#COVID19 Dar: Askofu Ruwai’chi aagiza mapadri wote kupata chanjo dhidi ya UVIKO-19

#COVID19 Dar: Askofu Ruwai’chi aagiza mapadri wote kupata chanjo dhidi ya UVIKO-19

Kiunyenyekevu angetoa wito au ushauri mapadre wachanje sio Agizo! HAPANA!
 
Hawa jamaa ndiyo weupee hawana nguvu ya Mungu ujanja2 tu. Sijui kwanini wanaitwa baba!
 
Tulimwomba Mungu awajalie utashi wanasayansi ili chanjo ipatikane mapema. Tumepata mapema, tena tunaanza kuhoji.

Wana wa Mungu, tumshukuru Mungu kwa kuwa amesikia sala na maombi yetu, tukachanjwe..

Nilichanjwa wiki 3 zilizopita. Nilikiuka masharti kidogo, baada ya kuchanjwa sikusubiri dakika 30 kama wanavyoshauri. Kwa sababu nilikuwa safarini, nilchanjwa na kuingia kwenye gari, nikaendesha umbali wa kilometa 600 kwa masaa 8. Nimeendelea na kazi zangu kama kawaida. Bega kidogo lilinisumbua kwa maumivu siku ya pili na ya tatu. Na siku moja nilisikia homa kidogo, otherwise I am perfect 100%.
Sawa, hongera kwa hilo ila chanjo ni hiari.
 
Askofu anatoa agizo mapadre wote wachanjwe? Hata Papa hajatoa agizo popote! Kiukweli hilo agizo linastua sana! Seems ukichanja unatamani kila mtu achanje na wala si tu kwa nia njema bali kibinadamu tuna hulka hiyo.

Askofu hili haupo sawa. Mapadre watakupinga waziwazi na kuingiza Kanisa kwenye mgogoro ambao hukuutegemea. Kwanza unawaambia waache "utoto" kweli? Unafikiri kwa nafasi yako ya uaskofu maana yake umezidi mapadre wote akili?

Nimesikiliza hiyo hotuba nikawa very disappointed [emoji20] na Askofu wetu huyu.

Chanjo ni hiari, kama serikali inasema ni hiari wewe kiongozi wa dini unasema lazima? Kesho serikali ikiongoza kwa imla utapinga wewe? Very disappointed [emoji20]
Wewe Muumini wa Father Nkwera tulia
 
Sema tu ni maagizo Toka Roma.
Wewe mwenyewe unajua ukweli hata ukichanjwa Corona itakuua tu.

Wafanyabiashara maarufu waliokufa karibuni kwa nature ya kazi zao,ni ukweli usiopingika kuwa walichanjwa lakini Israel amewapitia.
 
Uko disappointed wewe mwenyewe. Ruwaichi msimamo wake dhidhi ya Corona aliuweka wazi, Mpaka JPM akamnanga Kiaina.. Jamaa alishahimiza sana Tahadhari dhidhi ya covid kitambo.. Huu ni muendelezo
Usibishane na huyo mfuasi wa Kayafa Jiwe,anaendeleza upumbuvu wa Mwendazake.
 
Askofu anatoa agizo mapadre wote wachanjwe? Hata Papa hajatoa agizo popote! Kiukweli hilo agizo linastua sana! Seems ukichanja unatamani kila mtu achanje na wala si tu kwa nia njema bali kibinadamu tuna hulka hiyo.

Askofu hili haupo sawa. Mapadre watakupinga waziwazi na kuingiza Kanisa kwenye mgogoro ambao hukuutegemea. Kwanza unawaambia waache "utoto" kweli? Unafikiri kwa nafasi yako ya uaskofu maana yake umezidi mapadre wote akili?

Nimesikiliza hiyo hotuba nikawa very disappointed [emoji20] na Askofu wetu huyu.

Chanjo ni hiari, kama serikali inasema ni hiari wewe kiongozi wa dini unasema lazima? Kesho serikali ikiongoza kwa imla utapinga wewe? Very disappointed [emoji20]
Usilazimishe lisilokuhusu. Hapo anaongea na vijana wake. Yeye.kahamasisha na hajamsema mtu au hajamlazimisha mtu kuchanjwa. Mapadre ni waelewa sio wapenda sifa na ligi kuona Nani mshindi. Neno acha utoto maana yake ni umri ambao binadamu anaupenda sana. Ukiambiwa utoto unakasirika ujana unakasirika, uzee unakasirika, Sasa upo hatua gani mzee baba? Au upo hatua ya Masters katika hatua ya ukuaji.

Kwanza wanakushangaa kauli zako za kichochezi. Huwezi kugombanisha hii nyumba ni ngumu sana. Ogopa anaekusikiliza huku ameinamisha kichwa, akinyanyua kichwa na kukuangalia usoni utafute shimo haraka lakujificha.

Tusaidiane katika kumwondoa huyu mdudu atoweke.
 
View attachment 1906131
PICHA: Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi

Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi ameagiza mapadri wote wa jimbo hilo kupata chanjo dhidi ya Uviko 19 kwa kuwa ugonjwa huo unaumiza na kuondoa uhai.

Ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 24, 2021 katika adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea Padri Paul Haule aliyekuwa Paroko Msaidizi katika Parokia ya Mtakatifu Petro na Mkurugenzi wa Tumaini Media.

Ruwai’chi amesema mwaka 2020 wakati wa awamu ya kwanza ya janga la Uviko-19 watu walimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo, ambayo sasa imepatikana.

“Tulimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo sasa imepatikana badala ya kutumika watu wameingia katika malumbano ya kusema haya na yale dhidi ya chanjo,” amesema.

“Tusingojee hadi mambo haya yatutinge, tutumie vizuri fursa alizotupa Mungu kujikinga na kujihami na kwa sababu hiyo, sijui ni mapdri wangapi ambao mmeshachanjwa, lakini leo naomba nitoe agizo, kila padre akachanjwe, kila padre akachanjwe, tusifanye utoto, tusifanye lelemama, hii uviko 19 haina mjomba na shemeji na inatuondolea uhai,” amesema Ruwai’chi

Amesema ni utashi wa Mungu kwa watu wawe hai na kuwa na uhai tele hivyo ni vyema kuujali uhai waliopewa.

“Tujihami na tuendelee kumuomba Mungu, atuhurumie na tujihami na atuondolee hili janga,” amesema Ruwai’chi.

Mwananchi
Now, this is HUGE!
 
Anajua anayemtumikia, naye hanaga hiari bali lazima...neno linasema, ataonekana kama kondoo lakini anaongea kama joka...
Hakika tutawajua kwa matunda yao kama kweli kweli imo ndani yao. Binafsi nimeshangazwa na agizo hili. Lakini sitashangaa sana kutokana na matendo mengine ya nyuma, huu ni mwendelezo tu.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
View attachment 1906131
PICHA: Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi

Askofu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Yuda Tadheus Ruwai’chi ameagiza mapadri wote wa jimbo hilo kupata chanjo dhidi ya Uviko 19 kwa kuwa ugonjwa huo unaumiza na kuondoa uhai.

Ametoa agizo hilo leo Jumanne Agosti 24, 2021 katika adhimisho la Misa Takatifu ya kumuombea Padri Paul Haule aliyekuwa Paroko Msaidizi katika Parokia ya Mtakatifu Petro na Mkurugenzi wa Tumaini Media.

Ruwai’chi amesema mwaka 2020 wakati wa awamu ya kwanza ya janga la Uviko-19 watu walimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo, ambayo sasa imepatikana.

“Tulimuomba Mungu ajaalie kupatikana kwa chanjo sasa imepatikana badala ya kutumika watu wameingia katika malumbano ya kusema haya na yale dhidi ya chanjo,” amesema.

“Tusingojee hadi mambo haya yatutinge, tutumie vizuri fursa alizotupa Mungu kujikinga na kujihami na kwa sababu hiyo, sijui ni mapdri wangapi ambao mmeshachanjwa, lakini leo naomba nitoe agizo, kila padre akachanjwe, kila padre akachanjwe, tusifanye utoto, tusifanye lelemama, hii uviko 19 haina mjomba na shemeji na inatuondolea uhai,” amesema Ruwai’chi

Amesema ni utashi wa Mungu kwa watu wawe hai na kuwa na uhai tele hivyo ni vyema kuujali uhai waliopewa.

“Tujihami na tuendelee kumuomba Mungu, atuhurumie na tujihami na atuondolee hili janga,” amesema Ruwai’chi.

Mwananchi
katumwa huyo
 
Usichanganye Ukatoliki na agizo la Askofu labda hujui Ukatoliki ni nini! Hilo ni agizo lake binafsi kwa muono wake.

He is very wrong bora angekaa kimya na wengine tulifikiri ukimya wao una ujumbe au pengine kuna utafiti wanafanya maana nyenzo wanazo.

Mimi binafsi sikubaliani nae! Kwa ufupi hili agizo na namna alivyolitoa kama umesikiliza mapadre watampinga... Mark my word.
🤣 🤣 🤣 🤣Mbona mnateseka sana mkisikia watu wanachanjwa? Wewe ni padri? Hili agizo linakuhusu?
 
Askofu anatoa agizo mapadre wote wachanjwe? Hata Papa hajatoa agizo popote! Kiukweli hilo agizo linastua sana! Seems ukichanja unatamani kila mtu achanje na wala si tu kwa nia njema bali kibinadamu tuna hulka hiyo.

Askofu hili haupo sawa. Mapadre watakupinga waziwazi na kuingiza Kanisa kwenye mgogoro ambao hukuutegemea. Kwanza unawaambia waache "utoto" kweli? Unafikiri kwa nafasi yako ya uaskofu maana yake umezidi mapadre wote akili?

Nimesikiliza hiyo hotuba nikawa very disappointed [emoji20] na Askofu wetu huyu.

Chanjo ni hiari, kama serikali inasema ni hiari wewe kiongozi wa dini unasema lazima? Kesho serikali ikiongoza kwa imla utapinga wewe? Very disappointed [emoji20]
Ukisikia kanisa la wasomi, kanisa la kweli ndilo hili sasa. Siyo hivi vibushuti vya kuokoteza vinavyojipachika uaskofu vinavyodanganya watu wakichanjwa watageuzwa ndondocha. Askofu ni kiongozi wa kanisa na ameshuhudi kwa macho yake jinsi mapadri wake waliathirika na UVIKO. Chanjo imekuja anawahimiza kuchanja, kuna ubaya huko ng'ambo kwenu?
 
Askofu anatoa agizo mapadre wote wachanjwe? Hata Papa hajatoa agizo popote! Kiukweli hilo agizo linastua sana! Seems ukichanja unatamani kila mtu achanje na wala si tu kwa nia njema bali kibinadamu tuna hulka hiyo.

Askofu hili haupo sawa. Mapadre watakupinga waziwazi na kuingiza Kanisa kwenye mgogoro ambao hukuutegemea. Kwanza unawaambia waache "utoto" kweli? Unafikiri kwa nafasi yako ya uaskofu maana yake umezidi mapadre wote akili?

Nimesikiliza hiyo hotuba nikawa very disappointed [emoji20] na Askofu wetu huyu.

Chanjo ni hiari, kama serikali inasema ni hiari wewe kiongozi wa dini unasema lazima? Kesho serikali ikiongoza kwa imla utapinga wewe? Very disappointed [emoji20]
Mapadre na watumishi wengi wa Kanisa, wapo katika kundi linalohudumia mamia ya watu.

Ni uamuzi mzuri na wa busara sana kama Mapadre watafuata muongozo wa Baba Askofu.
 
Kiunyenyekevu angetoa wito au ushauri mapadre wachanje sio Agizo! HAPANA!
Wewe hujui chochote kuhusu Kanisa katoliki. Toka lini askofu wa jimbo husika akatoa ushauri kwa mapadre wa jimbo lake. Siku zote askofu huwa anatoa 'maagizo' na sio 'ushauri' kwa walio chini yake.
Na kamwe haiwezi tokea wala haitokaa itokee chini ya jua akatokea 'Padre wa Kanisa katoliki' akampinga 'Askofu wa kanisa katoliki' HADHARANI.
Narudia haijawah tokea na wala haitokaa itokee padre ampinge Askofu wa jimbo lake. Ndivyo ilivyo na itabaki kuwa hivyo. Wamefunzwa nidhamu ya hali ya juu miaka yao yote wakiwa seminari ndogo mpaka seminari kuu.
Migogoro itabaki ndani ya madhehebu madogo madogo au taasisi nyingine lakini si ndani ya Kanisa Katoliki. Askofu Awe amekosea au awe hajakosea itabaki kuwa maoni kwako na kwa wengineo ila kwa Mapdre watatii amri yake na maisha yataendelea. Hutokaa usikie malumbano au mgogoro wa aina yoyote ile kwa kanisa katoliki. Ndo imetoka hiyo. Ni suala la nidhamu. Agizo limetoka na litatekelezwa na Mapadre wote walio chini yake. Malumbano yatabaki kwa kina Gwajima lakini si kwa Kanisa katoliki
 
Askofu anatoa agizo mapadre wote wachanjwe? Hata Papa hajatoa agizo popote! Kiukweli hilo agizo linastua sana! Seems ukichanja unatamani kila mtu achanje na wala si tu kwa nia njema bali kibinadamu tuna hulka hiyo.

Askofu hili haupo sawa. Mapadre watakupinga waziwazi na kuingiza Kanisa kwenye mgogoro ambao hukuutegemea. Kwanza unawaambia waache "utoto" kweli? Unafikiri kwa nafasi yako ya uaskofu maana yake umezidi mapadre wote akili?

Nimesikiliza hiyo hotuba nikawa very disappointed [emoji20] na Askofu wetu huyu.

Chanjo ni hiari, kama serikali inasema ni hiari wewe kiongozi wa dini unasema lazima? Kesho serikali ikiongoza kwa imla utapinga wewe? Very disappointed [emoji20]
Fuatilia mambo mkuu.

Papa alishashauri na alishasisititiza watu wachanjwe.
Screenshot_20210824-163303_1.jpg
 
Back
Top Bottom