Uchaguzi 2020 Dar: Jeshi la Polisi lasitisha wito wake kwa Tundu Lissu, lamtaka aendelee na Kampeni zake

Uchaguzi 2020 Dar: Jeshi la Polisi lasitisha wito wake kwa Tundu Lissu, lamtaka aendelee na Kampeni zake

G Sam

JF-Expert Member
Joined
Apr 20, 2013
Posts
11,795
Reaction score
36,704


Mambosasa: Polisi tumesitisha kumuita Tundu Lissu, tunamtaka aendelee na Kampeni zake

Baada ya mgombea wa urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tundu Lissu, kukataa kuitikia wito uliotolewa na Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro, uliotolewa jana ukimtaka aripoti kituo cha Polisi Kilimanjaro.

Lissu kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika kuwa ataendelea na ratiba zake ikiwemo kikao cha mabalozi kinachofanyika leo.

“Wito wa polisi sio barua ya kirafiki ni amri kisheria, wito huo unatakiwa kueleza kosa la mtuhumiwa barua hii haielezi kosa ninaloitiwa na imepelekwa kwa Mwenyekiti wa chama, huu sio wito wa polisi kwa mujibu wa sheria, nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi kesho” ameandika Lissu kupitia kaunti yake ya Twitter.

Kwa mujibu ya barua iliyotumwa kwa Mwenyekiti wake wa Chama, Freeman Mbowe, Lissu alitakiwa kuripoti polisi 02/10/2020 kwa ajili ya mahojiano kufuatia kauli na matamshi yake ambayo amekuwa akiyatoa kwenye mikutano yake ya kampeni dhidi ya maafisa wa polisi.
Uchaguzi 2020 - Tundu Lissu: Wito wa Polisi siyo barua ya kirafiki, Nitaendelea na ratiba yangu ya kikao na mabalozi

20201002_110551.jpg
Video ya maelezo ya kamanda wa kanda maalum Lazaro Mambosasa akithibitisha kusitisha wito wa kumtaka Tundu Lissu kuripoti kwa jeshi hilo kanda ya Dar es Salaam
 
"Kanda Maalum Ya Polisi Dar Es Salaam" inahusika vipi na uhalifu wa mkoa mwingine, swala la kosa aliloitiwa (Japo halijatajwa) Mh Tundu Lissu ni mkoa wa Mara na akatakiwa ku report Kilimanjaro. Mambosasa yanamhusu nini maswala ya mikoa mingine?.

Nchi yetu jeshi la polisi limekosa weredi kabisa, viongozi wanakurupuka na kujiamulia tu anachojisikia, hawajui "TERRITORIAL JURISDICTION/MAMLAKA YA KIENEO" yanakwenda vipi na yana nguvu gani kisheria na mipaka ya mamlaka hayo.

Mambosasa anatakiwa afanye kazi kulingana na "TERRITORIAL JURISDICTION" ya eneo lake, eneo lake na mamlaka aliopewa kisheria ni ya Kanda Maalum Ya Dar Es Salaam, hana mamlaka kisheria ya kuingilia maswala ya kikazi ya mikoa mingine. Aache kukurupuka kwani atalinajisi jeshi la polisi kuonekana halifuati sheria na mamlaka. Anapaswa arudishwe darasani na apelekwe kusoma upya sheria.

Barua ingekua imetokea "MAKAO MAKUU YA POLISI" raia tusingekua na pingamizi, na tungeiheshimu, kwasababu makao makuu ya polisi wana mamlaka ya mikoa yote kisheria. Ila barua inatoka "KANDA MAALUM YA DAR ES SALAAM". Kwa hilo watuache.

Acha lissu awanyooshe hawa vibwengo wenye vyeo vikubwa bila ya kuwa na elimu ya kukidhi matakwa ya kazi yao. Nchi inaendeshwa na kikundi cha watu wachache wanaojiamulia mambo bila kufuata sheria, wanatumia mamlaka na mabavu, ila sio sheria wala haki.

Au lasivyo wakiachiwa, kesho tutasikia Mhalifu amefanya kosa la Kubaka Morogoro halafu Jeshi La Polisi Mkoa Wa Kigoma limetoa barua ya kuachiliwa mara moja mhalifu huyo.

#KUFICHA AIBU, kesho utasikia Mambosasa anaongea na vyombo vya habari na kusema barua hio inayozunguka mitandaoni imeandikwa na watu "WASIOJULIKANA", wananchi tunaombwa tuipuuze.[emoji38][emoji16]
 
Hawa policcm hawajitambui kabisa na ni aibu kubwa hadi Lissu awafundishe kazi na sheria ndio wanaelewa?! Kweli watazicheza ngoma za Lissu mwaka huu.

mkuu wangehariri barua ungesema kawafundisha.

wameamua kuwa madogo ili kuepusha vurugu mnawazomea,lakini wote tunajua kwamba wakiamua kufanya ujinga huwa wanaufanya ujinga uliokomaa.

tufurahi maana amani ndicho kitu tunachoulizia.
 
Back
Top Bottom