mose
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 422
- 395
KWELI KABISA...Huku mtaani kuna mikopo kausha damu, nini maana ya mikopo kausha damu ni mikopo ambayo mzunguko wako wa maingizo,(cash flow),kwa siku ama kwa mwezi ni kidogo kuliko hela za marejesho mfano maingizo yako kwa siku ni elfu 5 halafu marejesho ni elfu 8 huo utakuwa ni mkopo kausha damu, vile vile nasisi kama maingizo yetu pamoja na matumizi ya lazima haywawezeshi kuulipa mkopo utakuwa ni kausha damu
Mfumo mzima wa fedha wa Dunia una mazuri na mabaya yake khasa unavyoingiliana na 'tabia' za Walimwengu..
Dhamira na Tabia mbovu, Kwa Ujumla wake hupelekea mifumo mibovu!
BASI, ubovu wa mfumo ni zao la ufahamu kumbaizi wa wanajamii wenyewe--wanajamii wanapokuwa wamejisahau ama 'wamejaa kwenye mfumo'; basi kinachowasibu ni 'Saizi yao'...
Inawezekana kuachana na mfumo huu, lakini hili si suala la kuamuliwa na mtu fulani ama kikundi fulani cha watu; ni jambo lenye kuhitaji 'kuwasanua' wanajamii wenyewe katika kule 'kujua ilivyobora'...
SASA, ikiwa kwa mfano wanajamii hawatambui maana ya 'Mapinduzi'; basi ndiyo wanabakia kuwa 'mifugo' kwenye mifumo mibovu' ya watawala na watawaliwa...
Mfumo wa mibovu ya fedha na tawala, ni zao la 'Majaribu ya Kiutu' ambayo huamua hatma za viumbe vyenye (1) Usentienti, (2) Konsayansi, na (3) Nuru ya Ufahamu...
Mifumo yote ya Mikopo na Riba, ina 'Uhuni' kwa 'ukweli wake wa ndani khasa'...
Kukopa na Madeni, yote mawili yanaasili ya kulipika ama/na kutolipika--kuna namna ya hisabati za kialama kuhusiana na ukweli wake; Hata kwa mfano, hili suala wa 'kuvutia uwekezaji wa miundo mbinu ya NIshati' -- 'Wawekezaji watarajiwa/wadau' kuja na shauri la ule wasiwasi na 'marejesho ya Kiuwekezaji', ni jambo ambalo daima linafahamika kwa 'Wadau wa Akilikubwa'... Jambo hili huwa ndiyo mwanzo wa 'mtama kwa watoto' --kimisaada ama nasibu ya 'ushirika wa maendeleo'...
Kasi ya Maendeleo, Ukuaji wa Uchumi na Kujitosheleza Kijamii/Taifa kwa taifa lenye mseto wa rasilimali 'watu mzigo' ni kizungumkuti kwa 'Mataraji ya Kibepari'. Hata kuwaalika 'Wawekezaji' kuna namna hili ni 'jambo kichekesho'--kipi bora kupata--mali ama akili?... Ama ndiyo isemwe majibu mepesi kwa maswali magumu?
Je, nani ambaye hubeba mzigo wa madeni yasiyolipika katika 'Uchumi Mpana wa Dunia'? Je, kuna 'kujisahaulisha fulani', mambo ya kutathminika uhimilifu wa kimadeni, kwa upande wa mkopeshaji--na mawakala wa utundu wa wenye 'kuuma na kupuliza'? ama/na Je, ni kujinyonga mwenyewe kwa upande wa mtu mwenye kuwa 'mtumwa wa madeni'?
Watu Binafsi waliovibopa ndiyo husemwa ni 'Wafadhili wenye Utu'--nani anayewafanya hao kuwa ni 'Matajiri' wenye kuja kuwa na moyo wa kutoa/kujitolea kifedha za misaada ya ruzuku(Philanthropists?)--Washirika wa Maendeleo wa Kujitegemea ukiondoa 'Mashirika Rasmi' ya Udau wa Maendeleo Duniani?
... Mwanzo wa 'Serikali Kimvuli' ya Dunia...
Watu Maskini 'wasio na akili' ni 'Mzigo' hapa Duniani; lakini upo utundu wa kuficha dhana za 'ubinadamu wenye ujinga' kwa 'Usahihi wa Kisiasa' kuhusiana na 'Elimu'... Hawa, wanajamii wasiojitambua, nao ni 'Mtaji' wa 'Mifumo yenye Kudumisha wenye nacho na wasionacho'.
Kwa sehemu, na wakati mmoja hata mwingine, wachache wa hawa huonekana kana 'kustahili msaada'--wengi huachwa wateseke na kuangamia kwa shida zao... Vita, Njaa na Maradhi. Wanaotoa misaada wananufaika na pande zote mbili za 'Shida ama/na raha za walimwengu'; kwa kuwa uwezeshaji wa kifedha na mikopo ni 'Panya anayeuma na Kupuliza'...
Mara nyingine hata wadau hawa wa 'kuuma na kupuliza' hutamania jamba/mambo yaliyo 'mabaya zaidi' kwa 'sukari ya sumu' -- kwa jumuiya ya kimataifa... Kwa kuwa ni unaivu kudhani kila mtu 'Tajiri basi ana akili nyingi'... Utajiri yaweza kuwa ndiyo akili nyingi lakini siyo 'Maadili'; na tena akili nyingi inaweza kuwa na maana/mapelekeo ya nasibu ya 'figisu' ama/na 'utundu wa kula na vipofu'...
Kuna namna, kuna Wanaokuwa ni 'Matajiri'-- matajiri ile chafu, kwa kuwa 'Wamenyonya Jasho na Damu' la wengine kwa unaivu wa kimifumo -- watu wenye wametoa kibali kwa 'Statusi Kwou' kutokana na 'Kutoku-JUA ilivyobora... Iwe kupitia biashara za mikondo mipana ya 'Fedha', 'Tekinolojia' ama/na 'Viwanda vya Silaha/Madawa' n.k; Hata pia 'Pesa za Kuchapishwa tu na 'kupeana chini ya meza'...
Kaka Kafulila yuko Sahihi kabisa...
Tunahitaji kuishi na mashetani kwa kufikiri kama mashetani; lakini hili lisitutolee utu wa kujiongeza ili kujua ilivyobora.
Viongozi hawawezi kwenda kinyume na mifumo inayotawala Dunia--Madhara yake ni Makubwa! Yanaweza kugharimu maisha ya viongozi, ustawi wa jamii na hata usalama wa jamii yote husika.
Namna pekee ya 'kumalizana na mifumo inayotawala Dunia', kwa kheri, ni kuongeza 'Mwangaza kwa Wanajamii' ili hatua zote za Mipango, Maendeleo ya Mikakati ya Kitaifa inashirikishiwa kwa jamii yote pana ya watu/Umma; na si jambo la viongozi/watumishi wachache/serikali na 'usanii'.
Kwa hapa Tanzania, hili linakumbusha sisi wote tudhamirie ku-JUA ilivyobora kwa kila jambo na utendaji wetu; Tujisahihishe na Tuisahihishe mifumo yetu kwa Kudhamira (1) Utaasisi Bora na (2) Maarifa Sahihi.
Mpaka hapo tutakapojiongeza, tujifanye 'vipofu' kimustakabali na mikakati--mikakati ya Uisho...
Tusiwe na nongwa sana na 'Viongozi'; ila tuwe na 'Maelewano nao' kadiri ilivyobora...
Hmmm
View: https://www.youtube.com/watch?v=N87PRcYuqkM