Faana
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 38,657
- 44,759
Mkuu najaru kusoma upepo tu..majambazi yafichwe majina yao? kweli?
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu najaru kusoma upepo tu..majambazi yafichwe majina yao? kweli?
Acha UONGO,haikuwa hivyo issue ya ZombeBado nakumbuka zombe aliyekuwa RCO dar na RPC Rukwa na wenzake walivyoua wafanyabiashara 3 na taxi driver na kuwapora fedha na madini, licha ya tume ya jaji kipenka kuthibitisha lakini wakaachiwa na mahakama kisa askari aliyekiri kutoroka na shahidi muhimu askari Bageni kufariki (inasemekana).
Bageni anatumikia Hukumu yake ya Kunyongwa mpaka KufaBageni alikufa!?
Siwezi kukupa bunduki kisha tarehe 15 unakuja ofisini kuomba adivansi ya mshahara, nitakufuta kazi.View attachment 2801995
Upande wa Jamhuri umelazimika kubadili hati ya mashtaka dhidi ya waliokuwa Maafisa wa Jeshi la Polisi kwa kuondoa namba za Utambulisho wao ambazo ni F 7149 D/ Coplo Ramadhani (42), G. 7513 D/ Coplo Majid Abdallah na WP 6582 D/ Coplo Stela Mashaka ambapo sasa wameshtakiwa kwa majina yao halisi bila ajira za Kipolisi.
Awali, wote kwa pamoja wakiwa Waajiriwa na Jeshi la Polisi kwa nafasi za Askari Kanzu (Askari Wasiovaa Sare za Jeshi) wenye vyeo vya Koplo, walifikishwa Mahakamani Oktoba 31, 2023 na kusomewa shtaka moja la ungang’anyi wa kutumia Silaha .
Agosti 28, 2023 katika eneo la Kurasani, karibu na ofisi za Uhamiaji, Ilala, kwa pamoja Washtakiwa waliiba Tsh. Milioni 90 kutoka kwa Grace D. Matage baada ya kumtishia Bunduki. Hata hivyo wamekana Mashtaka na kurudishwa Mahabusu kwasababu kosa hilo halina dhamana na kesi imeahirishwa hadi Novemba 13, 2023.
==============
Serikali imefanya mabadiliko katika hati ya mashtaka ya shitaka linalowakabili maofisa watatu wa Jeshi la Polisi kwa kuondoa namba zao za utambulisho wa ajira.
Maofisa hao wanakabiliwa na shtaka moja la unyang’anyi wa kutumia silaha na kuiba Sh90 milioni, mali ya Grace Matage.
Kufuatia mabadiliko hayo, sasa hati mpya ya mashtaka itasomeka kama waliokuwa askari Polisi, baada ya kuvuliwa namba zao za utambulisho wa ajira na wamefukuzwa kazi na mwajiri wao, ambaye ni Jeshi la Polisi.
Wakili Serikali, Erick Kamala amewataja washtakiwa hao, kuwa ni Ramadhani Tarimo (42) maarufu kama Rasta na mkazi wa Kipawa;Majid Abdallah (35) mkazi wa Kunduchi na Stela Mashaka, ambao wote walikuwa waajiriwa na jeshi la Polisi na walikuwa askari kanzu wenye vyeo vya koplo.
Itakumbukwa kuwa Oktoba 31, 2023, washtakiwa hao walifikishwa mahakamai hapo na kusomewa shtaka moja la ungang’anyi wa kutumia silaha pamoja namba zao za utambulisho wa ajira kutoka jeshi hilo la Polisi.
Siku hiyo, washtakiwa hao walisomewa majina na mamba zao ambazo ni F 7149 D/ Coplo Ramadhani (42) maarufu kama Rasta; G. 7513 D/ Coplo Majid Abdallah (35) mkazi wa Kunduchi na WP 6582 D/ Coplo Stela Mashaka.
Wakili Kamala, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Alhamsi Novemba 2, 2023, kuwa kesi hiyo ililetwa kwa ajili ya upande wa mashtaka kufanya mabadiliko ya hati ya mashtaka kwa kuondoa namba zao za ajira askari hao.
Kamala amedai mbele ya hakimu Mkazi Mkuu, Amiri Msumi, kuwa upande wa mashtaka unaomba kufanya mabadiliko katika hati ya mashtaka chini ya kifungu namba 234(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), sura ya 20, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.
Wakili Kamala baada ya kueleza hayo, aliwasomewa upya shtaka lao, ikiwemo majina yao bila kutaja namba zao za ajira.
Akiwasomewa shtaka lao, wakili Kimala, alidai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na kesi ya jinai namna 197/2023.
Alidai washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo, Agosti 28, 2023 katika eneo la Kurasani, karibu na ofisi za Uhamiaji, lililopo wilaya ya Ilala, ambapo siku hiyo ya tukio, washtakiwa kwa pamoja waliiba Sh90 milioni kutoka kwa Grace Donald Matage.
Ameendelea kudai mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kabla na baada ya kufanya wizi huo, walimtishia Grace kwa bunduki ili waweze kujipatia fedha hizo bila kikwazo.
Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka linalowakabili walikana.
Upande wa mashtaka wamedai kuwa bado wanaendelea na upelelezi wa shauri hilo, hivyo wanaiomba Mahakama hiyo, ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Hakimu Msumi amewaambia washtakiwa hao, kuwa shtaka linalowakabili halina dhamana kwa mujibu wa sheria hivyo, wataendelea kubaki rumande.
Baada ya kueleza hayo, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 13, 2023 itakapotajwa na washtakiwa wamerudishwa rumande.
MWANANCHI
Kwahiyo walioshtakiwa ni wale wa awali waliochukua 90m au wa mara ya pili wengine waliochukua 50m akiwa na mmojawapo wa wale aliyechukua 90m awali?Hao ni tamaa tu iliwaponza. Habari iliyopo ni kwamba awali walishachukua 90m kwa makubaliano yenye kunufaisha pande mbili yaani mtoaji na wapokeaji ili kuzima jambo. Mmoja wao katika hao waliochukua 90m akaona deal na kuwatafuta wenzie wapya ili waibuke upya kwa mtoaji. Mtoaji akalazimika kutoa zaidi 50m lakini pasipo kuridhika. Baada ya hapo mtoaji akapanda juu na "kupanga mipango".
Ila polisi kwa michezo haramu wamo sana. Wenyewe wanaita DiliView attachment 2801995
Upande wa Jamhuri umelazimika kubadili hati ya mashtaka dhidi ya waliokuwa Maafisa wa Jeshi la Polisi kwa kuondoa namba za Utambulisho wao ambazo ni F 7149 D/ Coplo Ramadhani (42), G. 7513 D/ Coplo Majid Abdallah na WP 6582 D/ Coplo Stela Mashaka ambapo sasa wameshtakiwa kwa majina yao halisi bila ajira za Kipolisi.
Awali, wote kwa pamoja wakiwa Waajiriwa na Jeshi la Polisi kwa nafasi za Askari Kanzu (Askari Wasiovaa Sare za Jeshi) wenye vyeo vya Koplo, walifikishwa Mahakamani Oktoba 31, 2023 na kusomewa shtaka moja la ungang’anyi wa kutumia Silaha .
Agosti 28, 2023 katika eneo la Kurasani, karibu na ofisi za Uhamiaji, Ilala, kwa pamoja Washtakiwa waliiba Tsh. Milioni 90 kutoka kwa Grace D. Matage baada ya kumtishia Bunduki. Hata hivyo wamekana Mashtaka na kurudishwa Mahabusu kwasababu kosa hilo halina dhamana na kesi imeahirishwa hadi Novemba 13, 2023.
==============
Serikali imefanya mabadiliko katika hati ya mashtaka ya shitaka linalowakabili maofisa watatu wa Jeshi la Polisi kwa kuondoa namba zao za utambulisho wa ajira.
Maofisa hao wanakabiliwa na shtaka moja la unyang’anyi wa kutumia silaha na kuiba Sh90 milioni, mali ya Grace Matage.
Kufuatia mabadiliko hayo, sasa hati mpya ya mashtaka itasomeka kama waliokuwa askari Polisi, baada ya kuvuliwa namba zao za utambulisho wa ajira na wamefukuzwa kazi na mwajiri wao, ambaye ni Jeshi la Polisi.
Wakili Serikali, Erick Kamala amewataja washtakiwa hao, kuwa ni Ramadhani Tarimo (42) maarufu kama Rasta na mkazi wa Kipawa;Majid Abdallah (35) mkazi wa Kunduchi na Stela Mashaka, ambao wote walikuwa waajiriwa na jeshi la Polisi na walikuwa askari kanzu wenye vyeo vya koplo.
Itakumbukwa kuwa Oktoba 31, 2023, washtakiwa hao walifikishwa mahakamai hapo na kusomewa shtaka moja la ungang’anyi wa kutumia silaha pamoja namba zao za utambulisho wa ajira kutoka jeshi hilo la Polisi.
Siku hiyo, washtakiwa hao walisomewa majina na mamba zao ambazo ni F 7149 D/ Coplo Ramadhani (42) maarufu kama Rasta; G. 7513 D/ Coplo Majid Abdallah (35) mkazi wa Kunduchi na WP 6582 D/ Coplo Stela Mashaka.
Wakili Kamala, ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo Alhamsi Novemba 2, 2023, kuwa kesi hiyo ililetwa kwa ajili ya upande wa mashtaka kufanya mabadiliko ya hati ya mashtaka kwa kuondoa namba zao za ajira askari hao.
Kamala amedai mbele ya hakimu Mkazi Mkuu, Amiri Msumi, kuwa upande wa mashtaka unaomba kufanya mabadiliko katika hati ya mashtaka chini ya kifungu namba 234(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA), sura ya 20, iliyofanyiwa marekebisho mwaka 2022.
Wakili Kamala baada ya kueleza hayo, aliwasomewa upya shtaka lao, ikiwemo majina yao bila kutaja namba zao za ajira.
Akiwasomewa shtaka lao, wakili Kimala, alidai kuwa washtakiwa wanakabiliwa na kesi ya jinai namna 197/2023.
Alidai washtakiwa wanadaiwa kutenda kosa hilo, Agosti 28, 2023 katika eneo la Kurasani, karibu na ofisi za Uhamiaji, lililopo wilaya ya Ilala, ambapo siku hiyo ya tukio, washtakiwa kwa pamoja waliiba Sh90 milioni kutoka kwa Grace Donald Matage.
Ameendelea kudai mahakamani hapo kuwa washtakiwa hao kabla na baada ya kufanya wizi huo, walimtishia Grace kwa bunduki ili waweze kujipatia fedha hizo bila kikwazo.
Washtakiwa baada ya kusomewa shtaka linalowakabili walikana.
Upande wa mashtaka wamedai kuwa bado wanaendelea na upelelezi wa shauri hilo, hivyo wanaiomba Mahakama hiyo, ipange tarehe nyingine kwa ajili ya kutajwa.
Hakimu Msumi amewaambia washtakiwa hao, kuwa shtaka linalowakabili halina dhamana kwa mujibu wa sheria hivyo, wataendelea kubaki rumande.
Baada ya kueleza hayo, aliahirisha kesi hiyo hadi Novemba 13, 2023 itakapotajwa na washtakiwa wamerudishwa rumande.
MWANANCHI
Hili Jeshi la polisi linahitaji maboresho ya lazima. Maana lina mapungufu mengi sana.
Mkuu wewe utakuwa umeajiriwa mwenzako kajiajiri.Duh mtoaji pesa zote hizo za nini au kuna biashara haramu ilikuwa inaendelea
Polisi wanadhurumiwa sana posho zao,polisi wakienda kwenye operation pamoja na Wanajeshi kwenye kulipwa posho utakuta wenzao wanajeshi wanalipwa laki tatu, wao polisi wana lipwa elfu 30, Kwenye kusaini posho wanakuta imeandikwa elf 30 na wakisha maliza kusaini mabosi wao wanaongeza sifuri, kwenye kila laki tatu polisi anaporwa laki mbili na sabini.hakuna cha maboresho wala maboshori,walipwe pesa zinazoeleweka.
tunakoelekea matukio kama haya yatanawiri sana.
Mimi ni joblessMkuu wewe utakuwa umeajiriwa mwenzako kajiajiri.
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Polisi wanadhurumiwa sana posho zao,polisi wakienda kwenye operation pamoja na Wanajeshi kwenye kulipwa posho utakuta wenzao wanajeshi wanalipwa laki tatu, wao polisi wana lipwa elfu 30, Kwenye kusaini posho wanakuta imeandikwa elf 30 na wakisha maliza kusaini mabosi wao wanaongeza sifuri, kwenye kila laki tatu polisi anaporwa laki mbili na sabini.
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Yani polisi ni jeshi la kipuuzi kweli, yaani Jeshi linaendeshwa kama kampuni ya Ulinzi, utakuta askari kapanda cheo lakini mshahara haupandi, yani askari anaweza akatumikia cheo kipya bila kubadilishiwa mshahara kwa miaka kumi na bila kufuatilia anaweza kulipwa mshahara wa private wakati ni sagent.ni taasisi pekee ambayo imekosa usimamizi kabisa,inajiendea tu na hakuna anayeona hatari iliyopo.
Yani polisi ni jeshi la kipuuzi kweli, yaani Jeshi linaendeshwa kama kampuni ya Ulinzi, utakuta askari kapanda cheo lakini mshahara haupandi, yani askari anaweza akatumikia cheo kipya bila kubadilishiwa mshahara kwa miaka kumi na bila kufuatilia anaweza kulipwa mshahara wa private wakati ni sagent.
Sent from my TECNO BB2 using JamiiForums mobile app
Ulichosema kina angalau 20% ya ukweli wa hii kesi. Lakini, kimsingi kuna jambo nyuma ya pazia ambalo linaendelea. Tuendelee kufuatilia hii kesi lakini, kwa kuziweka hai na kuziongezea tamaa ya kufikiri akili zetu, tunapaswa kujua kwanza kwamba hawa watuhumiwa walikua askari kanzu kitengo cha kupambana na dawa za kulevya. Hii pengine itasaidia kufungua baadhi ya code.Hao ni tamaa tu iliwaponza. Habari iliyopo ni kwamba awali walishachukua 90m kwa makubaliano yenye kunufaisha pande mbili yaani mtoaji na wapokeaji ili kuzima jambo. Mmoja wao katika hao waliochukua 90m akaona deal na kuwatafuta wenzie wapya ili waibuke upya kwa mtoaji. Mtoaji akalazimika kutoa zaidi 50m lakini pasipo kuridhika. Baada ya hapo mtoaji akapanda juu na "kupanga mipango".