Daudi Ballali's Death

Daudi Ballali's Death

Status
Not open for further replies.
Naomba unijibu...ZITTO ALIMWAKILISHA NANI KWENYE ZIARA YAKE ALIYOALIKWA NA STATE DEPT??


Sasa na wewe unataka kuanzisha jambo jingine, nani alikuambia Zitto amekuja kumwakilisha mtu yeyote? Kabla hujaanza kujibu tafuta press statement kwenye ubalozi wa Marekani Tanzania na utajua Zitto alikuja kwa ajili gani na kama alikuja kuwakilisha kitu alikuwa anawakilisha nini. Na hilo unaweza kulianzishia mada nyingine kwani hii inahusu mazishi ya Ballali.

So, thank you but no thank you.
 
Sasa na wewe unataka kuanzisha jambo jingine, nani alikuambia Zitto amekuja kumwakilisha mtu yeyote? Kabla hujaanza kujibu tafuta press statement kwenye ubalozi wa Marekani Tanzania na utajua Zitto alikuja kwa ajili gani na kama alikuja kuwakilisha kitu alikuwa anawakilisha nini. Na hilo unaweza kulianzishia mada nyingine kwani hii inahusu mazishi ya Ballali.

So, thank you but no thank you.

Ok naona unatofautiana na Mwafrika wa Kike kwenye uwakilishi wa Zitto!
Nia yangu hapa si mbaya!
Ila State Dept waliniambia kuwa mtu ambaye ni Diplomatic anayeiwakilisha serikali/nchi anaweza kupewa taarifa zote zinazohusu mambo ya uchunguzi wa Ballali na mahali alipo!
ONLY KAMA WAKIULIZA!
 
Jaribu kusachi Daudi Makange uone utapata nini mkuu!

Why not search for "Daddy Yankee Nyaga" "Puff Daudi Yankinyaga", etc etc? And if none of those turn up anything useful, try "Daudi Yankee"/"Daddy Kinyaga"/""Puff Daudi" or some such similar combinations from celeb names having "Daddy" in them. Or even "Daddy Makande" for godsake!
 
unaonaje ukianzisha thread ya kuomba msamaha wana JF na hao vijana..

kwi kwi kwi kwi....

Nitafanya hivyo...Ila kwasasa bado tuna majukumu ya kuendelea kusisitiza kuwa wananchi nao wanataka kujua ukweli ili tusiendelee kuibugudhi familia ya Ballali ambao sasa hivi wanahitaji msaada wa kuwaliwaza!
 
Daudi Kinyaga na Muthoni munyi wanafahamiana na Ballali na wamekuwa wakiwasiliana na kuachiana jumbe kwenye web!
Hivyo basi haya mambo yote ni familia nao wamejitakia!
Uamuzi wa kukaa kimya mpaka afe na huku wakiendelea kufanya siri kubwa..The hakuna wa kulaumiwa pale watu wanapo pekenyua pekenyua kivyao vyao!


Mushi,

You are a liar and rumour monger!

About 10 hours ago, you had posted a thread about same thing that Kinyaga is Ballali and Ballali is Kinyaga. Ukagundulika kuwa ni mfupi wa kuelewa mambo na ukaonywa acha kuzusha mambo ambayo hujui. Now you are bringing the issue again!
 
Ok naona unatofautiana na Mwafrika wa Kike kwenye uwakilishi wa Zitto!
Nia yangu hapa si mbaya!
Ila State Dept waliniambia kuwa mtu ambaye ni Diplomatic anayeiwakilisha serikali/nchi anaweza kupewa taarifa zote zinazohusu mambo ya uchunguzi wa Ballali na mahali alipo!
ONLY KAMA WAKIULIZA!

Si lazima tukubaliane kila kitu na Mkjj...

Jaribu tena kufuatilia uone kama hili pia ni kweli. Sitaki kukuanzishia debate kwenye hili hapa kwenye hii thread ya Balali BUT kama ukianzisha thread kwa ajili ya hili, I will be more than happy kuonyesha the other side of this issue.

Natumaini hata ndugu yangu Kuhani Mkuu atakuja kusaidia kutoa maelezo kwenye hiyo thread.
 
Nitafanya hivyo...Ila kwasasa bado tuna majukumu ya kuendelea kusisitiza kuwa wananchi nao wanataka kujua ukweli ili tusiendelee kuibugudhi familia ya Ballali ambao sasa hivi wanahitaji msaada wa kuwaliwaza!

Asante Mkuu,

Nimekuelewa!
 
Ok naona unatofautiana na Mwafrika wa Kike kwenye uwakilishi wa Zitto!
Nia yangu hapa si mbaya!
Ila State Dept waliniambia kuwa mtu ambaye ni Diplomatic anayeiwakilisha serikali/nchi anaweza kupewa taarifa zote zinazohusu mambo ya uchunguzi wa Ballali na mahali alipo!
ONLY KAMA WAKIULIZA!

walikuambia ukweli; na mtu anayeiwakilisha nchi au serikali kwenye nchi nyingine anaitwa B A L O Z I na ndiyo anakuwa na hicho "Diplomatic cover". Zitto aliteuliwa lini kuwa Balozi? Naomba usijibu hapa bali anzisha mada nyinginie kuhusu Zitto na ubalozi na itakuwa furaha yangu kukusaidia kuelewa kuwa ingawa Mbunge ana pasipoti ya Kibalozi lakini ki protokali haiwakilishi nchi katika nchi nyingine.

Of course anaoujiko wa aina fulani lakini yanapokuja maswali ya serikali to serikali wanaouhusika ni balozi. So ningekuwa mimi wewe ningewauliza ubalozi wetu DC au NY.
 
Hili ni swali zuri sana mkuu wangu Mushi.

Zitto aliwawakilisha watanzania kwenye ziara yake hapa US na kama kumbukumbu zangu zinavyoonesha, alikutana na watanzania wengi kila mara alivyokuwa akimaliza mikutano yake.

Sasa kama aliwawakilisha watz..Then kwanini hakuwawakilisha kwenye kilio chao kuhusiana na ufumbuzi wa suala la Ballali?
Kwanini hakuitumia nafasi hiyo kuwaambia kuwa kilio cha watanzania kuhusu ripoti za Ballali ni kikubwa sana?
 
Mushi,

You are a liar and rumour monger!

About 10 hours ago, you had posted a thread about same thing that Kinyaga is Ballali and Ballali is Kinyaga. Ukagundulika kuwa ni mfupi wa kuelewa mambo na ukaonywa acha kuzusha mambo ambayo hujui. Now you are bringing the issue again!

Mchungaji.. maneno makali hayo.. msamehe kijana wetu na umuombee tu alighafikirika kidogo lakini baadaye mwanga wa ukweli umemzukia. Kwa hiyo, nadhani amejifunza na atajitahidi kuwa na roho ya unyenyekevu kidogo ili anapokoselewa awe na haraka ya kuona kosa lake na isikuchuku masaa au siku nyingi kutambua amekosea.
 
walikuambia ukweli; na mtu anayeiwakilisha nchi au serikali kwenye nchi nyingine anaitwa B A L O Z I na ndiyo anakuwa na hicho "Diplomatic cover". Zitto aliteuliwa lini kuwa Balozi? Naomba usijibu hapa bali anzisha mada nyinginie kuhusu Zitto na ubalozi na itakuwa furaha yangu kukusaidia kuelewa kuwa ingawa Mbunge ana pasipoti ya Kibalozi lakini ki protokali haiwakilishi nchi katika nchi nyingine.

Of course anaoujiko wa aina fulani lakini yanapokuja maswali ya serikali to serikali wanaouhusika ni balozi. So ningekuwa mimi wewe ningewauliza ubalozi wetu DC au NY.

OOps!
Mada yangu ya majukumu ya ubalozi ulichangia?
MKJJ Nimepiga simu ubalozi na kuzungushwa sana!
Mwishowe wakanipatia Joseph Sokoine ambaye anahusiana na mambo ya siasa!
Na yeye akanijibu kisiasa...Kuwa eti niandike barua ya maelezo ya malalamiko yangu!
The rest unajua..Habari za kifo zikatangazwa kesho yake!
Sasa mimi binafsi nisijiulize?
 
Mchungaji.. maneno makali hayo.. msamehe kijana wetu na umuombee tu alighafikirika kidogo lakini baadaye mwanga wa ukweli umemzukia. Kwa hiyo, nadhani amejifunza na atajitahidi kuwa na roho ya unyenyekevu kidogo ili anapokoselewa awe na haraka ya kuona kosa lake na isikuchuku masaa au siku nyingi kutambua amekosea.

Mwenzetu yuko kwenye mission hapa na so far naona facts zinakuwa nyuma sana kwenye arguments zake. Taratibu tu ataelewa na kama kwa kuwa ana nia nzuri na taifa la watanzania basi atakuwa pia mstaarabu asiharibu majina ya watu wasiokuwa na hatia.
 
...kama ukianzisha thread kwa ajili ya hili, I will be more than happy kuonyesha the other side of this issue.

Natumaini hata ndugu yangu Kuhani Mkuu atakuja kusaidia kutoa maelezo kwenye hiyo thread.

Kama ambavyo huwa unasaidia kutoa maelezo ya ndugu yangu Mwanakijiji! LOL

Ambaye sijawahi hata siku moja kukuona unatafautiana nae.
 
Jamani,

Naomba tumsamehe Mushi. Ni mwanafunzi ambaye anajaribu kujifunza mambo ya ulimwengu huu. Tumvumilie kwa ajizi na ung'ang'anizi wake ambao unaonekana kuwa ni wa kupotoka.

Mushi, jifunze kuwa msikivu, Mungu atakujalia uwe mahiri na hodari kwenye kazi zako.
 
Wakuu,

Inanisikitisha kuwa JF inageuzwa kuwa jamvi la hovyo hovyo. Nimesoma thread zote tangu Mkuu Mwanakijiji alivyotuarifu kuhusu taarifa za mazishi na kweli sipendezewi na mwenendo huu.

Mwanakijiji alisema vizuri...Ballali amekufa bila kushtakiwa hivyo ni raia huru. Kama wengine hatupendi hili, basi tuondolee uvivu vyombo ambavyo havikuweza kumshtaki na kumtia hatiani. Kama wengine hatuamini kuwa amekufa, basi endelea kuamini hivyo na kwa wanafamilia (na wengineo ambao wanaamini amekufa) wapeni nafasi ya kumaliza msiba wao.

Imedhihirika kuwa tunapoteza utu, mwelekeo, heshima na busara. Tukianzia na utu, desturi zetu zinaheshimu wafu, shughuli za msiba (hususan kwa wanafamilia) na maziko. Kama ukipata nafasi kuangalia tovuti ya nyumba ya mazishi tuliyopatiwa na Mwanakijiji, utaona kuwa haya mazishi na kila kitu ni private. Sasa kama wanafamilia wametaka iwe private, kwanini tuingilie? Inanishangaza kuwa watu wanafuatilia kuona ni state ngapi Ballali aliishi na kuna connection gani kati ya Ballali na watu wengine. Nafikiri hata kama wanaJF hawa wana nia nzuri, nafikiri imevuka mpaka kufikia kitu kinachoitwa stalking Hii ni kuivunjia hadhi JF na ni sawa na mapaparazi wenye kutafutia picha za uchi za celebrities kwa tabloids.

Baada ya kusema hayo, ningependa nisieleweke kama sina uchungu na nchi yangu au wizi uliotokea BoT. Lakini naamini kuwa tunapoteza mwelekeo. Bila kujali kuwa Ballali amefariki au la, yeye ni "tip of an iceberg". Kuna wengi waliohusika na ufisadi, wapo bado wanadunda tu na mali walizoiba, wengine bado wapo madarakani. Hivi kweli nguvu na juhudi zetu zielekezwe kwa Ballali ambaye haikujulikana alipo, hakuwa na nguvu kutokana na ugonjwa, na sasa tunaambiwa amekufa? Mch. Kishoka na wengineo waliuliza, mbona tumewaacha kina Meghji, Mramba, Mgonja, Yona, Mkapa, Chenge, Jeetu na wengine wengi? Naamini tuna uwezo wa kutambua zaidi ya kifo cha Ballali. Hivi kama kweli amekufa, na kuzikwa hiyo kesho, tutapata nini? Siri amekufa nayo (labda), pesa zimeibwa...tunataka tumfufue ili ajibu tuhuma?

Nilifadhaishwa pale mkuu Mushi aliposema "nobody cares" about MwK's friend. Personally I believe this is the lowest point of humanity na huyo asemaye hivyo hana tofauti na mafisadi wanaoliibia taifa. Inawezekana huyo rafiki wa MwK hatumjui wala hatuhusu, lakini ukweli ni kuwa kuna watu aliwagusa, akiwemo MwK ambaye ni mwenzetu. Kukebehi kifo chake kutotangazwa ni sawa na mafisadi wakisema "sijali kuwa watu wa Chole Samvula hawatapata zahanati kutokana na kuiba kwangu fedha za umma. Mimi naishi Dar."

Basi ombi langu ni kwenu wanaJF tuendelee na kuendeleza nchi yetu, Ballali aachwe apumzike kwani kuna wengi tu ambao ni wabaya zaidi yake na bado wanatucheka. Tuwe na usongo na hao.
 
Kama ambavyo huwa unasaidia kutoa maelezo ya ndugu yangu Mwanakijiji! LOL

Ambaye sijawahi hata siku moja kukuona unatafautiana nae.

kwi kwi kwi..

Mwenzako niko kwenye competition hapa na Lydia Ngosha kisha unataka nijiharibia na nianze kupingana na Mkjj.

Kuhani, unapingana na mtu pale ambapo kuna cha kupinga. Siwezi kuanzisha tu ugomvi na Mkjj ili nionyeshe watu kuwa napingana naye. BTW, this is the baddesst boy ambaye amewapa 'em boyz kule serikalini hell kwa kiwango kikubwa. Kama Lowasa alishindwa mimi nitaweza .....lol
 
una hakika na hili?

Unayajua yote aliyofanya Zitto alipokuwa hapa kwa mwaliko huu? una script ya mazungumzo yote aliyofanya hapa US?

Unaona?
Tumerudi tena kwenye yale mambo ya siri!
Nimeshasema kuwa siri ambazo hazimsaidii wala kuwahi kumsaidia mtanzania wa kawaida hazina mpango!
Misiri miiingi...Na ile ya KAMATI YA MADINI JE? mIsIrI mIiNgIi!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom