Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Dar es Salaam: Machinga wa Karume waandamana kuelekea ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Wasema hawana imani na Viongozi. Mabomu ya machozi yarindima

Hawana imani na kiongozi gani sasa?? Viongozi wao wamachinga au mkuu wa mkoa??

Labda awe kiongozi wao ila kama ni RC hawawez kumfanya chochote kwa utawala huu wa kulindana. Labda mwendazake angewasikiliza ila pia sio kwa bashite hapo angewatoa baru.

Kwa bahati mbaya hawa wamachinga wanateseka na nahisi wataendelea kuteseka bila ya kua na mtetezi si upinzani wala serikali. Wamebaki wao kama wao, waliemtegemea hayupo tena ni HUZUNI.
 
Wanadeserve wanachokipata kwa kuwa wakati CCM inapora chaguzi walikenua meno.

Watulia hivyo hivyo sindano iingie vizuri hadi watakapopata akili ya kuikataa CCM na mambo yake yote.

Nashukuru sana Mungu kuwa leo wamepelekewa askari wa kikosi cha mbwa ambao wameenda kubomoa vile vibanda vyao ambavyo walikuwa wameshaanza kuvijenga jana.
Hii ngoma kila mtu ataisoma kwa wakati wake. Hata Ndugai hakuwa hujua ipo siku atalala na viatu.

Katiba Mpya Katiba Mpya
 
Wanadeserve wanachokipata kwa kuwa wakati CCM inapora chaguzi walikenua meno.

Watulia hivyo hivyo sindano iingie vizuri hadi watakapopata akili ya kuikataa CCM na mambo yake yote.

Nashukuru sana Mungu kuwa leo wamepelekewa askari wa kikosi cha mbwa ambao wameenda kubomoa vile vibanda vyao ambavyo walikuwa wameshaanza kuvijenga jana.
Ni kweli wote walikenua meno? Nadhani tunasema uongo hapa, yani wafanyabiashara wote wa karume wawe ccm?
 
Wanadeserve wanachokipata kwa kuwa wakati CCM inapora chaguzi walikenua meno.

Watulia hivyo hivyo sindano iingie vizuri hadi watakapopata akili ya kuikataa CCM na mambo yake yote.

Nashukuru sana Mungu kuwa leo wamepelekewa askari wa kikosi cha mbwa ambao wameenda kubomoa vile vibanda vyao ambavyo walikuwa wameshaanza kuvijenga jana.
Kwahiyo unataka kusema
Anayebomoana Aliyechoma ni mtu mmoja?

Nchi ngumu hii
 
Tuliolia kipindi cha mwendazake sasa ni wakati wa kucheka tu.

Tunataka mamalishe, machinga, wakulima & co wateseke kabisa maana ndiyo kubwa na hao ndiyo waliompa jeuri mwendazake.

Yako wapi sasa tuliwaambia wakashupaza shingo zao, acha sasa zivunjike.
Kucheka na kulia huwa ni Kwa zamu kwenye haya maisha
 
Tuliolia kipindi cha mwendazake sasa ni wakati wa kucheka tu.

Tunataka mamalishe, machinga, wakulima & co wateseke kabisa maana ndiyo kubwa na hao ndiyo waliompa jeuri mwendazake.

Yako wapi sasa tuliwaambia wakashupaza shingo zao, acha sasa zivunjike.
Wana wazalendo wao huko ccm watawatetea.
 
Tatizo watz hatupendi mabadiliko, hapo hiyo ni nafasi ya Serikali kupajenga ni eneo zuri sana wamachinga walishajengewa ile machinga complex
 
kabisa yani, hapo utakuta wote ni ccm na hata wanaoonekana kulaumu wanatupia lawama kwa awamu hii na kusema ingeluwa awamu iliyopita haya yasingetokea

Yani kiufupi hawajaona tatizo la kuongozwa na ccm
Tatizo sio ccm weka chuki na siasa zako Pemben kwani JPM alikuwa ukawa? Yaani nyie wafia vyama ndio mnachelewesha maendeleo ya nchi hii mnaonekana kujali vyama kuliko nchi.
 
Wafanyabiashara ndogondogo maarufu machinga wa soko la Karume (Mchikichini) wameandamana hadi kwenye Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla kushinikiza kiongozi huyo atoe tamko la kuwaruhusu waendelee kufanya shughuli zao kwenye soko hilo.

Wafanyabiashara hao wameandamana leo Jumatatu Januari 17, 2022 ambapo walikuwa wanaimba "Tunataka Soko letu" wakiwa wamezingira geti la ofisi hiyo, ikiwa ni siku moja imepita tangu soko hilo kuteketea kwa moto usiku wa kuamkia jana.

Wakizungumza katika tukio hilo, baadhi ya wafanyabishara hao wamesema wanafanya hivyo baada ya kukosa imani na maamuzi yaliyochukuliwa na viongozi hao huku wakionyesha kusikitishwa kwao na kitendo cha wenzao kuvunjiwa mabanda yao waliyojenga usiku wa kuamkia leo na jeshi la polisi.

Silvanus Mwakipesile amesema Mkuu wa Mkoa aliwaahidi leo saa 2:00 asubuhi angefika kwenye soko hilo kuwaona na kuwapa muongozo lakini wanashangaa kabla ya kiongozi huyo kwenda kuna watu wamevunjiwa mabanda yao na sehemu hiyo kuwekwa chini ya ulinzi mkali ukisimamiwa na Jeshi la Polisi.

"Tumekosa imani na viongozi jana alisema anakuja lakini hadi sasa hatujamuona na chakushangaza waliojenga vibanda vyao wamebomolewa, sisi hatuwezi kuwasubiri wao maisha yetu magumu watuache tujenge wenyewe ili tuendelee kufanya kazi zetu," amesema

"Siku zilizotolewa kwa ajili ya kufanya uchunguzi ni nyingi tunataka tuachwe tujenge mabanda wakati uchunguzi ukiendelea na si kubaki hivihivi tutakula Nini na tunawatoto wanatakiwa kwenda shule,"amesema Saida Mohamed


Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ng'wilabuzu Ludigija amewaomba wafanyabishara hao kuwa wavumilivu na kufuata utaratibu uliotangazwa na Serikali kwamba waiachie kamati ifanye kazi kwa siku saba na kutoa ripoti badala ya kuandamana kutaka kushindana na Serikali.

"Mnatakiwa kujiongeza pamoja na kwamba mnadai haki lakini lazima mfuate utaratibu Jana Waziri tuiachie Kamati ifanye kazi na walete ripoti tunaomba kuweni na subira,"amesema.

Jana baada ya soko hilo kuungua Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam (RC), Amos Makalla aliwataka wafanyabiasha wa soko hilo kuwa watulivu huku akiahidi kuundwa kamati ambayo itachunguza chanzo cha moto huo kwa siku 14 akipiga marufuku shughuli zozote kuendelea wakati wa uchunguzi huo.

Muda mfupi baada ya RC Makalla kutoa tamko hilo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Innocent Bashungwa aliagiza kamati hiyo kufanya uchunguzi kwa siku saba badala ya 14.

Chanzo;- Mwananchi
Uchunguzi ufanyike kwa Sikh Saba ama kumi na NNE watakuwa awakila wapi? Mtawapa hela? Uchunguzi hauwezi kufanyika huku machinga wakiendelea na biashara zao? Nina maswali kibao hapo....
 
Wanadeserve wanachokipata kwa kuwa wakati CCM inapora chaguzi walikenua meno.

Watulia hivyo hivyo sindano iingie vizuri hadi watakapopata akili ya kuikataa CCM na mambo yake yote.

Nashukuru sana Mungu kuwa leo wamepelekewa askari wa kikosi cha mbwa ambao wameenda kubomoa vile vibanda vyao ambavyo walikuwa wameshaanza kuvijenga jana.
Mwenyekiti wa machinga alikuwa anaambatana na mgombea wa CCM kila anapoenda
 
Back
Top Bottom