Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Sgr unazindua baada ya kuijenga kichawi? Dodoma to tabora mtapajenga usiku kichawi?
Unabisha huwek data kwa sasa stesheni ya Morogoro tayr na ya DSM tayr now kuna ujenzi wa daraja la juu kabla hujaingia Dodoma ambapo juzi juzi treni ilisombwa na maji daraja la juu DSM wameandika reli tayar na wameweka pembe za ndovu like.
 
Kusema kweli mimi sina akili nyingi sana na ndiyo maana nimeendelea kuwa masikini mwenye nafuu, ila kujenga kipande cha Dar to Moro alafu ukaruka kwenda kuanza kipande cha Mwanza Isaka ni kuweka akili mfukoni kabisa. Serikali ingekuw inajiamini kuwa mradi utaendelea kuwa kipaumbele ata baada ya JPM kuondoka wangeifikisha reli Dodoma kwanza kutoka Dar then mchakato wa maeneo mengine uendelee, ila inachofanya serikal baada ya kuona kuwa mradi hautamalizika ni kujenga kutokea mwisho na kuyaacha yale maeneo ya muhimu zaidi[emoji45][emoji53]
 
Hii nchi imejaa wasomi waoga hawawezi kumwambia ukweli mkuu.
Hii tuna shida kubwa, unajiuliza tunakosaje vipaumbele kama taifa?!

Una deploy mradi wa train ya umeme, sawa ni jambo jema lakini je, huo umeme tunao wa kuendesha train? Maana huu wa kuchajia simu tu bado unaleta utata.

Reli kwa kiasi kikubwa ni miundombinu inayo tarajiwa kusafirisha mizigo mingi na pengine mizito ambayo kwa barabara si efficient kuisafirisha, na kwa nchi yetu hiyo volume tungetarajia itokane na bidhaa za kilimo, viwanda na imports.

Imports zimedorora kutokana na kodi kubwa pale bandarini, kilimo ndio hivyo tena na viwanda kila mtu anaelewa sinema za awamu hii ya viwanda elfu 4.

Kwa maoni yangu nadhani ingepaswa kuwa;

-Boresha sekta ya kilimo ambayo inagusa watu wengi (>75%) ya watanzania, kisha tutapata boost kwenye uchumi kutokana na uzalishaji wa kilimo.

-Stimulate sekta ya viwanda na umeme kwa pamoja ili tuanze kusindika bidhaa kuongeza thamani kuanzia huko mashambani.

-Kisha wekeza kwenye transportation, hapa ndipo reli ingekuwa na tija kwa kuwa tuna volume ya mizigo kufeed trains zetu na kupeleka maeneo mengine ya masoko.
 
Uchambuzi wako hauna facts,na bahati umeeleza kuwa wewe sio mtaalamu,sasa kumbuka huo ni ujwnzi wa reli ya mwendo kasi,una yjenzi tofauti na reli ya kawaida,pia hiyo kampuni ni kampuni kubwa sana na imwjenga reli kuliko hiyo huki kwao uturuki,nenda kaone waluvyojenga instambul
 
Huo mradi kwa wingi wa graduates mtaani wangetangaza dau mradi ungeisha ndani ya miezi 6 tu. Kupanga matofali na kufunga reli ndio iwe ishu hivyo? Waturuki wao wangejenga sehemu zenye madaraja tu
Mkuu kama ilikuwa hujuwi waturuki ndio wauza maneno number moja Duniani usiwahi Kumwamini wala kufanya naye biashara! Yani ni Malaya wa maneno sijuwi ata ni tumie neno gani
 
Mimi ikija suala kwa maendeleo naunga mkono nauhakika hii ni project nzuri kwa faida ya Taifa kama sio leo hata kesho, najuwa kutakuwa na changamoto lakini nadhani ni mradi utakuwa na faida kwa nchi ukija kusimamiwa vizuri kibiashara. Ikija kutokea mizigo bandarini inatolewa na kupakiwa kwenda kwenye bandari kavu labda maeneo ya kati ya nchi itapunguza gharama za usafirishaji kwa mikoa mingi na foleni Dar. Abiria pia watanufaika na huu usafiri. Tuunge mkono miradi ya kimkakati.
 
Sanga hatamki maneno haya bure bure.

Tuendelee kunywa mtori nyama
Naomba mwenye uelewa, technical/economical aniambie kulikuwa ma sababu gani kuruka vipande vyote hapa kati na kuanza ujenzi wa reli Mwanza to Isaka? Hapa TL ndio anashindwa kupata jibu, kama ni akili au matope yanatumika kufanya maamuzi
 
Siyo vibaya ila kaonyesha njia au wewe ulitakaje mkuu
Majigambo ya mwanzo haikuwa kuonyesha njia bali kujenga, tena kwa fedha za ndani. Kiburi hicho ndio kilipelekea watu kutekwa, kupigwa risasi, kuuwawa, kukataa katiba mpya kuwa watu wanataka maendeleo na sio makatiba. Kuminya uhuru wa vyombo vya habari. Hata hii kunajisi chaguzi za nchi, ziko kwenye kisingizio cha wananchi kukubali huo ujenzi jambo ambalo si kweli.

Toka mwanzo nilisema hakuna uwezekano wa kukamilisha miradi miwili inayozidi 15t ndani ya miaka 10, labda kama uwe ni mwepesi kulishwa propaganda za kijinga. Kuna ule utapeli mwingine wa bomba la mafuta ya Uganda, ule ni utapeli wa mchana kweupe.
 
This week wamesema imekamilika kwa zaidi ya 90%, hebu nenda kaangalie kama ni kweli maana wabongo huwa wabishi mno.
 
Hii tuna shida kubwa, unajiuliza tunakosaje vipaumbele kama taifa?!

Una deploy mradi wa train ya umeme, sawa ni jambo jema lakini je, huo umeme tunao wa kuendesha train? Maana huu wa kuchajia simu tu bado unaleta utata.

Reli kwa kiasi kikubwa ni miundombinu inayo tarajiwa kusafirisha mizigo mingi na pengine mizito ambayo kwa barabara si efficient kuisafirisha, na kwa nchi yetu hiyo volume tungetarajia itokane na bidhaa za kilimo, viwanda na imports.

Imports zimedorora kutokana na kodi kubwa pale bandarini, kilimo ndio hivyo tena na viwanda kila mtu anaelewa sinema za awamu hii ya viwanda elfu 4.

Kwa maoni yangu nadhani ingepaswa kuwa;

-Boresha sekta ya kilimo ambayo inagusa watu wengi (>75%) ya watanzania, kisha tutapata boost kwenye uchumi kutokana na uzalishaji wa kilimo.

-Stimulate sekta ya viwanda na umeme kwa pamoja ili tuanze kusindika bidhaa kuongeza thamani kuanzia huko mashambani.

-Kisha wekeza kwenye transportation, hapa ndipo reli ingekuwa na tija kwa kuwa tuna volume ya mizigo kufeed trains zetu na kupeleka maeneo mengine ya masoko.
Mimi sipingi maelezo yako ila kwa maoni yangu unaweka miundombinu kwanza kuvutia hayo yote uliyosema. ukijenga sehemu barabara, maji, umeme basi ujuwe watakuja watu kujenga makazi. Serikali kazi yake kuweka miundombinu na sera. Kilimo na viwanda ni sera tu wala haihitaji mtaji weka sera rafiki watakuja tu.
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Aliyekwambia SGR inafika Tabora ndani ya awamu ya 5 ya miaka 10 nani?
SGR ndani ya awamu ya 5 inaishia Makutupora tu.
Ndio maana tunataka tumwongezee muda ili SGR ifike huko Tabora mpaka Isaka.
Umeelewa?
 
Wazo hili mkubwa angelipata mapema leo tungekuwa tungekuwa tunaongea mafanikio

Maamuzi ya mihemuko,kutokuwasikiliza wataalamu tumejikuta tuna miradi mikubwa inatekelezwa kwa pamoja(Bwawa la umeme mto rufiji, Treni ya mwendo kasi).
Na kuamua kufanya matumizi makubwa ya fedha yasiyozingatia bajeti na ushauri wa wataalam.
Mkuu we acha, afu watu wameshupaza shingo kusifu ujinga. Unawatazama wale wanaomsifia unaona dhahiri zile ni dhihaka wanamfanyia Rais labda sababu wamegundua anapenda kusifiwa.

Viongozi kama kina Charles Mwijage, Kangi Lugola, kina Aggrey Mwanri unaona kabisa wanajaribu kutetea matumbo yao tu.

Kama rais angepata washauri wazuri (sina hakika kama anasikiliza ushauri), tungekuwa tumepiga hatua kama taifa.

Ila kwa hali ilivyo sasa ni kama tumepoteza miaka 6 hadi sasa ya kupiga hatua na pengine tumerudi nyuma kwa mambo kadhaa, na kama mambo yasipo badilika tuna hatari ya kupoteza miaka mingine zaidi ya kupiga hatua.
 
Back
Top Bottom