DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Mungu anajua kuwaumbua watu tena kwa muda mfupi sana, watu waliposema Rais amchunge huyu mtoto yeye mwenyewe akawaona watu wanampangia na kumuonea wivu mwanae kumbe walikuwa na nia njema ya kumsaidia huyu kijana asije kumtia aibu akajitokeza hadharani kumsifu akidhani anawakomoa watu kumbe anajikomoa mwenyewe.

Ona sasa Rais alivyotegwa kirahisi, tuone sasa mvunja sheria na msimamia sheria nani ataibuka mshindi mbele ya msema kweli ni mpenzi wa Mungu.

Ukiwa mnafiki usisahau kuwa muda si mrefu utajulikana tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mpango hajipendi anamchokoza mtoto mpendwa yasije yakamkuta ya Nape.
Acha wafu wazikane

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa si anatekeleza maagizo ya mkuu wake ya kukusanya kodi inavyotakiwa?

Mimi Mpango kusimamia wajibu wake sina tatizo naye, tatizo ni haya malumbano ya kwenye vyombo vya habari.

Yanaonesha serikali yetu ina matatizo makubwa zaidi ya hii incident.

Watu hawafanyi kazi kama serikali moja, kabla ya kupigiana simu na kuzungumza, wanapigana malumbano kwenye vyombo vya habari.

Ni namna ya kijinga kabisa ya kufanya kazi serikalini.

Kazi ya serikali ni teamwork, si mashindano ya ulimbwende na malumbano tuone nani zaidi.
 
#MwananchiNukuu Wengine hugawa watu katika mafungu. Mtu fulani akifanya kosa hata liwe kubwa, hasemwi lakini mwingine akifanya kosa japo dogo hukuzwa likawa kama Mlima Kilimanjaro" Hayati Baba wa Taifa, Julius Kambarage Nyerere #MwananchiLeo


Sasa huyu bashite kafanya bonge la kosa lakini baba yake anamlinda tu hapo ndo utajua jiwe alivyombaguzi.
Jiwe ni nani? Mpango?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanazingua tu ni movi wanatufanyia ili serikali ionekane inatenda haki kwa watu wote lkini in fact hayo makontena hayatanunuliwa na atakayenunua ni mtu maalum aliyepangwa kwa kiini macho tu.

Kamani movie, ni ujinga zaidi.

Nikama mama na baba watengeneze ugomvi wa uongo, wawaoneshe watoto wanapigana kwa sababu wanawapenda watoto.

Ile heshimainayovunjwa kwa haowazazi kuwaonesha watoto wanapigana itakuwa na madhara makubwa kulikofaida itakayoletwa kuonesha wazazi wanapigana kwa sababu wanawapenda watoto.

Wazazi hata wakipigana, wanatakiwa wapigane chumbani huko, watoto wasiwaone wanavyopigana.

Viongozi ni watu, watakuwa na tofauti, watalumbana, hilo halinamjadala.

Ila, viongozi bora watawezakulumbana kwenye vikao, behind closed doors, wakija ku present vitu kwa watu, wanakuwa washamaliza tofauti zao, au hata kama zipoi, haziwi exposed kwenye public.

Uongozi ni kazi ya imani. Imani ya wananchi kuwamini hawa viongozikwamba wanaweza kazi ya kuongoza watiu.

Viongozi kulumbana lumbana kijinga,kunatupa picha wananchi kwamba "kumbe hawa hata wao kwa wao wenyewe waliokaribu katika uongozi hawawezi kusikilizana, wataweza vipi kutuongoza sisi tulio mbali na uongozi?"
 
Back
Top Bottom