DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Na kwenye Mnada lazima niende nikanunue hizi samani unless TRA waweke bei isiyolipika
 
Siku nyingine ukitaka kuchangia tumia akili na uzifahamu sheria za nchi.

TrumP leo kwa kumnunua malaya, kavunja sheria ya nchi huko USA.
 
#JumapiliAugust26
"Makontena yenye vifaa vya elimu hayatapigwa mnada. Na anayetaka kuyanunua, Mungu atamlaani" Paul Makonda, RC DSM.

#VijanawaCCM: Hureee. Hongera sana mheshimiwa. Wewe ni mtetezi wa wanyonge. Tupo pamoja nawe katika kupigania maslahi ya wanyonge. Wapinzani walifanya fitina ili makontena yapigwe mnada, sasa wameumbuka.

#JumatatuAugust27
"Nimeapa kulinda na kusimamia sheria za nchi, sitishwi na mikwara ya mwanasiasa yeyote. Mpuuzeni huyo anayesema atakayenunua haya makontena atalaaniwa. Mungu hasikilizi maombi ya aina hiyo" Dr.Phillip Mpango, Waziri wa Fedha na uchumi.

#VijanaWaCCM: Hureee. Hongera sana Mheshimiwa Waziri. Serikali makini ni inayoweza kukusanya kodi. Endelea kusimamia sheria ili mapato yaongezeke na uchumi ukue. Tupo pamoja nawe mheshimiwa waziri.

#MyTake:
Najaribu kufikiria aina ya zamadamu waitwao CCM nakosa majibu.! Na malisa G

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mwandishi yuko sawa Tanzania ni ngumu hata kuisaidia. Kwa wanaokaa TZ wengi hawawezi kuamini haya lakini sisi wa nje tunajua ndugu zetu. Tunaenda kwenye ma hospital na mashule kuombea vifaa mfano Ali ambaye ni Mtanzania mwenye asili ya Zanz ndiye aliyetuma hivyo vifaa cha ajabu akituma nchi nyingine hakuna hizi shida! Yuko seattle na watu wanajitolea kupakia kwenye makontena, watu wanachangia gharama za kutuma na storage halafu zikifika TZ eti tulipe kodi wakati vifaa ni vya watoto wanaokaa chini ndiyo wameomba. Sasa hiyo kodi ni ya nani kama haitasaidia watoto wanaokaa chini! Tulifikiri kodi ni kusaidia Watanzania.... Halafu watu hao hao wanasema sisi watu
Wa nje hatuna faida maana hatusaidii. Mna mkomoa nani Makonda yupo kwenye jumba la serikali, sisi tuko huku US anayepata shida ni yule mtoto. Sasa wazuri wakitucheka tutasema nini mlitaka watu wasaidiaje kutoa pesa tu ambazo zitaishia kwa wajanja..!
 
[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukiona makonda hadi anaingia kanisani na vyombo vya habari vinatangaza na baba yake anamuangalia tu ujuwe mzigo ni wao wote wamefumwa tuu vinginevyo wangeingiza kama wanavyofanya siku zote mafisadi makubwa
 
ha ha mwambieni makonda baba yake anamruka akomae na mzigo wake hasaidii mtu yeyeote mzigo wake binafsi na wahindi na waaravu wake
 
Sheria za kodi ndio hizo zinasema hivyo.Mbona kuna gari la zimamoto la jiji la mwanza walipewa msaada na shirika moja la ujerumani sasa ni mwaka mmoja lipo bandarini!!kisa lazima lilipiwe kodi ya kuliingiza nchini!!!licha ya umuhimu wake ktk jamii,ndio iwe hizo samani ambazo mala mwenye nazo alizikana mala nitamwambia baba!!nchi lazima ifuate utaratibu na sio kwa vitisho na leo waziri mpango amepigilia msumali wa mwisho kwa watendaji wa TRA,kuwa wasiogope vitisho waangalie sheria nasemaje tu..
 
Tatizo ni kwamba pamoja na umuhimu wa bidhaa zinazosemekana kuwa kwenye makontena, msaada uliombwa na mtu binafsi na ukatumwa kwake in a personal capacity. Mh P. M na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ni vitu 2 tofauti. Lazima tutofautishe kati ya official na personal transaction. Hadi leo sijaona mkono wa wizara ya elimu, serikali za mitaa, ofisi ya waziri mkuu nk ili kudhihirisha mkono wa serikali ndani ya shughuli hiyo. Kwa nini hakutaka kuhusisha vyombo vingine vya serikali mapema ? Katika siasa, kila kitu kinawezekana: mzigo huo wa mabilioni unaweza kutumika kujizolea umaarufu wa kisiasa au hata kubadili kabisa status quo ndani ya chama. Au yeyote aliyetumiwa makaontena haya, angebahatika yakatoka bandarini na kuingia uraiani, angeweza kuamka multibilionea.
 
Kwann jina lake?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…