CCM ina mizizi mirefu mno, CCM wanalindwa na Dola, CCM wana nguvu ya msajili wa vyama, CCM wanalindwa na mkurugenzi wa uchaguzi, CCM wamefanikiwa kupandikiza woga kwa watanzania WOTE! Hivyo hata kije chama gani, bure tu!
Hao loyal wa Magufuli watajuta kupinga katiba mpya na tume huru🤣🤣🤣
CCM sio li-dude au li-mashine furani complex. Ni watu tuu walioji'organize tangia hapo na Watu ni binadamu na binadamu hubadirika
Kuna genge ndani ya CCM linatajwa kuunda Umoja Party kuendeleza Umagufuli Tanzania, sasa kati ya vitu muhimu ambavyo Magufuli anakumbukwa navyo ni kuzuia vyma vya siasa kujieneza kwa kupiga marufuku mikutano yao pamoja na sheria kali za vyama
Magufuli mara nyingi alisikika akisema CCM itatawala milele na alichukulia wanaoikosoa CCM kama ni wahaini wasiotakiwa kuonewa huruma, Umoja Party hawaoni watakuwa wanasaliti maono ya Magufuli?
pia watashinda vipi uchaguzi? Magufuli alianzisha ujtaratibu wa kuchagua makada wa CCM kuwa Wakurugenzi ambao ndio watakuwa wanasimamia uchaguzi na kutangaza matakoeo, na kamwe hawatatangaza mtu wa upinzani labda CCM yenyewe iamue kuwaachia, je Umoja Party watashinda vipi hata kiti kimoja cha ubunge kwa misingi hii ya Magufuli?
Kuanzisha chama cha upinzni kumuenzi Magufuli ni usaliti mkubwa kwa Magufuli ambaye alikuwa akiona upinzani ni maadui
Alifariki tena akiwa CHADEMA
Bado muda wa kufanya hivyo, vumiliaKama Ni wa kweli wajiuzuru wajiunge na hicho chama. Halafu wabunge gani hao, wa hili bunge la CCM . Tusubiri tuone.
Alifariki Apumzike kwa Amani
Bado muda wa kufanya hivyo, vumilia
Safi sana, hii ndiyo demokrasia tunayoitaka Tanzania.
Wameshajifunza.. Hili kundi la Samia kulitoa madarakani labda jeshi liingilie kati.Hili suala la kukataa katiba mpya na mfumo mpya kabisa wa utawala Tanzania limewaliza wanasiasa wengi na bado litaendelea kuliza wengine. Ni suala la muda, na ni kundi gani liko jikoni tu. Lowassa baada ya kutemwa na CCM alikiona cha mtema kuni na akabaki kulialia wakati alikuwa na uwezo wa kubadilisha mfumo kabla. Haya, Magufuli naye alipokuwa jikoni, timu Msoga na kina Kinana walikuwa wanalialia. Likatokea lililotokea na sasa wako jikoni, gemu limegeukia kwa timu mwendazake. Na timu Samia nayo isipokubali kuleta mabadiliko ni jambo la muda tu wanaweza kujikuta kwenye wakati mgumu kuliko makundi mengine yote yaliyopita.
Falsafa ya Magufuli ni zipi?Watu hawatii marehemu wanatii falsafa zake za uongozi. Kwa kuwa yeye ndo alianzisha aina hiyo ya uongozi watu sasa wanapitia kivuli chake kujipambanua/kujinadi Kwa jamii.
Si mtiifu wa marehemu. Ni watiifu Kwa maono aliyoyaamini marehemu. Matendo MAZURI ya mtu HAYAFI kamwe. Mf Hadi Leo Mandela anatajwa Afrika nzima Kwa aliyoyatenda.
Daah masikini, RIP
Duuh Mungu aweke mahali panapostahili roho yake! asante kwa taarifa
NDOTO YANGU YA ALFAJIRI
..Ninasikia nyimbo za mapambio kwa mbaaali sana.. ghafla ninawaona Chadema na ACT wakitangulia mbele na msalaba, mashada ya maua. Sanduku lina rangi mbili likiwa limebebwa kwa UMOJA wakielekea malaloni. Ninajaribu kusogelea kwa karibu ninakuta ndio wanamalizia shughuli ya kupumzisha mwili.
Mwisho ninayasikia maneno haya toka kwa waombolezaji
"Vita umeipigana, pumziko la milele liwe nawe"
Bwana ametoa, wana ametwaa
Ninashtuka toka usingizini ninaangalia saa yangu inasoma saa 10 alfajiri, tar 20 April 2022. Ninakwenda kuhakikisha kama nilifunga mlango vizuri ninakunywa maji ninarudi tena kulala.
UP imeshaanza kuwapa pumzi ya moto
Hujui lolote wewe!Muulize Membe alidhani kuchukua madaraka Ni kazi nyepesi akaishia kupata kura elfu tisini. Mtu ambaye aliiyingisha CCM Ni Lowassa tu wengine Ni wafa maji. Hicho chama kimepewa karipio kwamba kimeanza harakati bado hakijasajiliwa.