Dar es Salaam: Askari 300 waongezwa kudhibiti panya road

Dar es Salaam: Askari 300 waongezwa kudhibiti panya road

Wanauwa watu halafu uogope retaliation eti haki za binadamu !! Wao mbona hawaogopi haki za binadamu ???!
Unakumbuka lile tukio huko kenya
Yule askari Ahmed rashid,alimtandika
Dogo mmj mbele ya umati risasi
Yule dogo alikuwa gangster na alishashindikana.....
Ah watu walimwambia tu Yule dogo sasa popote ukatapoonekana,uhai wako tunauchkua ...mbn walimmaliza
Police inabd iwe na watu dizain ya Ahmed rashid....yaani mtu mwenye file chaf,hasiki hataki kuacha uhalifu au kubadilika wao ni kumngoa tu
Hata Brazil police wao maalum wanafanya sana hiyo,maana kuna watu wTukutuku hawasiki..

Ova
 
Umeongea kitu sahihi kabisa.

Kutatua hili tatizo ni lazima kuliangalia kuanzia kwenye mzizi wake(Malezi ya watoto). Jamii tumejisahau sana katika hili.

Natoa mfano: Nili kaa mwanza mjini (Ilemela) kwa muda wa wiki 2 hivi hapo mwezi wa tatu mwaka huu, nilishangaa kukuta idadi kubwa ya watoto umri kati ya miaka 10 - 15 wakizagaa zagaa mitaani kutafta msaada wa chakula, hii ikimanisha hakuna mtu wa kuwasiamia au hawataki kusimamiwa na wametoroka nyumbani. Na mara nyingi watu wamekua wakiwafukuza wasionekane kwenye maeneo yao.

Ukiwatazama zaidi ubagundua wengi wao wameacha shule mapema kabisa au hawajawai kwenda shule kabisa.Kuna watu wanaleta siasa kua hao vijana wamekosa ajira binafsi sikubaliani nao na hata ksma wapo walio soma wakosa ajira ndo waamue kujiunga huko basi hao wamekosa sifa kabisa kuajiriwa popote. Issue ni kwamba vijana hawa washakata tamaa hakuna future wanayoiona mbele kwao kuishi na kufa yote sawa tu ndo mana wako hivo.

Sasa jiulize mtoto kama hyu akikua kufikia miaka 18 akakutana na ushawishi wa genge lolote la kiuhalifu, sidhani kama atakua na chembe ya huruma kwa jamii ambayo haikuonyesha kumjali kipindi chote alipo kua anakua.

Na kiukweli hao panya road wakipata support ya kisiasa let's say Alshababu au Jirani yetu EA asiependa amani kwa majirani zake, akawaongezea nguvu(Silaha + Mafunzo kdg) kwa kweli miji mingi itakua haikaliki.

Nguzo ya malezi izingatiwe kwenye jamii zetu. Iwe ni kosa kabisa kukuta mtoto chini ya miaka 15 anazagaa mtaani, halmashauri zitenge fungu kabisa la kuchukua hawa vijana na kuwawekea mazingira rafiki kwao. Nje ya hayo yajayo yanafurahisha.

Sent from my CPH1819 using JamiiForums mobile app
Baba za watoto hao wamo humu wanashangilia POLICE waende kuwauwa!!!!!!

Serikali imetokana na wananchi.

Wananchi ndo wanawaajiri Rais, Wabunge, Waziri wa Ulinzi nk.

Tusiwape tiketi ASKARI kuua raia, Lissu ilikuwa hivyo hivyo .

Tuwawajibishe Viongozi waliobeba dhamana Kwa kushindwa kulinda RAIA na Mali zao.

JAMII pia ijiangalie ilipokosea, tusiruhusu Damu kumwagika ktk Nchi

Ameeeen.
 
Hawa wanaharakati humu wanaandika kama wanavuta bangi hawana tofauti kabisa na panyaroad.
Nasema police ikikamata hawa mbwa ni kupiga mpaka kifo hakuna kuonea huruma wauaji wa raia wasio na hatia.

Kama ndugu yako ni panyaroad hata mimi nikimshika napiga vilevile. navunja na miguu.
 
Vijana hujiingiza kwenye makundi ya kihalifu baada ya kukosa ajira.
Asilimia kubwa ya panya road ni watoto na vijana kuanzia miaka 15 na kuendelea.
Watoto na Vijana ambao wengi wameishia la saba kwa kufeli au kuacha shule, ajira zinahusika vipi hapo?

Mtu mwenye elimu ya university hawezi kushika panga akaingia mitaani kuiba, kupiga watu na kuua.
 
Hao sio panya road bali ni majambazi mbona mnawapaka mafuta.
Na Hawa panya road wa KIKE wanaojiuza kuanzia miaka 10 tuwafanyeje???!

JAMII inapojivua yanapotokea matatizo ambayo chanzo ni SISI wenyewe.

Ameeen
 
Mikoa mingine mbona hawa vijana wanadhibitiwa?

========

Dar es Salaam. Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla amesema mkoa huo umeongeza askari 300 kwa ajili ya msako wa kuwakamata wahalifu maarufu 'panya road'.

Makalla ameyasema hayo leo Alhamisi Septemba 15, 2022 alipokuwa akizugumza na wananchi wa Kata ya Zingiziwa mara baada ya kutembelea ujenzi wa barabara ya Chanika -Homboza.

Amesema msako wa wahalifu huo umeanza tangu jana Alhamisi na kuwaambia wazazi ambao watapotelewa na vijana wao kuanzia leo Alhamisi wakawafuate vituo vya polisi au hospitali za wilaya.

"Hawa panya road wamezaliwa na wazazi, ni watoto wetu, na kwa kuwa baadhi mmeshidwa kuongea nao sisi tutashughulika nao na tayari tumemwaga askari 300,” amesema

"Hivyo kuanzia leo naomba mzazi au mlezi ambaye hatamuona kijana wake afike vituo vya pilisi na hospitali kubwa za wilaya ikiwemo Amana Mwananyamala, Muhimbili wodi ya Mwaisela na Temeke," amesema Mwenyekiti huyo wa kamati ya ulinzi na usalama

Hata hivyo, Makalla amesema inasikitisha ķatika matukio mawili yaliyotokea siku mbili hizo katika maeneo ya Kawe na Tabata, waliokamatwa kuhusika wengi na vijana waliotoka kutumikia vifungo vya miezi sita hadi mwaka mmoja jela.

Mwananchi
Waache waendelee kuwaficha wahalifu watawanyoosha..
 
Na Hawa panya road wa KIKE wanaojiuza kuanzia miaka 10 tuwafanyeje???!

JAMII inapojivua yanapotokea matatizo ambayo chanzo ni SISI wenyewe.

Ameeen
Oi! kama una ndugu yako ni panya road na anatembea usiku basi mwambie leo alale nyumbani au tukikamata atapigwa tu mpaka kifo.
Naona unatetea ujinga.
 
Dar ndio mkoa pekee wakazi wake wanalala na TV vyumbani mwao asubuhi wanaipeleka sebuleni
 
Asilimia kubwa ya panya road ni watoto na vijana kuanzia miaka 15 na kuendelea.
Watoto na Vijana ambao wengi wameishia la saba kwa kufeli au kuacha shule, ajira zinahusika vipi hapo?

Mtu mwenye elimu ya university hawezi kushika panga akaingia mitaani kuiba, kupiga watu na kuua.
Kwann wameshindwa kuendelea na shule secondary au kuingia veta nk.

Lipo jambo JAMII na Serikali Kwa ujumla tunajitoa uhusika.
 
kwani wale wa kipindi kile walikua panya wa michongo au waiku really?
 
Oi! kama una ndugu yako ni panya road na anatembea usiku basi mwambie leo alale nyumbani au tukikamata atapigwa tu mpaka kifo.
Naona unatetea ujinga.
Ninyi ndo watu wasiojulikana. Mnafanya KAZI Kwa Zima moto, hamuangalii CHANZO Cha tatizo Ili kulitatua once and for all!!!
 
Kwann wameshindwa kuendelea na shule secondary au kuingia veta nk.

Lipo jambo JAMII na Serikali Kwa ujumla tunajitoa uhusika.
Oi! swali gani hili la ajabu kudadadeki?
Sababu hawataki shule, mtu mzima hataki shule mpaka anatoroka nyumbani unataka umbembeleze arudi shule kama mtoto mchanga?

Maswali ya ajabu kabisa.
Police ua hawa mbwa.
 
Hivi JPM alikomeshaje hawa mapanya. Kipindi chake wote walijificha mashimoni.

Mama anawambembeleza sana hawa.
 
wawe askari mia 300 kama task force ya muda wote tena itumike akili sio kuua na kukamata watu hovyo hovyo.

isiwe kigezo cha kukamata vijana hovyohovyo na kujipatia rushwa kwa kisingizio cha Panya road baadala yake iwe operation yenye kutumia akili.
 
Tunaomba ushauri wako wa kina kifanyike nini? kama wanakaa jela miezi sita halafu wanatoka wanarudi yaleyale what shoud we do? Umesikia binti aliekatwa mapanga kawe? imagine angekua mwanao ungesjisiakiaje? dawa ya mot ni moto, police waachwe wafanyake kazi zao tusiwangilie.
Eti Hosipitali ya Mwananyamala wodi ya Mwaisela!!?? Makala aache uhuni. Hao wanatakiwa watafutwe mochuary nansio waodini. Wapuuzi mno hao
 
Ninyi ndo watu wasiojulikana. Mnafanya KAZI Kwa Zima moto, hamuangalii CHANZO Cha tatizo Ili kulitatua once and for all!!!
Nimekuuliza mwanzo:
Wewe mpaka sasa hivi umeshindwa nini kwenda kuwashitaki viongozi husiki juu ya huyo binti aliyeuliwa na panyaroad.
Sababu ni ushahidi tosha juu ya kushindwa kutimiza wajibu wao wa kulinda raia na mali zao?

Kwanini wewe usiende kushtaki hao viongozi badala unalialia hapa au huyo binti sio mwananchi wa Tanzania?
 
Oi! swali gani hili la ajabu kudadadeki?
Sababu hawataki shule, mtu mzima hataki shule mpaka anatoroka nyumbani unataka umbembeleze arudi shule kama mtoto mchanga?

Maswali ya ajabu kabisa.
Police ua hawa mbwa.
Anyway, Mungu na Akubariki.
 
Back
Top Bottom