Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Maalim Seif aandike kiingereza kibovu hivyo? Ni uzee au? Siamini,labda umenakili hovyo

Mzee Tupatupa
 
Hao polisi wana maelekezo maalum, hakuna cha unga wala ugali.

Hii serikali ya awamu ya 5 imezidiwa maarifa.
 
Hivi hakuna viongozi ccm wanao jihusisha na madawa..? Mbona mm naona wapinzani wanabeba mzigo mzito sana
 
Duh polisi wetu wanashangaza wanavyopelekeshwa mpaka aibu naona mimi,Mungu ninusuru mimi na kizazi changu na kazi hii hakika kwa Tz jamaa wanaburuzwa sana na wanasiasa ambao wengi wao ni wehu tu.
 
Iyo njia ni batili aitazaa matokeo chanya , pili ndani ya iyo vita zimeingizwa siasa.
 
Ujinga wa wapinzani ni kudhani sheria zipo kwa baadhi ya watu tu na kujiona wao wapo juu ya sheria. Ishu ya madawa wameitwa watu wengi, lakini kuitwa Mbowe eti sio haki. Huyo Mbowe mnalala naye kwamba mnajua kila anachokifanya? Huyo Mbowe mnatembea naye kila sehemu kwamba mnajua anachokifanya? Suala binafsi la Mbowe mnalifanya kuwa la chama, si upuuzi huu. Au labda hayo madawa anayotuhumiwa ndio yanawafaidisha kwenye vyama vyenu?
 
Hao polisi wana maelekezo maalum, hakuna cha unga wala ugali.

Hii serikali ya awamu ya 5 imezidiwa maarifa.
Ninachojiuliza...hivi hawa jamaa kweli wanajua wanachokifanya? Wiki mbili toka umemtuhumu mtu ana madawa ya kulevya, na ameshaona mnachowafanyia wengine mliowatuhumu, kweli huyo mtu kama ni kweli anafanya mambo hayo, atakuwa bado ameyaacha tu nyumbani kwake! Hii kitu ni kichekeaho cha karne na aibu kubwa kwa taasisi. Hii presha wanayopelekeshwa nayo na bw. Daud No-rinda, itawaua aisee!
 
Huo sio upekuzi, bali ni udhalilishaji. Upekuzi ungeishafayika kitambo

Polisi bwana tokea wamtanganze,yeye kwani mjinga aache ushahidi ndani?

Wastage of resources and police time.

Wazee wa comedy unasachi kwa mtu baada ya tangazo kwenye media,[emoji2][emoji2]only in tz

nashangaa maana ni muda sasa. kama tatizo ni lile lile ni kama walimpa nafasi basi

Mkuu hata kama mimi ninayo haya madawa tangia mbiu ya mgambo inaanza sijasafisha nyumba tu.
Wengi wetu humu jamvini kumbe tunajifanya kuwa wajuzi kwa kila fani na taaluma.

Serikali (RC na Polisi) inamwita Mh kiongozi Mkuu wa Chama cha Siasa na Kambi ya Upinzani Bungeni, kumhoji, na kwa jeuri anatangaza hadharani kutokwenda;

Wasaidizi wake nao wanatangaza hadharani kwamba wanakubaliana naye asiitikie mwito;

Lakini bado wanamkamata Kiongozi huyo na kwenda kumsachi nyumbani kwake;

Nabado mnatia mashaka uwezo na weledi wa Polisi! Hakika, kama siyo mapenzi kwa Mh, ni umbumbu wa hali ya juu ya kazi, ujuzi na uwezo wa Polisi.

Ati, mwasemaje nyie mlioandika hivyo!
 
Pole sana...na ahsante Kwa kutuonesha zilipoishia akili zako
Kwa sasa polisi wanamfanyia upekuzi nyumbani Kwake ili kujiridhisha ...

source:John Mrema (CHADEMA).
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…