Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Mbona mnamsemea mhusika! Tusubiri kauli yake kabla na baada ya kuwa kituo cha Polisi, kama walivyofanya wengine akiwemo Mch Gwajima. Tukumbuke aliiitisha wanahabari kabla kuwa hatokwenda, akaungwa mkono na wafuasi wake.
 
watanzania sie waoga....hatuwez kufikia yaliyotokea Rwanda au Burundi..so achana na habari za kumwaga damu! hakuna atakaye mwaga damu rabda amwage jasho
Jiongopee Mkuu, Cyprus walimwaga damu, endelea na ujinga wako.
 
Makonda amepata wapi pesa za kununua Lexus, Benz, na kujenga maghorofa na kununua apartment kama ilivyosemwa na wabunge? nani wa kumchunguza makonda kama na yeye anajihusisha na biashara za madawa ya kulevya au la?
 
Nyie Chadema ni wapuuzi sana, mnawalea hawa polisi na uongozi wa Mbowe ni goigoi hadi kufikia polisi sasa wanawashika sehemu za siri nakuzichezea. Ifike wakati tukubali hali halisi kuwa kwa siasa za huyu kiongozi wa sasa Mbowe hafai kuwa mwenyekiti anatakiwa kuachia ngazi chama apewe Lema. Hili tamko mnalialia tu lakini hakuna tamko lolote la nini kinafuata. Mzee Lowassa ndio amewapumbaza mpigeni chini turudi kwenye siasa za harakati
... Hili bandiko linanikumbusha lile tangazo la Vodacom la kudata.. mtu anaulizwa Jina lako nani anajibu kuku akipanda baiskeli ana mbio.. Jikite kwenye hoja.
 
Kwani red brigade ya chadema IPO Kenya??au lile shamba lao la ujasusi lipo bagamoyo ya somalia..?? Humu mnajifanya kuongea..wakishughulikiwa mnasema chuki za kisiasa..nikuulize swali..kipindi cha kampeni ulikuwa unawaona hawa Jamaa na lowasa ofisi za ufipa?? Hilo ndio jumba lao la kukutana..linaitwa ngome..huingii hovyo hovyo..lina CCTV kila kona..lina story ndefu hilo jengo
Hivi hayo yote maovu ya vyama bado yanapita na kusabanishwa na sheria za vyama ya Tanzania. Je hakuna haja ya kuangalia mienendo ya vyama na kufanya kitu, kwa nini tunatuhumu na kulalamika tu.
 
Breaking news
a98fe565ad728260e7ce917e14fb0297.jpg
 
Chadema bana Mara wanakanusha hakukamatwa alijipeleka Mara wanakiri kakamtwa daah
 
Na Tundu Lissu usiku huu:

Waheshimiwa habari za usiku huu. Naomba kutoa updates juu ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama Mh. Freeman Mbowe. Mimi na Katibu Mkuu Dkt. Vincent Mashinji tumeshuhudia sehemu ya sachi iliyofanyika nyumbani kwa Mwenyekiti kati ya saa tatu unusu na saa sita usiku huu. Kama nilivyosema kwenye ujumbe wangu wa awali, hii sio vita dhidi ya wafanya biashara ya madawa haramu bali ni vita ya kisiasa dhidi ya sisi wapinzani wa CCM na Rais Magufuli. Kwa uthibitisho wa kauli yangu naomba niwapatie orodha ya vitu walivyokamata polisi nyumbani kwa Mwenyekiti Mbowe. Vitu hivyo vimeorodheshwa kwenye fomu na. DCEA 003 inayoitwa 'Hati ya Ukamataji' iliyotolewa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kama ifuatavyo:
(1) Hati moja ya CHADEMA CHASO kwenda kwa Mwenyekiti ya tarehe 16/7/2013
(2) Picha mbali mbali nane za matukio ya uhalifu - picha za wahalifu wanaoharibu mali
(3) Hati moja ya Rasimu ya Kwanza ya CHADEMA kuhusu uundwaji wa Red Brigade
(4) Hati moja ya kurasa 13 inayoongelea mambo ya Muungano.

Hivi ndivyo vielelezo vilivyokamatwa nyumbani kwa Mwenyekiti vinavyothibitisha kwamba yeye ni muuza unga!!! Kama isingekuwa ukweli kwamba hivi ninavyoandika Mwenyekiti wangu yuko mahabusu Central, hiki kingekuwa kichekesho cha mwaka. Lakini Mwenyekiti anasota mahabusu usiku huu. Huu ndio ushahidi ambao Kamanda Sirro na polisi wake wamekuwa wanamtafutia Mwenyekiti wetu kwa amri ya Paul Makonda. Hatuna budi, katika hali hii, kuomboleza - kama alivyofanya Mwalimu katika kitabu chake 'Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania' - juu ya mahali ilikofikishwa nchi hii yetu. Nitawatumia picha ya orodha hiyo shortly.

Update: Mwenyekiti Mbowe aachiwa

Kama tulivyowajuza kwamba iwapo itatokea jambo lolote la umuhimu kujuzana kabla ya asubuhi tutafanya hivyo, tunapenda kuwatangazia wanachama wetu,wadau,wapenzi, na wapenda haki,amani na demokrasia ya kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe ameachiwa huru punde tu mnamo majira ya SAA saba na robo usiku huu.

Tunawashukuri wote kwa sala,maombi na subira na hivyo kuhitimisha salama SAA KUMI za Mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi nchini katika kituo kikuu cha Polisi jijini Dar es salaam.

Taarifa za ziada juu ya jambo hili zitatolewa kesho.

Salum Mwalim
Naibu Katibu Mkuu
Chadema

Mimi sijalala kila nikiwaza makonda ni nani sipati jibu,bigup mbowe wewe ni HERO
 
Na Tundu Lissu usiku huu:

Waheshimiwa habari za usiku huu. Naomba kutoa updates juu ya kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Chama Mh. Freeman Mbowe. Mimi na Katibu Mkuu Dkt. Vincent Mashinji tumeshuhudia sehemu ya sachi iliyofanyika nyumbani kwa Mwenyekiti kati ya saa tatu unusu na saa sita usiku huu. Kama nilivyosema kwenye ujumbe wangu wa awali, hii sio vita dhidi ya wafanya biashara ya madawa haramu bali ni vita ya kisiasa dhidi ya sisi wapinzani wa CCM na Rais Magufuli. Kwa uthibitisho wa kauli yangu naomba niwapatie orodha ya vitu walivyokamata polisi nyumbani kwa Mwenyekiti Mbowe. Vitu hivyo vimeorodheshwa kwenye fomu na. DCEA 003 inayoitwa 'Hati ya Ukamataji' iliyotolewa na Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya kama ifuatavyo:
(1) Hati moja ya CHADEMA CHASO kwenda kwa Mwenyekiti ya tarehe 16/7/2013
(2) Picha mbali mbali nane za matukio ya uhalifu - picha za wahalifu wanaoharibu mali
(3) Hati moja ya Rasimu ya Kwanza ya CHADEMA kuhusu uundwaji wa Red Brigade
(4) Hati moja ya kurasa 13 inayoongelea mambo ya Muungano.

Hivi ndivyo vielelezo vilivyokamatwa nyumbani kwa Mwenyekiti vinavyothibitisha kwamba yeye ni muuza unga!!! Kama isingekuwa ukweli kwamba hivi ninavyoandika Mwenyekiti wangu yuko mahabusu Central, hiki kingekuwa kichekesho cha mwaka. Lakini Mwenyekiti anasota mahabusu usiku huu. Huu ndio ushahidi ambao Kamanda Sirro na polisi wake wamekuwa wanamtafutia Mwenyekiti wetu kwa amri ya Paul Makonda. Hatuna budi, katika hali hii, kuomboleza - kama alivyofanya Mwalimu katika kitabu chake 'Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania' - juu ya mahali ilikofikishwa nchi hii yetu. Nitawatumia picha ya orodha hiyo shortly.

Update: Mwenyekiti Mbowe aachiwa

Kama tulivyowajuza kwamba iwapo itatokea jambo lolote la umuhimu kujuzana kabla ya asubuhi tutafanya hivyo, tunapenda kuwatangazia wanachama wetu,wadau,wapenzi, na wapenda haki,amani na demokrasia ya kwamba Mwenyekiti Freeman Mbowe ameachiwa huru punde tu mnamo majira ya SAA saba na robo usiku huu.

Tunawashukuri wote kwa sala,maombi na subira na hivyo kuhitimisha salama SAA KUMI za Mwenyekiti wetu kuwa chini ya Jeshi la Polisi nchini katika kituo kikuu cha Polisi jijini Dar es salaam.

Taarifa za ziada juu ya jambo hili zitatolewa kesho.

Salum Mwalim
Naibu Katibu Mkuu
Chadema
We huna Akili, eti hii vita ya madawa ni ya chadema! Unataka kutuambia akina Wema, TID, Manji(diwani wa ccm) hao wote ni chadema? Uwe unatumia angalau sehemu kidogo ya ubongo wako iliyobakia kuacha mihemko na kuwa mkweli. Ovyo sana wewe.
 
Back
Top Bottom