DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

DAR: Licha ya RC Makonda kusema atakayenunua Makontena yake atapata laana kali, Waziri Mpango aagiza yapigwe mnada

Mwaka 1997 Tanzania iliamua kukua kufikia uchumi wa kati kwa kutengeneza dira ya maendeleo ya Taifa 2025. Mpaka sasa tuna takribani miaka 7 tu imebakia ili kuona realization ya njozi ikiwa dhahiri katika maisha ya Watanzania.

Binafsi natambua mara kwa mara tunahimazana kuwa wazalendo. Na uzalendo tafsiri yake imekuwa na mkanganyiko kwelikweli. Ila ukikaa na wanajeshi ukawauliza, utaelewa tafsiri ya uzalendo kwa vitendo. Wamarekani au Wa-Israel hali kadhalika, unawaelewa, ila sisi… huenda tunahitaji kuwekewa mikono… Mungu tusaidie.

Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam kaja na mpango mahsusi wa kuhakikisha anatoa mchango wake kwa vitendo ile kuboresha elimu mkoani Dar es Salaam. Amejenga madarasa, nyumba za walimu, ofisi za walimu na kupata uhakika wa madawati ya kutosha. Wasamalia wema wamempatia madawati na viti vya walimu mara vitu vimekwama toka Januari, leo hii ni tunakaribia kabisa kufika September, baadooo havijatoka.

Waziri Mpango kwa nia njema na vijana wake wa mamlaka ya mapato nao wanataka kodi. Toka Januari mpaka leo kama hela hajalipwa tafsiri rahisi bajeti ya kulipia haikuwepo ndiyo maana Paulo Makonda aliomba msamaha wa kodi. Waziri na vijana wake wanazingatia sheria na taratibu za ki-kodi.

Kuna sheria duniani nzuri na mbaya, ila zote zinabaki kuwa sheria katika dunia hii hii. Kuna bilioni 133 ya EPA zilitoka BOT 2005 kwa mujibu wa taratibu. Baadae ikaonekana ni wizi ulifanyika. Ila mpaka zinatoka, hakuna polisi aliekama mtu, “huenda sheria ilizingatiwa”. Sote pia tunakumbuka mabilioni ya ESCROW yalitoka BOT, hapo napo bila shaka kuna sheria na taratibu zilifuatwa mpaka yakalipwa.

Leo walimu wanahitaji viti na meza kama vitendea kazi. Kwa kuwa sheria hajafuatwa (maana furniture sheria hajatamka zinapaa msamaha wa kodi) pamoja na nia njema ya aliefanya initiatives, yet, kuna kukwama. Je tunaijenga Tanzania kuelekea dira ya maendeleo ya Taifa 2025?

Kodi kama italipwa, sehemu ya kodi hiyo hiyo mbona ndiyo itanunua viti na meza hizo hizo. Tunajenga nyumba moja Tanzania yet tunagombania fito.

Hii yanikumbusha habari ya taasisi moja ilianza mwaka 2009 na mtaji wa USD 100 mil nchi zaUlaya mashariki. Mwaka huu (miaka 9 baadae) hao jamaa wamekwenda nchi nyingine na uwekezaji kama huo huo kwa mtaji wa zaidi ya USD 2 bilion.

Kuna Mtanzania namfahamu ana model ya mradi kama hao jamaa wa Ulaya Mashariki, anataka kuleta uwekezaji wa mradi na technology ili kutengeza bidhaa katika ubora kwa soko la ndani na nje. Kwa projection, mradi huo utaanza na ajira za Watanzania 100+ na kwa mwaka malipo ya kodi yakawa kati ya billion 15 na kuendelea. Achilia mbali manunuzi ya huduma mbalimbali za kiwanda hicho kama vile maji, umeme na tozo za huduma kama TFDA, TBS, GS1 na ambazo zitaingia serikalini.

Mradi huu utakuwa mchango pia kwa vituo vya utafiti Ukiriguru na vituo vingine vinavyojihusisha na kilimo achilia mbali ku-replicate out-growers scheme.

Mradi huu wa uwekezaji ukiuza mauzo ya nje ya bidhaa kwa kuwa unatumia technology ya kisasa kwenye soko la mazao ya Kilimo AGOA Marekani, kuna fursa za hela ya kigeni kuingia nchini pia.

Sheria na taratibu ambazo zaweza kufanyiwa kazi kujenga ushirikiano kufanikisha lengo, unachelewesha jambo zuri kufanyika.

Jana Mkurugenzi wa kituo cha uwekezaji amewataka “wakubwa” kushirikiana na wawekezaji kuijenga Tanzania. Imeonekana kuna “wakubwa” kuwabalasa baadhi ya wawakezaji Tanzania hii hii.

JPM amejipambanua anataka twende mbele, ila wasaidizi wake ndiyo hivyooo kama tulivyoona Waziri na Mkuu wa Mkoa, Director wa TIC na baadhi ya wakuu wa Wilaya na Mikoa.

Adui yetu Tanzania ni Ujinga, umasikini na maradhi.Kama sheria, sera na taratibu zinatuchelewesha, hizo sheria, sera na taratibu zinatufaa kweli.

JPM alinunua ndege mpya kwa cash, baadhi wakamzodoa, oohhh, Rais kanunua ndege bila kuzingatia sheria za manunuzi ya umma. Je, lengo ni kunua ndege au sheria ya manunuzi ambayo inaweza kuchelewesha mambo na wakati mwingine kuongeza gharama kwa jina la “mchakato”.

Nazipenda sheria na taratibu. Ila sheria zingine ni mbaaaya. Badala ya kututumikia twende mbele zinatuchelewesha.

Tunaipenda Tanzania. Tukiwa wazalendo kweli, tutashirikiana kwa nia njema kwenda mbele kuijenga Tanzania badala ya kukwamishana kwa jina la sheria na taratibu.Tunawajibika moja kwa moja kulenga kumtumikia Mtanzania kwa kushindana na maaduni Umasikini, ujinga na maradi. Wazalendo huwa wana-eliminate maadua with it take. Sisi hivi tunatumia strategy ipi
Wapambe wa Bashite mtapata tabu sana. Hizi ni dalili kwamba mwanzo wa mwisho wake umewadia. Endeleeni kutumika

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kusafirisha container moja toka US mpaka Dar ni silingi karibia milioni saba.
Containers 20 ni milioni karibia 140. Hapo hujaweka gharama za hizo furnitures.
Je, ingekuwa vizuri kutoa dola laki moja(100,000$) ili utengeneze furnitures Dar (keko) na kutoa ajira kwa vijana wa Dar, kuweka hizo hela (za kigeni) kwenye mzunguko wa fedha mitaani Dar.
Au ni bora, kulipa kampuni za meli za nje fedha za kigeni kusafirisha fenicha kutoka nje, zilizotengeneza ajira nje?

Tuwe tunafikiria kichumi zaidi ili tupate faida kwa kidogo tulicho nacho. Some decisions huwa hazina faida sana, making you wonder .....
 
Kusafirisha container moja toka US mpaka Dar ni silingi karibia milioni saba.
Containers 20 ni milioni karibia 140. Hapo hujaweka gharama za hizo furnitures.
Je, ingekuwa vizuri kutoa dola laki moja(100,000$) ili utengeneze furnitures Dar (keko) na kutoa ajira kwa vijana wa Dar, kuweka hizo hela (za kigeni) kwenye mzunguko wa fedha mitaani Dar.
Au ni bora, kulipa kampuni za meli za nje fedha za kigeni kusafirisha fenicha kutoka nje, zilizotengeneza ajira nje?

Tuwe tunafikiria kichumi zaidi ili tupate faida kwa kidogo tulicho nacho. Some decisions huwa hazina faida sana, making you wonder .....
Tanzania ya viwanda jamaawanataka iwe US ya viwanda Wakati tayari ni ya viwanda. Ningekuwa Mimi ningesema letini hiyo misaada katika Hali ya cash ili wale madogo wa jkt keko watutengenezee fanicha. Badala yake wanakamata watupa taka.
 
Wanasema kuna maajabu ya dunia yanayopatikana katika nchi mbali mbali, ila Tanzania yenyewe ni ajabu miongoni Mwa maajabu,

Watu wanajitolea kukusanya vifaa kuwasaidia watanzania walioko katika shule zisizo na vifaa Alafu inafika bandarini eti viuzwe,??

Kama wanajali sana hela basi vinunuliwe na wizara ya elimu,

Tanzania ilivyonikatisha Tamaa mimi kuhusu michango ya kujitolea kuokoa majanga nadhani hata wengine wamekata tamaa,

Kuna rafiki yangu mtoto wa mtu mkubwa wa zamani anakaa Norwich nilipomtembelea juma lilee akanambia kuna vifaa vya hospital tuvikusanye tutume visaidie hospital za Tanzania, nisiwe mnafiki nilimjibu Tokea serikali imeleta zuruzunga kwenye Hela ya Tetemeko niliyochangia USD 400 nikidhani zitamfikia yule mama ambaye alitumika kukusanya Hela Mara matembezi masaki Mara changia bukoba, kumbe picha yake inatumika tu, sitakuja kuchangia Janga lolote Tanzania, acha wenye za kuchezea wachange,

Sasa Leo huyo jamaa yangu baada ya kusikia makontena ya makonda ya msaada yamezuiliwa ili yauzwe kanipigia moja kwa moja kwamba ulisema kweli, nami sivikusanyi

Mnakatisha wanaojitolea tamaa,
Ni bora ukatumia hela yako kuinua familia yako kuliko kuchangia Majanga ambayo serikali haithamini mchango wako,

Britanica
Mkitaka kuchanga mchange kama Kwa ajili kusaidia taasisi sio ifike Kwa jina binafsi, Sheria za msamaha wa kodi utambua taasisi, na lazima wajiridhishe ili kuzuia michezo isiyofaa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kusafirisha container moja toka US mpaka Dar ni silingi karibia milioni saba.
Containers 20 ni milioni karibia 140. Hapo hujaweka gharama za hizo furnitures.
Je, ingekuwa vizuri kutoa dola laki moja(100,000$) ili utengeneze furnitures Dar (keko) na kutoa ajira kwa vijana wa Dar, kuweka hizo hela (za kigeni) kwenye mzunguko wa fedha mitaani Dar.
Au ni bora, kulipa kampuni za meli za nje fedha za kigeni kusafirisha fenicha kutoka nje, zilizotengeneza ajira nje?

Tuwe tunafikiria kichumi zaidi ili tupate faida kwa kidogo tulicho nacho. Some decisions huwa hazina faida sana, making you wonder .....
Hao ni wabinafsi sana na mpaka leo hii siamini kama kweli hizo Furniture ni Kwa ajili ya Walimu,huo ni mradi wake binafsi ila Kwa kuwa Walimu wa Bongo ni daraja la watu kujinufaisha na kupata madaraka ndio hivyo tena wanatumika vibaya.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbushia na ule mtambo wa kuprosesi taka meya wa kinondoni alivyolalamika kuhujumiwa .
Alitakiwa kulipa Kodi hata kama ulikuwa na faida kwa wote na zoezi likafeli. Meya Yakobo.
Bother ...two wrongs make a right...
Hata JPM walimhujumu wakati akiwa Waziri wa Uvuvi pale alipokamata meli ya wavuvi haramu.
Wanasheria wa serikali kupitia ofisi ya DPP walipeleka shitaka weak, inturn serikali ikashindwa kesi... wakati wavivu walikuwa haramu na walikamatwa ready handed
 
Waziri Mpango ajitayarishe kuachia uwaziri very soon. Hata pona na hili kama yalivyo mkuta Nape.
 
Bother ...two wrongs make a right...
Hata JPM walimhujumu wakati akiwa Waziri wa Uvuvi pale alipokamata meli ya wavuvi haramu.
Wanasheria wa serikali kupitia ofisi ya DPP walipeleka shitaka weak, inturn serikali ikashindwa kesi... wakati wavivu walikuwa haramu na walikamatwa ready handed

"two wrongs don't make aright"
 
makonda ni mwizi tu, vipi analeta makontena yote hayo kwa jina lake binafsi tena jina lenyewe mpaka leo lina utata, kulikuwa na ugumu gani kuiomba serikali kutoa msamaha wa kodi kabla ya hizo bidhaa kusafirishwa? Huyu alijua mzigo utapita bandarini kwa kumuogopa yeye lakini kitu imebuma. Na Raisi akikalia kimya hili jambo basi na yeye atakua amejijafua.
 
Kusafirisha container moja toka US mpaka Dar ni silingi karibia milioni saba.
Containers 20 ni milioni karibia 140. Hapo hujaweka gharama za hizo furnitures.
Je, ingekuwa vizuri kutoa dola laki moja(100,000$) ili utengeneze furnitures Dar (keko) na kutoa ajira kwa vijana wa Dar, kuweka hizo hela (za kigeni) kwenye mzunguko wa fedha mitaani Dar.
Au ni bora, kulipa kampuni za meli za nje fedha za kigeni kusafirisha fenicha kutoka nje, zilizotengeneza ajira nje?

Tuwe tunafikiria kichumi zaidi ili tupate faida kwa kidogo tulicho nacho. Some decisions huwa hazina faida sana, making you wonder .....
Brother... tayari fanicha ziko bandarini. Walimu hawana fanicha.
Misaada mingapi ya mahindi inakuja toka Marekani inapita bila kodi wakati kuna mahindi Iringa, Katavi na Ruvuma yanaharibika?

Tukiamua kuijenga nchi tuijenge. Tukiamua kufuata sheria sawa tutakuwa sawa pia. Ila suuala je tunapiga hatua au tunarejea nyuma?
...Coming together is a beginning; keeping together is progress; working together is success...
 
Brother... tayari fanicha ziko bandarini. Walimu hawana fanicha.
Misaada mingapi ya mahindi inakuja toka Marekani inapita bila kodi wakati kuna mahindi Iringa, Katavi na Ruvuma yanaharibika?

Tukiamua kuijenga nchi tuijenge. Tukiamua kufuata sheria sawa tutakuwa sawa pia. Ila suuala je tunapiga hatua au tunarejea nyuma?
...Coming together is a beginning; keeping together is progress; working together is success...
Sheria ifuate mkondo wake

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Brother... tayari fanicha ziko bandarini. Walimu hawana fanicha.
Misaada mingapi ya mahindi inakuja toka Marekani inapita bila kodi wakati kuna mahindi Iringa, Katavi na Ruvuma yanaharibika?

Tukiamua kuijenga nchi tuijenge. Tukiamua kufuata sheria sawa tutakuwa sawa pia. Ila suuala je tunapiga hatua au tunarejea nyuma?
...Coming together is a beginning; keeping together is progress; working together is success...
Taja misaada iliyotoka marekani ya mahindi, wakati kuna mahindi mengi Tanzania.
Usipende kuongea vitu visivyo na ukweli ili kuthibitisha vitu ambavyo havina ukweli.
Try another argument.
 
Back
Top Bottom