DC. Jokate Mwegelo: Ametoa siku saba kwa wenyeviti wa serikali za mitaa kuunda Vikundi vya Ulinzi Shirikishi katika Mitaa yao.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo ametoa siku saba kwa wenyeviti wa serikali za mitaa wilayani humo kuhakikisha wanaunda vikundi vya ulinzi shirikishi.
Agizo hilo amelitoa leo Aprili 29,2022 alipokuwa akizungumza na wenyeviti hao katika ukumbi wa Iddi Nyundo uliopo katika Manispaa hiyo.
Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka viongozi hao kuhakikisha suala la ulinzi na usalama linapewa kipaumbele ili kuwezesha wananchi kuishi kwa usalama.
"Ninatoa siku 7 muhakikishe kule ambapo hakuna vikundi vya ulinzi shirikishi mnaanzisha vikundi hivyo na kule ambapo vilikuwepo ila vinalegalega mviimarishe".Alisema Mhe.Jokate
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa kanda maalum ya Dar es salaam,Muliro Jumanne Muliro amesema kuwa uhalifu unatokea pale ambapo hakuna ulinzi na kusisitiza kuwa suala la ulinzi ni jukumu la kila raia.
"Ili uhalifu utokee lazima kuwepo na fursa,na fursa ni pale ambapo hakuna ulinzi kwa kile ambacho mhalifu anachokusudia kufanya".Alisema Afande Muliro.
Kikao hicho ambacho kilihusisha kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya,wenyeviti wa serikali za mitaa pamoja na baadhi ya vikundi vya ulinzi shirikishi kilikuwa na lengo la kuweka mikakati ya jinsi ya kukabiliana na wimbi la vitendo vya uhalifu ambavyo vimeanza kujitokeza kwa siku hizi za karibuni.
Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo ametoa siku saba kwa wenyeviti wa serikali za mitaa wilayani humo kuhakikisha wanaunda vikundi vya ulinzi shirikishi.
Agizo hilo amelitoa leo Aprili 29,2022 alipokuwa akizungumza na wenyeviti hao katika ukumbi wa Iddi Nyundo uliopo katika Manispaa hiyo.
Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka viongozi hao kuhakikisha suala la ulinzi na usalama linapewa kipaumbele ili kuwezesha wananchi kuishi kwa usalama.
"Ninatoa siku 7 muhakikishe kule ambapo hakuna vikundi vya ulinzi shirikishi mnaanzisha vikundi hivyo na kule ambapo vilikuwepo ila vinalegalega mviimarishe".Alisema Mhe.Jokate
Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa kanda maalum ya Dar es salaam,Muliro Jumanne Muliro amesema kuwa uhalifu unatokea pale ambapo hakuna ulinzi na kusisitiza kuwa suala la ulinzi ni jukumu la kila raia.
"Ili uhalifu utokee lazima kuwepo na fursa,na fursa ni pale ambapo hakuna ulinzi kwa kile ambacho mhalifu anachokusudia kufanya".Alisema Afande Muliro.
Kikao hicho ambacho kilihusisha kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya,wenyeviti wa serikali za mitaa pamoja na baadhi ya vikundi vya ulinzi shirikishi kilikuwa na lengo la kuweka mikakati ya jinsi ya kukabiliana na wimbi la vitendo vya uhalifu ambavyo vimeanza kujitokeza kwa siku hizi za karibuni.