DED Magu angalia sana Idara ya Elimu Msingi

DED Magu angalia sana Idara ya Elimu Msingi

Angalia ulivyo hopeless!! Haha yaani unaiwaza mil 80 baada ya kustaafu? Unawaza mkopo wa mil 20 ukatwe 7 years?

Kwa mentality hii wewe ni mwalimu tu usijifiche.
Sina sababu yoyote ya kujificha hata kama nikiwa mwalimu maana huna unachoweza kunidhuru kwa kejeli na majigambo yako huku ukishindwa kusimamia mada iliyopo mezani ya malalamiko dhidi ya waliotajwa. Badala yake, unajikita kuonyesha dharau kwa waalimu, unajiinua kujionyesha kwamba hata mkopo wa 20M/= au mafao ya 80M/= kwako ni hopelessness!!
Wewe kama uko nchi hii, unafanya kazi gani halali inayokupa riziki yako ya kila siku hadi ufikie hatua ya kumdharau mtumishi wa umma na kumwita hopeless?
Mtumishi wa umma ana security ya maisha yake na familia yake na anaaminika hata na taasisi za kifedha maana yuko guaranteed.
Ni mbumbumbu tu, mpumbavu au mjinga na asiyejitambua ndiye anaweza kumdharau mtumishi wa umma. Mtu wa aina hiyo hana future wala hana msingi wowote katika maisha yake na hajui mustakabali wake, maisha yako yamemgomea na anaishi kwa kubangaiza na amejawa na hasira.
Mtu wa aina hiyo hawezi kutoa hoja zenye kujenga au kutanzua tatizo zaidi ya kutukana, kubeza na kudharau kama wewe ulivyo. Wewe ndiwe hopeless, huna tumaini, maisha yako yananing'inia (hanging), hayajatulia (unsettled) na umebebeshwa mizigo bila hiari yako kama ID yako ilivyo "lusungo" ndio maana badala ya ku-counter hoja, unajifariji kwa kutukana!!
 
Haha hapo walimu ndo mnaniachaga hoi, kwahiyo hako kamshahara mbuzi mwenyewe unajiona ndo una bima ya maisha!

Teh teh ukute hapo unapokea laki nne unajiona umewin wakati wenzio hyo tunaimaliza club kwa night moja tuu....

Yaani uumie na chaki ukiisubiri 80M ukistaafu ilhali wenzako wanaingiza kwa mwaka!!

Poor you!
Sina sababu yoyote ya kujificha hata kama nikiwa mwalimu maana huna unachoweza kunidhuru kwa kejeli na majigambo yako huku ukishindwa kusimamia mada iliyopo mezani ya malalamiko dhidi ya waliotajwa; badala yake unajikita kuonyesha dharau kwa waalimu na ukijiinua kujionyesha kwamba mkopo na mafao ya 80M/= kwako ni hopelessness!!
Wewe kama uko nchi hii na unafanya kazi gani halali inayokupa riziki yako ya kila siku hadi ufikie hatua ya kumdharau mtumishi wa umma na kumwita hopeless?
Mtumishi wa umma ana security ya maisha take na familia yake na anaaminika hata na taasisi za kifedha maana yuko guaranteed.
Ni mtu mbumbumbu tu, mpumbavu au mjinga ndiye anaweza kumdharau mtumishi wa umma maana huyo huwa hajitambui. Anaweza akawa hana future wala hana msingi wowote katika maisha yake na hajui mustakabali wake na huenda maisha yamemgomea na anaishi kimkandamkanda.
Mtu wa aina hiyo hawezi kutoa hoja zenye kujenga au kutanzua tatizo zaidi ya kutukana, kubeza na kudharau kama wewe ulivyo. Wewe ndiwe hopeless, huna tumaini lolote, maisha yako yananing'inia (hanging), hayajatulia (unsettled) na umebebeshwa mizigo bila hiari yako kama ID yako ilivyo "lusungo".
 
Issue za hao akina Johari zinakuhusu nini? We utanifundisha nini mimi?
Huna uwezo wa kusoma na kuelewa nilichoandika, ndiyo maana unauliza hilo swali. Ungekuwa umeisoma mada na kuelewa usingeuliza swali hilo, labda ungeuliza jingine.
Naweza kukufundisha mambo mengi tu; one of them is how to express yourself, you are not capable of.
 
Haha hapo walimu ndo mnaniachaga hoi, kwahiyo hako kamshahara mbuzi mwenyewe unajiona ndo una bima ya maisha!

Teh teh ukute hapo unapokea laki nne unajiona umewin wakati wenzio hyo tunaimaliza club kwa night moja tuu....

Yaani uumie na chaki ukiisubiri 80M ukistaafu ilhali wenzako wanaingiza kwa mwaka!!

Poor you!
Kwa hiyo kwa sababu wewe unaingiza 80M/= kwa mwaka unataka kila mtu aingize hizo kama wewe?
Wako wenzako wanaingiza 100M/= weekly na wametulia.
Kwa hiyo ukiingiza 80M/= kwa mwaka, kazi zingine zote zisizoingiza that much zisimame zisifanyike?
Una mawazo mgando sana wewe, unajidhihirisha umbumbumbu wako; hujui hata division of labour? Pity!!
 
Inaelekea wewe kangodi una mengi unayoyajua kuhusu hiyo ofisi ya DEO; good. Unasema DEO Glory amesimamia taaluma mpaka Magu imeshika nafasi ya tatu kimkoa kwenye PSLE 2019. Glory alikuja lini Magu mpaka awe na impact ya kufanikisha matokeo ya PSLE? Glory hana muda mrefu tangu ashike ofisi hiyo akitokea Taaluma Msingi Ilemela; amekuja Magu amekuta ofisi ina-run, ikiendeshwa na maofisa wasomi wabobezi, chikaka Majura na chikaka Nyagabona, achana na yeye Glory mwenye ka-dirii kamoja kama mwalimu wa kawaida sekondari.
Idadi ya ziara za Huyo Glory kwenye mashule huwezi kuzilinganisha na idadi ya ziara za Majura. Mimi niko Kisesa, nina ushuhuda wa shule yetu hapa na maeneo mengine kuhusu ukaguzi wa mara kwa mara uliokuwa unafanywa na huyo SLO; na kwa muda mfupi waalimu wengi walikwishamfahamu Majura kwa ufuatiliaji wake, na alikuwa na impact kwa waalimu.
Ni hodari pia wa utatuzi na usuluhishi wa migogoro baina ya waalimu wakuu na waalimu, uongozi wa shule na vijiji, hiyo ni moja ya sifa za kiongozi bora.
Alikuwa anashirikisha ofisi nzima kwenye ziara hizo tena kwa kuwalipa posho kwenye kaguzi hizo kutoka kwenye 10% ya fedha za P4R ambazo SLOs ndio wanazisimamia; alikuwa anawalipa posho hadi ma-secretary; niambie lini ulimwona JJ akifanya ziara ya ukaguzi mashuleni zaidi ya kukaa ofisini na kupiga ile 10% ya P4R ambayo inatakiwa kutumika ofisini?
Haya ninayoyasema hata DED anayajua hata huyo Glory na Johari wako wanayajua.
Wewe unaongea leo kwamba Majura alikuwa analala na waalimu na amevuruga ndoa za watu; OK, WHERE WERE YOU BEFORE TO RAISE THAT ISSUE? Leo DEO wako ametuhumiwa, badala ya ku-counter malalamiko yaliyotolewa dhidi yake unaamua kutoa tuhuma dhidi ya Majura!! Unataka ku-nuturalize hoja dhidi ya Glory, Johari na Prisca kwa kumchafua Majura? Shindwa na ulegee!! Kumbuka, TWO WRONGS DOES NOT MAKE IT RIGHT.
Hagwila uko sawa; huyu anaeyasema hayo sasa alikuwa wapi kuyasema kabla? Huu ni mkakati wa walalamikiwa na wapambe wao kufifisha hoja yako; pambana, dawa imewaingia.
 
Haha hapo walimu ndo mnaniachaga hoi, kwahiyo hako kamshahara mbuzi mwenyewe unajiona ndo una bima ya maisha!

Teh teh ukute hapo unapokea laki nne unajiona umewin wakati wenzio hyo tunaimaliza club kwa night moja tuu....

Yaani uumie na chaki ukiisubiri 80M ukistaafu ilhali wenzako wanaingiza kwa mwaka!!

Poor you!
We mjamaa una fuba sana eeh? Au ndiyo defensive mechanism ya Glory & Co.?
 
We

Weka mambo hadharani; hata kama ni afisa usalama, hajatumwa kuja kunyanyasa watu. Tena mimi naamini kama kweli huyo DEO wa Geita (V) ni afisa usalama, angekuwa mtendaji bora sana maana angekuwa ameiwa. Mfikishieni taarifa zake Mhe. Msukuma adili nae.
Msukuma kachemka ana ishu zake kibao sana
 
Wewe Ligaba ni Premium Member kwenye jukwaa hili adhimu la JF; haitarajiwi uandike hoja zisizo na mashiko kama huyo anayetaka picha ya afisa aliyehamia Misungwi eti amzuie asilale na wake za watu!!
Unasema mimi ni mwenye sifa lakini sijapewa nafasi; mantiki ya kauli yako hiyo ni kwamba mimi naandika haya kwa sababu nawaonea gere au wivu Glory mtui, Johari Mwasha na Prisca.
Umekosea, mimi siyo mwalimu wala si mtumishi wa umma. Lakini kutokuwa mtumishi wa umma hakumaanishi kuwa sina uwezo wa kutambua mambo mbalimbali yanayonizunguka kiasi cha kushindwa kuyatathmini na kuyadadavua.
Nina uwezo huo kwa sababu ninayaona, nayasikia na mengine yananiathiri nikiwa raia wa nchi hii ambaye nastahili kuhudumiwa na watumishi wa umma kama madaktari, manesi, askari, maafisa ardhi, mahakimu, waalimu, na wengine wengi. Hawa ni watu ambao wapo miongoni mwetu, tunaishi nao, tunazungumza nao na tunashirikiana nao; kwa nini nishindwe kujua yanayoendelea kwenye ofisi hizo za umma wakati mimi ni mteja kwazo?
Siyo lazima matatizo yanayojiri katika ofisi za umma ziandikwe na mtumishi wa umma; zinaweza kuandikwa na mtu yeyote huru kama mwandishi wa habari, mwanaharakati, au raia yeyote wa kawaida mwenye uwezo wa kupata taarifa sahihi juu ya jambo analotaka kuliwasilisha kwa wahusika, ilimradi ana maslahi nalo; kama mimi nilivyofanya.
Nimemwandikia DED Magu ili achukue hatua ya kurekebisha udhaifu unaoendelea kwenye ofisi ya DEO Magu maana mimi ni mwana - Magu, mzazi mwenye watoto wanaosoma kwenye shule za umma wilayani Magu; kwa nini ninyamazie ubovu unaoendelea kwenye ofisi ya elimu kwenye halmashauri yetu?
Unasema niache kupambana na system!! Glory, Johari na Prisca wamekuwa system ya elimu Magu? Huyo Glory Mtui aachane na ujinga anaoufanya hapo ofisini kwa sababu ya kukamatwa masikio na Johari Mwasha; atamharibia kazi na atakuwa anazimia mara kwa mara hapo ofisini kama ilivyotokea juzi na leo ametinga ofisini akiwa na cannula, wakati mwenzake anadunda na juba lake tu.
Kufua chupi za maofisa wa elimu siyo kazi yangu, ingekuwa kazi yangu ningefua tu!! Wewe ni JF Premium member; mchango wako unatarajiwa kustawisha mjadala kwa kutoa hoja na si vinginevyo.
Bado wito wangu kwa DED Magu ni uleule; aangalie ofisi ya DEO Magu.
Mbona 2014 yuko serikalini hafu anaandika????
 
UNALALAMIKA NILIKUWA WAPI KUTOA HOJA MAPEMA , WEWE ULIKUWA WAPI KUTOA HOJA ZA D.O GLORY,JOHARI...AMEHAMISHWA MAJURA NDIO UNASEMA ETI KIJA NA MSOMI ....ANAUSOMI UPI?

MBONA KUNA VIJANA WASOMI WANA MASTER LAKINI WAHATAMBI TENA NI WAALIMU WA KAWAIDA NA WENGINE NI WARATIBU

DEGREE HOLDER NDIO USOMI???
MAJURA ALIKUWA AKIZUNGUKA KWENYE MASHULE HASA YENYE WALIMU MABINT NA KUJITAMBULISHA

ALIKUWA FEDHULI ,LUGHA CHAFU ,ALIKUWA ANAJIONA YEYE NDIYO YEYE ANATUKANA WALIMU

WALIMU MARAFIKI ZAKE NI WALE WALIOKUWA WAMESHINDIKANA KWA WAKOPESHAJI KESI ZIKILETWA ANAWASAIDIA KUZIZIMA

MUULIZE !! MAJURA VP KUHUSU YULE MADAM MKE WA MTU AMBAYE WALIKUWA WANAENDA ..ILUNGU MARA KWA MARA UNADHANI TULIKUWA HATUMUONI???

MAJURA KAHAMISHWA KWA MASILAHI YA OFISI KUINUSURU OFISI ....SABABU YA UWOZO WAKE ....
ALIKUWA AKICHUKUA RUSHWA NA KUMLAZIMISHA D.O AWAAMISHE WALIMU WALIMU WALE WENYE UHITAJI WA KUHAMA VITUO D.O ALIKUWA AKIMKATALIA

KAMA NINAYOYASEMA HAYA NI YA UWONGO ASEME NI TAJE ILUNGU ALIKUWA ANAENDA GEST IPI ?NA A LIKUTA NA NANI NA ALIKUWA ANATUMIA USAFIRI WA PRAIVET. CAR NA WAKATI MWINGINE BODA BODA....!!

VIPI KUHUSU YULE MADAMU MKE WA MTU ALIYEKUWA ANAMWAMBIA WAENDE TWIGA GEST AKIBISHA NAWEKA SCREEN SHOT ZA CHAT

HUYU SIO MSOMI...NI MTONGOZA WANAWAKE ZA WATU, NA NI MCHAPAKAZI WA GEST SIO OFISINI

....WATU WA MISUNGWI KUWENI MAKINI NAYE ANATAKA KULETA MAMBO YA KIKABILA ETI CHIKAKA ,YEGO APELEKE HUKO UPUUZI WAKE

POLENI MARAFIKI ZAKE MMEKOSA MXINZI WENZENU KAHAMISHWA
Mbona 2014 yuko serikalini hafu anaandika????
 
Ni kweli; acha na mimi nizungumze machache ninayoyajua kuhusu hiyo ofisi ya DEO Magu ambayo imekumbwa na kashfa nyingi tangu enzi za Saryankanga. Huyu DEO wa sasa ni mpiga hela tu; amekutana na mchagga mwezake Johari rushwa mtindo mmoja.
Naanza na mfano mmoja ambao hata DED Lutengano ataukumbuka. Hivi karibuni tu kuna Mratibu (mama mjane) alihamishiwa kata ya Itumbili kwa uhamisho wa malipo. Mama huyo baada ya kulipwa, DEO Glory na timu yake walimtoza yule mratibu pesa kama shukrani kwao!! Mama yule alikwenda kulalamika kwa DED Lutengano; sijui hatua zilizochukuliwa na DED kama zipo.
Wewe mwenyewe DED, siku za karibuni uliitisha kikao cha Finance ambapo wakuu wa idara walikuwepo. Uliwapongeza wajumbe kwa matokeo mazuri ya mitihani ya darasa la VII; na Katibu wa TSD alichangia kwa kuitaka ofisi ya elimu kuwa na ushirikiano miongoni mwao, badala ya kupigana majungu na kuchongeana hadi kufikia kuhamishwa baadhi ya watendaji chapa kazi kama SLO aliyehamishwa alivyopigwa jungu. Baada ya kikao DEO Glory alimfuata Katibu huyo wa TSD na kuanza kumshambulia kwa maneno; mpaka sasa mahusiano ya watu hao wawili siyo mazuri; lakini pia mahusiano kati ya DEO na Mkaguzi Mkuu siyo mazuri vilevile kwa sababu ya ofisi ya DEO kupanga wasimamizi kwa mapatano na baadhi ya waalimu wakuu ili watahiniwa wa darasa la VII katika shule zao wasaidiwe. Kwa mahusiano haya hafifu kazi zitafanyikaje kwa ufanisi?
Palifanyika semina au kongamano la Juma la Elimu ya Watu Wazima kimkoa hivi karibuni kule Buchosa. Maofisa wanne wafuatao:- SLO aliyehamishwa, Afisa Elimu ya Watu Wazima, DEO Glory na Johari walilipwa posho kwa ajili ya kuhudhuria na kushiriki kongamano hilo la Juma la Elimu ya Watu Wazima. Waliokwenda Buchosa ni wawilo tu; SLO aliyehamishwa na Afisa Elimu ya Watu Wazima. DEO Glory na Johari hawakwenda Buchosa licha ya kulipwa posho, wala hawakuwa ofisini Magu siku zote za kongamano hilo. Huyo ni ubadhirifu wa mali ya umma.
Uhamisho wa SLO kwenda Misungwi pia ni ubadhirifu kwa sababu umetolewa kwa majungu. Afisa huyo amekaa Magu kwa muda wa chini ya mwaka mmoja toka alipohamia Magu akitokea Ukerewe na alilipwa. Kwa uhamisho huu amelipwa tena kumhamishia Misungwi kwa sababu tu Glory na Johari wamekwenda kulalamika kwa Afisa Elimu Mkoa Mwanza eti SLO huyo anawanyima raha!! R.E.O. Mwanza nae kwa sababu hao wawili wote ni wapenzi wake (kama hawajui wajijue sasa), akaamua kufanya alivyofanya TAMISEMI hatimae SLO amehamishwa!!
Mhe. Jaffo, Mhe. Ndalichako, Mhe. Mkuchika afande wangu, tafadhali fuatilieni mambo haya; kuna watu bado hawajamwelewa Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Dr. John Pombe Magufuli kwamba dhamira yake kwa dhati ya moyo wake amekusudia kuipeleka mbele nchi yetu. Baadhi ya watendaji wanafanya yao tu bila kuzingatia Vision, Mission wala Spirit ya Rais wetu. Nitakwenda Magu kumweleza Rais uozo huu siku akija kuzindua mradi wa maji; tutaonana wabaya.
Qummer-maye wallah,ni mwendo wa kuchongeana tu!
 
Nyeusi ni nyeusi tu, ukiita nyeupe ni uongo; lakini ukiwa mnafiki unaweza kufanya hivyo ili kujifariji, lakini wenye kutambua mambo watang'amua.
Kanusha kwa hoja tuhuma zinazotolewa dhidi ya hao wanaolalamikiwa; na kama una malalamiko dhidi ya SLO aliyehamishwa yiweke bayana.
Tunajua taratibu za kiutumishi zipo lakini lazima ziwe na mahali pa kuanzia na panaweza kuwa hapa.
Tamaa ikikomaa huzaa dhambi, na dhambi ikikomaa huzaa mauti; huo ndio mtiririko. Mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba.
Noma sana!
 
Walimu wengi hasa wa msingi majungu Ni mengi Sana mikopo ndio inawachanganya kadi ziko kwa wakopeshaji ...mmebaki ..TU KUCHONGEA D.O..NA CO....HEBU TUACHE MAJUNGU HUYO CHIKAKA NA MAJURA NI RUBISH KABISA ...WASIMAMIZI WA MITIHANI DRS LA VII WALIKUWAWANACHAGULIWA NI WALIOSOMA MOUNT MERU TU DIPLOMA KISA YY NI RECHOR ....
KIONGOZI MZURI NI YULE ANAYESEMWA NA WATU ,MAZUZU KAMA NYINYI ...MNAPOKUNYWA HIVYO VIBALIMI NA EANGLE NDIO MNAJIONA MMEFIKA

MLIKUWA MNAMFURAHIA SANA MAJURA MFATENI ALIKO HAMIA SANA !!!
D.O CLORY KANYAGA KABISA HAPO HAPO USIACHIE HUO MWENDO NI MZURI NA UNATUFAA TUNAKUKUBALI KWA UTENDAJI KAZI WAKO NA BUSARA ZAKO....

HAKIKA MAMBO SASA HIVI NI SHEARI KABISA TUKAAHIDI HATUTAKUANGUSHA ......


 
Walimu wengi hasa wa msingi majungu Ni mengi Sana mikopo ndio inawachanganya kadi ziko kwa wakopeshaji ...mmebaki ..TU KUCHONGEA D.O..NA CO....HEBU TUACHE MAJUNGU HUYO CHIKAKA NA MAJURA NI RUBISH KABISA ...WASIMAMIZI WA MITIHANI DRS LA VII WALIKUWAWANACHAGULIWA NI WALIOSOMA MOUNT MERU TU DIPLOMA KISA YY NI RECHOR ....
KIONGOZI MZURI NI YULE ANAYESEMWA NA WATU ,MAZUZU KAMA NYINYI ...MNAPOKUNYWA HIVYO VIBALIMI NA EANGLE NDIO MNAJIONA MMEFIKA

MLIKUWA MNAMFURAHIA SANA MAJURA MFATENI ALIKO HAMIA SANA !!!
D.O CLORY KANYAGA KABISA HAPO HAPO USIACHIE HUO MWENDO NI MZURI NA UNATUFAA TUNAKUKUBALI KWA UTENDAJI KAZI WAKO NA BUSARA ZAKO....

HAKIKA MAMBO SASA HIVI NI SHEARI KABISA TUKAAHIDI HATUTAKUANGUSHA ......
Badili kuandika kwako haueleweki kabisa 🤔
 
UNALALAMIKA NILIKUWA WAPI KUTOA HOJA MAPEMA , WEWE ULIKUWA WAPI KUTOA HOJA ZA D.O GLORY,JOHARI...AMEHAMISHWA MAJURA NDIO UNASEMA ETI KIJA NA MSOMI ....ANAUSOMI UPI?

MBONA KUNA VIJANA WASOMI WANA MASTER LAKINI WAHATAMBI TENA NI WAALIMU WA KAWAIDA NA WENGINE NI WARATIBU

DEGREE HOLDER NDIO USOMI???
MAJURA ALIKUWA AKIZUNGUKA KWENYE MASHULE HASA YENYE WALIMU MABINT NA KUJITAMBULISHA

ALIKUWA FEDHULI ,LUGHA CHAFU ,ALIKUWA ANAJIONA YEYE NDIYO YEYE ANATUKANA WALIMU

WALIMU MARAFIKI ZAKE NI WALE WALIOKUWA WAMESHINDIKANA KWA WAKOPESHAJI KESI ZIKILETWA ANAWASAIDIA KUZIZIMA

MUULIZE !! MAJURA VP KUHUSU YULE MADAM MKE WA MTU AMBAYE WALIKUWA WANAENDA ..ILUNGU MARA KWA MARA UNADHANI TULIKUWA HATUMUONI???

MAJURA KAHAMISHWA KWA MASILAHI YA OFISI KUINUSURU OFISI ....SABABU YA UWOZO WAKE ....
ALIKUWA AKICHUKUA RUSHWA NA KUMLAZIMISHA D.O AWAAMISHE WALIMU WALIMU WALE WENYE UHITAJI WA KUHAMA VITUO D.O ALIKUWA AKIMKATALIA

KAMA NINAYOYASEMA HAYA NI YA UWONGO ASEME NI TAJE ILUNGU ALIKUWA ANAENDA GEST IPI ?NA A LIKUTA NA NANI NA ALIKUWA ANATUMIA USAFIRI WA PRAIVET. CAR NA WAKATI MWINGINE BODA BODA....!!

VIPI KUHUSU YULE MADAMU MKE WA MTU ALIYEKUWA ANAMWAMBIA WAENDE TWIGA GEST AKIBISHA NAWEKA SCREEN SHOT ZA CHAT

HUYU SIO MSOMI...NI MTONGOZA WANAWAKE ZA WATU, NA NI MCHAPAKAZI WA GEST SIO OFISINI

....WATU WA MISUNGWI KUWENI MAKINI NAYE ANATAKA KULETA MAMBO YA KIKABILA ETI CHIKAKA ,YEGO APELEKE HUKO UPUUZI WAKE

POLENI MARAFIKI ZAKE MMEKOSA MXINZI WENZENU KAHAMISHWA
Kongodi; umetumia muda wako mwingi kueleza kile unachokieleza kuwa ni umalaya wa Majura na umetoa details ambazo unataka jamii iziamini!
Lengo lako ni ku-nutralize malalamiko yangu kwa DED Magu dhidi ya ofisi ya DEO Magu kwamba siyo ya kweli kwa sababu tu Majura analala na wake za watu?
Kama unataka ku-nutralize malalamiko yangu niliyomwandikia DED Magu, kanusha kwa ushahidi hoja zangu nilizoziorodhesha kwenye thread yangu. Huo unaouita "umalaya" wa Majura na unautolea details, hautafuta malalamiko yangu ya msingi kwa DED Magu dhidi ya DEO Magu kwa sababu saula la mapenzi ni personal issue, hata wewe inawezekana tu unalala na mke au mme wa mtu; na inawezekana labda umeshindana na Majura kwa mwanamke au umebwagwa na mwanamke mwenzako kwa Majura kwa hiyo you are crying over spilled milk.
Suala la mapenzi ya Glory Mtui REO Mwanza, mimi nimeliweka kwa sababu mapenzi yao ndiyo yaliyosababisha Glory Mtui kupewa nafasi hiyo aliyo nayo sasa; lakini tatizo lililotokea kwa yeye Glory ni underperformance kwa sababu ya uwezo wake mdogo. Tatizo linakuwa kubwa zaidi kwa sababu Glory badala ya kujazia maarifa akiwa kazini kwa kuwatumia maofisa wazoefu walio chini yake, yeye anawapiga vita na majungu hatimaye ofisi kukosa amani na utulivu; otherwise kama angeweza kumudu ofisi apigwe miti tu maana ni hiyo ni ada ya kimaumbile. Wewe unasema Majura analala na wake za watu Ilungu; kama ni kweli si jambo lenye afya maana linavunja amani na linaweza kuwa na matokeo mabaya sana kijamii hata kama kiofisi inaweza kuwa haina effect.
Lakini, wewe umepataje screenshot ya conversations za Majura na huyo mke wa mtu? Ni mkeo au na wewe ni hawara yako kwa hiyo ulikamata simu yake? Maana huwezi kuingia kwenye chartroom ya mtu iliyo kwenye simu ya mtu mwingine; vinginevyo uwe na shared account. Fafanua uliipateje hiyo screenshot il ueleweke, isije ikawa ni majungu tu.
 
Nimewafuatilia kwa siku kadhaa sasa... Naona mnajaribu kuwa chafua wasiochafuka...
Vipi una msongo wa mawazo? Mimi nimemchafua nani?kabla ya kupost hakikisha unakula Milo zaidi ya mitatu
 
Nimewafuatilia kwa siku kadhaa sasa... Naona mnajaribu kuwa chafua wasiochafuka...
Baada ya kupitia Mjadala huu Ushauri wangu kwa DED Magu, Ndugu; Lutengano Mwalwiba...

Nakuheshimu sana kwa usikivu wako, uhodari, ubunifu na uchapa kazi wako ukiwa kama Karani Mkuu wa Halmashauri ya Wilaya Magu...

Aidha, naomba nikushauri ufanyie kazi mambo kadhaa ikikupendeza
1. Maofisa waliokaa zaidi ya Miaka kumi Wilayani Magu, ikikupendeza wakahudumie na Wilaya zingine..

Hapa usimsahau Afisa taaluma Nyakabona.... Yaani huyu awe wa kwanza kuondoka, amesha kuwa Mwananzengo anamtandao mkubwa wa walimu wakuu, walimu, Waratibu elimu kata.. Ni mkongwe sana huyu, wapo aliofundisha nao, wapo aliwafundisha juzi juzi hapa kwenye course zile za kuunga unga..Ha! Ha! Ha! Huoni hapa haguswi na Mtu.. Usisahau kuwa alijiandaa kuwa Afisa Elimu (DEO) utadhani Babu yake ndio anagawa Vyeo, sasa ilipogeuzwa gia angani hajawahi kukubali mpaka leo.. Usipoteze muda mshauri ahame kama utashindwa TAMISEMI watasikia tu, halafu Nyakabona sijui anakwama wapi? angeondoka Magu, naamini asingechelewa hivi na kugeuka kuwa Mkanga sumu....

Ili Madame Glory-DEO. Aweze kufanya mabadiliko ni lazima huu Mbuyu Udondoke..

2. Naomba uache kukumbatia hawa Maafisa Wachafu, Ooooh! Utachafuka... Najua wengine ni Marafiki zako, achana nao... Wakubalie waondoke... Hawa wanajua vyema figisu za huku Local Government..... Itakuja kula kwako siku moja... Ushauri wangu naomba ikikupendeza wakubalie waondoke...

3. Umewahi kujiuliza kwa nini Maafisa wa Wilaya ya Magu wakipata Uhamisho wa kwenda wilaya zingine wengi wao hukataa na kupangua uhamisho? Magu pazuri bwana...Ha! Ha! Ha! Shamba la Bibi, unakuja Maskini baada ya Muda wewe ni tajiri.... Sasa utakubali kuhama? Hivi huoni SLO- MAJURA anavyo lalamika nyuma ya pazia....ha! ha! ha! ha! Mbona hana hata miaka Miwili hapa Magu akitokea Ukerewe? Magu pakuchota hakuna mwenyewe....

4. Hawa walioshutumiwa wa chunguze lakini ukweli utabaki pale pale mikono yao ni mieupe kabisa... Unajua kwa nini wanashutumiwa? Ni kwa sababu DEO- Glory ameamua kufanya kazi nao, Mbona wakati wa DEO- Salyankanga walikuwa utumwani tu, japo kuwa Leo mmewangushia mzigo...

Kimsingi Migogoro katika utumishi haiwezi kuisha kwa sababu kila mtu anasaka tonge...

Rai yangu kwa Madame Glory -DEO, piga kazi achana na Wakanga sumu, watazinywa Wenyewe..... .Madaraka anatoa Mungu.... Simama katika ukweli, acha kusikiliza majungu, wapende walimu na Viongozi wao, watie moyo... utaona kazi itakapo pigwa na ufaulu utapanda Mara dufu katika wilaya ya Magu..

Kimsingi, Mchukie anaekuambia flani hawezi..Je? Nani anaweza? Kwa maana walimu hatusemeani vyema abadani..... Please JIAMINI WEWE NDIO DEO. Walinde wanawake wenzio hapo awali ilikuwa ngumu kwa Mwalimu wa kike kuhama kutoka Nyasato kuja Kahangara bila kuvuliwa chupi na wanazengo, kanyagia hapo hapo.. Ukisikia kelele jua limewapata..
 
Walimu wengi hasa wa msingi majungu Ni mengi Sana mikopo ndio inawachanganya kadi ziko kwa wakopeshaji ...mmebaki ..TU KUCHONGEA D.O..NA CO....HEBU TUACHE MAJUNGU HUYO CHIKAKA NA MAJURA NI RUBISH KABISA ...WASIMAMIZI WA MITIHANI DRS LA VII WALIKUWAWANACHAGULIWA NI WALIOSOMA MOUNT MERU TU DIPLOMA KISA YY NI RECHOR ....
KIONGOZI MZURI NI YULE ANAYESEMWA NA WATU ,MAZUZU KAMA NYINYI ...MNAPOKUNYWA HIVYO VIBALIMI NA EANGLE NDIO MNAJIONA MMEFIKA

MLIKUWA MNAMFURAHIA SANA MAJURA MFATENI ALIKO HAMIA SANA !!!
D.O CLORY KANYAGA KABISA HAPO HAPO USIACHIE HUO MWENDO NI MZURI NA UNATUFAA TUNAKUKUBALI KWA UTENDAJI KAZI WAKO NA BUSARA ZAKO....

HAKIKA MAMBO SASA HIVI NI SHEARI KABISA TUKAAHIDI HATUTAKUANGUSHA ......
Kwa uandishi wako huo ndugu KANYEGELO una haki ya kumsifia huyo DEO Glory kwa sababu na wewe uko hoi kama yeye.
Staili yako ya uandishi iko sawa kabisa na staili ya Glory ya kuendesha idara; hakuna mpangilio wa uandishi ili ufikishe ujumbe unaoeleweka kwenye hadhira. RENCHOR ndio nini na EANGLE ni kinywaji gani?
Kwa taarifa yako, kadi za watumishi kuwa kwa wakopeshaji ni suala linalomhusu mtu binafsi na namna anavyosimamia bajeti zake na nidhamu yake ya pesa. Kadi zilozoko kwa wakopeshaji siyo za waalimu wa msingi peke yake; ziko za kadi za watumishi wa idara mbalimbali na wenye ngazi tofauti, usirahisishe.
Wewe kama ni mwalimu kweli kama unavyotaka kuaminisha jukwaa, kwa uandishi wako huo hufai kuwa mwalimu maana wewe mwenyewe unatakiwa kufundishwa kuandika. Sijui kwenye namba (hesabu) ukoje, kama kuandika tu umechoka hivyo!
lnawezekana pia umeandika kwa staili hiyo ili kuwadanganya watu waamini kwamba mwandishi ni mtu asiyejimudu kiuandishi wapeleke mawazo yao kwa mtu wa aina hiyo.
Vyovyote iwavyo, bado Glory hana viwango vya kuwa DEO, alitakiwa aendelee kufanya kazi chini ya Maofisa waandamizi ili apate maarifa. Kusimamia idara ni kazi inayotaka uwezo unaostahili; acha porojo.
 
Back
Top Bottom