018 wadai walirudi mahakamani mbele ya Jaji Mruma, madai ya Euro Africa Bank Tanzania Ltd yaliwasilishwa tena ..... na Euro Africa Bank Tanzania Ltd wakapewa invoice ya gharama za matunzo gerezani watoe shs. 300,000 kila mwezi kwa magereza ili mdaiwa aweze kutunzwa gerezani ..
Hivyo kwa Cyprian Majura Musiba anaweza kuwekwa gerezani kama mfungwa wa kimadai huku akilipiwa gharama za gerezani na Bernard Membe baada ya Mahakama kusikiliza utetezi wa Cyprian Majura Musiba kuwa hana uwezo wa kulipa madai ....
Mfungwa wa madai ikitokea kwa Cyprian Musiba ni tofauti na mfungwa wa jinai gerezani hivyo hatatumikishwa kazi za wafungwa wa jinai kama kazi za kulimishwa mashamba, kupasua mawe n.k ....
Mwanasheria msomi wakili Emmanuel Augustino anasema Je sheria inasemaje ikiwa mwanaharakati huru Cyprian Majura Musiba akishindwa kulipa kufuatia hukumu ya Mahakama Kuu
Inawezekana Cyprian Majura Musiba hana hela , hilo halijalishi anatufahamisha mwanasheria msomi.
Hukumu hii ya Mahakama Kuu inaishi miaka 12 hivyo hata kama leo mwaka 2023, Cypria Musiba hana hiyo fedha basi Bernard Carmillus Membe anaweza kusubiria siku Musiba akiibuka kiutajiri ndani ya miaka yote 12 tangu hukumu kukaziwa .
Hivyo deni hilo Cyprian Musiba alilowajibishwa nalo kupitia hukumu hii atakuwa anatembea nayo shingoni hadi atekeleze wajibu wa kulipa fidia kama madai (decree) ya Mahakama Kuu ilivyoamuru .
Namna nyingine ni kumfunga mdaiwa Cyprian Majura Musiba kama mfungwa wa kimadai ambapo Benard Membe pia inawezekana ....
Mwanasheria msomi anaturejesha katika mfano wa hukumu ya kesi ya madai ktk mahakama ya biashara namba 80 / 2006 aliyoamua jaji F. Werema kuhusu kesi ya madai ya Euro Africa Bank (T) Ltd dhidi ya Wolfgang, Christine Springer & wenzake walipe deni .... sasa kabla ya miaka 12 kuisha mwaka 2018 wadai walirudi mahakamani mbele ya Jaji Mruma, madai ya Euro Africa Bank Tanzania Ltd yaliwasilishwa tena ..... na Euro Africa Bank Tanzania Ltd wakapewa invoice ya gharama za matunzo gerezani watoe shs. 300,000 kila mwezi kwa magereza ili mdaiwa aweze kutunzwa gerezani ..
Hivyo kwa Cyprian Majura Musiba anaweza kuwekwa gerezani kama mfungwa wa kimadai huku akilipiwa gharama za gerezani na Bernard Membe baada ya Mahakama kusikiliza utetezi wa Cyprian Majura Musiba kuwa hana uwezo wa kulipa madai ....
Mfungwa wa madai ikitokea kwa Cyprian Musiba ni tofauti na mfungwa wa jinai gerezani hivyo hatatumikishwa kazi za wafungwa wa jinai kama kazi za kulimishwa mashamba, kupasua mawe n.k ....