DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Mkuu ni kweli..kule IG ukimsoma huwezi kujua kama huyu ni mvamia studio, mtekaji na muuwaji.
 
Ni jambo la aibu kabisa kwa watendaji wa serikali moja, chama kimoja, wameteuliwa na rais mmoja, wanalumbana wazi wazi kama watoto wasio na adabu.

Jambo hili linaonesha udhaifu wa serikali yetu, haifanyi maamuzi kwa pamoja na kuzingatia "collective responsibility".

Kila mtu anafanya maamuzi kivyake.

Na panapotokea mgongano, viongozi hawana ukomavu wa kuongea na kumaliza tofauti zao kwenye vikao vya ndani.

Wanagombana kwenye vyombo vya habari kama wendawazimu.

Hapo, kitu cha kwanza kabisa, sijali nani yuko sawa na nani kakosea, kule kulumbana hivi tu, kunawafanya wote wawe wamekosea.

Kama viongozi wakubwa kabisa wa serikali wanatoa mfano huu, watoto wa shule ya msingi wanajifunza nini hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…