DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Umekosea mkuu,maoni yako yamekaa vizuri ila hapo kwa Mpango umekosea,.. hamtaji Makonda kwenye media ila anahalalisha watu wakanunue hayo makontena baada ya mkwara wa DAB kuwa watakaothubutu kununua watalaaniwa, jaribu kufuatlilia alichoongea Mipango.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Uungwana ni vitendo...Majuto ni mjukuu!!!!

Kumekuwepo na sakata la muda ninaoweza kusema ni mrefu juu ya uingizwaji wa makontena yenye vifaa mbalimbali vya kusaidia maendeleo jijini Dar.

Nampongeza mkuu wa mkoa kwa initiative zake kwa ajili ya kuhakikisha jiji la Dar linaboreka.

Hakuna doubt kwamba katika awamu hii mambo yote ni lazima yafuate taratibu zilizopo bila kujali ni mambo ya namna gani au ni ya nani.

Sakata la haya makontena limeanza kitambo sana ....limegusa wengi na mengi lakini kwa umuhimu limekugusa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ambaye ni hardworking na inovative na influential.

Kwa sasa inaonekana kuna mkwamo kuhusu procedures vs intention za kuingizwa kwa Makontena haya.

Kwa sasa najionea 'stance' kati ya mamlaka za Serikali zinazotakiwa kufanya kazi kwa umoja....yaani breach of collective responsibilities!

Kuondoa utata,mkwamo na matokeo mabaya ni muhimu kufanya majadiliano ya kina na kuombana/kupeana misamaha ili mambo yasonge mbele kwa mustakabali wa wanaDAR na Taifa kwa ujumla.

Mheshimiwa RC nenda TRA ukaoombe msamaha ikibidi au kuweka sawa procedures ili kufikia suluhisho.

CIAO!!
 
Dr Mpango naye ni jiwe, hatishiki Wala haogopi mutu
 
Tena mwambie collective responsibility ktk level ya waziri ni ya cabinet ambako m/kiti ni rais, na huko RC haingii, na ndo serikali na ndo mamlaka ya juu na chombo cha juu cha maamuzi ktk serikali,who is DAB
 
Ila kimsingi wadau mi naona hivyo vifaa vingetaifishwa na serikali na ikavichukua na kusambaza kwenye mashule ama hata ma-hospitali na zahanati (kama vitafaa huko) kwa sababu vitakwenda kutoa ama kusaidia utoaji wa huduma kwa wananchi walipa kodi.... haya malumbano ya wenye mamlaka sioni kama yana tija kabisa.. sisi tutafurahia kuona mtanage kati ya Bashite na Dk Plan lkn kuna watu wanasomea ama kufanya kazi kwenye mazingira magumu sana.. hapa Serikali kupitia TRA ingetoa msamaha wa kodi ili hivi vifaa vikatumike kwenye taasisi za serikali naona ingekuwa poa sana...
Mwisho wa siku vifaa vilivyotolewa msaada na Diaspora (kama ni kweli) vitaishia kuuzwa na walengwa wataendelea kusota..
N way....
 
Mzigo ni wa GSM,bashite ana 10%
 
Inawezekana tuna viwango tofauti vya ustaarabu, na katika viwango vyako, Mpango hajakosea,na katika viwango vyangu, kakosea.

Na inawezekana viwango vyangu ni vya juu sana katika realpolitik za Tanzania za sasa, kwa hivyo, kiujumla, mimi nimekosea kwa kutaka viwango vya juu sana katika nchi ambayo haipo katika hali ya kuwa na viwango vya juu sana vya uongozi.

Yani naleta zile sheria za 1920s za Zanzibar, mtoto ukionekana unakula huku unatembea, kesho unachapwa viboko shuleni kwa "kula majiani".

Hapo vipi?
 
Ili yasonge alipe kodi
Biblia inasema MTU wa Kodi, Kodi MTU abaestahili heshima heshima
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…