TANZIA Dar: Ali Mohamed Kibao, kiongozi wa CHADEMA auawa na mwili kutelekezwa Ununio ukiwa umeharibika sana

Duh

Mtu mmoja mwenye haki alisababisha mabadiliko makubwa Misri na Tunisia 🐼
 
Huwezi kuwa na furaha wewe uko hai na salama lakini nduguzo na jirani zako wanaomboleza misiba inayosababishwa na binadamu wenzao...

Nimekushangaa kidogo kusema "kuuana ni mambo ya kawaida......" Na kwamba nchi za wenzetu ni ya kawaida tu....

Bila shaka siku mwanao kapitiwa na ukaenda kuokota maiti yake huko shimoni ndiyo utakuja kujua kuwa Mungu hajapenda kauli yako ya "....shukuru Mungu wewe ni mzima pamoja na kuwa nduguzo na jirani zako wanaomboleza vilio tokana na vifo vya kusababishwa na binadamu wenzako..."

Biblia Neno la Mungu inasema;

"...Lieni na waliao, ombolezeni na wanaomboleza na furahini na wanaofurahi..."

Cha ajabu wewe uko kinyume na kauli ya Mungu. Why? Are you among the killers...?
 
Mungu akiamua kukuumbua juu ya muumba wake hashindwi
 
Inawezekana serikali INAHUJUMIWA....

Iko siku hili litathibitika....

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app

Serikali ina mkono mrefu sana ,tukio kama lile la watu waliojiamini kuteka basi na kuja kumtoa abiria ndani na mitutu kisha wakaondoka naye kwenda kumuua unadhani ni raia wa wakawaida? Unafikiri wangekuwa raia wa kawaida wangefika hata bahari beach bila kukamatwa?
 
Hili suala watu wangu wa ndani wananiambia si suala la muungano.
Ukitaka kuikosoa serikali vuka maji nenda zako Zanzibar.
Huku hamna mtu anayeguswa hata kidogo.
Huku wakosoaji hadi tunapewa Internet ya bure, asubuhi pia tunakunywa uni wa bure maeneo ya mnazi mmoja.
Akili mtu wangu.
 
Expect unexpected, siku zote ukweli huwa unashangaza
 


Hivyo una ushahidi Chadema ndiyo wameajiri usalama wa taifa kumteka kiongozi wao tena mzeeπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€”πŸ€” . Bora unyamaze maana unajishusha sana next time kama ndiyo kipaji chako hivi na uelewa wa chini basi nitakuomba usichangie topic zangu maana ni aibu
 
Tujaribu kumrudisha jela kwa miezi kama mitatu tuangalie hali ya utekaji itaendeleaje
 
Nashauri, tuchange Hela, yatafutwe magaidi ya alshababu na sisi tuanza kuwatungua hao watekaji na hao waliowatuma kimya kimya, hii ndio dawa Yao fire by fire
 
Kulaumu Polisi kwa ujumla, hapana...

Tatizo la Jeshi la polisi lipo kwa ma - Commanding Officers wao au maafisa wa juu wa Jeshi la Polisi IGP, MA - RPC nk ambao ndio wenye mamlaka na watoa amri na maelekezo kwa hawa walio chini.....

Hawa ndio wameoza kwa kuwa wamenunuliwa na kuwekwa kwenye mikono ya genge la wanasiasa walio madarakani kiasi cha maamuzi yao ku - abuse sheria na Katiba ya nchi. Mfano ni tukio la Mbeya juzi kwa polisi kupambana na vijana wa CHADEMA ktk mazingira ya uonevu kabisa na aliyeongoza Operesheni hiyo ni afisa mkubwa wa polisi Awadhi Haji....

Ukiona serikali ya nchi imejaa wizi na ufisadi wa fedha na Mali ya umma, jua kuwa fedha inayoibwa inakwenda ku - consolidate madaraka ya viongozi vya kisiasa walio madarakani kwa kuhonga na kuunda vikundi vya kigaidi na kuvifadhili Ili viteke na kuua wapinzani wa mabwana zao....!

Genge hili la wanasiasa hawa wa CCM walio madarakani mission yao kuu ni ya kisiasa - kuhakikisha kila aliye kinyume nao na anahatarisha uwepo wao madarakani anakwenda chini, anakufa......

Genge hili liko polisi, mahakamani, magerezani, bungeni....

Ukipigwa nje na kujifanya unaenda mahakamani, huko nako utawaluta na kamwe huwezi kupata haki yoyote...

Njia pekee iliyobaki kwa Sasa ni kumlilia na kumwomba Mungu wetu muumba wa mbingu na nchi na vyote vilivyomo atumie nguvu na mamlaka yake kupambana na watu hawa waovu waliokubali kutumiwa na shetani kutesa na kuua binadamu wenzao....

Alifanya hivyo kule Misri ya kale, Urumi ya kale, Babeli (Babylon) ya kale dhidi ya watu wa Mungu....

Hata Tanganyika anaweza....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…