Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Dar: Mfanyabiashara Mohamed Dewji(Mo Dewji) atekwa na watu wasiojulikana maeneo ya Oysterbay

Kumbuka kuna raia wako vizuri kwenye crime and investigation kuliko hata askari, penye wengi hapaharibiki kitu,Ukiwaambia raia watoe ushirikiano bila kuwapa ushirikiano ni kuwadhiaki.
Nimesoma soma articles za mauaji mbalimbali na katika kesi hata kama CCTV footage ipo askari kuileta kwa raia hua ni last resort ambapo hua wanaamua kufanya open investigation.

Kesi za abduction/ kidnapping hua zinafanyiwa sana mtindo huu kwakua abductors tupo nao mitaani. Mfano katika kesi ya Rostov Ripper Askari waliprofile wanahisije mhusika wao atakavyokua kutokana na matukio yalivyoonekana.
Same kwa kesi ya BTK, na watu walitoa tips, ingawa nyingi ni za hovyo il za msaada zinakuepo.

Kwa hizo articles nilizosoma zinasema kwamba, mtu aliyetekwa hua na window of opportunity la kumpata akiwa hai. Kadri muda unavyoenda dirisha linazidi kutanuka na inaanza kua ni kuhisi zaidi kuliko kuongozwa na facts. Mfano kwa sasa hivi askari wanaweza kua na theory hata mia za wapi watekaji watakua wameelekea, ila lingekua jeshi la kisasa ilibidi wajitahidi dirisha lisitanuke zaidi.

Pia ninachoamini ni kwamba kama waliomteka ni pros na wanachohitaji ni ransom watasema ila kama siyo pros wanaweza kureact savagely kwa namna serikali na nchi ilivyolipokea hili swala.

Nchi nyingi hua hazinegotiate na kidnappers, simply kwakua mkiwapa leo ransom kesho watakuja kumteka Samata, wakifanikiwa kila mtekaji atajua hili ni shamba la bibi. Sijui nchi yetu sera yake juu ya negotiation ikoje.

Ila askari wana eneo lao la kulaumiwa katika hili.
 
ishu ya kutafuta billionare haijawahi kuwa rahisi kama unavyo fikiria, isitoshe watu wameacha vitu vyte vya kum trace kwa simu na gari lake mkuu
Ukiwa kwenye risk ya kutekwa ni vizuri kujiwekea mfumo wa kujitrak mfano body camera,chips,bodyguard, 360 inside and outside car camera.
 
Matajiri wengi ujichunguza ishu huwa watekaji wanadai Pesa nyingi ukifatilia crime and investigation
 
Wewe ni kiduchu cha akili kweli kweli walahi
Ndio maana lijamaa la ubeligiji likawaita boys, mtu mzima ovyo kabisa walahi
 
Kumbuka kuna raia wako vizuri kwenye crime and investigation kuliko hata askari, penye wengi hapaharibiki kitu,Ukiwaambia raia watoe ushirikiano bila kuwapa ushirikiano ni kuwadhiaki.
Nishasoma article ya mzee aliyekua anamfuatilia mtekaji wa watoto kwa kupitia CCTV camera na akampata. Hivyo ni kweli kuna raia wako vizuri.
Ila alifanya huku askari wakiwa washaona ile ni cold case wameachana nayo na hawakuomba msaada, mzee alifanya bila shinikizo. Kama kuna raia ana uwezo inatakiwa afanye kisha apeleke tip kwa askari.

Wakiona wana uhitaji na tips kutoka kwa raia pengine watafanya open investigation, probably tutakua tumeshachelewa lakini.
 
Shida ya hawa wapanga matukio hua hawanaga uwezo mkubwa wa kufanya matukio ndo maana wwnaishia kuumbuka yani hapa kuna kila dalili za dola kuhusika sema ndo hauwezi kusema yani kiongozi mkubwa akiwa na uwezo mdogo bila shaka huwaambukiza na viongozi wake wa chini
 
Unajua wapo RAIA ni ma ex soldiers, ma ex criminal and investigation wa international firm,wengine wana links na international organization za investigation, wengine wana natural IQ kuhusu investigation, wengine ni wazuri kwenye supernatural power nk.
Nishasoma article ya mzee aliyekua anamfuatilia mtekaji wa watoto kwa kupitia CCTV camera na akampata. Hivyo ni kweli kuna raia wako vizuri.
Ila alifanya huku askari wakiwa washaona ile ni cold case wameachana nayo na hawakuomba msaada, mzee alifanya bila shinikizo. Kama kuna raia ana uwezo inatakiwa afanye kisha apeleke tip kwa askari.

Wakiona wana uhitaji na tips kutoka kwa raia pengine watafanya open investigation, probably tutakua tumeshachelewa lakini.
 
Usipokuwa makini unaweza kusema hivi "ni kama vile kuna mpango mkakati wa kutenganisha MATABAKA baina ya MATAJIRI, MASKINI, WATAWALA na WATAWALIWA.
NDIPO WALALA HAI NA WALALAHOI KILA MMOJA ATATAMBUA NAFASI YAKE
Soko la Mbaazi la Manji limewaumiza sana wakulima wa Kusini.
Watoto walikuwa wanaenda shule bila bugdha.
Chakula kilikuwa kinapatikana.
Nyumba za kisasa zilikuwa zinajengwa.
Watu walianza kufulahia maisha, ghafla bin vuu, Mbaazi zikakosa soko, wanunuzi wakajitoa, aliyetafuta soko kabanwa huku na huku.
Umasikini ukarudi tena kwa wananchi. Morali ya kilimo ikashuka.
Mimi nasema hivi, hawa matajiri kama wanatuhumiwa jambo fulani basi washughulikiwe kwa staha, nasikia hata huko jera kuna vyumba vya VIP.
Wakulima walianza kuchimba visima vya umwagiliaji kwenye mashamba yao.
Mimi pia nilichimba kisima kimoja kwenye shamba langu tayari kwa kuendesha kilimo cha kisasa na ili nizalishe mbaazi kwa wingi.
Sikuwa na haja na kazi ya mtu, kilimo kilikuwa ajira tosha kabisa kwa kujitodheleza kiuchumi.
Sasa nimerudi tena mjini kubangaiza, mazao mengine hayana soko kabisa, gunia la mahindi ni 20,000/- na linakosa soko vilevile.
Manji yuko mtaani na kipato cha mwananchi kimekufa.
Ndio maana kuna kiongozi mmoja watu wanamchukia sana sana, mwenyewe hajui kwanini anachukiwa hivi, chuki nyingine zinatokana na mambo kama haya ya kutukimbizia wateja wazuri wa mazao yetu.
Viongozi lazima muwe makini, kwa kauli zenu, na maamuzi yenu mnayoyafanya, mengine yana athali kubwa kwa wananchi.
Mwananchi hawezi kumchukia kiongozi bila sababu, kwani nchi hii chuki za ukabila, udini, ukanda hazipo.
Mambo mengine ni bora kuyachukulia kirahisi kwa mustakabari wa kuinua uchumi wa taifa au mtu mmoja mmoja.
Ona Raisi wetu mpendwa alivyoamua kuwaacha Wamachinga kuuza biashara zao maeneo mengi sana ambayo mengine ni karibu na barabara na kusababisha kero kwa usafiri wa magari , pikipiki na watembea kwa miguu.
Ingawa kuna kero lakini wamachinga wamepata fulsa ya kujiinua kiuchumi.
Kama ni hivyo, Manji angeshughulikiwa kwa staha, ili wanachi wengi tunao nufaika na biashara zake tuendelee kunufaika.
Wamachinga na Wakulima wote ni raia wa Tanzania na wanastahili kulindwa kwa kila kinacho waingizia kipato, bila kujari sana hasara nyepesi ya upande mwingine.
Hawa matajiri ni hazina ya nchi na wanachi wake.
Bila matajiri hakuna maendeleo, dunia yote ina waheshimu na kuwalinda kwa hali na mali, kama wamehalibu mahali basi wanachukuliwa kwa uzito wa kipekee wasije yumbisha uchumi kama uchumi wa wakulima wa Mbaazi.
Viongozi kuweni makini na maamuzi yenu, hatima ya mwananchi ipo mikononi mwenu.
Kwa sasa tunamuhitaji sana MO.
 
Hiyo No.6 ni tatizo kubwa kwenye matukio kama haya. Kumbuka katika tukio hili mtu huyohuyo alitoa taarifa kwamba Mo ameshapatina kitu ambacho siyo kweli. Kachukuliwa hatua gani kwa kusababisha mkanganyiko huo? Huyu haguswi ingawaje siyo mtu makini kwenye matukio anayoshiriki. Ni mtu ambaye hawezi kuficha vitendo dhanifu vya uhalifu (conduct) baada ya kutenda.
Huyu tumemuachia Guru Nanak subiri KARMA
 
Hii nchi ishafananishwa na nchi ya wajinga tena watu wasio na akili ndio wamepewa madaraka makubwa kuongoza wenye akili.

Polisi wanasema tutoe ushirikiano kwa lipi labda?

1. Wametoa plate namba za magari wanayoyahisi?
2. Wametoa cctv footage kuomba msaada wa raia?
3. Hawana teknolojia ya satelite kufatilia mwenendo wa gari ilimbeba mo?
4. Hawana picha hata rangi ya gari inayohusishwa?
5. Hao wazungu wakoje? Nchi hii ina idadi kubwa ya wazungu kushindwa kuwatambua?
6. Waliomteka saa roma mpaka leo walishapatikana baada ya makonda kutoa mda je makonda alishawai kuhojiwa?

7. Hiyo risasi na ganda lake hazina usajili kujua ni nani kamilikishwa

Huo ni msaada gani wakati mnasema jeshi la kisasa au ni jeshi la kisiasa?

Bila shaka naamini wahusika ni serikali yenyewe wananchi tunazugwa tu
Angalia wasije kukuzingira
 
What???![emoji116]....... Tanzania tupo katika hali mbaya kuliko hata tunavyodhania!!
Screenshot_20181013-102139~01.jpeg
 
What???![emoji116]....... Tanzania tupo katika hali mbaya kuliko hata tunavyodhania!!
Screenshot_20181013-102139~01.jpeg
 
Kwa vile kila mtu yuko entittled kutoa mawazo yake acha na mimi nitoe yangu, MODS MODS MODS mjifunze kuvumilia mawazo tofauti na mpungeze kuunganisha nyuzi.
Watoto kila siku wanapotea,watu wazima wanapotea, wengine wanatekwa mara Nondo mara Roma.
Tuseme Mo akaamua kutumia nafasi yake kwenye jamii na kuamua kuaddress tatizo kwa njia ambayo wengi hatukutegemea, yaani akastage utekaji na kila kitu, na hili kulifanya tukio likaribiane na ukweli basi ikabidi hata familia yake hasiishirikishe ili kuongeza awareness kuhusu matukio ya utekaji yanayoshika kasi kwenye jamii.
Wakuu naomba ije kuwa hivi ili Mo arudi akiwa salama bila kuumia hata kucha.
 
Back
Top Bottom