DART Special Thread: Tunaomba Maoni Ushauri, Malalamiko, Pongezi na Mapendekezo kuhusu Mabasi ya Mwendokasi

DART Special Thread: Tunaomba Maoni Ushauri, Malalamiko, Pongezi na Mapendekezo kuhusu Mabasi ya Mwendokasi

Hatutaki mkandarasi anayejenga mwendo kasi ya mbagala aje kujenga ya Tegeta, kwa sababu sipendezwi na spidi yake. Ni hilo tu.
Hayo ya mkandarasi hayawahusu DART watafute wazee wa 10% ndio wahusika
 
Naomba ufafanuzi hua sielewi kwanini mnakatisha ruti ya Mbezi kutoka Gerezani au kivukoni sa 2 : 30 ilihali abilia ni wengi ila mnataka afike kimara achukue gari nyingine. Hii inafanya mnapoteza fedha kwa sababu kuna baadhi akifika kimara kachoka kusubiri gari zenu mpaka zijae tena anahisi uvivu anaamua kwenda kupanda bajaji n'je kwanini kusiwepo na gari mpaka sa 4 : 30 angalau abiria wanaweza kua wamepungua kuliko kukatisha ruti ilhali bado kuna abira wengi.
 
Naomba ufafanuzi hua sielewi kwanini mnakatisha ruti ya mbezi kutoka gerezani au kivukoni sa 2 : 30 ilihali abilia ni wengi ila mnataka afike kimara achukue gari nyingine. Hii inafanya mnapoteza fedha kwa sababu kuna baadhi akifika kimara kachoka kusubiri gari zenu mpaka zijae tena anahisi uvivu anaamua kwenda kupanda bajaji n'je kwanini kusiwepo na gari mpaka sa 4 : 30 angalau abiria wanaweza kua wamepungua kuliko kukatisha ruti ilhali bado kuna abira wengi.
Sio kweli huwa wanakatisha kwenye saa nne hivi na wanarudisha huduma saa tisa na nusu, na kwakweli mimi naamua kuwatetea muda huo abiria wa moja kwa moja ni wachache sana, ni bora wapande gari mbili tu
 
Nyie dart mbona mmekosa utu, yule jamaa mliyemgonga na video yake kusambaa kumbe mkewe aliwaomba muwe mnamsafirisha bure kwenda muhimbili kumpelekea chakula mumewe mkagoma
 
Hivi zile kadi za mwanzo zilizokatishwa huduma ghafla na bado zilikua na hela mnafidia vp au ndio tuandike maumivu
Mimi kadi yangu ilikua na shilingi 30k
Je huduma ya kadi itarudi au ndo imekufa
 
Kwa sasa kazi zinaendelea kukamilishwa ikiwemo kumalizia ujenzi wa vituo vya kupandia na kushuklia abiria na kazi nyingine ndogo ndogo, muda ukifika wananchi watatangaziwa.
Najua tutatangaziwa ila mimi nlikuwa nataka tu kujua kwa makadirio yenu nyinyi mnadhani ni lini au mwezi gani mtakuwa mmekailisha ujenzi na kuanza root
 
Nilikuwepo Dar tangu tarehe 24-28 may 2023 nilifikia Kimara Suka na nilikuwa nahudhuria mkutano pale Diamond Jubilee! Kwa karibu 95% ya safari zangu nilikuwa natumia usafiri wa wa UDAR! Kwakweli nashukuru safari zangu zote nilipata huduma nzuri! Hongereni mnajitahidi!
 
Ndio ilivyo unalipa 750/- pale Kibaha na tiketi haichanwi unakuja kimara unaendelea na safari ama kwenda gerezani au kivukoni!!! Swali kwani huwezi safiri kwa bei hiyo kutoka kivukoni/gerezani kwenda kibaha? Fanya utafiti kabla ya kuropoka!!!
wewe ndio ujuelewi tiketi ya combo tu kutoka mbezi hadi gerezan ni 750+500 unalipa 1250 ndio utoke kibaha hadi gerezani kwa 750 labda ungesema unalipa tiketi mbili ya 700 kutoka kibaha hadi kimara na pia unalipa 750 kutoka kimara hadi gerezani jumla 1450 halfu iyo ya 750 unakuja kuchaniwa kimara ndio ningekuelewa lkn sio kibaha to gerezani kwa 750
 
Jaribuni kusimamia foleni za kupanda kwenye magari, hasa vituo vya mwanzo wa safari.
Vilevile kuongeza idadi ya magari hasa peak hours.
 
Jaribuni kusimamia foleni za kupanda kwenye magari, hasa vituo vya mwanzo wa safari.
Vilevile kuongeza idadi ya magari hasa peak hours.
Tunashukuru kwa ushauri wako tutaendelea kusimamia jambo hili kwa umakini zaidi , aidha zipo jitihada za kuhakikisha idadi ya mabasi inaongezeka tunawaomba mvute subra wakati huu serikali yenu ikipambana kuhakikisha kila jambo linakuwa sawa ikiwemo hili la kuongeza idadi ya Mabasi.
 
Nilikuwepo Dar tangu tarehe 24-28 may 2023 nilifikia Kimara Suka na nilikuwa nahudhuria mkutano pale Diamond Jubilee! Kwa karibu 95% ya safari zangu nilikuwa natumia usafiri wa wa UDAR! Kwakweli nashukuru safari zangu zote nilipata huduma nzuri! Hongereni mnajitahidi!
Tunashukuru kwa pongezi japo huduma bado haijafika katika viwango stahiki, tunaendelea na jitihada za kuongeza idadi Mabasi ama kwa hakika muda sio mrefu mambo yatabadilika kabisa.
 
wewe ndio ujuelewi tiketi ya combo tu kutoka mbezi hadi gerezan ni 750+500 unalipa 1250 ndio utoke kibaha hadi gerezani kwa 750 labda ungesema unalipa tiketi mbili ya 700 kutoka kibaha hadi kimara na pia unalipa 750 kutoka kimara hadi gerezani jumla 1450 halfu iyo ya 750 unakuja kuchaniwa kimara ndio ningekuelewa lkn sio kibaha to gerezani kwa 750
Mimi na watu wote wanasafiri hivyo. Pale kibaha kuna tiketi ya 750/- haichanwi pale inakuja kuchanwa Kimara! Mimi nimesafiri hivyo na ndio sbb ya mshangao niliouelezea!!!
 
Asante kwa kuja.
Ni lini hayo mabasi mtayapeleka Mwanza pia ili wananchi wapate huduma ya usafiri..??
Sababu jiji la Mwanza limekua na tayari limechangamka na mkituletea hizo Bus zikaanzia route ya Kisesa, Igoma, Neshno, Buzuruga, Mabatini, Nata, Pepsi, Mkuyuni, Nyegezi, Buhongwa, Nyashishi hadi Usagara and Return.
Wewe Kweli unatoka hood MOYA na Mimi.....

Nimetoka huko kitambo sanaa 😊😊😊
Way back 🔙
 
Tunashukuru kwa pongezi japo huduma bado haijafika katika viwango stahiki, tunaendelea na jitihada za kuongeza idadi Mabasi ama kwa hakika muda sio mrefu mambo yatabadilika kabisa.
There is any information kuhusu kuanza Kwa huduma ya mwendokasi mbagala route??

Best regards
 
Wewe Kweli unatoka hood MOYA na Mimi.....

Nimetoka huko kitambo sanaa 😊😊😊
Way back 🔙
Nami nimeondoka rasmi mwaka 2000, na skuizi pamebaki kama njia tu pamoja na kwenda kuwaslimia wazazi.
But Mwanza inajengeka kwa kasi sana....
 
Ongezeni mabasi ili kuondoa msongamano vituoni usio na lazima! Hasa hasa Kariakoo na Kivukoni kwa jioni,harafu Mbezi,Kibaha,Morocco,Kimara kwa asubuhi.
 
Thread imekua kama danganya toto tu hata ikifutwa haina maana.. hoja na maswali ya msingi unaruka unijibu maswali mepesi, basi zinajaza mno kama mikungu ya ndizi hata ule u special wa huduma unakua hamna
 
View attachment 2625074
DART Tumeanzisha ukurasa huu rasmi wa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa lengo la kupata maoni, ushauri , mrejesho na hata malalamiko yanayohusu huduma zetu. Aidha tunawahakikishia watumiaji wa huduma zetu kuwa maoni, ushauri, malalamiko, Pamoja na hoja zenu juu ya huduma zetu yatafanyiwa kazi kwa uharaka na hatua stahiki zitachukuliwa ili kuboresha huduma.

Kwa kupata msaada wa haraka kuhusu huduma zetu unaweza kutupigia simu 0800110147 ni bure. Kuanzia saa 11 alfajiri hadi saa tano na nusu usiku

Pia unaweza kutufuatilia katika tovuti ya www.dart.go.tz na mitandao yetu ya kijamii ya Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka ya FACEBOOK, INSTAGRAM, TWITTER, LINKEDIN, YOUTUBE.

Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka

Anuani
S.L.P 724, 16103
Ubungo Maji, Morogoro Road
Dar es Salaam, Tanzania

Barua pepe: info@dart.go.tz.

#usafiri wa umma nadhifu

#mwendokasi app
Huduma either imewashinda au mnafanya kwa mipangilio yenu wenyewe.

Labda km mmebadili hii mifumo ndani ya miezi miwili hii ambayo situmii huduma yenu.

1). Mfumo mbovu wa ukataji wa tiketi, yaani nyie na makonda wa daladala za kawaida hamna tofauti ( hamuwezi kucontrol mapato, na ni UHUJUMU UCHUMI )
2). Idadi ndogo ya mabasi yanayotoa huduma, waiting time was supposed to be less than 5 minutes kwa sasa mtu anaweza kusubiri dk 40 mpk saa zima during normal times and 15 - 30 minites during the peak times
3). Mfumo hafifu au mbovu wa upakiaji abiria, huwezi kuwasimamisha watu kwenye foleni kwa muda zaidi ya masaa , wekeni viti vya kutosha vilivyo kwenye mpangilio ili watu wasiende kazini wamechoka
4). Mnapaswa kuanzisha magari maalumu kwa wahitaji maalumu, mfumo uliopo sasa umefeli, kwasbb viti ni vichache, na hawa wenye uhitaji watafnikiwa kupanda tu kwenye terminal, ila vituo vya kati hawatoweza kupata nafasi maaalumu,
Mwiba wa tatizo hili ni kuanzisha gari za wenye uhitaji
5). Ongeeni na mamlaka husika wawese kuanisha kadi za malipo za vivuko, viwanjani, na hapo kwenu huduma zozote.
Mtatupunguzia mizigo

Ahsanteni
 
Back
Top Bottom