Dawa ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa!

Dawa ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa!

Huu upumbavu upo Afrika tu [emoji3]
Fuatilia rekodi na historia ya top ya matajiri duniani wanaotumia njia hiyo sana.

Wenzio wamevuka KANUNI ya Kutoa ZAKA ya 1/10 wanatoa Hadi ZAKA ya 7/10 wewe hata ZAKA ya 1/10 unashindwa.

Nenda kaangalie matajiri wa Dunia wanatoa Bei Gani Kwa asasi zinazosgughulika na wajane na maskini duniani utarudi kuniambia.

Afrika pia tusipobadilika kurudi kuanza Kutoa Kwa wengine ,tutabaki tulipo.

Kutoa ni KANUNI Mungu ameweka Ili kupokea. Ficha vipesa vyako uvunguni uone kama utatoboa.
 
Kwenye lak Moja 10% yake ni 10,000hiyo ni ya Mungu, ukiila unakula mtaji.

Ndugu Yako msaidie kiasi utakachoona kinafaa kwenye 90 ilobaki.

Kumjaribu Mungu ni zaidi ya hapo.

Kumjaribu Mungu ni kuchukua mshahara mzima 100,000 na kwenda kuwagawia maskini Kisha wewe ukarudi nyumbani mikono mitupu na kumjaribu Mungu ukimwambia nimekujaribu Leo nione ikiwa utakubali nice njaa au la, sadaka ya namna hiyo ndiyo inayoweza kukutoa kwenye Umaskini Si kumpa Mungu change zilizobaki kwenye nauli ya daladala.

Ukitoa sadaka sarafu zilizobaki, Mungu atakurudishia sarafu hizo hizo,

SHERIA ya utoaji inasema, kile ukitoacho ndicho hukurudia Kwa kuzidishwa.

Kuna matajiri wengi duniani wamefika hapo walipo Kwa Kutoa ZAKA 5/10 ,7/10 Badala ya ZAKA ya 1/10.

Mungu ni mwaminifu sana.

Ubarikiwe.
Kuna sehem niliona maandishi kua usimtafute mchawi Lipa zaka
 
Ukipeleka sadaka Yako Kwa manabii wa uongo imekula kwako,

Peleka sadaka pale muhimbili Kuna wazazi hawana pesa watoto wao wafanyiwe operation,

Peleka sadaka Kwa wajane, au somesha yatima.

Mungu atakubariki sana.

Amen
Kazi kweli
 
Yesu akajibu akamwambia, Imenenwa, Usimjaribu Bwana Mungu wako.
Haikuhusiana na kutoa
Hapa ilikuwa kitu kingine kabisa,kisa Cha shetani na Yesu!
Luka 4 pale soma vzr
Halafu soma Malaki 10....
Utaona tofauti yake
 
INTRODUCTON.

Leo naongea na wote wenye uhitaji wa pesa, Kila mpango wako kupata pesa umekwama,

Naongea na wote wenye ukata wa pesa, walioajiriwa na Wana mishahara lakini wanadaiwa Kila Kona, mshahara hautoshi.

Naongea na wenye biashara ndogo na za kati ambao wanafanya juhudi zote kujitoa walipo kiuchumi lakini wanazidi kudidimia kwenye dimbwi la Umaskini.

Naongea na wote wenye madeni Sugu Kila Kona, wangependa kulipa madeni hayo Ili wawe huru lakini hawaoni njia ya Kupata kipato kulipia, ndo wanawaza kukopa tena.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa kidato Cha SITA, jobless, wakati nikisubiri mchakato wa kujiunga na chuo kikuu, nilirudi nyumbani kwetu.

Nikiwa nyumbani, nilipata shida sana kuishi nyumbani bila KAZI yoyote Kwa kipindi kile.

Siku moja, nilipewa pocket money na Mzee ya Tshs 20,000, nilikuwa na mahitaji mengi zaidi ya pesa niliyopokea, nilishukuru kupokea pesa hiyo kidogo na kuondoka kwenda kununua mahitaji yangu binafsi,

Nilinunua mahitaji machache na nilibakiwa na 2,000 tu.

Jumatano siku iliyofuata ilikuwa siku ya maombi Kanisani kwetu, niliondoka nyumbani mdogo mdogo nikielekea Kanisani, njiani nilinunua vitu vingine vidogo vidogo na kubakia na shs 600.

Nilianza kupata mawazo sababu pesa imeisha na mahitaji yangu hayajaisha na sijui lini tena ntabahatisha kupata pesa ingine.

Nikiwa njiani kuelekea Kanisani, niliwaza nisitoe sadaka niitunze hiyo 600 Ili ilinde mfuko wangu maana sikujua lini tena ntapata pesa,

Nikiwa katika kuwaza huko, ndipo lilinijia wazo la kumjaribu Mungu kupitia matoleo.

Niliwahi soma BIBLIA (Malachi 3:10-12). Nikakutana na andiko linaloongelea jinsi ya kumjaribu Mungu Kwa matoleo.

Niliwaza kuwa, sh 600 niliyonayo ni ndogo, isingenifikisha popote, kwanini nisiitumie hiyo kumjaribu Mungu?

Niliongea na Mungu ndani ya NAFSI yangu na kumwambia Mungu, Ewe mwenyezi Mungu, umesema katika neno lako kuwa nikujaribu Kwa matoleo na ZAKA Ili nisipungukiwe, Nami Leo hii naitoa pesa hii yote,akiba pekee niliyonayo Ili nione ikiwa utanibariki au la, nililenga kumjaribu Mungu kupitia neno lake.

Nilitoa sadaka Ile na kuondoka kurudi nyumbani, wakati natoa sadaka Ile ilikuwa saa tisa jioni,

Ilipofikia saa mbili usiku, nilipigiwa simu na Rafiki yangu ambaye Yeye baada ya kumalisha masomo, alipata ajira ya mkataba Mahali Fulani. Aliniambia kuwa anajisikia kunitumia pesa kidogo Kwa ajili ya matumizi madogo muda huu nikiwa Sina KAZI.

Haukupita muda, message mbili za mpesa ziliingia Kwa kufuatana, Nilipoangalia, alikuwa amenitimia 30,000/=

Tangu hapo, maisha yangu ya utoaji yalibadilika, Kila kipato nilichokipata nilitenga sadaka kwanza na kuinenea nilichotaka sadaka hiyo ifanye.

Hadi sasa navyoongea nawe, ninaishi maisha yangu vizuri sana, sio tajiri sana, lakini sipingukiwi na chochote ninachohitaji.

Nikiona naeekea kuishiwa, huchukua akiba kidogo niliyonayo huenda kuitoa nikinuia mahitaji ambayo ningependa Mungu anisaidie kuyatimiza na hujibiwa Kwa haraka sana.

USHUHUDA WA MWL MWAKASEGE.

Akiwa kwenye semina mahala Fulani, alitoa ushuhuda akisema:

Alipokuwa nje ya nchi Mungu alimsemesha apeleke sadaka Kwa mama mjane aliyeko Arusha. Baada ya kurudi nchini, alisahau kupeleka sadaka hiyo, baada ya muda kupita, alikumbushwa kwenda Kutoa sadaka Ile.

Alipofika Kwa mama yule mjane, alimkuta na alipomweleza alichoambiwa na Mungu kufanya, mama yule alijibu akisema, ameugua Kwa muda mrefu, na alikuwa akiuza nyanya na mboga sokoni, alipougua akashindwa kulipa ada ya wajukuu wanaomtegemea na Hali ikazidi kuwa ngumu.

USHUHUDA huu utupe kujua kuwa IPO haja ya kupendana na kusaidia majirani na watu wenye uhitaji na hatutapungukiwa

JINSI ZAKA,SADAKA NA MATOLEO YANAVYOFANYA KAZI.

Huzuia majanga kukuandama.
Wapo watu akipata tu mshahara, huja taarifa za misiba, wagonjwa, HASARA, Ajali Ili pesa ziende huko, pesa zikikata, matatizo yanapungua, ukipata tena pesa majanga haya hapa,

Ukitoa sadaka, matoleo ZAKA Mungu huzuia majanga hayo kukujia, na utashangaa pesa kidogo upatayo inakidhi mahitaji Yako yote.

SOLUTION.

-Kwa wenye Madeni.
Chukua pesa yote kidogo uliyonayo, tafuta mtumishi wa Mungu anayeishi maisha magumu, mpe sadaka hiyo, inenee sadaka Yako Yale Mungu ungependa akutendee.

-Kwa wanaopokea mshahara na haufiki mwisho wa mwezi.

Chukua mshahara wako Tenga sadaka kabla ya kufanya matumizi yoyote, peleka sadaka Yako Kwa maskini au wahitaji maskini, au hospitalini Kwa walioshindwa kulipa gharama za matibabu, au peleka Kwa mtumishi wa Mungu inenee sadaka Yako na utanipa majibu.

-Wazee wa betting.

Chukua pesa ambayo umepanga kupeleka betting, nenda tafuta familia maskini, wanunulie chakula na mahitaji, inenee sadaka Yako ukimwambia Mungu, nakujaribu Kwa sadaka hii, utaniambia majibu.

- Kwa Wafanyabiashara.

Chukua pesa kwenye mtaji wako, usitoe mabaki, Chukua sadaka kubwa itakayokuuma, ichukue peleka Kwa wahitaji mahispitalini, wapewe ombaomba barabarani, au toa Kwa wahubiri INJILI mabarabarani Kisha mwambie Mungu kuwa unamjaribu Kwa kupitia neno lake mwenyewe na asipolitimiza ni Yeye sasa.

HAKIKA Mungu hawezi vumilia jaribu Hilo, atakujibu haraka iwezekanavyo, Mimi nakushuhudia maisha ninayoishi halisi Hadi Leo.

NB: Wanaokwenda Kwa Waganga na wachawi kutafuta utajiri ni "WAPUMBAVU" Kwa maana Mungu ameruhusu ajaribiwe kupitia matoleo na hawezi shindwa kuwajibu sawasawa na NENO lake.

Amen.

Karibuni Kwa maswali na shuhuda Kwa watakaochukua ushauri huu na kuufanyia KAZI🙏
Ni kweli mkuu!

Hawa vijana wanaosoma sekondari ambao huishiwa wakati mwingine ukiwalisha chakula hakikauki ndani yaani huja na kufurika!!
 
Sadaka sahihi, sehemu sahihi, yenye Iman sahihi inamajibu makubwa zaidi kwako binafsi au hata na uzao wako. Mfano Sadaka ya Malimbuko, watu hawajui tu hii ni ulinzi mkubwa sana na ina baraka za ajabu katika ajira zenu.
 
Haikuhusiana na kutoa
Hapa ilikuwa kitu kingine kabisa,kisa Cha shetani na Yesu!
Luka 4 pale soma vzr
Halafu soma Malaki 10....
Utaona tofauti yake
Basi sawa, itakuwa kweli Biblia inajikanganya.
 
INTRODUCTON.

Leo naongea na wote wenye uhitaji wa pesa, Kila mpango wako kupata pesa umekwama,

Naongea na wote wenye ukata wa pesa, walioajiriwa na Wana mishahara lakini wanadaiwa Kila Kona, mshahara hautoshi.

Naongea na wenye biashara ndogo na za kati ambao wanafanya juhudi zote kujitoa walipo kiuchumi lakini wanazidi kudidimia kwenye dimbwi la Umaskini.

Naongea na wote wenye madeni Sugu Kila Kona, wangependa kulipa madeni hayo Ili wawe huru lakini hawaoni njia ya Kupata kipato kulipia, ndo wanawaza kukopa tena.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa kidato Cha SITA, jobless, wakati nikisubiri mchakato wa kujiunga na chuo kikuu, nilirudi nyumbani kwetu.

Nikiwa nyumbani, nilipata shida sana kuishi nyumbani bila KAZI yoyote Kwa kipindi kile.

Siku moja, nilipewa pocket money na Mzee ya Tshs 20,000, nilikuwa na mahitaji mengi zaidi ya pesa niliyopokea, nilishukuru kupokea pesa hiyo kidogo na kuondoka kwenda kununua mahitaji yangu binafsi,

Nilinunua mahitaji machache na nilibakiwa na 2,000 tu.

Jumatano siku iliyofuata ilikuwa siku ya maombi Kanisani kwetu, niliondoka nyumbani mdogo mdogo nikielekea Kanisani, njiani nilinunua vitu vingine vidogo vidogo na kubakia na shs 600.

Nilianza kupata mawazo sababu pesa imeisha na mahitaji yangu hayajaisha na sijui lini tena ntabahatisha kupata pesa ingine.

Nikiwa njiani kuelekea Kanisani, niliwaza nisitoe sadaka niitunze hiyo 600 Ili ilinde mfuko wangu maana sikujua lini tena ntapata pesa,

Nikiwa katika kuwaza huko, ndipo lilinijia wazo la kumjaribu Mungu kupitia matoleo.

Niliwahi soma BIBLIA (Malachi 3:10-12). Nikakutana na andiko linaloongelea jinsi ya kumjaribu Mungu Kwa matoleo.

Niliwaza kuwa, sh 600 niliyonayo ni ndogo, isingenifikisha popote, kwanini nisiitumie hiyo kumjaribu Mungu?

Niliongea na Mungu ndani ya NAFSI yangu na kumwambia Mungu, Ewe mwenyezi Mungu, umesema katika neno lako kuwa nikujaribu Kwa matoleo na ZAKA Ili nisipungukiwe, Nami Leo hii naitoa pesa hii yote,akiba pekee niliyonayo Ili nione ikiwa utanibariki au la, nililenga kumjaribu Mungu kupitia neno lake.

Nilitoa sadaka Ile na kuondoka kurudi nyumbani, wakati natoa sadaka Ile ilikuwa saa tisa jioni,

Ilipofikia saa mbili usiku, nilipigiwa simu na Rafiki yangu ambaye Yeye baada ya kumalisha masomo, alipata ajira ya mkataba Mahali Fulani. Aliniambia kuwa anajisikia kunitumia pesa kidogo Kwa ajili ya matumizi madogo muda huu nikiwa Sina KAZI.

Haukupita muda, message mbili za mpesa ziliingia Kwa kufuatana, Nilipoangalia, alikuwa amenitimia 30,000/=

Tangu hapo, maisha yangu ya utoaji yalibadilika, Kila kipato nilichokipata nilitenga sadaka kwanza na kuinenea nilichotaka sadaka hiyo ifanye.

Hadi sasa navyoongea nawe, ninaishi maisha yangu vizuri sana, sio tajiri sana, lakini sipingukiwi na chochote ninachohitaji.

Nikiona naeekea kuishiwa, huchukua akiba kidogo niliyonayo huenda kuitoa nikinuia mahitaji ambayo ningependa Mungu anisaidie kuyatimiza na hujibiwa Kwa haraka sana.

USHUHUDA WA MWL MWAKASEGE.

Akiwa kwenye semina mahala Fulani, alitoa ushuhuda akisema:

Alipokuwa nje ya nchi Mungu alimsemesha apeleke sadaka Kwa mama mjane aliyeko Arusha. Baada ya kurudi nchini, alisahau kupeleka sadaka hiyo, baada ya muda kupita, alikumbushwa kwenda Kutoa sadaka Ile.

Alipofika Kwa mama yule mjane, alimkuta na alipomweleza alichoambiwa na Mungu kufanya, mama yule alijibu akisema, ameugua Kwa muda mrefu, na alikuwa akiuza nyanya na mboga sokoni, alipougua akashindwa kulipa ada ya wajukuu wanaomtegemea na Hali ikazidi kuwa ngumu.

USHUHUDA huu utupe kujua kuwa IPO haja ya kupendana na kusaidia majirani na watu wenye uhitaji na hatutapungukiwa

JINSI ZAKA,SADAKA NA MATOLEO YANAVYOFANYA KAZI.

Huzuia majanga kukuandama.
Wapo watu akipata tu mshahara, huja taarifa za misiba, wagonjwa, HASARA, Ajali Ili pesa ziende huko, pesa zikikata, matatizo yanapungua, ukipata tena pesa majanga haya hapa,

Ukitoa sadaka, matoleo ZAKA Mungu huzuia majanga hayo kukujia, na utashangaa pesa kidogo upatayo inakidhi mahitaji Yako yote.

SOLUTION.

-Kwa wenye Madeni.
Chukua pesa yote kidogo uliyonayo, tafuta mtumishi wa Mungu anayeishi maisha magumu, mpe sadaka hiyo, inenee sadaka Yako Yale Mungu ungependa akutendee.

-Kwa wanaopokea mshahara na haufiki mwisho wa mwezi.

Chukua mshahara wako Tenga sadaka kabla ya kufanya matumizi yoyote, peleka sadaka Yako Kwa maskini au wahitaji maskini, au hospitalini Kwa walioshindwa kulipa gharama za matibabu, au peleka Kwa mtumishi wa Mungu inenee sadaka Yako na utanipa majibu.

-Wazee wa betting.

Chukua pesa ambayo umepanga kupeleka betting, nenda tafuta familia maskini, wanunulie chakula na mahitaji, inenee sadaka Yako ukimwambia Mungu, nakujaribu Kwa sadaka hii, utaniambia majibu.

- Kwa Wafanyabiashara.

Chukua pesa kwenye mtaji wako, usitoe mabaki, Chukua sadaka kubwa itakayokuuma, ichukue peleka Kwa wahitaji mahispitalini, wapewe ombaomba barabarani, au toa Kwa wahubiri INJILI mabarabarani Kisha mwambie Mungu kuwa unamjaribu Kwa kupitia neno lake mwenyewe na asipolitimiza ni Yeye sasa.

HAKIKA Mungu hawezi vumilia jaribu Hilo, atakujibu haraka iwezekanavyo, Mimi nakushuhudia maisha ninayoishi halisi Hadi Leo.

NB: Wanaokwenda Kwa Waganga na wachawi kutafuta utajiri ni "WAPUMBAVU" Kwa maana Mungu ameruhusu ajaribiwe kupitia matoleo na hawezi shindwa kuwajibu sawasawa na NENO lake.

Amen.

Karibuni Kwa maswali na shuhuda Kwa watakaochukua ushauri huu na kuufanyia KAZI🙏
.
 
Nani amemjaribu Mungu Kwa matoleo na aje kutupa ushuhuda?

Usipotumia njia hiyo na upo katika ukata wa kifedha, utazidi kudidimia.

Mjaribu Mungu kupitia matoleo.

Amen
 
Tarehe 4/4/2024 nimepata kingine Cha kushuhudia kupitia kumjaribu Mungu Kwa matoleo.

Nina nyumba za kupangisha, ikapita kipindi Cha karibia wik mbili bila kupata mpangaji mpya baada ya waliokuwepo kuhama,

Nilipigiwa simu Kutoka Kwa Mchungaji mmoja mwenye huduma changa aliyeniomba nimchangie pesa kutimiza hitaji Fulani,

Nilimwambia, nakumbuka AHADI niliyokuahidi, ila napata changamoto ya kukosa wapangaji ,niombee,

Wakati namjibu hayo, ilikuwa saa nne asubuhi, ulipofika saa Moja jioni, alikuja mtu akapenda nyumba na kulipia hapo hapo rent ya miezi mitatu.

Nikisema Kweli Mungu unajibu maombi, pale pale nilituma pesa Kwa Mchungaji na kushukuru Kwa maombi.

Tumjaribu Mungu Kwa matoleo, anajibu.

Amen
 
Kwa hii habari ya sadaka, Mungu alinisemesha jambo Moja muhimu sana; tusitoe sadaka kama rushwa ili Mungu atutendee jambo fulani Kwa maana rushwa ni adui wa haki na Mungu katu hapokei rushwa. Rushwa wapeni wanadamu lakini si MUNGU. Unapotoa sadaka jiulize kama hiyo sadaka ni SHUKRANI au ni RUSHWA!!?? Ukiona umetoa sadaka na haupati majibu jua kabisa sadaka Yako ilikuwa na viashiria vya rushwa. Sadaka inaweza kuwa na viashiria vya rushwa kama imetolewa Kwa shinikizo la nje, imetolewa Mahali pasipo sahihi au watu sahihi, imetolewa wakati usio sahihi, imetolewa Kwa Nia isiyosahihi( hatupati kwasababu twaomba vibaya), imetolewa ungali ukiwa na uchungu na watu, imetolewa pasipo kuambatana na Toba( hakuna aliye mwema, mwema ni Mungu tu). Sadaka inaweza kuwa na viashiria vya shukrani ikiwa; utaongozwa na roho mtakatifu pasipo shinikizo la nje, utakuwa na amani wakati wa utoaji, itaendana na maelekezo aliyotoa Mungu mwenyewe, sadaka sahihi na Mahali sahihi n.k .Ukitoa sadaka kama shukrani mbele za Mungu inalipa sana.
 
Usitukane,

Nenda kamjaribu Mungu Kwa kuwanunulia chakula yatima wanaorandaranda usiku huu Kwa akiba ndogo iliyo nayo ukimjaribu Mungu sawasawa na (Malachi 3:10-12).

Amini nakuambia, utajibiwa haraka sana, na utarudishiwa zaidi ya ulichotoa.

Amen
Umejibu vyema! Hekima hii idumu kwako milele
 
Kwa hii habari ya sadaka, Mungu alinisemesha jambo Moja muhimu sana; tusitoe sadaka kama rushwa ili Mungu atutendee jambo fulani Kwa maana rushwa ni adui wa haki na Mungu katu hapokei rushwa. Rushwa wapeni wanadamu lakini si MUNGU. Unapotoa sadaka jiulize kama hiyo sadaka ni SHUKRANI au ni RUSHWA!!?? Ukiona umetoa sadaka na haupati majibu jua kabisa sadaka Yako ilikuwa na viashiria vya rushwa. Sadaka inaweza kuwa na viashiria vya rushwa kama imetolewa Kwa shinikizo la nje, imetolewa Mahali pasipo sahihi au watu sahihi, imetolewa wakati usio sahihi, imetolewa Kwa Nia isiyosahihi( hatupati kwasababu twaomba vibaya), imetolewa ungali ukiwa na uchungu na watu, imetolewa pasipo kuambatana na Toba( hakuna aliye mwema, mwema ni Mungu tu). Sadaka inaweza kuwa na viashiria vya shukrani ikiwa; utaongozwa na roho mtakatifu pasipo shinikizo la nje, utakuwa na amani wakati wa utoaji, itaendana na maelekezo aliyotoa Mungu mwenyewe, sadaka sahihi na Mahali sahihi n.k .Ukitoa sadaka kama shukrani mbele za Mungu inalipa sana.
Umenena vyema,

Sadaka haipaswi kuchukua viashiria vya RUSHWA,

Mada imelenga zaidi utoaji wa kumjaribu Mungu kama ambavyo ameruhusu katika maandiko.

Ubarikiwe 🙏
 
Ulivyo muingiza mwakasenge nimepuuza uzii.wewe ndo walewalee
 
Back
Top Bottom