Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Dalili za mvua ni mawingu: Mradi wa SGR hautakamilika wote ndani ya utawala wa Magufuli

Pole sana Mkuu. Hauko peke yako kwani wako wengi wakiwemo Kampuni za Ulinzi wameporwa malindo na kupewa SUMA JKT. Cha kusikitisha ni kwamba nado wanasakamwa na Serikali hii hii wakati walishawapora Wateja.
Hakuna sekta ambayo haijaguswa awamu hii.

Sekta binafsi huzalisha ajira mara dufu kuliko Serikali ifanyavyo.

Sasa sekta binafsi imekufa ndiyo sasa unasikia kilio cha ukosefu wa ajira kila kona
 
[emoji23][emoji23][emoji23] dah mkuu, ndio sababu wanazotoa za kumuongezea muda kana kwamba huyu mtu akifa leo hii nchi nayo ndio inakufa.
Kawaida ukishakutana na watu ambao kazi yao ni kuitikia kiitikio, hawajui mashairi ya wimbo yanasemaje

Utasikia tu

Kwetu mwanza Nyegezi
Nyege nyege nyegezi

Hawajui kama huko ndani kuna masuala ya ambaruth wala nini
 
Mantiki ni kuwa walidanganya ili wapate justification ya kuanzisha miradi isiyo na tija kwa wakati husika.

Fedha yote imepotelea huko, deni la taifa limekua kwa ghafla, miradi mingine inasua sua, sekta ya elimu, afya, viwanda, biashara, kilimo nk zimezorota kisa hii miradi ya kukurupuka.

Watumishi hawapati nyongeza ya mishahara, hawapandi madaraja, wakistaafu hawapati mafao yao kwa wakati, serikali haiajiri, makato kwa wafanyakazi yameongezeka, mikopo kwa wanafunzi haitoshi, kodi kwa wafanyabiashara ni mzigo na sababu ni moja tu wanayoweza kutoa, kwamba eti tuna miradi ya kimkakati hadi tutapo maliza ndio mambo mengine yataboreshwa.

Kwa hiyo watu wanapo lalamika miradi haiishi kwa wakati uliosemwa awali, maana yake ni kuwa 'MATESO' yanaendelea kwa kipindi kisicho julikana kwa kisingizio cha 'miradi ya kimkakati'.
Hizo hesabu zako za uchumi za wapi? Ati pesa imepotela huko, kwa maana hakuna kinachofanyika hela imepotea. Tumejenga Kibiti Lindi kwa awamu tatu za Uongozi wa nchi kwako ilikuwa ni ni kupoteza pesa? vibanda vyetu wenyewe tunajenga kwamkuunga unga hatimae tunamaliza na kuhamia, huko ni kupoteza pesa? Maendeleo ni mchakato mnafeli wapi?
 
Hizo hesabu zako za uchumi za wapi? Ati pesa imepotela huko, kwa maana hakuna kinachofanyika. Tumejenga Kibiti Lindi kwa awamu tatu za Uongozi wa nchi kwako ilikuwa ni kazi bure? Maendeleo ni mchakato mnafeli wapi?
Kwani ahadi ya kukamilisha Sgr Dar to Moro ni awamu tatu za uongozi?
 
Hizo hesabu zako za uchumi za wapi? Ati pesa imepotela huko, kwa maana hakuna kinachofanyika.
Ninaposema pesa zimepotelea huko namaanisha sekta zingine zina starve, hii siyo serikali ya kwanza nchi hii.

Kama ni miradi ya reli, barabara, viwanda na hata ununuzi wa ndege haijaanza awamu hii. Na mambo mengine kama elimu, afya, maji, ajira, kilimo, umeme nk yalifanyika pia kwa pamoja na miradi hiyo.

Sasa awamu hii inayojificha kwenye hiyo miradi ya kimkakati kunyanyasa watu wake ndio unataka tuisifie?
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM Majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Iyo train ya umeme unayosubiri mfano umeme ukikatika mtakuwa abiria mnashuka mnaisukuma au mnasubiri hadi umeme urudi?
 
Hata usipokamilika ndani ya muda wake sisi hatuna shida watakuja kufaidi wajukuu zetu kwani shida iko wapi?Marekani anapanga mipango ya miaka 50 namna nchi yao itakuwaje sembuse sisi?
 
Ninaposema pesa zimepotelea huko namaanisha sekta zingine zina starve, hii siyo serikali ya kwanza nchi hii.

Kama ni miradi ya reli, barabara, viwanda na hata ununuzi wa ndege haijaanza awamu hii. Na mambo mengine kama elimu, afya, maji, ajira, kilimo, umeme nk yalifanyika pia kwa pamoja na miradi hiyo.

Sasa awamu hii inayojificha kwenye hiyo miradi ya kimkakati kunyanyasa watu wake ndio unataka tuisifie?
Tofauti na watangulizi wake, yeye yote hayo anafanya kwa wakati mmoja. Ndiyo maana nchi nzima ni miradi na amefanya kwa kiwango kikubwa kuliko awamu zote zilizo mtangulia. Utapenda au hupendi ndio ukweli.
 
Wazo hili mkubwa angelipata mapema leo tungekuwa tungekuwa tunaongea mafanikio

Maamuzi ya mihemuko,kutokuwasikiliza wataalamu tumejikuta tuna miradi mikubwa inatekelezwa kwa pamoja(Bwawa la umeme mto rufiji, Treni ya mwendo kasi).
Na kuamua kufanya matumizi makubwa ya fedha yasiyozingatia bajeti na ushauri wa wataalam.
Umesahau na daraja la Busisi mkoani Mwanza?
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM Majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Tuna bahati mbaya kuwa na uongozi kama huu.
 
Shida yenu mmekaririshwa kuwa watu wanawachukia ama kuwaonea wivu.

Hivi hiyo miradi ikifanikiwa me kama mtanzania sitanufaika nayo? Tunaposhauri ama kutoa mawazo tuna maana ya kujenga ama kuboresha. Kama ambavyo ikifanikiwa nasi tunanufaika vivyo hivyo ikifeli nasi tunaathirika.

Kuna haja gani ya kufanya miradi yote hiyo kwa mara moja wakati fedha zenyewe hatunazo? Tusipokuwa makini tutajikuta tuna miradi mingi ambayo haijakamilika na imetumia fedha zetu nyingi.

Dalili za awali kuwa uwezo wetu wa kuifanya hii miradi kwa pamoja ni mdogo tayari zimejiweka wazi ikiwemo rais mwenyewe kutamka wazi kuwa kuna mambo hayawezekani hadi tumalize miradi kwanza, mambo ambayo ni ya msingi na mengine ni stahiki za watu tena kwa mujibu wa sheria.

Tumenunua mandege ya masafa marefu bila kuwa na mpango kazi matokeo yamepaki tu na bado tunaambiwa zingine zitaagizwa hali ya kuwa hizi zilizopo hazileti tija yoyote.
Tofauti na watangulizi wake, yeye yote hayo anafanya kwa wakati mmoja. Ndiyo maana nchi nzima ni miradi na amefanya kwa kiwango kikubwa kuliko awamu zote zilizo mtangulia. Utapenda au hupendi ndio ukweli.
 
Sio ahadi unajenga kulingana na uwezo wako. Kumbuka hii sio pesa ya mkopo

Nilidhani hata unajua lolote kumbe hujui lolote, mpaka sasa serikali imeshakopa zaidi ya 1.5b sawa na 3.t. inaonekana hiki kitendo cha vyombo vya habari kuminywa hamjui lolote ndio maana mkianza kutetea watu wanawashangaa.
 
Bandugu sehemu pekee ya kuambiana ukweli hapa Tanzania imebaki Jf maana sioni gazeti, radio au Tv ambayo inaweza kujilipua na kusema ukweli au kutoa wazo lenye mantiki ya ukweli ili kuiambia ukweli serikali yetu.

Mfano ni dhahiri kuwa ujenzi wa Sgr toka Dar to Morogoro ulipangwa kukamilika 2019 na kipande hiki kina umbali wa km 202. Lakini leo hii tupo mwaka 2021 lakini nimezungumza na wadau ambao wapo site wanasema huu mwaka hawawezi kukamilisha.

Mmmoja wa wadau alie site japo kuwa sio mtaalamu sana wa civil works ila kwa uzoefu wake ameniambia kuwa kampuni ya Yapi merkez wapo slow katika kuchapa kazi. Maana anasema amefanya kazi za ujenzi kwa muda mrefu na haoni ugumu wa ujenzi wa reli maana kazi kubwa ni kujaza tuta na kisha kutandaza reli.

Kwa hiyo kukata udongo na kujaza tuta sio kazi ya kuchukua miaka minne,japokuwa kuna ujenzi wa madaraja,vituo na miundo mbinu ya umeme. Bora hii tenda wangepewa wachina tangu awali hizo km 202 zingekamilika.

Kuambia watu kuwa tutamilisha ujenzi wa Sgr ndani ya miaka 5 iliyobaki ya utawala wa JPM ni ndoto za mchana. Maana kwa kasi hii ya kampuni ya Yapi merkez ni kujidanganya kuwa vipande vya Makutupora to Moro,Dom to Tabora na Tabora to Isaka vitakamilika kwa wakati.

Inashangaza kwa nini PM Majaliwa haoni aibu kila mara kutuambia kuwa tupo karibu kuanza kupanda treni ya umeme wakati kiuhalisia bado sana.
Kusema kwamba ukamilishaji wa mradi unachelewa kutokana na uchapaji kazi wa mkandarasiwa Kituriki na kwamba ingekuwa Wachina wangekamilisha kwa wakati si kweli.

Kama ni hivyo serikali inashindwaje kumuonya mkandarasi au kuvunja kabisa mkataba kama tunavyoona kwa miradi mingine ya ujenzi?

Kwa maoni yangu tatizo linaweza kuwa ni pesa.
 
Tofauti na watangulizi wake, yeye yote hayo anafanya kwa wakati mmoja. Ndiyo maana nchi nzima ni miradi na amefanya kwa kiwango kikubwa kuliko awamu zote zilizo mtangulia. Utapenda au hupendi ndio ukweli.
Uko sahihi sana, Sasa ukipata nafasi kapitie deni la taifa baina ya hao marais wengine na huyu, kisha uje na mrejesho.
 
Nilidhani hata unajua lolote kumbe hujui lolote, mpaka sasa serikali imeshakopa zaidi ya 1.5b sawa na 3.t. inaonekana hiki kitendo cha vyombo vya habari kuminywa hamjui lolote ndio maana mkianza kutetea watu wanawashangaa.
Mradi una phase tatu, mleta mada anazungumzia phase1 Dar to Moro na ndiyo ameambiwa na msiri wake haitakamilika kwa kipindi cha awamu hii, wewe unazungumzia phase gani?
 
Back
Top Bottom