Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Mtikisiko wa uchumi tokana na covid19 utayumbisha vingi. Siyo kwetu tu, hata kwao.
Tangazo la awali mradi kpande cha Dar - Moro kingekamilika Nov 2019. Kabla hata covid haijaanza. Hawana cha kusingizia covid hawa.

 
Kama flow ya malipo haiko vizuri watawezaje kukimbiza Ujenzi??

Kumbuka Serikali ina miradi mikubwa miwili ya ujenzi wa bwawa la Umeme na hiyo sgr, kwahiyo wasiwasi wangu ni hiyo flow ya malipo kama inafanyika kwa wakati.

Sisi huku kwenye miradi midogo dogo ni kawaida kusubirishwa malipo kwa miezi 8 hadi 14 na zaidi

Tena unakuta unadai pengine milioni 400 tu lakini unatakiwa kusubiri muda wote huo, sembuse hizo sgr zenye gharama za matrilioni?
Mkuu unajishughulisha na ukandarasi?
 
Sawa mkuu, nimeshauri hivyo kwa kuzingatia tayari tuna miundombinu ya awali ( barabara), reli ni miundombinu ya kimkakati huwezi kuijenga kama huna cha kufanyia tayari.

Hata mkoloni aliimarisha kilimo kwanza kabla ya reli, alivyoona kuna rasilimali za kubeba ndipo akajenga reli ila kwa kuanzia alianza na barabara kufika maeneo ya kilimo.

Bado naamini hiyo sequence ya mkoloni ina mantiki hata leo.
Unajuwa siku hizi dunia imebadilika na kuna ushindani sana sababu ya maendeleo ya mitandao mpaka bandari zetu. Mashindano ya siku hizi ni kupunguza gharama operation cost. Barabara zetu kweli zipo lakini zinaharibika haraka sababu ya hii mizigo mikubwa na foleni inasababisha pia kuongeza gharama. Ufanisi ndio mashindano ya siku hizi, je nikitaka kufungua kiwanda itachukuwa muda gani, sheria zikoje, hapa ndio tunashida tunaweka mazingira magumu sana duka dogo tu utakuta vibali 20, ni mambo hayana gharama lakini tunayafanya magumu. Reli itawavutia wawekazaji kuwa gharama za usafirishaji zitapungua kwa sababu njia za transportation nyingi kuwafikia wateja au walengwa. Leo hii ukichukuwa eneno kubwa pori tu, safisha, weka lami, umeme, maji utauza eneo au viwanja mara kumi au zaidi. Miundombinu kwanza kwa maana tranpsortation za uhakika, communication, umeme, maji na mengine mengi plus sera bora utaona wawekezaji wengi.
 
Nimeacha Mkuu, baada ya kuona Tender nyingi wanafanya TBA na wenzao SumaJKT.

Saivi tunagombania kazi za kujenga vyumba vya madarasa ambazo wanatumia Force accounts hivyo naambulia kuwa Fundi tu😇😇
Industry imevurugwa sana
 
Tatizo sio kampuni bali ni fedha. Mwanzo JK alikuwa ameshakubaliana mkopo wa ujenzi wa huo ujenzi na bank ya exim bank ya China ya $7.6b, kwa masharti ya kampuni ya ujenzi iwe ni toka China. Ilibaki hatua ya utekelezaji. Alipoingia mzalendo academia akaja na hadithi kiwa huo Mkata uko overestimated, ila yeye ataujenga kwa fedha za ndani, na ujenzi akampa huyo mturuki. Mpaka sasa ameshakopa zaidi ya $2b na mradi bado unasuasua, na dalili zinaonesha bei itakuwa juu kuliko aliyoikataa mwanzo. Ninadhani motive ya kukataa mkataba wa mwanzo asingepata 10%, ndio maana akaanza makubaliano mapya ambayo atapata 10%.
Hizo usd bil 7.6 toka China exim bank zilikuwa kwa ajili ya Sgr ya umeme? Lakini kwa kasi ya utendaji Wachina wapo vizuri kuliko mturuki.
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Yapi Merkez nimewapita jana Dodoma,wako bize usiku wanapiga kazi,sijajua kama ni kila siku wanafanya vile au ni jana tu.
 
Unabisha huwek data kwa sasa stesheni ya Morogoro tayr na ya DSM tayr now kuna ujenzi wa daraja la juu kabla hujaingia Dodoma ambapo juzi juzi treni ilisombwa na maji daraja la juu DSM wameandika reli tayar na wameweka pembe za ndovu like.
Kwani nani hajui kuwa kuna reli imetandazwa? Madraja yamejengwa? Je itakamilika kabla JPM hajatoka madarakani?
 
Kama flow ya malipo haiko vizuri watawezaje kukimbiza Ujenzi??

Kumbuka Serikali ina miradi mikubwa miwili ya ujenzi wa bwawa la Umeme na hiyo sgr, kwahiyo wasiwasi wangu ni hiyo flow ya malipo kama inafanyika kwa wakati.

Sisi huku kwenye miradi midogo dogo ni kawaida kusubirishwa malipo kwa miezi 8 hadi 14 na zaidi

Tena unakuta unadai pengine milioni 400 tu lakini unatakiwa kusubiri muda wote huo, sembuse hizo sgr zenye gharama za matrilioni?
Hili ni tatizo kubwa.
 
Unajuwa siku hizi dunia imebadilika na kuna ushindani sana sababu ya maendeleo ya mitandao mpaka bandari zetu. Mashindano ya siku hizi ni kupunguza gharama operation cost. Barabara zetu kweli zipo lakini zinaharibika haraka sababu ya hii mizigo mikubwa na foleni inasababisha pia kuongeza gharama. Ufanisi ndio mashindano ya siku hizi, je nikitaka kufungua kiwanda itachukuwa muda gani, sheria zikoje, hapa ndio tunashida tunaweka mazingira magumu sana duka dogo tu utakuta vibali 20, ni mambo hayana gharama lakini tunayafanya magumu. Reli itawavutia wawekazaji kuwa gharama za usafirishaji zitapungua kwa sababu njia za transportation nyingi kuwafikia wateja au walengwa. Leo hii ukichukuwa eneno kubwa pori tu, safisha, weka lami, umeme, maji utauza eneo au viwanja mara kumi au zaidi. Miundombinu kwanza kwa maana tranpsortation za uhakika, communication, umeme, maji na mengine mengi plus sera bora utaona wawekezaji wengi.
Nadhani pia tatizo letu hatuna "National Vision and Mission" ndio maana kila rais anayekuja anaweza kuacha aliyo yakuta na kuanza michakato yake binafsi.

Umegusia suala la urasimu pia, kweli ni kikwazo sana. Kukamilisha jambo dogo tu kunakuhitaji upitie ngazi nyingi tofauti na tozo/kodi za kero kila unapopita. Hii inatupotezea muda na kukwamisha maendeleo.

Issue ya technology ndio naona kama tumeipa kisogo kabisa, hadi leo unaenda ofisi za umma eti unaambiwa subiri labda baada ya wiki 2 tunatuma taarifa makao makuu, seriously?!

Pia awamu hii inaua sekta binafsi kwa kutaka ifanye kila kitu, hilo haliwezi zaa matunda ni suala la muda tu.

Unakazana kuua sekta binafsi then unafanya miradi kama SGR, Hydro power, Ndege sasa unajiuliza serikali huwa ina mizigo gani ya kusafirisha? Serikali itafanyia nini huo umeme wote kama sio sekta binafsi? Ndege ni mtumishi gani wa umma anayemudu huo usafiri ukiacha wachache wa ngazi za kati na juu?
 
Ni kweli, kuna kampuni ya kichina ilitaka kusaini na Jakaya kwa dau kubwa lenye mizengwe,lakini haikuwa sababu ya kuwanyima wachina kazi maana kampuni zipo nyingi.
Na Jakaya tena, hivi huu mradi ni ubunifu wa Jakaya eeh!! Sikuwa najua
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Sielewi mantiki ya mada hii, kwani miradi mikubwa ya kimkakati huwa ni lazima imalizwe na Rais aliyeko madarakani. Mbona kila aliyeingia alikuta miradi ya awamu iliyotangulia inachofanya ni kuiendeleza, cha ajabu nii?
 
Huo mradi kwa wingi wa graduates mtaani wangetangaza dau mradi ungeisha ndani ya miezi 6 tu. Kupanga matofali na kufunga reli ndio iwe ishu hivyo? Waturuki wao wangejenga sehemu zenye madaraja tu

basi kama ni ivo watanzania wote ni maenginer wa reli
 
Back
Top Bottom