Daudi Ballali's Death

Daudi Ballali's Death

Status
Not open for further replies.
..wasamehe,si makosa yao! and the msg is sent!

Hata mimi naona daily news wasamehewe tu! ila next time watoe majina ya source zao na ikiwezekana waseme jamii forums ili kusaidia kuitangaza kwa wale ambao hawajajua mabadiliko toka jambo kwenda jamii!
 
Kwi kwi kwi kwi...

naona unataka kuingia mkenge mkuu wangu!
fuatilia vizuri chanzo chako maana unapotezwa. Angalia usiwe kama Mushi aliyeanza kuwachafua vijana wa watu hapa kuwa wanahusiana na Balali.

Ni ushauri tu!

Unaanzisha utani halafu baadae unachukulia vitu seriously. You never get me MWK, damn! Chanzo changu cha habari kimenitumia intelligence kwamba Lydia Ngosha ni fundi mitambo wa Mwnkjj, lakini ni fictitious character. Kweli, si kweli?

Kwa hiyo nilikuwa nakupeleka (was joking) tu kuhusu competition na Ms. Ngosha.

Kama unavyo penda kusema, Get it?
 
Unaanzisha utani halafu baadae unachukulia vitu seriously. You never get me MWK, damn! Chanzo changu cha habari kimenitumia intelligence kwamba Lydia Ngosha ni fundi mitambo wa Mwnkjj, lakini ni fictitious character. Kweli, si kweli?

Kwa hiyo nilikuwa nakupeleka tu (joking) kuhusu competition na Ms. Ngosha.

Kama unavyo penda kusema, Get it?

Yeah,

I get it!

I am on the mission to get in'tcha nerve yaoouuu''

Usijali mkuu nilikuelewa kwenye hili ila nilitaka kuclear minds za wasomaji. Get it?
 
Yeah,

I get it!

I am on the mission to get in'tcha nerve yaoouuu''

Usijali mkuu nilikuelewa kwenye hili ila nilitaka kuclear minds za wasomaji. Get it?

Got it baby!

I am on the mission to get inda nerve ya Mwnkjj!
 
Unaanzisha utani halafu baadae unachukulia vitu seriously. You never get me MWK, damn! Chanzo changu cha habari kimenitumia intelligence kwamba Lydia Ngosha ni fundi mitambo wa Mwnkjj, lakini ni fictitious character. Kweli, si kweli?

Kwa hiyo nilikuwa nakupeleka (was joking) tu kuhusu competition na Ms. Ngosha.

Kama unavyo penda kusema, Get it?

Mhn! Conspiracy Theories!
 
..hivi tuna sheria hiyo tayari? just asking!

Kusema kweli sina hakika, lakini nitakuwa safe nikiassume kuwa chombo kama Daily News (serikali) chenye umri mkubwa kuliko vyombo vingi, na kina wasomi wengi, watakuwa na walau mwongozo mzuri kuripoti habari.
 
Mwana kijiji nafikiri uko sahihi lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba bahati mbaya sana vyombo vya habari vya hapa kwetu mara nyingi huwa ahavitaki kutoa source ya habari ili waonekane wao ndiyo hodari kwa utafutaji wa habari lakini Michuzi namjua ni rafiki yangu yeye analijua hilo ni mategemeo yangu kuwa ataomba radhi pole sana MWANAKIJIJI
 
Good luck!

Utakuwepo Columbus memorial day? kila jina hapa JF litakuwepo akiwemo one and the only one Lydia Ngosha!

Sasa cheki ma conflict of interest yangu yalivyo changanyika:

Kwenda kwenye pati Columbus... au
Kwenda Ubalozini kuandamana... au
Kudili na Mwnkjj Columbus... au
Kufuatilia petition ya JMUSHI... au
Kudili na Latina interests, (nimeshauriwa na Brazameni, niachane na rally ubalozini...) au
Kutetea haki na kupigana na Mafisadi...

Duuuh! Nita data. Kisa, MWK. Ambae nae ana mi conflict of interest kibao. I mean nothing is guaranteed! I don't know if it worth it!
 
Sasa cheki ma conflict of interest yangu yalivyo changanyika:

Kwenda kwenye pati Columbus... au
Kwenda Ubalozini kuandamana... au
Kudili na Mwnkjj Columbus... au
Kufuatilia petition ya JMUSHI... au
Kudili na Latina interests, (nimeshauriwa na Brazameni, niachane na rally ubalozini...) au
Kutetea haki na kupigana na Mafisadi...

Duuuh! Nita data. Kisa, MWK. Ambae nae ana mi conflict of interest kibao. I mean nothing is guaranteed! I don't know if it worth it!

DC kwenye mazishi ni kesho saa nne na baadaye kuandamana kwa balozi.

Jumamosi asubuhi, kuingiza timu Columbus na kuparry hadi jumatatu wii hrs.

Jumanne kurudi kwenye libeneke na kupigana na mafisadi.

Fair?
 
.Balozi wa Tanzania Washington DC kuhudhuria

MWANDISHI WETU
Dar es Salaam

MAZISHI ya aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania Marehemu Dk. Daud Timoth Said Ballali (65) aliyefariki Ijumaa iliyopita nchini Marekani yanafanyika leo na kuhudhuriwa na wageni waalikwa pekee.

Habari kutoka Washington DC, nchini Marekani yanakofanyika mazishi hayo zimeeleza kwamba familia ya Dk. Ballali imeamua mazishi hayo kushirikisha waalikwa pekee.

Kwa mujibu wa tovuti ya KLH News inayoratibiwa na Watanzania wanaoishi nchini Marekani, mwili wa marehemu Ballali umehifadhiwa katika Nyumba ya Maziko ya De Vol iliyoko Washington DC, kabla ya kuzikwa leo.

“Kuna mwaliko katika mazishi hayo na hivyo sina hakika kama nitakwenda maana hadi sasa sijapata mwaliko,” alisema Mtanzania mmoja anayeishi Washington DC, jana alipoulizwa na KULIKONI kama atahudhuria mazishi hayo kutokana na kuwahi kufanya kazi na Ballali.

Taratibu za mazishi zinaeleza kwamba Gavana Balali aliyefariki Mei 16, 2008, Washington DC atazikwa leo baada ya ibada itakayofanyika katika Kanisa Katoliki la Mt. Stephen Shahidi mjini Washington DC. Kanisa hilo lipo 2436 Pennsylvania Ave, NW Washington, DC 20037.

“Ibada hiyo ya mazishi itaenda sambamba na kuuona mwili wa marehemu kuanzia saa nne asubuhi. Hata hivyo shughuli hiyo nzima ni kwa ndugu, jamaa, na marafiki wa karibu na si kwa hadhara ya kila mtu atakaye kushiriki,” inaeleza taarifa ya tovuti hiyo ya KLHN.

Imeelezwa kwamba marehemu Ballali anatarajiwa kuzikwa katika makaburi ya Wakatoliki ya Gate of Heaven eneo la Silver Spring, MD.

Miongoni mwa watu mashuhuri walioalikwa mazishi hayo ni Balozi wa Tanzania nchini Marekani Ombeni Sefue, watumishi wa idara mbalimbali alizowahi kuzitumikia ikiwemo Shirika la Fedha Duniani (IMF), ndugu zake ambao wamewasili siku chache zilizopita, na baadhi ya Watanzania kadhaa waishio maeneo ya Washington DC na miji jirani.

Hata hivyo, taarifa za tovuti hiyo zimegusia kitu ambacho sio cha kawaida kwa mila na desturi za Waafrika kwamba upo uwezekano wa mwili huo kuteketezwa kwa moto kwani makaburi hayo pia hutoa huduma hiyo.

“Kama ulikuwa ni wosia wake kuteketezwa, basi kwa kanuni za Kanisa Katoliki zitafanyika mara tu baada ya ibada. Kwa kanuni za Kanisa Katoliki mwili uliolazwa kwa njia ya kuteketezwa kwa moto mabaki yake (majivu) hawapewi familia, kusambazwa au kugawanywa katika mafungu madogo madogo na badala yake ni lazima yawekwe ardhini au kwenye sehemu maalumu inayotumika kwa maziko ya namna hiyo,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo ya KLH.

Ballali ambaye amefariki akiwa amezungukwa na ‘wingu’ kubwa la kashfa dhidi yake na dhidi ya taasisi aliyoiongoza inasemekana aliacha wosia uliotaka atakapofariki basi azikwe Marekani.

Hata hivyo, pamoja na kashfa nyingi zilizoandikwa na vyombo mbalimbali, hasa magazeti na kutangazwa majukwaani, Ballali hakuwahi kushtakiwa rasmi pamoja na kuwapo taarifa kwamba aliwahi kuhojiwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).

Ballali ambaye ameacha mke na familia, amekuwa akitamka wazi kwamba hajawahi kuiba hata senti moja ya umma katika kipindi chote akiwa BoT na kuwashutumu watu ‘aliowakwamisha’ kuwa chanzo cha kuandamwa kwake na tuhuma mbalimbali kabla ya kukataliwa kujiuzulu na hatimaye kufukuzwa na Rais Jakaya Kikwete.

Kifo cha Ballali kimetokea katika mazingira na wakati nchi ikiwa katika wimbi kubwa la tuhuma za ufisadi na misukosuko ya kisiasa, hali ambayo inazidisha utata wa kifo hicho kutokana na baadhi ya mambo kumgusa moja kwa moja marehemu.

Hali hiyo imesababisha watu wengi wakiwamo watu mashuhuri kuhoji uhalisia wa kifo hicho na kupendekeza kufanyika kwa uchunguzi huru na makini kuthibitisha kifo cha Ballali kabla ya kuzikwa kwake.

Marehemu Ballali alijiunga na Benki kama Gavana Julai 14 1998 hadi Januari 8, 2008.

Ballali ambaye alikwenda ghafla nchini Marekani mwishoni mwa mwaka jana akiwa na nia ya kurejea nchini, alikwama huko baada ya kubainika na matatizo makubwa tumboni kabla ya kulazwa hospitali na kufanyiwa upasuaji mkubwa.

Kwa mujibu wa habari hizo za awali, Ballali aliieleza familia yake kwamba alikuwa akihofia kula kitu chenye madhara makubwa hasa baada ya madaktari wa Marekani kumfanyia uchunguzi mara tu alipowasili nchini humo.

Wakati akiendelea na matibabu, Ballali aliandika barua kuelezea nia yake ya kuomba kujiuzulu kutokana na kuendelea kuzorota kwa afya yake huku akiwa bado na majukumu mazito ya kusimamia uchumi wa Taifa.

Hata hivyo, hakukuwa na taarifa zozote za upande wa serikali kuthibitisha kupokea barua ya kujiuzulu kwa Ballali siku kadhaa kabla ya serikali kutangaza matokeo ya ukaguzi wa kampuni ya nje iliyopewa kazi ya kukagua hesabu za Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA).

Ni baada ya Rais Jakaya Kikwete kutangaza kupitia ripoti ya wakaguzi hao, ndipo alipotamka kumfuta kazi Ballali bila kuzungumzia lolote kuhusu kujiuzulu kwake.

Hata hivyo baadhi ya watumishi ndani ya BoT, walieleza wazi kwamba kabla hata ya taarifa za kujiuzulu na hatimaye kufutwa kazi kwake, Ballali aliondoka nchini akijua kwamba hatorejea tena nchini hasa baada ya serikali kuteua Manaibu Gavana wawili, Juma Reli aliyekuwapo na Profesa Prof. Benno Ndulu (ambaye aliteuliwa kuwa Gavana mpya).

Ballali amekuwa Gavana wa Benki Kuu kwa miaka saba na alielezwa kupatiwa matibabu katika hospitali moja mjini Boston, huko Marekani, lakini kabla ya kuanza tiba alikuwa nchini akipambana na shutuma nzito za ufisadi dhidi yake na taasisi ya umma anayoongoza.

Katika mkutano na waandishi wa habari makao makuu wa Benki Kuu Julai mwaka jana, Ballali alisema hawezi kujiuzulu na kwamba tuhuma dhidi yake ni za “uzushi na uongo mtupu.”

Pamoja na kukanusha kwake, Ballali alipata kuhojiwa na Takukuru kabla hajaondoka nchini, mahojiano ambayo yalielezwa kumkera kiongozi mmoja wa juu serikalini. Kiongozi huyo hayupo madarakani kwa sasa baada ya kujiuzulu kwa kashfa ya ufisadi.

KULIKONI-Ijumaa 23 Mei, 2008
 
DC kwenye mazishi ni kesho saa nne na baadaye kuandamana kwa balozi.

Jumamosi asubuhi, kuingiza timu Columbus na kuparry hadi jumatatu wii hrs.

Jumanne kurudi kwenye libeneke na kupigana na mafisadi.

Fair?

Whats happenin' miss lady?
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom