Uchaguzi 2020 Dar: Jeshi la Polisi lasitisha wito wake kwa Tundu Lissu, lamtaka aendelee na Kampeni zake



Hata Maalim seif aliambiwa amekamatwa na nyaraka za siri . Mnataka kuzusha zengwe dakika za lala salama , mumechelewa sana . The world is watching , , Mwisho wa mwezi nakualika kuja kula nyama choma za bure .

CCM kifo cha mende . CHALI
 
watake wasitake kwa sasa Tundu Lissu ni 'untouchable' ………..
 
Nani katukana?

Sisi tunamsema huyu kibaraka anaetaka urais ambae wakati wenzake tunapigania kujitoa kwenye makucha yao yeye yuko busy kuturudisha nyuma.
Mnataka kutoa makucha ya wakoloni ili mchomeke ya ccm. Bora yabaki makucha ya mkoloni og kuliko nyie fake
 
Hahahahaha hutaki kuamini Lissu kawazidi ujanja polisi? Hadi unatia huruma

Ujanja uko kwenye box la kura ndugu!

Na binafsi nlishauri hawa polisi waachane na Lisu afanye chochote anachotaka maana pia ni tiba kwake kwa yaliyomsibu.

Wakati mwingine Lisu anapata point za bure kwa mihemuko ya polisi tu.

Mtu inajulikana hawezi kushinda, yanini kuhangaika nae?
 
Polisi imetumia busara. Nchi hii ni yetu sote, tukikosea tunarekebisha, tukipatia tunapambana kufanya vizuri zaidi.
Nalipongeza jeshi la polisi kwa kurudi kwenye msitari, huu siyo udhaifu huku ni kuonyesha ukomavu!
 
Haaaaaaaaaaaa[emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji2957][emoji1787][emoji1787]
 
mkuu wangehariri barua ungesema kawafundisha.

wameamua kuwa madogo ili kuepusha vurugu mnawazomea,lakini wote tunajua kwamba wakiamua kufanya ujinga huwa wanaufanya ujinga uliokomaa.

tufurahi maana amani ndicho kitu tunachoulizia.
Kwa mfano ujinga gani unaoweza kufanywa ambao ni mpya hapa duniani?
 
Lissu atampangia kazi nyingine.
 
Ushauri wangu:
CCM wajitahidi kuingia madarakani tena kupitia sanduku la kura na si vinginevyo!
 
Polisi imetumia busara. Nchi hii ni yetu sote, tukikosea tunarekebisha, tukipatia tunapambana kufanya vizuri zaidi.
Nalipongeza jeshi la polisi kwa kurudi kwenye msitari, huu siyo udhaifu huku ni kuonyesha ukomavu!
Kabisa mkuu! Wamwache Lisu atachapika kwenye box la kura kihalali kabisa.
 
Polisi imetumia busara. Nchi hii ni yetu sote, tukikosea tunarekebisha, tukipatia tunapambana kufanya vizuri zaidi.
Nalipongeza jeshi la polisi kwa kurudi kwenye msitari, huu siyo udhaifu huku ni kuonyesha ukomavu!
Hawajatumia busara yeyote.Wamerudi nyuma (surrendering) baada ya kugundua kuwa wamejichanganya na kujikoroga.Walichofanya ni ujanja ujanja wa kufukia makosa yao.Wewe uliona wapi mtu anafanya kosa Moshi halafu akatakiwa kuripoti Dar?Sheria ya namna hiyo haipo.Jeshi letu la polisi ni jeshi dhaifu na legelege sana
 
Basi usalama ndio wanapiga kura sawa na kama kweli wamemwambia hivyo ujue wanamwingiza chaka atakuja kushtuka lisu anatangazwa mshindi
Mkuu Lisu hafiki popote yule!
Akipata kura nyingi sana basi ni asilimia 20

Sasa kwanini Magu ahangaike kukimbizana na loser?
 
Kwa hio hata huyu anayesema anapinga mafisadi inawezekana hata yeye baadae ikagundulika ni bonge la fisadi sio?
 
Wakuu, Mimi ninawambia lisu ni mpango wa MUNGU, kwa Leo muda huu polisi kanda maalum imejitokeza hadharani nakutamka kuwa ile barua wameifuta wanamtakia lisu kampeni njema, naaawaambia lisu ni mpango wa MUNGU Hakuna mhemuko wowote utakaofaulu haya sasa wale walionikatalia waje hapa
Kuna mambo sisi Kama binadam tunapaswa kuyaangalia na kuyatafakari kisha kuchukua hatua.

Kumbuka kuwa lisu aliwekewa mitego tangu alipokuwa ubeligiji kuwa akikanyaga tu Tanzania anakamatwa na hili lilikuwa ni Jambo rahis Sana kupangwa na kutamkwa kutokana na hali ilivyokuwa Tanzania, lakini hawakuweza, wakasema watamkamata Siku ya kesi hawakuweza wakasema watamkamata, akiwa tume Siku ya kuchukua form hawakuweza, wakasema watamkata hawakuweza, wakapanga watamsumbua kwenye kesi zake na kuvuruga ratiba yake hawakuweza, wakapanga kutumia tume Ya Uchaguzi hawakuweza, wakapanga kule tarime hawakuweza, wakapanga Moshi hawakuweza, Jana akajitokeza IGP ambae ndio wamwisho Kabisa kwenye Jeshi la polisi gafla akashindwa akaja kanda maaalum hakuweza Leo amejitokeza kuomba radhi na kumwambia aendelee na kampeni asivuruge ratiba yake, unaweza ukakataa kuwa mipango niliyoitaja hapo haikupangwa Lakini utakuwa unakataa uhalisia huo.

Haya sasa hiii Kwa Hali ya kawaida ni kwamba polisi wamemfanyia kampeni pasipo kujua, wapo watu weeengi Sana watampenda lisu Kwa kumuona Kama mwamba wa sheria, wapo watakaochukia polisi waliokuwa wanategemea kuwa lisu ataadhibiwa nao wataufyata tu, wapo watakaotoka pangoni kuungana na lisu hiii wamempigia kampeni pasipo wao kujua,

Lakini pia hiii itawapa Wakati mgumu Sana vyombo Kama vya tume na hao hao Polis Kwa kurudi tena huko mbele kumtuhumu Au kutaka kumwaadibu, na hii itaanza kuleta mgawanyiko kwenye vyombo hivyo na Kwa Ccm

Hiii ndio maaana na Sema kuwa lisu ni mipango Ya MUNGU, MUNGU akiamua mtakuwa mnashika hiki mwisho mnajikuta mnahangaika wenyewe na mnaempangia mipango mkijikuta mnamuongezea mwendo, Kwan wale wanaosema aaah wapi subirini lisu ndio rais wa sita
 
jo taratibu...pia kunywa maji mengi
 

".....Mawazo yangu, siyo mawazo yenu (binadamu) na njia zangu, wala siyo njia zenu, asema BWANA WA MAJESHI...."

Ndugu acha kujiapiza. Mungu ni Mungu na ana namna yake na njia zake kufanya kazi yake...

Mawazo yetu sisi binadamu ni ujinga mtupu. Na unapoishia ujinga wetu, ndipo HEKIMA ya Mungu inapoanza...!

Mwacheni Mungu aitwe Mungu. Siku zote Mungu huviinua vitu dhaifu na vinyonge ili aviabishe vyenye nguvu...!!


Weka hilo akilini na moyoni mwako...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…