DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika

DAR: Barabara 9 kufungwa kwa siku sita kupisha mkutano wa madini chini ya Viongozi kadhaa wa Afrika

Wangesema njia mbadala ni ipi ili watumiaji wa
hizo barabara wasihangaike
labda angani mkuu, mfano mtu anatoka Chanika anaelekea city centre atapita njia ipi nyingine ukiondoa Nyerere road
 
JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Polisi Dar es Salaam imetangaza kuwa Barabara tisa Jijini Dar es Salaam, zimefungwa kwa siku sita kuanzia leo Januari 25 hadi Januari 30, 2025 ili kupisha misafara ya viongozi wanaokuja kutoka nchi mbalimbali kuhudhuria mkutano wa Nishati Afrika.

Taarifa ya Polisi iliyotolewa leo Jumamosi Januari 25,2025 na Kamanda Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Jumanne Muliro, imesema Mkutano huo utakaofanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Januari 27 hadi Januari 28, 2025, unatarajiwa kuhudhuriwa na zaidi ya marais 25 na mawaziri 60 kutoka nchi mbalimbali za Afrika ambapo pia bajaji na bodaboba hazitaruhusiwa kuingia katikati ya Jiji katika kipindi chote ambacho mkutano huo utakuwa ukifanyika.

Barabara zitakazofungwa ni pamoja na Barabara ya Nyerere kutokea Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwenda katikati ya Jiji, Barabara ya Sokoine, Kivukoni na Lithuli kuanzia taa za Gerezani kwenda Hoteli ya Johari Rotana, Hyatt Regency hadi Ikulu; Barabara ya Ohio kutokea Kivukoni kwenda Hoteli ya Serena na Barabara ya Ghana kutokea barabara ya Ohio kwenda Hoteli ya Onomo

Zingine ni Barabara ya Bibi Titi kutokea makutano ya barabara za Ohio na Ally Hassan Mwinyi kwenda Hoteli ya Crowne; Barabara ya Azikiwe kwenda Hoteli ya Four Points, Hoteli ya Golden Tulip City Center na Hoteli ya Holiday Inn; Barabara ya Morogoro kutokea Sokoine kwenda Hoteli ya Tiffany No. 1; Barabara ya Makunganya kutokea Azikiwe kwenda Hoteli ya Tiffany No. 2 na Barabara ya Garden kutokea barabara ya Lithuli kwenda Hoteli ya Southern Sun pamoja na Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa JNICC.

sisi wa Mandela na Kawawa tuendelee kugonga glass🥂

#KitengeUpdates
Watoto,wagonjwa na walemavu mmeweza kuwafikiria kuwa watapitia njia zipi ili wapate huduma?
 
Yaani hii moja tu ni tatizo. Watu wa Goms sijui wataendaje makazini.
Aisee mbna ni wapuuzi hvyo utakuta hapo ni mtu mmoja tu kalala kaamka ndo kaja na maamuzi hayo ya hovyo
sasa watu watapitia wapi ?
kwann wasifunge njia moja wakaruhusu njia nyingine itumike wakaacha watu wapite sasa unafunga njia MUHIMU kabisa na hakuna mkatisho unless upitie kinyerezi TABATA ukitokea GMBOTO atilist wangefunga kuanzia TAZARA kwenda CITY CENTRE kuna option za kupita kwa hiyo watu wa JETI wazungukie BUZA huko
na Gari za G/MBOTO TANDIKA zitapitia wapi ? tabata au zizungukie MWANAGATI

kwann wasingefunga labda kuanzia muda fulani mpk muda fulani hii barabara muhimu sana
katika MAISHA sikuwahi kuona ikifungwa hata kwa siku yote nzima
zaidi ya zille siku Kuompkea NYERERE alivyofariki na kipindi cha MARAISI wa marekani walivyokuja tena ilifungwa kwa masaa kadhaa kipindi waliyokuwa wanawasili na kuondoka

tuna VIONGOZI wa hovyo sana
 
Huu ni usumbufu mkubwa sana usio na ulazima wowote,Shughuli nyingi za uchumi zitavurugwa.Hao wageni wangetumia chopa toka Airport hadi Ikulu, ukumbi wa mkutano na hotelini
 
Aisee sasa watu watapitia wapi
kwann wasifunge njia moja wakaruhusu njia nyingine itumike wakaacha watu wapite sasa unafunga njia MUHIMU kabisa na hakuna mkatisho unless upitie kinyerezi TABATA ukitokea GMBOTO atilist wangefunga kuanzia TAZARA kwenda CITY CENTRE kuna option za kupita kwa hiyo watu wa JETI wazungukie BUZA huko
na Gari za G/MBOTO TANDIKA zitapitia wapi ? tabata au zizungukie MWANAGATI

kwann wasingefunga labda kuanzia muda fulani mpk muda fulani hii barabara muhimu sana
katika MAISHA sikuwahi kuona ikifungwa hata kwa siku yote nzima
zaidi ya zille siku Kuompkea NYERERE alivyofariki na kipindi cha MARAISI wa marekani walivyokuja tena ilifungwa kwa masaa kadhaa kipindi waliyokuwa wanawasili na kuondoka

tuna VIONGOZI wa hovyo sana
Mkuu, yaani usumbufu utakao tokea iyo siku nadhani itakua historia. Tena hao Marais na Mawaziri wageni nadhani watakuja mida tofauti tofauti kwahiyo kuna uwezekano road ikafungwa siku nzima.
 
labda angani mkuu, mfano mtu anatoka Chanika anaelekea city centre atapita njia ipi nyingine ukiondoa Nyerere road
Treni au unaambaa sambamba na reli ya kati unatokea buguruni, ilala kkoo hii hapa, tambuka taa mnazi mmoja chugua waenda wapi Barclays ya Ohio au pale Twin Tower?
 
Mkuu, yaani usumbufu utakao tokea iyo siku nadhani itakua historia. Tena hao Marais na Mawaziri wageni nadhani watakuja mida tofauti tofauti kwahiyo kuna uwezekano road ikafungwa siku nzima.
acha tu mkuu wangu
UISLAM ulisema hivi
MWANAMKE amepewa DARAJA LA KWANZA katika kila kitu DUNIANI na AKHERA
lakini akanyimwa UONGOZI
Kwa maana MWANAMKE afai kuwa KIONGOZI afai kabisa

ndio mana hata WAMAREKANI hawakukubari UPUUZI huo

kama anajiamini aweka TUME HURU YA UCHAGUZI Halafu aone kitakachomkuta ndo mana alivyoambiwa aende NJE kagoma alijua WAJUMBE wangekinukisha
 
Back
Top Bottom