DC Jokate Mwegelo atoa siku saba kwa wenyeviti wa Serikali za Mitaa kuunda Vikundi vya Ulinzi Shirikishi katika Mitaa yao

DC Jokate Mwegelo atoa siku saba kwa wenyeviti wa Serikali za Mitaa kuunda Vikundi vya Ulinzi Shirikishi katika Mitaa yao

JUMA JUMA

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
790
Reaction score
964
DC. Jokate Mwegelo: Ametoa siku saba kwa wenyeviti wa serikali za mitaa kuunda Vikundi vya Ulinzi Shirikishi katika Mitaa yao.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Temeke Mhe.Jokate Mwegelo ametoa siku saba kwa wenyeviti wa serikali za mitaa wilayani humo kuhakikisha wanaunda vikundi vya ulinzi shirikishi.

Agizo hilo amelitoa leo Aprili 29,2022 alipokuwa akizungumza na wenyeviti hao katika ukumbi wa Iddi Nyundo uliopo katika Manispaa hiyo.

Mwenyekiti huyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya hiyo amewataka viongozi hao kuhakikisha suala la ulinzi na usalama linapewa kipaumbele ili kuwezesha wananchi kuishi kwa usalama.

"Ninatoa siku 7 muhakikishe kule ambapo hakuna vikundi vya ulinzi shirikishi mnaanzisha vikundi hivyo na kule ambapo vilikuwepo ila vinalegalega mviimarishe".Alisema Mhe.Jokate

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi wa kanda maalum ya Dar es salaam,Muliro Jumanne Muliro amesema kuwa uhalifu unatokea pale ambapo hakuna ulinzi na kusisitiza kuwa suala la ulinzi ni jukumu la kila raia.

"Ili uhalifu utokee lazima kuwepo na fursa,na fursa ni pale ambapo hakuna ulinzi kwa kile ambacho mhalifu anachokusudia kufanya".Alisema Afande Muliro.

Kikao hicho ambacho kilihusisha kamati ya ulinzi na usalama ya Wilaya,wenyeviti wa serikali za mitaa pamoja na baadhi ya vikundi vya ulinzi shirikishi kilikuwa na lengo la kuweka mikakati ya jinsi ya kukabiliana na wimbi la vitendo vya uhalifu ambavyo vimeanza kujitokeza kwa siku hizi za karibuni.

20220429_175733.jpg

20220429_175750.jpg

20220429_175757.jpg

20220429_175742.jpg

20220429_175739.jpg

20220429_175736.jpg
 
Kwa hiyo polisi wanalipwa kwa kazi gani?
Does it mean ule upuuzi wa kulinda sungusungu?
Yaani nikeshe usiku nazunguka mitaani na rungu bila malipo halafu kesho yake niende ofisini kwangu?
Hivi vidangaji vya bongo muvi vilipewa vipi machaka kama haya!!!
 
Ulinzi shirikishi haupo kisheria na ni wa hiari, wananchi waelimishwe umuhimu wake na washawishiwe kujiunga nao na sio kutumia nguvu kama DC wangu anavyofanya, police ni wajibu wao kulinda raia na mali zao (wamekula kiapo),police watching na siasa na watekeleze wajibu wao bila y kuingiliwa na politicians. Wazo ni zuri ila lifanyike kiustaarabu sio vitisho(mrema na sungusungu yake...Adv.Mabere alimfundisha sheria)
 
Kwa hiyo polisi wanalipwa kwa kazi gani?
Does it mean ule upuuzi wa kulinda sungusungu?
Yaani nikeshe usiku nazunguka mitaani na rungu bila malipo halafu kesho yake niende ofisini kwangu?
Hivi vidangaji vya bongo muvi vilipewa vipi machaka kama haya!!!
Polisi wana kazi gani? Mbona mambo haya hayakuepo kipindi cha Magufuli?
Nikifanyiwa uhalifu wana mchango gani kwangu?
Sitachanga hata 100 kuwalipa hawa waganga njaa
 
Kwa hiyo polisi wanalipwa kwa kazi gani?
Does it mean ule upuuzi wa kulinda sungusungu?
Yaani nikeshe usiku nazunguka mitaani na rungu bila malipo halafu kesho yake niende ofisini kwangu?
Hivi vidangaji vya bongo muvi vilipewa vipi machaka kama haya!!!
Idadi polisi sio kubwa kiasi cha kuwawezesha kulinda mitaa na vitongoji vyote vya nchi hii.
Hivyo Ulinzi Shirikishi ni muhimu sana. Muhimu ni kuwekwa utaratibu maalumu wa jinsi gani ufanyike na wananchi waelimishwe juu ya umuhimu wa wao kujilinda. Tukiwaachia Polisi kila kitu tutaendelea kupigwa
 
Polisi wana kazi gani? Mbona mambo haya hayakuepo kipindi cha Magufuli?
Nikifanyiwa uhalifu wana mchango gani kwangu?
Sitachanga hata 100 kuwalipa hawa waganga njaa
Tuliwaambia kipindi cha Magufuri wizi ulikoma,watu wakawa wanabisha,hatukuwahi kusikia hizi ngojera,kila mtu aliwajibika kwa kazi yake,sasa kazi ya polisi tunapewa sisi wananchi, wakati kuna watu wanakula mshahara na mavx kwa kodi ya mlala hoi,Kama polisi kazi imewashinda kuna jeshi la ziada liazimwe
 
Tungepunguza police post maana sasa hivi polisi wetu ni maafisa wanangoja waletewe wahalifu. Uanze tena utaratibu wa doria. Polisi wawe usiku kucha wanazunguka kwenye makazi ya raia. Vituo vitakavyobaki vipatiwe usafiri ili likitokea tukio waweze kufika mapema. Ni aibu vibaka waachiwe kutamba kwa saa nzima wakati polisi wanangoja kupambazuke ndio wafike kwenye tukio.

Amandla...
 
Ukianza kuisema serikali vibaya wanatumia kodi wanakutafuta wakikudaba wanakubinya kende!,badala watumie hiyo kodi kutulinda!
 
Kuna tatizo la ulinzi Wilaya ya Temeke, suluhisho ni Wilaya kuajiri polisi watakaolipwa na mapato ya ndani ya Wilaya.

ULINZI SHIRIKISHI TANZANIA
Pia waende kisasa zaidi polisi-mtaa hao wawe na namba maalum za simu janja zinazowaunganisha na wajumbe wa nyumba kumi kumi waliochaguliwa na wananchi kupokea taarifa (sahihi /credible) on-time za matukio au kuwepo makundi yasiyoeleweka mtaani.

Wajumbe wa nyumba kumi kumi pia wawe na namba za simu za wakaazi wao ili wakaazi hao ikiwa ni usiku wa manane waweze kutoa ripoti kwa txt msg au wito na hao wajumbe baada ya kujiridhisha kwani wanawafahamu wakaazi wao mtaani, mara moja wawasiliane na Polisi-mtaa ili waweze kufika eneo husika kwa haraka.

Mbinu za za jeshi la Polisi katika kuzuia matukio kufanyika au kuwasili haraka katika eneo la tukio hukabiliana na changamoto nyingi ikiwemo upungufu wa askari polisi, vitendea kazi, utambuzi wa maeneo tukio lilopotokea au kulipo na uwezekano wa uhalifu kutendeka na pia usafiri wa haraka kufika eneo husika ni haba sana .


Mfano tunaona maeneo ya mabwanyenye ya Masaki jijini Dar es Salaam wanatumia mfumo huo kwa kuajiri makampuni ya ulinzi na kwa muda wote masaa 24 wanaweza kuwasiliana na wateja waliolipia ulinzi huo. Utaona magari ya kampuni binafsi za ulinzi yame-paki karibu na maeneo ya wateja wao ili ikitokea uhitaji basi wanafika haraka kwa mteja.

Ulinzi shirikishi unaweza kufuata mfumo wa Polisi-Mtaa kulipwa posho na pia wajumbe wa mitaa kufikiriwa kupewa aina ya posho na wakaazi wa eneo husika ili kuimarisha usalama ktk maeneo yao.

Ikiwa jeshi la polisi linakagua leseni za kampuni binafsi sioni changamoto yoyote ya jeshi la Polisi kukagua vikosi vya polisi-mtaa na wajumbe wa mitaa ili kuwapatia elimu zaidi ya ulinzi shirikishi na kupewa ushirikiano pale ambapo tukio litahitaji jeshi la Polisi kuhusika ili hatua za kisheria na PGO kutumika.
 
Kwa hiyo polisi wanalipwa kwa kazi gani?
Does it mean ule upuuzi wa kulinda sungusungu?
Yaani nikeshe usiku nazunguka mitaani na rungu bila malipo halafu kesho yake niende ofisini kwangu?
Hivi vidangaji vya bongo muvi vilipewa vipi machaka kama haya!!!
Polisi saivi wameinvest traffic mchana huko mapato ni makubwa zaidi kuliko doria za usiku kwenye nyumba za uswazi.
 
Polisi wana kazi gani? Mbona mambo haya hayakuepo kipindi cha Magufuli?
Nikifanyiwa uhalifu wana mchango gani kwangu?
Sitachanga hata 100 kuwalipa hawa waganga njaa
Unadhani polisi wapo wengi wa kutosha kulinda kila mtaa?

Isitoshe suala la usalama/ulinzi huanzia kwa mtu binafsi.

Kama hutaki kuchangia ulinzi wako binafsi shauri yako.
 
Back
Top Bottom