Dah sentensi fupi kweli ila ina maswali elfu moja juu yake aisee wewe programmer unatumia platform ya Laravel ? Yaani mkuu wa nchi mwenye majeshi yake hapumui kwa bashite ? Kupumua kivipi kwanza aisee ?Hana ubavu hapumui Kwa bashite
Amesema Watanzania walipe kodi bila shuruti venginevo watapata taabu sanaaa.
Mimi napendekeza msaada mkubwa kwa waalimu nchini ni kutokata kodi yoyote kwenye mishahara yao. Hii ya figisu za kuingiza viti bila kodi ama chochote kuwahusu ni dili la wezi wachache kuingiza bidhaa zao bila kulipa kodi kwa mgongo wa waalimu.Ishu hii Mshindi Mkuu wa Mkoa, hoja zake zina make sense.
Raisi kamuelewa ndio maana yuko kimya.
Hakuna atakaye ondolewa kazini.
Sent using Jamii Forums mobile app
Hajui kwa Yesu alisema ya Mungu mwachie Mungu na ya kaisar mwachie kaisariNa Benny Mwaipaja, WFM - Dar es Salaam
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la kuhifadhia makontena-Bandari Kavu Dar es Salaam (DICD), na kukagua makontena 20 yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea na mnada wa makontena hayo ili kupata kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni 1.2.
View attachment 848681
Dkt. Mpango amesema kuwa kodi hiyo inadaiwa kwa mujibu wa sheria za nchi baada ya mwenye mali kushindwa kulipa kodi na kwamba amesikitishwa na vitisho vinavyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa na vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akitumia vifungu vya Biblia kwamba yeyote atakaye nunua mzigo huo atalaaniwa.
"Sheria za nchi hazichagua sura wala cheo cha mtu, na mimi ndicho nilicho apa, kutekeleza sheria za nchi, sheria za kodi, ndiyo dhamana niliyo pewa kwahiyo Kamishna, simamia sheria za kodi bila kuyumba" alisisitiza Dkt. Mpango akitoa maelekezo kwa Kamisha wa Forodha Bw. Ben Usaje.
Alifafanua kuwa mzigo wa Samani ulioagizwa kutoka nje ya nchi hauna msamaha wa kodi na kwamba huyo aliye agiza (RC Paul Makonda) alipe kodi stahidi na asipo lipa kodi hiyo mchakato unaoendelea wa kuyapiga mnada makontena hayo uendelee.
"Napenda niwaombe viongozi wenzangu Serikalini, ni muhimu tukachuja maneno! Unasema mtu anayekuja kununua samani atapata laana, tena laana ya Mungu, kwanini tunamhusisha Mungu kwenye vitu vya namna hii" alieleza kwa masikitiko Dkt. Mpango
Dkt. Mpango alitoa wito kwa watanzania wanaotaka kununua bidhaa hizo ambazo nyingi ni vifaa vinavyoweza kutumika shuleni ama maofisini kama vile viti meza na makabati, kujitokeza bila hofu kununua mali hizo.
Aliwaomba walimu na wanafunzi wasiwe na wasiwasi na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua na kuwekeza kwenye elimu kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 20 kila mwezi kulipa ada ya wanafunzi ili wasome bila kulipa ada na ina mpango madhubuti wa kuboresha miundombinu ya elimu nchi nzima ikiwemo ujenzi wa madarasa na ofisi za walimu.
"Tunawapenda na kuwathamini sana walimu wetu, asitokee mtu yeyote akaanza kuwaambia hadithi kama vile Serikali hii inawapuuza! Si kweli hata kidogo" Aliongeza Dkt. Mpango
View attachment 848680
Kwa upande wake, Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Ben Usaje, alimweleza Dkt. Philip Mpango kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, aliwasilisha maombi ya kutaka kupewa msamaha wa kodi wa makontena 36 yenye samani kutoka Diaspora nchini Marekani.
Alisema kuwa kati ya makontena hayo, yaliyoingia nchini ni makontena 20 ambayo yanadaiwa kodi ya shilingi bilioni 1.2 na kwamba utaratibu kwa kumtaka Paul Makonda alipe kodi hiyo ili aruhusiwe kuyachukua makontena hayo ulifanyika kwa mujibu wa sheria na kwamba mpaka sasa hajayachukua ndio maana yanapigwa mnada.
Naye aliwatahadharisha watu wanao tumia masuala ya siasa na uongozi Serikalini kutaka kukwepa kulipa kodi a kwamba suala la kodi za samani zinaonekana ziko juu kwa sababu Bunge lilitunga sheria hiyo ili kulinda soko la ndani la samani na kuweka sheria ya kutokuwepo kwa msamaha wowote wa kodi kwenye bidhaa kama hizo.
Asante,na nia yangu wanielewe wachache ikibidi Mello tu
Hapo umeenda mbali!Hii series hii inaonyesha magu kashamchoka Bashite na ndio maana wateuliwa wa magu hawatishiki kwa sasa, na napata uhakika sasa kuwa ni kweli Bashite akili zake hazipo sawasawa maana mara ya kwanza aliyakana hayo makontena kuwa sio yake akaja tena akisema kuwa ni yake na anaomba msamaha wa kodi na sasa anawalaani wanaoyapiga mnada wakati ni yeye mwenyewe mwazo aliyakana kuwa sio yake
Alafu ukimkuta kule insta anavyopost mambo ya kilokole huwezi mshtukia kuwa ni shetani mkubwa huyu
Sent using Jamii Forums mobile app
Nitafute nipe hela nikakunulieMimi nina wasiwasi mwenzenu kuwa kuna mchezo hapa ili wanunuzi wakosekane na serikali itaifishe.Hivi kweli kuna mtu atayanununua hajitaki?
Kwani baada ya kuyanunua are you safe kwa hii serikali bila kutafutiwa sababu ikiwemo kodi hulipi, kesi zisizokuwa na kichwa wala miguu naota tu mnisaidie huyo mnunuzi kwa serikali hii atatoka wapi? Asipotezwe baada ya kunuunua unless watu wanaojulikana walishajulikana nafikiria nje ya box tu with all my senses
Ha ha ha hawataonekana mida hii!Walio bet watupe Matokeo ya Mikeka Kama imechanika au laa
huyu hapa msikilizeView attachment VID-20180830-WA0012.mp4Sema wana bavicha!
Ni mimi mwenyewe kipara hakuna mwingine chakaza kijana amezidi sasa anaingia msikitini na viatu!
Ujinga wa level za standard gaugeHao wenye elimu kubwa si ndio hao waliokuwa wanabuni miradi ya upigaji kama EPA,, ESCROW na uchafu mwingine wa aina hiyo!!?.
Hao wenye shule za maana si ndio hao ambao wanaendesha ma-vogue na magari ya milioni 400 wakati Mama zao vijijini wanajisaidia haja kubwa maporoni pembeni ya nyoka na chatu!!?.
Hao wenye shule nzuri si ndio hawa walioua mashirika makubwa mpaka yakawa yanashindwa kutoa gawio serikali kuu!!.
Hizi ndizo akili za mtanzania halisi, anajivunia elimu wakati hakuna cha maana ambacho elimu yake inaisaidia nchi hii.
Huyu dogo anaweza kuwa na matatizo yake binafsi lakini hizi juhudi za kuwatafutia waalimu furnitures, hizi juhudi za kusaidia kinamama wanaotelekezewa watoto, ni lazima Mungu atazilipa. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni.
Malipo duniani kwanza kabla ya kukutana na Mungu. Bashite kanyang'anya Mali za watu kwa vitisho sana. Amejitajirisha kwa kipindi cha muda mfupi sana kwa dhulma tupu. Mungu hayuko na mwenyewe kudhulumu wenzake. Sasa zamu yake, Mali zake ziuzwe kufidia hiyo 1.2b ambayo nauhakika hata kama zikiuzwa kontena 100 za Vifaa hivyo hazitafikia idadi hiyo ya kodi.Na Benny Mwaipaja, WFM - Dar es Salaam
WAZIRI wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, amefanya ziara ya kushitukiza katika eneo la kuhifadhia makontena-Bandari Kavu Dar es Salaam (DICD), na kukagua makontena 20 yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda na kuiagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea na mnada wa makontena hayo ili kupata kodi ya Serikali inayokadiriwa kufikia shilingi bilioni 1.2.
View attachment 848681
Dkt. Mpango amesema kuwa kodi hiyo inadaiwa kwa mujibu wa sheria za nchi baada ya mwenye mali kushindwa kulipa kodi na kwamba amesikitishwa na vitisho vinavyotolewa na Mkuu huyo wa Mkoa na vilivyonukuliwa na baadhi ya vyombo vya habari nchini akitumia vifungu vya Biblia kwamba yeyote atakaye nunua mzigo huo atalaaniwa.
"Sheria za nchi hazichagua sura wala cheo cha mtu, na mimi ndicho nilicho apa, kutekeleza sheria za nchi, sheria za kodi, ndiyo dhamana niliyo pewa kwahiyo Kamishna, simamia sheria za kodi bila kuyumba" alisisitiza Dkt. Mpango akitoa maelekezo kwa Kamisha wa Forodha Bw. Ben Usaje.
Alifafanua kuwa mzigo wa Samani ulioagizwa kutoka nje ya nchi hauna msamaha wa kodi na kwamba huyo aliye agiza (RC Paul Makonda) alipe kodi stahidi na asipo lipa kodi hiyo mchakato unaoendelea wa kuyapiga mnada makontena hayo uendelee.
"Napenda niwaombe viongozi wenzangu Serikalini, ni muhimu tukachuja maneno! Unasema mtu anayekuja kununua samani atapata laana, tena laana ya Mungu, kwanini tunamhusisha Mungu kwenye vitu vya namna hii" alieleza kwa masikitiko Dkt. Mpango
Dkt. Mpango alitoa wito kwa watanzania wanaotaka kununua bidhaa hizo ambazo nyingi ni vifaa vinavyoweza kutumika shuleni ama maofisini kama vile viti meza na makabati, kujitokeza bila hofu kununua mali hizo.
Aliwaomba walimu na wanafunzi wasiwe na wasiwasi na kwamba Serikali ya Awamu ya Tano imejipambanua na kuwekeza kwenye elimu kwa kutenga zaidi ya shilingi bilioni 20 kila mwezi kulipa ada ya wanafunzi ili wasome bila kulipa ada na ina mpango madhubuti wa kuboresha miundombinu ya elimu nchi nzima ikiwemo ujenzi wa madarasa na ofisi za walimu.
"Tunawapenda na kuwathamini sana walimu wetu, asitokee mtu yeyote akaanza kuwaambia hadithi kama vile Serikali hii inawapuuza! Si kweli hata kidogo" Aliongeza Dkt. Mpango
View attachment 848680
Kwa upande wake, Kamishna wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania-TRA, Ben Usaje, alimweleza Dkt. Philip Mpango kwamba Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda, aliwasilisha maombi ya kutaka kupewa msamaha wa kodi wa makontena 36 yenye samani kutoka Diaspora nchini Marekani.
Alisema kuwa kati ya makontena hayo, yaliyoingia nchini ni makontena 20 ambayo yanadaiwa kodi ya shilingi bilioni 1.2 na kwamba utaratibu kwa kumtaka Paul Makonda alipe kodi hiyo ili aruhusiwe kuyachukua makontena hayo ulifanyika kwa mujibu wa sheria na kwamba mpaka sasa hajayachukua ndio maana yanapigwa mnada.
Naye aliwatahadharisha watu wanao tumia masuala ya siasa na uongozi Serikalini kutaka kukwepa kulipa kodi a kwamba suala la kodi za samani zinaonekana ziko juu kwa sababu Bunge lilitunga sheria hiyo ili kulinda soko la ndani la samani na kuweka sheria ya kutokuwepo kwa msamaha wowote wa kodi kwenye bidhaa kama hizo.