Dawa ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa!

Dawa ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa!

(Yakobo 4:3).

Hata mwaomba Wala hampati,Kwa Sababu mwaomba vibaya, Ili mvitumie Kwa tamaa zenu.


NB: Nenda kafanye nilichokuagiza, Mungu asipokujibu Rudi kuniita mwongo.
Nipe mstari unaosema tumjaribu Mungu...
 
Amen, kuna siku kuna hela nilikua naiexpect muda mrefu na ikawa imekwama. Sasa hiyo siku, nilikua nasikiliza video ya mafundisho ya kiroho, mchana hivi. Katika kusikiliza prayer request, nikasikia mama mmoja akituma message namna ambavyo anapitia shida kali sana. Kumbuka na mm hapo nina shida na hela.

Sasa kwenye simu nilikua na 23000. Nilivyoingia kwenye yale maombi, nikasikia Roho Mtakatifu anasema omba namba ya huyo mama umtumie hiyo 20k. Nikataka kuobject kwamba mi mwenyewe apeche, Roho akanisisitiza sana. Basi nikasema sawa, hakuna shida. Baada ya prayer session, nikapiga simu redioni kurequest namba za huyo mama. Immediately nimekata ile simu, baada ya dkk moja, ikaingia ile hela niliyoisubiri kwa muda mrefu iliyokuwa imekwama.

Nilimshangaa sana Mungu. Sometimes ukiwa tayari kumtoa Isaka, Mungu huleta mwanakondoo na kukurejeshea tumaini mara moja. Hakika Bwana yu mwema.
Amen ubarikiwe.

Hakuna njia Rahisi kupata pesa kama kumjaribu Mungu Kwa matoleo, sadaka na ZAKA.

Mungu atusaidie.
 
Nimeshakugundua wewe ni mtoto wa mchungaji umekuja kivingine kupalilia sadaka za babaako
 
Itakuwa ulienda kupeleka sadaka Yako Kwa manabii wa uongo, wakakufunga.

Nenda saizi mpe Jirani Yako maskini mhitaji, au kamlipie maskini aliye hospitali, mnunulie madawa na lipa bill zake utaniambia.

Ubarikiwe.
Hiki umesema nitajaribu
 
Kwahiyo hiyo 600 uliitoa sadaka ya kujimaliza ?
ila ulipopokea mkwanja huku kumbuka 10%.
Safi sana
 
Nimeshakugundua wewe ni mtoto wa mchungaji umekuja kivingine kupalilia sadaka za babaako
Mimi ni mtoaji, naijua KANUNI hii Mungu aliyoweka ya kumjaribu Kwa matoleo.

Sijaweka namba kuomba sadaka, nimeelekeza pelekeni sadaka Kwa wagonjwa hospitalini, wasio na uwezo nk nk.

Mjaribu Mungu hata sasa,

Utakuja na ushuhuda hapa.

Amen
 
Hiki umesema nitajaribu
Amini nisemacho,

Njia hii ni Kweli, Mimi ni aiishi. Sipingukiwi na chochote nachohitaji.

Kumbuka mstari (Malachi 3:10-12). Uutumie huo kumkumbusha Mungu utakapomjaribu na kuweka AGANO nae.

Amen
 
ndugu yangu kwakweli naomba ellimu kidogo kuhusu sadaka
1.ivi nikitoa sadaka bila kuisemea maneno kwa utaratibu uliotoa ile inaenda kua hazina yangu mda wowote ninaweza mkumbusha Mwenyezi Mungu niitumie?
2.lakini pia kama naenda kutoa sadaka kwa utaratibu uliopendekeza yaani kwakuisemea sadaka kwa kuyapa maneno yangu uhai juu ya ile sadaka, na mimi ni mtenda dhambi je nitatakiwa nipate sala ya toba kabla ya kuisemea maneno sadaka na kuitoa ?
 
Na mstari unaosema Mungu hajaribiwi pia Upo!!

This is a complex material
Mungu hajaribiwi, amekataza,

Kwenye ZAKA, matoleo na sadaka ametoa mwanya ajaribiwe.

Tumia Siri hiyo Ili usipungukiwe,

Hutakopa, utakopesha bila kutaka urudishiwe ulichokopesha.

Kukosa pesa na kupungukiwa ni uchaguzi wako.

Amen
 
ndugu yangu kwakweli naomba ellimu kidogo kuhusu sadaka
1.ivi nikitoa sadaka bila kuisemea maneno kwa utaratibu uliotoa ile inaenda kua hazina yangu mda wowote ninaweza mkumbusha Mwenyezi Mungu niitumie?
2.lakini pia kama naenda kutoa sadaka kwa utaratibu uliopendekeza yaani kwakuisemea sadaka kwa kuyapa maneno yangu uhai juu ya ile sadaka, na mimi ni mtenda dhambi je nitatakiwa nipate sala ya toba kabla ya kuisemea maneno sadaka na kuitoa ?
Sadaka Ina mdomo inaweza kusema yaliyo ndani ya moyo wa mtoa sadaka.

Si Kila sadaka inahitaji kuinenea, zingine unatoa tu.

Pia ni muhimu kutubu na kujitakasa kabla ya Kutoa sadaka, Kutoa sadaka bila kutubu ni kujipalia makaa.

Bt ambao ni wageni, wasomjua Mungu sana, ni sawa kumjaribu kupitia sadaka na baadae utapata maelekezo juu ya nini Cha kufanya.
 
Hao wahitaji walioko mtaani wanatokea kwenye familia..


Saidia familia yako

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
Mungu ameelekeza sadaka zipelekwe hekaluni, Kwa wajane, wahitaji, wagonjwa hospitalini nk nk.

Ndugu na family Yako kuwasaidia ni WAJIBU wako Si sadaka hiyo.
 
INTRODUCTON.

Leo naongea na wote wenye uhitaji wa pesa, Kila mpango wako kupata pesa umekwama,

Naongea na wote wenye ukata wa pesa, walioajiriwa na Wana mishahara lakini wanadaiwa Kila Kona, mshahara hautoshi.

Naongea na wenye biashara ndogo na za kati ambao wanafanya juhudi zote kujitoa walipo kiuchumi lakini wanazidi kudidimia kwenye dimbwi la Umaskini.

Naongea na wote wenye madeni Sugu Kila Kona, wangependa kulipa madeni hayo Ili wawe huru lakini hawaoni njia ya Kupata kipato kulipia, ndo wanawaza kukopa tena.

MY LIFE EXPERIENCE.

Nilipokuwa kidato Cha SITA, jobless, wakati nikisubiri mchakato wa kujiunga na chuo kikuu, nilirudi nyumbani kwetu.

Nikiwa nyumbani, nilipata shida sana kuishi nyumbani bila KAZI yoyote Kwa kipindi kile.

Siku moja, nilipewa pocket money na Mzee ya Tshs 20,000, nilikuwa na mahitaji mengi zaidi ya pesa niliyopokea, nilishukuru kupokea pesa hiyo kidogo na kuondoka kwenda kununua mahitaji yangu binafsi,

Nilinunua mahitaji machache na nilibakiwa na 2,000 tu.

Jumatano siku iliyofuata ilikuwa siku ya maombi Kanisani kwetu, niliondoka nyumbani mdogo mdogo nikielekea Kanisani, njiani nilinunua vitu vingine vidogo vidogo na kubakia na shs 600.

Nilianza kupata mawazo sababu pesa imeisha na mahitaji yangu hayajaisha na sijui lini tena ntabahatisha kupata pesa ingine.

Nikiwa njiani kuelekea Kanisani, niliwaza nisitoe sadaka niitunze hiyo 600 Ili ilinde mfuko wangu maana sikujua lini tena ntapata pesa,

Nikiwa katika kuwaza huko, ndipo lilinijia wazo la kumjaribu Mungu kupitia matoleo.

Niliwahi soma BIBLIA (Malachi 3:10-12). Nikakutana na andiko linaloongelea jinsi ya kumjaribu Mungu Kwa matoleo.

Niliwaza kuwa, sh 600 niliyonayo ni ndogo, isingenifikisha popote, kwanini nisiitumie hiyo kumjaribu Mungu?

Niliongea na Mungu ndani ya NAFSI yangu na kumwambia Mungu, Ewe mwenyezi Mungu, umesema katika neno lako kuwa nikujaribu Kwa matoleo na ZAKA Ili nisipungukiwe, Nami Leo hii naitoa pesa hii yote,akiba pekee niliyonayo Ili nione ikiwa utanibariki au la, nililenga kumjaribu Mungu kupitia neno lake.

Nilitoa sadaka Ile na kuondoka kurudi nyumbani, wakati natoa sadaka Ile ilikuwa saa tisa jioni,

Ilipofikia saa mbili usiku, nilipigiwa simu na Rafiki yangu ambaye Yeye baada ya kumalisha masomo, alipata ajira ya mkataba Mahali Fulani. Aliniambia kuwa anajisikia kunitumia pesa kidogo Kwa ajili ya matumizi madogo muda huu nikiwa Sina KAZI.

Haukupita muda, message mbili za mpesa ziliingia Kwa kufuatana, Nilipoangalia, alikuwa amenitimia 30,000/=

Tangu hapo, maisha yangu ya utoaji yalibadilika, Kila kipato nilichokipata nilitenga sadaka kwanza na kuinenea nilichotaka sadaka hiyo ifanye.

Hadi sasa navyoongea nawe, ninaishi maisha yangu vizuri sana, sio tajiri sana, lakini sipingukiwi na chochote ninachohitaji.

Nikiona naeekea kuishiwa, huchukua akiba kidogo niliyonayo huenda kuitoa nikinuia mahitaji ambayo ningependa Mungu anisaidie kuyatimiza na hujibiwa Kwa haraka sana.

SOLUTION.

-Kwa wenye Madeni.
Chukua pesa yote kidogo uliyonayo, tafuta mtumishi wa Mungu anayeishi maisha magumu, mpe sadaka hiyo, inenee sadaka Yako Yale Mungu ungependa akutendee.

-Kwa wanaopokea mshahara na haufiki mwisho wa mwezi.

Chukua mshahara wako Tenga sadaka kabla ya kufanya matumizi yoyote, peleka sadaka Yako Kwa maskini au wahitaji maskini, au hospitalini Kwa walioshindwa kulipa gharama za matibabu, au peleka Kwa mtumishi wa Mungu inenee sadaka Yako na utanipa majibu.

-Wazee wa betting.

Chukua pesa ambayo umepanga kupeleka betting, nenda tafuta familia maskini, wanunulie chakula na mahitaji, inenee sadaka Yako ukimwambia Mungu, nakujaribu Kwa sadaka hii, utaniambia majibu.

- Kwa Wafanyabiashara.

Chukua pesa kwenye mtaji wako, usitoe mabaki, Chukua sadaka kubwa itakayokuuma, ichukue peleka Kwa wahitaji mahispitalini, wapewe ombaomba barabarani, au toa Kwa wahubiri INJILI mabarabarani Kisha mwambie Mungu kuwa unamjaribu Kwa kupitia neno lake mwenyewe na asipolitimiza ni Yeye sasa.

HAKIKA Mungu hawezi vumilia jaribu Hilo, atakujibu haraka iwezekanavyo, Mimi nakushuhudia maisha ninayoishi halisi Hadi Leo.

NB: Wanaokwenda Kwa Waganga na wachawi kutafuta utajiri ni "WAPUMBAVU" Kwa maana Mungu ameruhusu ajaribiwe kupitia matoleo na hawezi shindwa kuwajibu sawasawa na NENO lake.

Amen.

Karibuni Kwa maswali na shuhuda Kwa watakaochukua ushauri huu na kuufanyia KAZI🙏
Ndaga 🤝🤝
Ila hapo kwenye ombaomba sishauri
Kwingine kote sawa,naunga mkono hoja!
 
Kwahiyo hiyo 600 uliitoa sadaka ya kujimaliza ?
ila ulipopokea mkwanja huku kumbuka 10%.
Safi sana
Nimesema hapo juu kuwa,

Baada ya Muujiza huo, maisha yangu yalibadilika hata Leo,

Nisipotoa sadaka, sipati hatua yoyote maishani Hadi nitoe kwanza.

Ubarikiwe.
 
Ndaga 🤝🤝
Ila hapo kwenye ombaomba sishauri
Kwingine kote sawa,naunga mkono hoja!
Maskini wapo tangu enzi na enzi.

Mungu ameagiza tuwape msaada maskini.

Asema, amhurumiaye maskini......

Ubarikiwe. Amen
 
Back
Top Bottom